Amekutuma mwenyewe au? maana hiyo habari ni ya toka 2017.
Help Mahmood Mihile raise money to support WaterAid
www.justgiving.com
Huyo Mahmood Mihile ukitaka kumpata ‘google search’ inaonyesha sio muda mrefu alishirikiana na taasisi moja ya maji kwenye charity ya mpira watakuwa na details zake.
Number ya 01332 hiyo ni area code ya Derby na sio mbali na Leicester ni miji jirani, hayo maeneo kuna wabongo wasomali kadhaa, ukimpata mwenyeji wa Derby anampata.
Sasa shutuma za wizi wa watoto (sio za mzaha uingereza) na watoto wenyewe ukute wamejipiga wasomali kama njia ya kupata makaratasi yao. Ukiingiza polisi na immigration usije kuharibia kila mtu na hao watoto wenyewe.
Ni ushauri tu vitu vya kuzingatia kabla kukurupuka. Halafu hao watoto sasa hivi watakuwa washakuwa wakubwa wanajitegemea. Huyo mama angetafuta mtu anaemfahamu U.K. mradi huyo Mahmood Mihile anatumia jina hilo hilo atakuwa tu kwenye data base za serikali na kupatikana kwa njia za mtaa.
Kuliko haya makelele akaenda wapelekea matatizo makubwa kwa njaa zake, utampaje mtu watoto wako kisa waende ulaya.