Mnaoamini kuwa uchawi upo mnatumia vigezo gani?

Mnaoamini kuwa uchawi upo mnatumia vigezo gani?

Katika miaka niliyo nayo mpaka sasa sijawahi kukubali kuwa eti kuna uchawi sijui mtu anaweza kuloga sijiui mambo yako yasiende.

Kama kweli uchawi upo kwanini hao wachawi wasiende benki wakaloga wakachukua pesa.

Kama kuna mtu humu ndani alishawahi kulogwa njoo utupe mrejesho ilikuwaje.

Pia, kama kuna mtu anajiamini anaweza kuniloga njoo uniloge we taja unachotaka kutoka kwangu nitakupa we niloge kama kweli unaweza😂😂

Mwisho hakuna uchawi ni dhana za kufikilika tu.
Nipe majina yako matatu na Majina ya mama yako , pia nitaomba nikuone mwonekano wako .
 
Wewe una akili kuliko mtume paulo aliyemkemea mchawi hadharani?
Au wewe una akili kuliko Musa aliyepambana na wachawi mbele ya Farao? Au wewe una akili kuliko Darius mfalme wa Babeli aliyekua akiwatumia waganga na wachawi kuwapumbaza wengine ili aendelee kutawala au wewe una akili kuliko Wafalme wa ulaya walioamua kuagiza wachawi wote kwenye tawala zao wakamatwe na kuuawa (season of witch)
Ungejua hao wanaokutawala au watu Maarufu unaowasifia mitandaoni wanatumia nini usingeandika uzi kama huu.

Acheni kuwapumbaza wengine ili muwatese wasitafute solution ya matatizo yao
UCHAWI UPO.


Acha ujinga wewe. Biblia ni kitabu kilichoandikwa na watu kama mimi na wewe. Biblia ni kitabu chenye makosa na uongo mwingi sana.

Mfano Biblia inakuambia eva aliongea na nyoka. Je ni kweli nyoka huwa anaongea ?
 
Maombi mwombe Mungu kweli uchawi upo na tena wabaya na wengi wamekufunga hujui utaanzia wapi nimechelewa kila kitu kisa hao wachawi sasa weka maombi uwe nania yakuwa nikiwa na yesu yote naweza kwa anitiaye nguvu
 
Unataka kumuharibia biashara Tapeli mwamposa
 
Huwezi kujifanya mzungu wakati ni mweusi huu ndio upumbavu wa kuabudu elimu za kuletwa na wazungu ..
Hakuna hoja yeyote uliyoandika hapa.

Kinachokudrive wewe, na hilo li avatar lako la Ayatola wa Iran ni chuki tu dhidi ya wazungu.

Kuna tija gani wewe kujifanya muarabu wakati ni mbongo tu, kwa nini unaabudu elimu za waarabu na dini zao hizo?
 
Katika miaka niliyo nayo mpaka sasa sijawahi kukubali kuwa eti kuna uchawi sijui mtu anaweza kuloga sijiui mambo yako yasiende.

Kama kweli uchawi upo kwanini hao wachawi wasiende benki wakaloga wakachukua pesa.

Kama kuna mtu humu ndani alishawahi kulogwa njoo utupe mrejesho ilikuwaje.

Pia, kama kuna mtu anajiamini anaweza kuniloga njoo uniloge we taja unachotaka kutoka kwangu nitakupa we niloge kama kweli unaweza[emoji23][emoji23]

Mwisho hakuna uchawi ni dhana za kufikilika tu.

Biblia haiwezi kuandika kitu ambacho hakipo.

Vitabu vya dini vimetaja uchawi mara nyingi sana
 
sijawahi kukubali kuwa eti kuna uchawi
Uchawi upo au haupo??

Kuna kesi ilitokea hapa Zanzibar, jamaa wakaenda kwa mtaalamu ili awasaidie.Mtaalamu akasema aletwe ngamia!

Mtaalamu akaanza kumsomea yule ngamia, ngamia akaanza kuzama chini ya ardhi kisha akapotea kabisa! Namaanisha alizama na kupotea.Mimi ni shuhuda mwenyewe!

