Januari 11, 2019, serikali ilifanya uhamisho mkubwa wa kushitukiza kwa wahadhiri na watumishi wandamizi katika Chuo Kikuu cha Serikali cha Dodoma-UDOM. Waliohamishwa walikuwa 11, lakini wote walikuwa Waislamu: Dk. Maryam Khamis (Director of Graduate Studies), Dk. Ibun Kombo (Political Science), Dk. Mwinyikombo Amir (Mwalimu wa Udaktari wa Binadamu), Dk. Yusuf Kambuga (College of Education), Dk. Masoud Masoud (Informatics) , Bw. Subira Sawasawa (Mkurugenzi Mkuu Rasilimali Watu), Bw. Mohamed Mwandege (Bursar/Mhasibu Mkuu), Bi. Aziza Gendo (Seniour Estate Oficer), Bw. Simba Omary (Senior Supplies Oficer), Bw. Wema Mbegu (Legal Oficer), Bw. Khamis Mkanachi (Mwalimu wa Idara ya Historia).
Barua zao za uhamisho hazikuonesha makosa katika utendaji wao wa kazi au uongozi. Pamoja na kutokuwa wakosaji, uhamisho wao uliambatana na udhalilishaji mkubwa, kunyimwa haki stahiki za uhamisho, kuhamishiwa katika nafasi za chini kinyume na hadhi zao.
Baada ya uhamisho huo, Serikali ilifanya uteuzi mwingine katika chuo hicho hicho cha Serikali. Katika uteuzi huo walioteuliwa walikuwa 11, wote Wakristo: Prof. Leonard James Mselle, Prof. Adam B. Swebe Mwakalobo, Prof. Julius William Nyahongo, Prof. Justin Ntalikwa, Prof. Frowing Paul Nyoni, Prof. Odass Bilame, Prof. Ainory Piter Gasese, Dkt. Victor George Mareale, Dkt. Alex Shayo, Dkt. Calvin Swai, Dkt. Augustine Mwakipesile.
Kuhamisha wahadhiri 11, katika Chuo Kikuu si jambo dogo. Vilevile kuhamisha Wahadhiri 11, wa dini moja (Waislamu) katika Chuo Kikuu ukaingiza wahadhiri 11 wa dini moja (Wakristo), na hao Waislamu 11, baadhi yao ukawatoa kabisa katika mfumo wa elimu kwa kuwapeleka sekta nyingine na zisizo lingana na hadhi zao si jambo dogo. Wala si hatua ya kitaalamu ya kuboresha mfumo wa Elimu wa Taifa. Na wala si hatua ya kijinga bali ya werevu uliofurutu ada dhidi ya maslahi ya Taifa. Hatuwa hiyo ni salamu nzito kwa jamii yao na Taifa kwa ujumla. (Ndio maana katika maoni yetu ya Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tulipendekeza Katiba Mpya imtambuwa Mwenyezi Mungu na Dini liwe suala rasmi na la wazi katika uendeshaji wa nchi).
Uadilifu II
Serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani Mwaka (2015), Rais alifanya uteuzi wa Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakurugenzi mbalimbali. Uteuzi wake ulikuwa kama ifuatavyo:
Mawaziri na Manaibu: 30.
Waislamu 10, sawa na asilimia 33%.
Wakristo 20, sawa na asilimia 67%.
Makatibu Wakuu na Manaibu: 50.
Waislamu 10, sawa na asilimia 20%.
Wakristo 40, sawa na asilimia 80%.
Wakuu wa Mikoa na Wilaya: 166.
Waislamu 41, sawa na asilimia 25%.
Wakristo 125, sawa na asilimia 75%.
Makatibu Tawala wa Mikoa na Wilaya: 163.
Waislamu 24, sawa na asilimia 15%.
Wakristo 139, sawa na asilimia 85%.
Wakurugenzi mbalimbali: 249.
Waislamu 45, sawa na asilimia 18%.
Wakristo 204, sawa na asilimia 82%.
Manaibu Kamishna wa Polisi: 25.
Waislamu 5, sawa na asilimia 20%.
Wakristo 20, sawa na asilimia 80%.
Makamishna Wasaidizi Waandamizi wa Polisi: 33
Waislamu 7, sawa na asilimia 21%.
Wakristo 26, sawa na asilimia 79%.
Jumla Kuu ya Uteuzi:
Waislamu asilimia 20%.
Wakristo asilimia 80%.
Uteuzi huo umekuwa kama Sera kwa teuzi zinazoendelea ndani ya miaka yote mitano. Vilevile kama Mwongozo kwa wateule wenye mamlaka ya kuteuwa. Mwelekeo huo unakinzana na Katiba ya nchi ibara ya 13(4)(5), inayokataza ubaguzi wa aina zote. Kwa hakika Taifa halihitaji kiongozi wa nchi akiwa Muislamu basi ateuwe idadi kubwa ya Waislamu wenzake katika nafasi mbalimbali za uongozi wa nchi au akiwa Mkristo atumie uongozi wake kuteua idadi kubwa ya Wakristo wenzake katika uongozi nchini. Au akiwa Mzanaki ateuwe idadi kubwa ya Wazanaki wenzake katika nafasi mbalimbali za uongozi na mfano wa hayo.
Kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, Rais ana mamlaka makubwa kuliko chombo chochote. Baraza la Mawaziri jukumu lake ni kumshauri tu na Katiba inampa uhuru wa kufuata au kutofuata ushauri wa chombo hicho au mtu yoyote. Mamlaka ya Rais pia yako juu kuliko ya Bunge. Rais anateuwa sehemu ya wabunge na ana mamlaka ya kulivunja Bunge. Rais pia anateuwa Majaji wa Mahakama na watendaji wengine wa kitaifa. Kwa kifupi Rais wa Tanzania ndiye muhandisi mkuu na mwenye kutengeneza shakhsia (Personality) ya Taifa.
Katika jukumu hilo la kutengeneza shakhsia ya Taifa, miongoni mwa watumishi wa umma 1269, wanaoteuliwa na mamlaka ya Rais ambao ni pamoja na: Waziri Mkuu, Jaji Mkuu, Mawaziri na Manaibu, Majaji, Mkuu wa Majeshi, Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Mabalozi wa Nchi za Nje, Makatibu Wakuu na Manaibu Katibu Wakuu wa Wizara, Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala Wilaya (DAS), Makatibu Tawala Mikoa (RAS), Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Majiji, Manispaa, na Wilaya, Wakuu wa Bodi na Tume mbalimbali, Makamishna, Wakuu wa Mashirika ya Umma, Wakuu wa Vyuo Vikuu na kadhalika, asilimia 80 ya uteuzi huo unafanyika kwa Watanzania wa imani moja.
Na hao wateuliwa na wao wana mamlaka ya uteuzi katika maeneo yao au kusimamia masuala ya uteuzi, ajira, na kufanya maamuzi mbalimbali ya utendaji na uendeshaji kwa niaba ya Taifa. Wakitaka na wao wanaweza kufanya uteuzi ule wa asilimia 80 ya watu wa imani moja (au kabila moja).
Lingine la kuzingatiwa, uteuzi huo unawapa wateule hao Mamlaka, uwezo wa kufanya Maamuzi na Utawala. Lingine kubwa ni kwamba uteuzi huo unatoa fursa za mapato, maana yake ni kuwa, zaidi ya asilimia 80 ya pato la Taifa linalohudumia malipo na stahiki za watumishi wa umma linakwenda kwa kundi moja la kijamii na kuliacha kundi jingine.
Tunachotaka ni sera za Uwiano sahihi. Katiba za Kanya na ya Nigeria ni mfano mzuri wa dhana hii ya Uwiano sahihi. Ukurasa wa 75, Sura ya 9, sehemu ya kwanza, ibara ya 130 (1)(2), na uk 151 Sura 15, ibara ya 250 (4), ya Katiba ya Kenya inaelekeza, nafasi za Uteuzi za wafanya Maamuzi (Executives) na nafasi nyengine nyeti kama vile Mawaziri na Manaibu Waziri, Makatibu na Manaibu Katibu, Makamishna na Wakurugenzi, kuwepo Uwiano ulio Sawa na Ujumuishi (yaani pamoja na kuangalia weledi, uzoefu na uadilifu, lakin pia kuwepo na uwiano wa watu kwa kuzingatia walemavu, rangi, jinsia, Dini, makabila na mfano wa hayo) .
Katiba hiyo pia uk 143, sura ya 14, sehemu I, ibara ya 238 2(d), na uk 146, sura ya 14, sehemu ya II, ibara ya 241 (4), uk 149, sehemu ya IV, ibara ya 246 (4) inaelekeza mihimili ya Serikali ikiwa ni pamoja na Majaji, Majeshi yote ya Ulinzi na Usalama kama: Jeshi la Wananchi, Jeshi la Polisi, teuzi na ajira pamoja na kuangalia weledi, uzoefu na uadilifu kuwepo uwiano kama tulivyoona katika vifungu vya hapo nyuma.
Halikadhalika Katiba ya Nigeria, uk 8 Sura 2, ibara ya 4, maudhui yake yanaelekeza, Serikali Kuu, Serikali za Majimbo, Halmashauri za Miji, Mawakala (wanaofanya kazi kwa niaba ya Serikali, Vyama vya siasa) ni sharti ajira zao kuzingatia suala la uwiano wa mahala husika na Ujumuishi wa makabila na Dini.
Jambo muhimu ni mabadiliko ya fikra kwa viongozi wetu. Kama Isiwe Rais akiwa Muislamu ateuwe Waislamu wengi kwenye serikali yake, au akiwa Mkristo ateuwe Wakristo wengi kwenye serikali yake. Hakuna sababu yoyote ya msingi ya uteuzi huo.
Bismillahir Rahmanir Rahiim SHURA YA MAIMAMU TANZANIA WARAKA [MWONGOZO] UCHAGUZI MKUU WA TAIFA OKTOBA 2020 TANZANIA Umetolewa leo Tarehe 09. 07. 2020. UTANGULIZI Ugonjwa wa Korona – COVID-19 Sote Tunafahamu kuwa nchini mwetu na Dunia kwa ujumla kumekuwepo na taharuki kubwa ya Ugonjwa wa...