Mlioomba Ajira Ualimu utumishi Angalieni status zenu

Mlioomba Ajira Ualimu utumishi Angalieni status zenu

Aiseee, mimi binafsi ni muoga wa usahili, najijua tokea nasoma. Hivyo niliamua kujiajiri mapemaa kabla hizi mbanga za usahili hazijaanza. Ila kweli maisha yanabadirika jmn, siku hizi mambo yako serious kuliko zamani.
Tunacho kigombania hatukijui pale utakapopangwa isimikinyi ndani ndani uko na ukaona uhalisia wa mshahara na uko maporini ukija linganisha na maisha ya town na kipato ulichokuwa unaingiza utaja ona umegombania upuuzi tu
 
Tunacho kigombania hatukijui pale utakapopangwa isimikinyi ndani ndani uko na ukaona uhalisia wa mshahara na uko maporini ukija linganisha na maisha ya town na kipato ulichokuwa unaingiza utaja ona umegombania upuuzi tu
Mshahara umeainishwa kabisa
 
Tunacho kigombania hatukijui pale utakapopangwa isimikinyi ndani ndani uko na ukaona uhalisia wa mshahara na uko maporini ukija linganisha na maisha ya town na kipato ulichokuwa unaingiza utaja ona umegombania upuuzi tu
kuajiriwa ni utumwa sitaki utumwa,nendeni mkawatumikie mabwana zenu,wacha nipambane na hali yangu kitaa
 
Nimeamini kada ya ualimu serikali ilikuwa imejisahulisha kuwaajiri, yaani jukwaani hapatoshi. Siku ya usaili wale wa YouTube channel za mchongo hawatokosa habari.
 
Ok kwa mimi point zangu ni kuwa;

Mazingira ya kufanyia kazi ni duni kulingana na kada nyingine

Mshahara duni na mazingira duni ya kazi ya ualimu sio sawa kumtia mtu gharama za kwenda kurudi mikoani na wilayani kutafuta mshahara wa 400k

Ukiangalia ufaulu wa miaka hii ni wazi kuwa wanafunzi wanafaulu kupita matarajio na ndio maana wasio na ajira mtaani ni wengi sana hii ina maana walioajiriwa bila interview hawana mapungufu yoyote ambayo yangefanya kuwe na ulazima wa usaili ili kuchuja ubora

Kama ni kutafuta usawa au kuwapambanisha eti kwakuwa wanaohitaji ni wengi bado usawa huo hautakuwepo utake usitake rushwa lazima itatembea

Kigezo cha kupima competency ya mwalimu kwa mtihani wa kuchagua ni uwongo bora hata interview ya kufundisha sio multiple choice

Kuhusu izo kada nyingine wapigwe tu interview kwanza wanafanya kazi mijini na mtonyo wa kutosha lakini pia sio zote kwahiyo hata hizo ambazo mishahara na mazingira ni duni zenyewe kufanya interview za multiple choice ni kupotea rasilimali tu

Nyingine watajazia wengine
Mkuu nimeangalia sababu ulizozitoa kwa upande wangu nimeona hazima mashiko, Kwa sababu kila sababu uliyoitoa na Kada zingine zinapitia pia

Sababu ya kusema kuwa saizi watoto wanafaulu sana wala haina mahusiano na uwezo wa walimu, wote tunajua hili limetokana na SIASA za awamu ya 5 kutaka sifa kwenye kila kitu

Kuna watoto wengi tu na wengine wanatoka kwenye familia zetu, wanafaulu ilhali hawajui kusoma wala kuandika, na wala lawama hatuzipeleki kwa walimu bali wanasiasa

Mbali na walimu Kuna Maafisa Mifugo,kilimo,ustawi wa Jamii,watendaji nk, hawa wote wanatakiwa katika mazingira magumu lakini pia ata mshahara yao ni midogo pia

Lengo la interview kwenye kila sehemu waga linakuwa zuri, miongoni mwa sababu za kufanya interview ni pamoja na

1. UWAZI, kufanya usahili ili upate Jambo Fulani ni vizuri Kwa sababu kunaonesha uwazi katika upatikanaji wa mtu huyo badala ya kumteua tu kitu ambacho waga kinatoa hisia za uonevu

2. KIPIMO, kama mavyuoni walikuwa wanafanya mitihani ili kuonesha uwezo na uteyari wao basi bila Shaka wanastahili kufanya usahili pia ili iwe kipimo cha uwezo wao na uteyari wao wa kwenda kuitumikia hiyo nafasi

3. UWEZO, kama nafasi za kazi zipo 50 mkakutana mnaoigombania mpo 150, Kwa lugha nyepesi watakaopata ni kuwa wamekuwa Bora kuliko wale 100 waliokosa