Unakumbuka mkasa wa nyumba kuzama yenyewe hapa Zanzibar?? Unaifahamu ardhi ya Zanzibar?? Imejaa miamba, lakini nyumba ilizama!

Hivi visa ni maarufu huku Zanzibar! Ni uchawi au miujiza??Utajua mwenyewe!

Hii dunia ina mengi ambayo mimi na wewe hatuyafahamu na hatuwezi kuyafahamu mpaka tunakufa. Elimu ni bahari.

Ukipata kishahada chako unajihisi kama unaifahamu dunia, kumbe ni ushamba, ulimbukeni, kiburi, majivuno, mhemko, papara, dharau n.k ndivyo vimekutawala!

Nb: Toa elimu kuhusu huyo ngamia kuzama ardhini au nyumba kuzama kwenye miamba wakati wa kiangazi!Kwa taarifa yako wataalamu walikuja na hawakupata majibu.Ebu wewe tueleze ni kitu gani hiki!

Wahenga wenzangu watakuwa wanakumbuka kuhusu hii nyumba kuzama kwani ilitikisa vyombo vya habari!
 
Mleta mada huo niutoto unaleta.
Kutokuamini kwamba kitu flani hakionekani sio conclusion kwamba kitu hicho hakipo.
Harafu hiyo nitafiti unafanya kama nitafiti weka muda wako namali pia kuhakikishia tafiti yako inapata majibu sahihi.
Kama unacho chakutoa sh: laki2 tafuta hapa mashahidi watatu unao waamini wachukue namba tuwe tunawasiliana harafu upigwe kitu uamke macho yamepigwa ukungu yasione kabisa chochote wewe sasa ndio uwe shahidi kwahao mashahidi wako3 wewe ulete uzi waushahidi humu,na wao walete uzi wa ushahidi humo.
Nasio kuleta habari zako za utoto unadhani nguvu hasi inasafilishwa tuu kirahis yani kama unavyo dhani wewe kwamba nilogeni sasa.
Kama upo tayari haswa kwatafiti yako hiyo chukua namba hapo kwenye picha ya wasifu kisha njoo WhatsApp ntakuambia unitumie details zako muhimu naufanye malipo yahiko kiasi vitu vikanunuliwe uone kama wiki itaisha bila kufaulu mtihani wako.
 
Mleta mada huo niutoto unaleta.
Kutokuamini kwamba kitu flani hakionekani sio conclusion kwamba kitu hicho hakipo.
Harafu hiyo nitafiti unafanya kama nitafiti weka muda wako namali pia kuhakikishia tafiti yako inapata majibu sahihi.
Kama unacho chakutoa sh: laki2 tafuta hapa mashahidi watatu unao waamini wachukue namba tuwe tunawasiliana harafu upigwe kitu uamke macho yamepigwa ukungu yasione kabisa chochote wewe sasa ndio uwe shahidi kwahao mashahidi wako3 wewe ulete uzi waushahidi humu,na wao walete uzi wa ushahidi humo.
Nasio kuleta habari zako za utoto unadhani nguvu hasi inasafilishwa tuu kirahis yani kama unavyo dhani wewe kwamba nilogeni sasa.
Kama upo tayari haswa kwatafiti yako hiyo chukua namba hapo kwenye picha ya wasifu kisha njoo WhatsApp ntakuambia unitumie details zako muhimu naufanye malipo yahiko kiasi vitu vikanunuliwe uone kama wiki itaisha bila kufaulu mtihani wako.
😂😂😂😂 yaani kuniloga nitoe na hela yangu kudadeki
 
Hakuna hoja yeyote uliyoandika hapa.

Kinachokudrive wewe, na hilo li avatar lako la Ayatola wa Iran ni chuki tu dhidi ya wazungu.

Kuna tija gani wewe kujifanya muarabu wakati ni mbongo tu, kwa nini unaabudu elimu za waarabu na dini zao hizo?
Rudi kweny Uafrica elimu ya kuletwa tu na majahazi
 
Back
Top Bottom