Mlipuko mpya wa Virusi (HMPV) wazuka China, miaka 5 baada ya janga la COVID-19, Hospitali na sehemu za kuchomea maiti zazidiwa

Mlipuko mpya wa Virusi (HMPV) wazuka China, miaka 5 baada ya janga la COVID-19, Hospitali na sehemu za kuchomea maiti zazidiwa

Sijui itakuaje huku maana yule aliyekuwa na ujasiri na maoni ya mbali hayupo.
 
Bendera ya Marekani
Tovuti rasmi CDC About Human Metapneumovirus.

Kuhusu Metapneumovirus ya Binadamu - HMPV​

Pointi muhimu​

  • Metapneumovirus ya binadamu (HMPV) inaweza kusababisha ugonjwa wa kupumua.
  • HMPV huenea kutoka kwa mtu hadi mtu au mazingira unayogusa hadi mtu.
  • Dalili ni pamoja na kikohozi, homa, msongamano wa pua, na shida ya kupumua.
  • Mtoa huduma wako wa afya anaweza kupima, hata hivyo, hakuna matibabu.
  • Hatua za kuzuia ni pamoja na kunawa mikono, kusafisha nyuso, na kukaa nyumbani wakati mgonjwa.

Muhtasari​

Metapneumovirus ya binadamu (HMPV) inaweza kusababisha ugonjwa kwenye mfumo wa binadamu wa juu yaani pua, koo na wa chini yaani mapafu wa kupumua kwa watu wa umri wote, hasa kati ya watoto wadogo, watu wazima wazee, na watu walio na kinga dhaifu. Iligunduliwa mwaka wa 2001, HMPV iko katika familia ya Pneumoviridae pamoja na virusi vya kupumua vya syncytial (RSV). Utumiaji mpana wa uchunguzi wa uchunguzi wa molekuli umeongeza utambuzi na ufahamu wa HMPV kama sababu muhimu ya maambukizi ya mfumo wa binadamu wa juu na ya chini wa kupumua.

Maoni ya Mtaalam wa CDC na Medscape​

Maoni ya Mtaalam wa CDC na Medscape

Metapneumovirus ya Binadamu: Kawaida Bado Haijatambuliwa
Muda wa Kuendesha: [dakika 3:42]
Ilitolewa 8/15/2016

Dalili​

Dalili zinazohusishwa kwa kawaida na HMPV ni pamoja na kikohozi, homa, shida katika mfumo wa pua, na shida ya kupumua. Dalili za kimatibabu za maambukizo ya HMPV zinaweza kujitokeza kama kikohozi kikali (mkamba /bronchitis) au nimonia na ni sawa na virusi vingine vinavyosababisha maambukizo ya Mfumo wa njia ya juu na ya chini ya kupumua. Kipindi cha kabla ya dalili (incubation) kinakadiriwa ni siku 3 hadi 6, na muda wa wastani wa ugonjwa unaweza kutofautiana kulingana na ukali lakini ni sawa na magonjwa mengine ya kupumua yanayosababishwa na virusi.

Jinsi inavyoenea​

HMPV ina uwezekano mkubwa wa kuenea kutoka kwa mtu aliyeambukizwa hadi kwa wengine kupitia
  • majimaji / matone (secretions) kutokana na kukohoa na kupiga chafya
  • Kusalimiana kwa karibu kama vile kushikana au kupeana mikono
  • kugusa vitu au eneo lolote la mazingira ambazo zina virusi juu yake kisha kugusa mdomo, pua, au macho
Nchini Marekani, HMPV huzunguka katika misimu tofauti ya kila mwaka. Mzunguko wa HMPV huanza majira ya baridi na hudumu hadi au kupitia majira ya kuchipua.