4.UTHUBUTU, kama ulipigania kazi Kwa kupoteza pesa,kupoteza muda na kupata usumbufu wa kufanya mitihani na hatimae kuipata ni wazi kuwa ulikuwa unahitaji hiyo kazi hivo lazima utafanya kazi Kwa moyo

5.UWAJIBIKAJI, angalau mtu akisotea nafasi ya kazi kunakuwa na % za kuamini kwamba atakuwa muwajibikaji kwa sababu aliisotea hiyo nafasi, tofauti na mtu ambae amepata tu kama sandakalawe

6.THAMANI, kufanya usahili kunaipa thamani hiyo nafasi ambayo watu wamekutana kuipigania

7.UTAYALI, mtu ambae atakubali kufanya usahili ni wazi kuwa ana utayali wa kufanya hiyo kazi,kwenda popote atakapopangiwa,kupata mshahara wowote ule na hivo kupunguza malalamiko ambayo almost kila mtumishi wa TZ anayapitia

Kwahiyo tukumbuke kuwa walimu na wahudumu wa Afya nawao walikuwa wanafunzi kama wanafunzi wa Kada zingine, hakuna uspecial wowote ule ispokuwa mwanzo ilitumika busara ya kuvutia wanafunzi kuchagua kusomea hizo Kada

Kwa hiyo nawao wapo ambao hawana uwezo wa kufundisha vizuri kama ilivo kwenye Kada zingine, hivo tulidhike tu na ukweli kwamba kwa sasa interview haikwepeki
 
Mkuu nimeangalia sababu ulizozitoa kwa upande wangu nimeona hazima mashiko, Kwa sababu kila sababu uliyoitoa na Kada zingine zinapitia pia

Sababu ya kusema kuwa saizi watoto wanafaulu sana wala haina mahusiano na uwezo wa walimu, wote tunajua hili limetokana na SIASA za awamu ya 5 kutaka sifa kwenye kila kitu

Kuna watoto wengi tu na wengine wanatoka kwenye familia zetu, wanafaulu ilhali hawajui kusoma wala kuandika, na wala lawama hatuzipeleki kwa walimu bali wanasiasa

Mbali na walimu Kuna Maafisa Mifugo,kilimo,ustawi wa Jamii,watendaji nk, hawa wote wanatakiwa katika mazingira magumu lakini pia ata mshahara yao ni midogo pia

Lengo la interview kwenye kila sehemu waga linakuwa zuri, miongoni mwa sababu za kufanya interview ni pamoja na

1. UWAZI, kufanya usahili ili upate Jambo Fulani ni vizuri Kwa sababu kunaonesha uwazi katika upatikanaji wa mtu huyo badala ya kumteua tu kitu ambacho waga kinatoa hisia za uonevu

2. KIPIMO, kama mavyuoni walikuwa wanafanya mitihani ili kuonesha uwezo na uteyari wao basi bila Shaka wanastahili kufanya usahili pia ili iwe kipimo cha uwezo wao na uteyari wao wa kwenda kuitumikia hiyo nafasi

3. UWEZO, kama nafasi za kazi zipo 50 mkakutana mnaoigombania mpo 150, Kwa lugha nyepesi watakaopata ni kuwa wamekuwa Bora kuliko wale 100 waliokosa

4.UTHUBUTU, kama ulipigania kazi Kwa kupoteza pesa,kupoteza muda na kupata usumbufu wa kufanya mitihani na hatimae kuipata ni wazi kuwa ulikuwa unahitaji hiyo kazi hivo lazima utafanya kazi Kwa moyo

5.UWAJIBIKAJI, angalau mtu akisotea nafasi ya kazi kunakuwa na % za kuamini kwamba atakuwa muwajibikaji kwa sababu aliisotea hiyo nafasi, tofauti na mtu ambae amepata tu kama sandakalawe

6.THAMANI, kufanya usahili kunaipa thamani hiyo nafasi ambayo watu wamekutana kuipigania

7.UTAYALI, mtu ambae atakubali kufanya usahili ni wazi kuwa ana utayali wa kufanya hiyo kazi,kwenda popote atakapopangiwa,kupata mshahara wowote ule na hivo kupunguza malalamiko ambayo almost kila mtumishi wa TZ anayapitia

Kwahiyo tukumbuke kuwa walimu na wahudumu wa Afya nawao walikuwa wanafunzi kama wanafunzi wa Kada zingine, hakuna uspecial wowote ule ispokuwa mwanzo ilitumika busara ya kuvutia wanafunzi kuchagua kusomea hizo Kada

Kwa hiyo nawao wapo ambao hawana uwezo wa kufundisha vizuri kama ilivo kwenye Kada zingine, hivo tulidhike tu na ukweli kwamba kwa sasa interview haikwepeki
Mkuu nimependa umejibu kwa hoja na sio ushabiki, point zako zipo valid japo zingine umerudia zilezile nilizosema mimi

Mfano nimesema kwa kada ambazo zinafanana na ualimu kimazingira na mshahara pia nimeona kufanyiwa interview haikuwa lazima sana

