Mmoja kati ya walioiba vitu kwenye ajali iliyoua watu 17 Tanga ajinyonga

Mmoja kati ya walioiba vitu kwenye ajali iliyoua watu 17 Tanga ajinyonga

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Mtu mmoja kati ya watu 8 waliokamatwa, wakituhumiwa kuiba mali za waliofariki katika ajali iliyotokea Korogwe mkoani Tanga, ikihusisha gari la mizigo aina ya Fuso na gari la abiria aina ya Coaster, lililokuwa likisafirisha mwili kwa ajili ya maziko wilayani Rombo na kusababisha vifo vya watu 20, amekutwa amejinyonga katika mahabusu ya polisi iliyopo Jijini Tanga.

Mkuu wa Mkoa huo, Omari Mgumba ,amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, huku akibainisha kuwa, mtuhumiwa huyo ni yule ambaye wakati wa upekuzi nyumbani kwake alikutwa na baadhi ya vitu ikiwemo simu, begi na nguo zinazoshukiwa kuibiwa kwenye eneo la ajali vikiwa na damu.

ITV
 
Hii habari ya watuhumiwa kujinyonga wakiwa mahabusu inaleta ukakasi sana.
Polisi lazima wawajibike mtuhumiwa anajinyongaje akiwa mikononi mwao?
Huyu jamaa na huko mahabusu alikuwa pekeyake?
 
Mtu mmoja kati ya watu 8 waliokamatwa, wakituhumiwa kuiba mali za waliofariki katika ajali iliyotokea Korogwe mkoani Tanga, ikihusisha gari la mizigo aina ya Fuso na gari la abiria aina ya Coaster, lililokuwa likisafirisha mwili kwa ajili ya maziko wilayani Rombo na kusababisha vifo vya watu 20, amekutwa amejinyonga katika mahabusu ya polisi iliyopo Jijini Tanga.
.
Mkuu wa Mkoa huo, Omari Mgumba ,amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, huku akibainisha kuwa, mtuhumiwa huyo ni yule ambaye wakati wa upekuzi nyumbani kwake alikutwa na baadhi ya vitu ikiwemo simu, begi na nguo zinazoshukiwa kuibiwa kwenye eneo la ajali vikiwa na damu.

ITV
Laaana
 
Usipende kuhukumu ujui sababu ya kujinyoga ni ipi.imagine ujui lile wala lile jumba bovu limekuangukia bila kufanya au mambo mengine ambayo mimi na wewe tufahamu.
Angekuwa ni wa haki angesubiri makama itende haki yake, swala la kuwekwa mahabusu bila kuhusika linaweza tokea wakati wowote na kwa yeyote.

Mimi kuna mahali palitokea uwizi usiku na kwa kuwa niliwahi kufunga camera nikaitwa nikasaidie kuweka event kwenye fdd ili ipelekwe police.

Wahusika wa hilo eneo walikuwa ubalozini nje ya nchi na ndio walionipigia maana wkt nafunga wao ndio waliniita na niliwapa uwezo wa kuangalia hata huko walipo.

Sasa aliyekuwa pale home sijui alihusika nikajikuta naingizwa lupango ila hakujua mimi nimechukua data zangu na police wamechukua.

police nilipoona wanazingua na wale kule nje hawapati mawasiliano na mimi nikaomba kesi iende mahakamani maana pale sina imani napo na ikawa hivyo ila kwa mbinde.

Anyway story ni ndefu nilitoka kwa dhamana ila yule ndugu yao kesi ikamgemkia yeye.

Nilitaka kusema kama una haki hakuna haja ya kuogopa na kufikiria kufanya maamuzi ya kujiua, ni imani yangu jamaa alijua mvua ya miaka fulani inamfikia kwa kuwa hana pa kuchomokea kutokana na ushahidi.

Mwisho kama haki ni yako pambana hadi mwisho.
 
Angekuwa ni wa haki angesubiri makama itende haki yake, swala la kuwekwa mahabusu bila kuhusika linaweza tokea wakati wowote na kwa yeyote.

Mimi kuna mahali palitokea uwizi usiku na kwa kuwa niliwahi kufunga camera nikaitwa nikasaidie kuweka event kwenye fdd ili ipelekwe police.

Wahusika wa hilo eneo walikuwa ubalozini nje ya nchi na ndio walionipigia maana wkt nafunga wao ndio waliniita na niliwapa uwezo wa kuangalia hata huko walipo.

Sasa aliyekuwa pale home sijui alihusika nikajikuta naingizwa lupango ila hakujua mimi nimechukua data zangu na police wamechukua.

police nilipoona wanazingua na wale kule nje hawapati mawasiliano na mimi nikaomba kesi iende mahakamani maana pale sina imani napo na ikawa hivyo ila kwa mbinde.

Anyway story ni ndefu nilitoka kwa dhamana ila yule ndugu yao kesi ikamgemkia yeye.

Nilitaka kusema kama una haki hakuna haja ya kuogopa na kufikiria kufanya maamuzi ya kujiua, ni imani yangu jamaa alijua mvua ya miaka fulani inamfikia kwa kuwa hana pa kuchomokea kutokana na ushahidi.

Mwisho kama haki ni yako pambana hadi mwisho.
Unajua kuna msemo fulani "ukiwa mshangiliaji kwenye mpira utajiona wewe ndio unafahamu wachezaji wanavo cheza na kocha ni mjinga"

Subiri ikifika zamu yako kama ni kweli au sikweli ndio utajua kuimba Andhaa kanoon.

Mengine yasikie wala usiwe kama ulikuwepo
Andha_Kanoon%2C_1983_film.jpg
 
Unajua kuna msemo fulani "ukiwa mshangiliaji kwenye mpira utajiona wewe ndio unafahamu wachezaji wanavo cheza na kocha ni mjinga"

Subiri ikifika zamu yako kama ni kweli au sikweli ndio utajua kuimba Andhaa kanoon.

Mengine yasikie wala usiwe kama ulikuwepoView attachment 2527842
Shida kubwa inakuja uwezo wa kutambua kuwa hili lililotokea sina pa kutokea na hasa kwetu sisi wa ufahamu fulani, (Hapa nazungumzia elimu ya kupambanua mambo).

Tukiwa vizuri hapo haya mambo yatapungua ila sio kuisha.
 
Back
Top Bottom