Mlipuko mpya wa Virusi (HMPV) wazuka China, miaka 5 baada ya janga la COVID-19, Hospitali na sehemu za kuchomea maiti zazidiwa

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
China inakabiliana na mlipuko mpya wa virusi vya human metapneumovirus (HMPV), vinavyoenea kwa kasi katika majimbo ya kaskazini, hasa kwa watoto wenye umri chini ya miaka 14, ikiwa ni miaka mitano baada ya janga la Covid-19.

Ripoti na machapisho kwenye mitandao ya kijamii yanadokeza kuwa virusi hivyo vinasambaa kwa kasi huku wengine wakidai hospitali na sehemu za kuchomea maiti zimezidiwa.

HMPV husababisha dalili zinazofanana na mafua, huku nyingine zikiwa sawa na zile za Covid-19. Maafisa wa afya wanafuatilia kwa karibu hali hiyo wakati virusi hivyo vikiendelea kuenea.
Your browser is not able to display this video.

Dalili za HMPV, kama ilivyobainishwa na CDC, ni pamoja na: kikohozi na mafua makali au Pua iliyoziba, homa, maumivu ya koo, kupumua kwa shida na Uchovu wa mwili.

Your browser is not able to display this video.

Your browser is not able to display this video.

==

 
Na Hawa wapumbavu wamekataa kutoa data Wala za uviko 19 Wala kuruhusu WHO kufanya uchunguzi.

Juzi niliona kwenye world statistics kwamba mwaka huu wa 2025 Kuna mlipuko mwingine labda ndio huu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…