Lakini at the end nimekuja kujua kuwa lengo la interview kwa walimu na madoctor ni kuwapurura kwakuwa wapo wengi na sio kuchuja ubora kwahiyo kwa hapo nimefunga mjadala kuwa acha kipigwe tu hamna namna

Nmeshangaa baadhi ya kada za Afya mtu kapata 80% lakini kaachwa hapo ndipo ujue lengo ni kuwapurura sio kuangalia ufahamu wa mtu

Lakini bado nitaendelea kusema kuwa aina ya interview inayofanyika si kwa ajili ya kupima ubora bali ni kwa ajili ya kuwafyekelea mbali watumishi walio wengi wabaki wachache kwahiyo usije dhani aliyepata 20% ni mbumbumbu na aliyepata 90% ni intellect wewe utakuwa ndiyo mbumbumbu hasa
 
Mkuu nimependa umejibu kwa hoja na sio ushabiki, point zako zipo valid japo zingine umerudia zilezile nilizosema mimi

Mfano nimesema kwa kada ambazo zinafanana na ualimu kimazingira na mshahara pia nimeona kufanyiwa interview haikuwa lazima sana

Lakini at the end nimekuja kujua kuwa lengo la interview kwa walimu na madoctor ni kuwapurura kwakuwa wapo wengi na sio kuchuja ubora kwahiyo kwa hapo nimefunga mjadala kuwa acha kipigwe tu hamna namna

Nmeshangaa baadhi ya kada za Afya mtu kapata 80% lakini kaachwa hapo ndipo ujue lengo ni kuwapurura sio kuangalia ufahamu wa mtu

Lakini bado nitaendelea kusema kuwa aina ya interview inayofanyika si kwa ajili ya kupima ubora bali ni kwa ajili ya kuwafyekelea mbali watumishi walio wengi wabaki wachache kwahiyo usije dhani aliyepata 20% ni mbumbumbu na aliyepata 90% ni intellect wewe utakuwa ndiyo mbumbumbu hasa
Nimekupata mkuu, ila wote tunajua kuwa mitihani ndio kipimo cha uelewa wa mwanafunzi, kwahiyo sioni kama kuna haja ya kuwa na double standard katika kipimo hili

Na kuhusu kupata 80 na kuachwa hapo inaangaliwa cut off point, utumishi wao wana ratio ambayo ndio wanaitumia katika kupitisha watainiwa hatua 1 kwenda ingine

Utumishi hutumia ratio ya 1:3 so katika kila watu wa3 mmoja apate kazi, kupitia hiyo ratio ndio watajua kuwa tunataka watu wangapi waende hatua inayofata kulingana na ufaulu wa watainiwa ulivo, kwahiyo issue sio umepata 80 au umepata 90

Ni kweli umesema sio wote wanaofaulu mitihani ni best kuliko ambao hawajafaulu ila huwezi ukasema waliofaulu 50 wote ni wabovu kuliko 200 waliofeli

Mimi nachoona ni kuwa unaendeshwa na Hisia na sio uhalisia, ila usijali nawao watazoea tu hii Hali maana ni kitu cha kawaida kwenye Kada zingine zote washazoea wao ni kina nani walalamike kama watoto wa kike
 
Nimekupata mkuu, ila wote tunajua kuwa mitihani ndio kipimo cha uelewa wa mwanafunzi, kwahiyo sioni kama kuna haja ya kuwa na double standard katika kipimo hili

Na kuhusu kupata 80 na kuachwa hapo inaangaliwa cut off point, utumishi wao wana ratio ambayo ndio wanaitumia katika kupitisha watainiwa hatua 1 kwenda ingine

Utumishi hutumia ratio ya 1:3 so katika kila watu wa3 mmoja apate kazi, kupitia hiyo ratio ndio watajua kuwa tunataka watu wangapi waende hatua inayofata kulingana na ufaulu wa watainiwa ulivo, kwahiyo issue sio umepata 80 au umepata 90

Ni kweli umesema sio wote wanaofaulu mitihani ni best kuliko ambao hawajafaulu ila huwezi ukasema waliofaulu 50 wote ni wabovu kuliko 200 waliofeli

Mimi nachoona ni kuwa unaendeshwa na Hisia na sio uhalisia, ila usijali nawao watazoea tu hii Hali maana ni kitu cha kawaida kwenye Kada zingine zote washazoea wao ni kina nani walalamike kama watoto wa kike
Hahahha eti kama watoto wa kike,

Ni kweli mkuu acha watu wafanye usaili mwenye kupata apate mwenye kukosa akose

Mimi silalamikii usaili ila nalalamikia aina ya usaili ili kupata watu bora wangetumia summative assessment ingekuwa best ila kwakuwa inshu ni idadi tipo choice linafaa tu
 
Back
Top Bottom