Aisee,bila akili ya ziada unaweza kufa maskini yaani.Lakini hyo ndo take home ya ndugu zetu walimu wa shule za misingi.sijui wanaishije,Hata sio ku-fake mzee,
Tu-assume una mke na mtoto mmoja
Chai tu kwa nyumbani kwa hiyo familia watatumia 3000 kima cha chini kabisa,
Wewe pia chai huko kazini kwako assumption 1000 au 1500
Haya mchana familia inakula kiasi gani na wewe unakula nini?
Usiku vipi?
Hapo hujaweka usafiri hata kama ni wa daladala
Hujaweka vocha
Bado hujanywa maji
Mzeee hiyo pesa mjini mtihani
Chai ya 3000?
Hizo ni anasa mkuu, hiyo itakua ni soup
Kiuswazi mihogo au vitumbua vya 600 vinawatosha
Mchana watakula dagaa mchele au samaki kibua wa 3000 mpaka
Usiku wali mchele nusu inatosha baba mama na mtoto
Na chenji itabaki mkuu, hapo hata ikipigwa bajeti ya nyama nusu kilo 3000. Italiwa mchana na jioni plus mboga za majani na chenji ipo
Kweli mkuu huo ndio uhalisia ukiacha 7000 maisha yanaenda poa tuNadhani tunatofautiana maisha, mimi japo mshahara wangu ni zaidi ya hapo ila matumizi ya nyumbani hayazidi 7,000 labda siku moja moja tu niamue,huwa nikitoka kazini napita sokoni nanunua mihogo au viazi vya buku vikichemshwa vinatosha kabisa.
Michelle Obama, jibu huwa inawezekanaje ?, usikimbie kutoa mchango wako kwani wewe ni mdau muhimu sanaNgoja wanakuja..
Hata sio ku-fake mzee,
Tu-assume una mke na mtoto mmoja
Chai tu kwa nyumbani kwa hiyo familia watatumia 3000 kima cha chini kabisa,
Wewe pia chai huko kazini kwako assumption 1000 au 1500
Haya mchana familia inakula kiasi gani na wewe unakula nini?
Usiku vipi?
Hapo hujaweka usafiri hata kama ni wa daladala
Hujaweka vocha
Bado hujanywa maji
Mzeee hiyo pesa mjini mtihani
Tunaiba mpaka vitu tusivyovijua vinatumikaje usisikilize blah blah ya kuwa inatosha kiukweli haitoshi ni hela ndogo sanaNina Dogo ofisini anapata take home 200000,, kila siku Ana kunywa supu ya kuku asbh,mchana chakula cha 3000 na maji , ingawa hana family ila sielewagi,,
Asante kwa mchanganuo. Ila umeacha kipengele muhimu cha kodi ya nyumba. Au ni mchanganuo kwa mtu aliyejenga tayari?Nimeona watu wanasema tu inatosha inatosha bila kutoa mchanganua wa hiyo laki 3 utaitumia vipi?
-Mtoa mada amesema una mke na watoto utawezaje kuibalance hiyo laki 3 na kutosha kabisa?
-Mie natoa direction mpeni mchanganua wa kutumia hiyo laki 3 eg
-Apange vyumba vya Tsh ngapi?
-Mchana ale asubuhi na mchana ale nini akiwa kazini? Nauli?
-Kodi ya meza aache Tsh ngapi na wawe wanaitumia vipi kwa mlo wa asubuhi,mchana(mkewe) na Usiku(famillia)
-Watoto wanasoma chai asubuhi na hela ya kununua mihogo,aisikilimu akiwa shuleni(mtoto hawezi kukaa na njaa mpaka saa tisa ndio aje kula nyumbani)
-Matumizi ya umeme,maji,sabuni(kufua ,kuogea).
Mchanganuo wangu:-
-Awe ananua vitu kwa jumla eg kiroba cha unga cha kilo 5(7,500/=),Mchele kilo 10 wa 1800(18,000),Nyanya kisado (5000),Vitunguu kisado(elfu 6),Mafuta ya taa(elfu 20),mafuta ya kupikia(lita 5 elfu 15),Kiroba cha mkaa(kilo 25 , Tsh 15000)
Hapo Jumla ni 80,000/=
-Baada ya hapo awe anaacha elfu 4 tu ya mboga kila siku kwa Mwezi jumla ni 120,000/=
-Na yeye bajeti yake kwa mwezi awe anatumia elfu 3 kwa siku ,chai atumie za kwenye dispensa ofisini awe ananunua tu chapati mbili za 500 au 600 na mchana msosi wa buku jero na nauli 800 kwahiyo bajeti yake itakuwa elfu 60,000/= kwa mwezi(20 working days)
-Hiyo 40 iwe ni gharama za umeme na maji na vitu vigogo vidogo.
Samahani kwa kukukwazaAcha kumfatilia mwenzako[emoji16][emoji16][emoji16]
kiasi gani inatosha.....?Yaani 10000 kwa siku kwa familia
Yaani familia ile chai,lunch na dinner,
Watoto waende shule,
Mahitaji madogo madogo yatimie
Kiuhalisia haitoshi kabisa
Bado wewe mtafutaji unatoka asunuhi unatudi jioni maana yake lazima ule n utumie usafiri
Usimfanye mwamba akajiona anafuja pesa haitoshi laki tatu ila kwa kujibana kwa nguvu sawa inatosha
wakati naanza kazi yangu ya kwanza kwenye ajira nilikuwa nalipwa TZS 600K take home wakati dereva aliyekuwa ananiendesha alikuwa analipwa 250k .
Nilikuwa namuuliza huyu dereva anawezaje kuishi kwa mshahara huo kwa mwezi , wakati yeye alikuwa na mke mmoja na watoto wanne , halafu alikuwa na mchepuko una watoto wawili, mke wake alikuwa anaishi naye kwenye banda alilokuwa amejenga huko malamba mawili mbezi DSM.
Aliniambia yeye matumizi yasiyo ya lazima hafanyi wakati mimi mzee hiyo 600K hata mwezi hauishi nalikuwa napumulia mashine hapo sina mke wala mtoto.
Ila nilikuja kukaa sawa baadae baada ya kuwa na nidhamu ya matumizi ya pesa yangu kila inapoingia mwisho wa mwezi.
Hivyo mkuu 300K ni nyingi sana ukiiwekea nidhamu kwenye matumizi ya msingi na utaishi bila stress ingawa mikopo ya hapa na pale itakuwa haikauki kwa maisha ya kawaida.
Kila mtu anaishi kulingana na kipato chake, cha msingi ni kujipanga tu na ukipata mke mwenye akili maisha yanasonga vizuri tu.