Ufuatiliaji na Msimu​

Data ya uchunguzi kutoka kwa CDC ya Mfumo wa Kitaifa wa Ufuatiliaji wa Kupumua na Virusi vya Enteric (NREVSS) inaonyesha HMPV kuwa inapamba moto zaidi wakati wa majira ya baridi kali na masika katika hali ya hewa ya baridi. HMPV, RSV , na mafua yanaweza kuzunguka kwa wakati mmoja wakati wa msimu wa virusi vya kupumua.

Kuzuia​

Wagonjwa wako wanaweza kusaidia kuzuia kuenea kwa HMPV na virusi vingine vya kupumua kwa kufuata hatua hizi:
  • Nawa mikono mara kwa mara kwa sabuni na maji kwa angalau sekunde 20 (angalia Mikono Safi ya CDC Okoa Maisha! ).
  • Epuka kugusa macho yao, pua, au mdomo kwa mikono ambayo haijaoshwa.
  • Epuka mawasiliano ya karibu na watu ambao ni wagonjwa.
Wagonjwa ambao wana dalili za homa wanapaswa
  • kufunika midomo na pua wakati wa kukohoa na kupiga chafya
  • osha mikono yao mara kwa mara na kwa usahihi (kwa sabuni na maji kwa angalau sekunde 20)
  • epuka kushiriki vikombe vyao na vyombo vya kulia chakula na wengine
  • epuka kumbusu wengine
  • kukaa nyumbani wakati wao ni wagonjwa
Zaidi ya hayo, kusafisha vifaa ambavyo zinazoweza kuwa na vijidudu (kama vile vitasa vya milango na midoli ya kuchezea pamoja) kunaweza kusaidia kukomesha kuenea kwa HMPV.
Katika mipangilio ya huduma za afya, watoa huduma za afya wanapaswa kufuata Mwongozo wa 2007 wa CDC wa Tahadhari za Kutengwa: Kuzuia Usambazaji wa Mawakala wa Kuambukiza katika Mipangilio ya Huduma ya Afya .

Uchunguzi na utambuzi​

Kwa kuwa HMPV ni virusi vya upumuaji vilivyotambuliwa hivi majuzi, wataalamu wa afya wanaweza wasifikirie au kupima HMPV mara kwa mara. Hata hivyo, wataalamu wa afya wanapaswa kuzingatia upimaji wa HMPV wakati wa majira ya baridi na masika, hasa wakati HMPV inapozunguka kwa kawaida.
Kuambukizwa na HMPV kunaweza kuthibitishwa kwa kawaida na
  • kugundua moja kwa moja ya jenomu ya virusi kwa mtihani wa kukuza asidi ya nucleic (NAAT), na
  • kugundua moja kwa moja kwa antijeni za virusi katika sampuli za makohozi, majimaji kutoka mfumo wa kupumua kwa kutumia immunofluorescence au immunoassay ya enzyme.

Matibabu​

Kwa sasa, hakuna tiba mahususi ya kizuia virusi kutibu HMPV na hakuna chanjo ya kuzuia HMPV. Huduma ya matibabu inaunga mkono.



Metapneumovirus ya binadamu

Toa maelezo kuhusu metapneumovirus ya binadamu, jinsi inavyoenea, dalili zake, kinga na njia za matibabu

Jisajili kwa Barua pepe
Wasiliana NasiKuhusu CDCSeraLughaHifadhi


HHS.gov USA.gov
 
China wana mpango wa kupunguza idadi ya watu wao nini? Vitu vibaya hasa magonjwa ya mlipuko mengi huanzia China.
 
