Mlioomba Ajira Ualimu utumishi Angalieni status zenu

Pantomath

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2019
Posts
842
Reaction score
3,449
Log in > Nenda my Application > Employer.
Kuna watu washaanza kupangiwa sehemu za interview....

Interview ya kwanza(kuandika) utafanyia ulipoombea...

Interview ya pili(Oral)utafanyia mkoa watakayokupangia wao..

Kama uliomba masomo mawili,
Utashangaa Written ya hesabu na phy utafanyia hapa Dar ulipo,
Oral ya physics utafanyia Kigoma,
Oral ya Hesabu utafanyia Mbeya.

Watu niliokua nawaombea taratibu washaanza kuona mabadiliko,
Ila nahisi zoezi halijaisha.



KWA WALE WOTE WALIOOMBA AJIRA ZA UALIMU KATIKA MFUMO WA AJIRA PORTAL
________________________________

KUNA MABADILIKO MUHIMU YAMEFANYIKA
1. Wengi wamebadilishiwa mikoa ya kufanyiwa usaili na ndo mikoa itakayotumika kuwaajili.
2. Kama hujabadilishiwa mkoa na Bado panasoma MDAs & LGAs maana yake ni kwamba wewe hujapangiwa mkoa WA kwenda kufanya usajili, hivyo utaomba Ajira upya pindi zitakapotoka.
Ili kuona mabadiliko hayo , Fanya mambo/hatua zifuatazo
1. Ingia Ajira portal akaunt Yako ( )
2. Ingiza Email/username na Password Yako. Kisha bofya Login .
3. Kisha bofya sehemu ya My Application na utaona mwenendo WA maombi Yako ya Ajira
4. Angalia sehemu ya Job Title kipengere Cha Employer utaikuta kimefanyiwa mabadiliko na kuandikwa jina la mkoa ulilopangiwa kufanya interview , kama hakuna jina la mkoa ulilopangiwa inamaana kwamba Bado hujapangiwa sehemu pa kufanyia interview na huwenda hujakidhi vigezo ,hivyo utarazimika kufanya maombi mengine pindi Ajira zitakapotoka.
NB : Endelea kutembelea Akaunti Yako kila mara Ili kuona madailiko zaidi na siku na tarehe na kituonutakachopangiwa kwenda kufanyia interview
_______________________
Kila la kheli katika maombi Yako,
_______________________
 
Kio
Kila somo na mtihani wake au mtihani ni mmoja
 
Watendaji wa vijiji wanalipwa kias? Mbona wao hufanya interview aisee
 
Unapata faida gani kwa kudanganya mkuu??

Matangazo yote ya kazi, interview na placement yanatolewa waziwazi kupitia tovuti ya utumishi ambapo pia muhusika atapata taarifa pia kupitia profile yake

Hakuna taarifa ya kazi, interview wala kupangiwa kazi anataarifiwa mtu bila ya taarifa kuwa published kwenye tovuti

Tangazo la interview lililotoka ni la Kada ya afya na si la ualimu
 
Kumbuka kama familia ina kipato cha kutosha, mtoto hawezi kusomea ualimu
Huu mstari sidhani kama umekaa vizuri... ualimu ni wito mkuu kwahiyo hata wote mngekua matajiri lazima kuna watu wangekua walimu automatically... thou huko kwingine umeandika vizuri kwenye mambo ya interview ila hiyo line ungeiweka kivingine kwa maana watu wakikataza watoto wao kusomea ualimu it means shule hazitakuwepo.
 
Ualimu Tanzania umewekwa kuwa wa daraja la chini sana, walimu hawaheshimiki Tanzania japo ni taaluma ya muhimu na ya kipekee sana.
 
Ualimu Tanzania umewekwa kuwa wa daraja la chini sana, walimu hawaheshimiki Tanzania japo ni taaluma ya muhimu na ya kipekee sana.
Walimu wenyewe wa Tanzania ndio wamejiweka kwenye hiyo level ila ukichunguza mishahara ya walimu wenye degree utagundua mishahara yao ni ya kawaida ambayo wasomi wengi wa nchi hii wanaipokea katika field mbalimbali.

Walimu wengi kinachowaumiza ni mikopo coz walimu wanakopesheka sana na walio wengi wanaingia kwenye huo mtego then baadae wanapoanza kuteswa na hayo madeni ndio wanarudi kujificha kwenye kivuli cha mshahara mdogo.
 
Dharau mbaya sana, acha vijana waombe kazi
 
Jambo ni moja tuu, kama hutaki usaili bc acha, kaa nyumbani utaajiriwa bila usaili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…