China inakabiliana na mlipuko mpya wa virusi vya human metapneumovirus (HMPV), vinavyoenea kwa kasi katika majimbo ya kaskazini, hasa kwa watoto wenye umri chini ya miaka 14, ikiwa ni miaka mitano baada ya janga la Covid-19.
View attachment 3191486
Ripoti na machapisho kwenye mitandao ya kijamii yanadokeza kuwa virusi hivyo vinasambaa kwa kasi huku wengine wakidai hospitali na sehemu za kuchomea maiti zimezidiwa.
View attachment 3191487
HMPV husababisha dalili zinazofanana na mafua, huku nyingine zikiwa sawa na zile za Covid-19. Maafisa wa afya wanafuatilia kwa karibu hali hiyo wakati virusi hivyo vikiendelea kuenea.
View attachment 3191488
Dalili za HMPV, kama ilivyobainishwa na CDC, ni pamoja na: kikohozi na mafua makali au Pua iliyoziba, homa, maumivu ya koo, kupumua kwa shida na Uchovu wa mwili.
View attachment 3191491
View attachment 3191489
View attachment 3191490
==

View attachment 3191492View attachment 3191493
Nimeona manabii wengi wametabili hili janga na kweli limetokea
 
Jaribio lingine tena hili
Yaani biological weapon
Mchina hataki utani kila wakati anaanza na kwake halafu inasambaa
Sisi masikini ya Mungu hatuna la kufanya ni maombi kwa sana na Nyungu kama kawa
 
alafu bado unaendelea kuandika jumbe za kawaida kwa maandishi makubwa nani kakufundisha uandishi huo ? ukiona nipo kwenye mada serious alafu wewe unakuja kuleta utani kwaajili ya kupata sifa unaonesha uwezo wako ulivyo mdogo mda mwengine naweza kukosea uandishi kwa bahati mbaya hili ni sawa lakini tusilete masihara kwenye vitu serious kwaajili ya kupata sifa nazani umenielewa.
 
Huu mwaka huu Sina Imani nao kabisa, hawa jamaa wenye dunia Yao huenda Wana mipango Yao mikubwa ambayo ita-change systems dunia nzima ktk nyanja mbalimbali.

Soon tutaanza kushuhudia mengi, tuombe tu viongozi wetu wawe na utu kwa raia wao, waache ubinafsi+roho mbaya kupitisha Kila waambiwacho na hao mabwana zao wanaoicontrol dunia.

Dunia si salama kabisa kwa maisha ya viumbehai
 
China inakabiliana na mlipuko mpya wa virusi vya human metapneumovirus (HMPV), vinavyoenea kwa kasi katika majimbo ya kaskazini, hasa kwa watoto wenye umri chini ya miaka 14, ikiwa ni miaka mitano baada ya janga la Covid-19.
View attachment 3191486
Ripoti na machapisho kwenye mitandao ya kijamii yanadokeza kuwa virusi hivyo vinasambaa kwa kasi huku wengine wakidai hospitali na sehemu za kuchomea maiti zimezidiwa.
View attachment 3191487
HMPV husababisha dalili zinazofanana na mafua, huku nyingine zikiwa sawa na zile za Covid-19. Maafisa wa afya wanafuatilia kwa karibu hali hiyo wakati virusi hivyo vikiendelea kuenea.
View attachment 3191488
Dalili za HMPV, kama ilivyobainishwa na CDC, ni pamoja na: kikohozi na mafua makali au Pua iliyoziba, homa, maumivu ya koo, kupumua kwa shida na Uchovu wa mwili.
View attachment 3191491
View attachment 3191489
View attachment 3191490
==

View attachment 3191492View attachment 3191493
Duh!! Tena..
 
China wana mpango wa kupunguza idadi ya watu wao nini? Vitu vibaya hasa magonjwa ya mlipuko mengi huanzia China.
Sio kupunguza watu wao, Kuna wababe wengi nyuma ya china, kwa wasiojua mambo Iko hivi, USA,Russia,China na other big Players tunaowaona wanapingana kumbe nyuma ya keyboard hawa ni marafiki, na wakitaka jambo lao litimie, watalitimiza kivyovyote vile iwe kumwaga damu za raia wao wenyewe au hata machafuko nje ya mipaka yao, ilimladi tu mipango Yao itimie.

Huwa tunawaambia watu asilimia kubwa ya hayo magonjwa yanayopewa airtime ni man made kwa madhumuni ya kucontrol uhuru wa watu, kupitisha agenda ovu mfano upitishwaji wa Sheria kandamizi, upandizwaji wa maradhi kwa watu kwa mgongo wa chanjo ambazo zimelengwa si kuzuia magonjwa bali kuunda matatizo mapya(ugumba+utasa+vichocheo vya ushoga).
Bila kusahau kutengeneza utegemezi kwa baadhi ya mataifa kiuchumi kupitia control ya madawa ya magonjwa yanayosemekana hayana dawa/tiba au dawa zake hazipatikani kirahisi
 
Dsm joto Kali nyuzi 40 virusi vya mafua havina hivyo havina nguvu
Afrika tunapona sana na majanga yao sababu hali ya hewa inatupendelea, Kuna namna majanga mengi sana wanayatabiri lkn hayatokei kama watakavyo sababu kuu ni kwamba Afrika ndiko chanzo cha uhai wa dunia, ni ngumu maangamizi ya viumbehai yatokee Afrika kwa Ukubwa, japo kunakua na effects ambazo si sawa na continents zingine.
 
China inakabiliana na mlipuko mpya wa virusi vya human metapneumovirus (HMPV), vinavyoenea kwa kasi katika majimbo ya kaskazini, hasa kwa watoto wenye umri chini ya miaka 14, ikiwa ni miaka mitano baada ya janga la Covid-19.
View attachment 3191486
Ripoti na machapisho kwenye mitandao ya kijamii yanadokeza kuwa virusi hivyo vinasambaa kwa kasi huku wengine wakidai hospitali na sehemu za kuchomea maiti zimezidiwa.
View attachment 3191487
HMPV husababisha dalili zinazofanana na mafua, huku nyingine zikiwa sawa na zile za Covid-19. Maafisa wa afya wanafuatilia kwa karibu hali hiyo wakati virusi hivyo vikiendelea kuenea.
View attachment 3191488
Dalili za HMPV, kama ilivyobainishwa na CDC, ni pamoja na: kikohozi na mafua makali au Pua iliyoziba, homa, maumivu ya koo, kupumua kwa shida na Uchovu wa mwili.
View attachment 3191491
View attachment 3191489
View attachment 3191490
==

View attachment 3191492View attachment 3191493
Hao jamaa wanataka kuwaua watu wa afrika hao Moja HAPO
 
Jaribio lingine tena hili
Yaani biological weapon
Mchina hataki utani kila wakati anaanza na kwake halafu inasambaa
Sisi masikini ya Mungu hatuna la kufanya ni maombi kwa sana na Nyungu kama kawa
Katika vitu ambavyo hutakiwi kufanya ikiwa una shida ya kupumua ni kujifukiza utapotea
 
Jaribio lingine tena hili
Yaani biological weapon
Mchina hataki utani kila wakati anaanza na kwake halafu inasambaa
Sisi masikini ya Mungu hatuna la kufanya ni maombi kwa sana na Nyungu kama kawa
hakuna silaha itakayoshinda juu yetu
 
Huu mwaka huu Sina Imani nao kabisa, hawa jamaa wenye dunia Yao huenda Wana mipango Yao mikubwa ambayo ita-change systems dunia nzima ktk nyanja mbalimbali.

Soon tutaanza kushuhudia mengi, tuombe tu viongozi wetu wawe na utu kwa raia wao, waache ubinafsi+roho mbaya kupitisha Kila waambiwacho na hao mabwana zao wanaoicontrol dunia.

Dunia si salama kabisa kwa maisha ya viumbehai
ila kuna washenzi wanaiharibu dunia kwa maslahi yao
 
Nakumbuka The bold aliwahi kuleta Post inayohusiana na haya magonjwa yanavyotokea, Yote ni ya kutengeneza Maabara.
 
Back
Top Bottom