Mnaobeza mafanikio ya Awamu ya Sita, zungukeni Tanzania muone mafanikio ya Serikali ya Rais Samia katika utekelezaji wa miundombinu

Mnaobeza mafanikio ya Awamu ya Sita, zungukeni Tanzania muone mafanikio ya Serikali ya Rais Samia katika utekelezaji wa miundombinu

Kuna watu kazi yao wamekuwa ni kupinga na kubeza mafanikio ya Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Samia Suluh Hassan, yawezekana wanatumia uhuru wao wa kutoa maoni kikatiba au wameamua kupinga kwa sababu kazi yao ni kupinga bila kutambua hatuna Tanzania nyingine zaidi ya hii tunayoishi sasa, lakini niwakumbushe ndugu zangu hata wale wa upande wa pili kuwa MAFANIKIO YA SERIKALI YA AWAMU YA SITA WATANZANIA WANAYAONA, NAMBA HAZIDANGANYI.

Kwa muda ambao Samia Suluhu Hassan amekuwa madarakani kama Rais wa Jamhuri ya Muungano , kwa uwezo na kipawa alichopewa na Mwenyezi Mungu amejitahidi saana kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa manufaa ya Watanzania. Kwa sasa katika kata zote 3956 Tanzania kuna miradi ya maendeleo inatekelezwa, katika vijiji vyote 12,319 hakuna Mwanakijiji anayetoka nje ya kijiji chake kufuata huduma za Afya , Elimu au Maji.

Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, ameendelea kuelekeza fedha nyingi katika utekelezaji wa miradi ya maendelo. Ukizunguka mikoa yote Tanzania, kila Mkoa sasa unaendelea na ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Masomo ya Sayansi kwa Wasichana, hivyo baada ya mwaka huu kuisha Mikoa yote itakuwa na shule ya masomo ya Sayansi kwa kila Mkoa, Mhe. Rasis ameelekeza zaidi ya bilioni 30 katika kuhakikisha Tanzania inakuwa na akina Mama Wanasayansi wa kutosha. Akina Mama jipigeni kifua nahodha yuko imara.

Kwenye Kila kata ambayo haikuwa na shule ya Sekondari, Serikali ya Awamu ya sita imepeleka jumla ya Shilingi bilion 232 kwa ajili ya ujenzi wa Shule za kata kupitia mradi wake wa SEQUIP, Watanzania wanaona haya mambo yote yanayoendelea.

Mhe Rais, Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha kila mtoto anapata Elimu bora , ametoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Shule nyingine mpya za Sekondari 15 na Msingi 9, ujenzi wa Shule hizi uko hatua za mwisho, katika kutekeleza mradi huu mama ametoa Tsh bilion 17.25 kupitia mradi wa EP4R

Mhe. Rais anaposema anazunguka duniani kutafuta ni kweli anamaanisha na matokeo yake Watanzania wanaona, ukienda shule yeyote iwe ya Msingi au Sekondari lazima utakutana na ujezi wa darasa, ukamilishaji wa darasa au nyumba za Walimu, leo hii nchi zima jumla ya vyumba vya madarasa 304, mabweni 8, nyumba za Walimu 11, Matundu 548 ya vyoo, ujenzi wa Shule 10 za Msingi mpya na majengo ya Utawala 4 yamejengwa, Mhe. Rais ametoa zaidi ya bilion 12.37 kupitia mradi wa kuimarisha Ufundishaji na Ufunzaji katika Elimu ya Msingi.

Watanzania kwa umoja wetu tuendelee kumuombea Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kazi anayofanya usiku na mchana kuhakikisha gurudumu hili linasonga ni kubwa saana, toka amechukua kijiti hakuna mradi uliosimama, hakuna mkandarasii anayelalamika kutolipwa. Miradi yote ya barabara , maji vituo vya Afya, Umeme sasa karibia vitongoji vyote 64,384 vimeunganisha na umeme.

Mabilionsi ya fedha yanapelekwa kwenye Elimu, Afya, SGR,Bwawa la Mwalimu Nyerere, Ruzuku kwenye mbolea, mafuta Elimumsingi bure etc.

Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu, Serikali ya Awamu ya sita chini ya Samia Suluhu Hassan imeweka mkazo sana katika utoaji wa mikopo isiyo na riba kwa Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu ( Mikopo ya asilimia 10). Kwa mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetoa zaidi ya bilion 59.2 kutoka Halmashauri 184.

Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu badala ya kuendelea kutumika kwenye makongamano na kutukana kwenye mitandao, tujiunge kwenye vikundi tuazishe makapuni tukachukue mikopo isiyo na riba kutoka katika Halashauri zetu, Serikali kwa mwaka huu wa fedha imetenga zaidi ya bilioni 75.98 kwa ajili ya mikopo isiyo na riba ya Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu. Uamuzi ni wetu Vijana.

Hongera sana ndugu Innocent Bashungwa (MB) , Waziri Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,. Hongera sana Dr. Festo Dugange (MB) na David Silinde (MB) Naibu Waziri Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Timu yenu OR - TAMISEMI kwa usimamizi wa utekelezaji wa Miradi inayotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita, hakika mmekuwa wasimamizi wa nguvu kubwa anayopeleka Mh Samia Suluhu Hassan katika kuwaletea Watanzania maendeleo, licha ya changamoto zilizopo lakini Watanzania tunaona kazi mnazofanya. Watanzania wataendelea kuwaombea ili malengo, matamanio na matarajio ya Mh Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania yafikiwe.

Watanzania kwa Umoja wetu tuendelee kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mungu ampe Afya njema kwa kazi anayofanya usiku na Mchana.

TUJIANDAE KUHESABIWA KWA MAENDELEO YA TANZANIA, UJANJA NI KUSENSABIKA.
MUNGU IBARIKI TANZANIA
MUNGU MBARIKI RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, SAMIA SULUHU HASSAN

Tupe hela ya kuzunguka nchi nzima kwenye hiyo miradi, ili na sisi tuje tusifie kama ww.
 
Kuna watu kazi yao wamekuwa ni kupinga na kubeza mafanikio ya Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Samia Suluh Hassan, yawezekana wanatumia uhuru wao wa kutoa maoni kikatiba au wameamua kupinga kwa sababu kazi yao ni kupinga bila kutambua hatuna Tanzania nyingine zaidi ya hii tunayoishi sasa, lakini niwakumbushe ndugu zangu hata wale wa upande wa pili kuwa MAFANIKIO YA SERIKALI YA AWAMU YA SITA WATANZANIA WANAYAONA, NAMBA HAZIDANGANYI.

Kwa muda ambao Samia Suluhu Hassan amekuwa madarakani kama Rais wa Jamhuri ya Muungano , kwa uwezo na kipawa alichopewa na Mwenyezi Mungu amejitahidi saana kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa manufaa ya Watanzania. Kwa sasa katika kata zote 3956 Tanzania kuna miradi ya maendeleo inatekelezwa, katika vijiji vyote 12,319 hakuna Mwanakijiji anayetoka nje ya kijiji chake kufuata huduma za Afya , Elimu au Maji.

Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, ameendelea kuelekeza fedha nyingi katika utekelezaji wa miradi ya maendelo. Ukizunguka mikoa yote Tanzania, kila Mkoa sasa unaendelea na ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Masomo ya Sayansi kwa Wasichana, hivyo baada ya mwaka huu kuisha Mikoa yote itakuwa na shule ya masomo ya Sayansi kwa kila Mkoa, Mhe. Rasis ameelekeza zaidi ya bilioni 30 katika kuhakikisha Tanzania inakuwa na akina Mama Wanasayansi wa kutosha. Akina Mama jipigeni kifua nahodha yuko imara.

Kwenye Kila kata ambayo haikuwa na shule ya Sekondari, Serikali ya Awamu ya sita imepeleka jumla ya Shilingi bilion 232 kwa ajili ya ujenzi wa Shule za kata kupitia mradi wake wa SEQUIP, Watanzania wanaona haya mambo yote yanayoendelea.

Mhe Rais, Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha kila mtoto anapata Elimu bora , ametoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Shule nyingine mpya za Sekondari 15 na Msingi 9, ujenzi wa Shule hizi uko hatua za mwisho, katika kutekeleza mradi huu mama ametoa Tsh bilion 17.25 kupitia mradi wa EP4R

Mhe. Rais anaposema anazunguka duniani kutafuta ni kweli anamaanisha na matokeo yake Watanzania wanaona, ukienda shule yeyote iwe ya Msingi au Sekondari lazima utakutana na ujezi wa darasa, ukamilishaji wa darasa au nyumba za Walimu, leo hii nchi zima jumla ya vyumba vya madarasa 304, mabweni 8, nyumba za Walimu 11, Matundu 548 ya vyoo, ujenzi wa Shule 10 za Msingi mpya na majengo ya Utawala 4 yamejengwa, Mhe. Rais ametoa zaidi ya bilion 12.37 kupitia mradi wa kuimarisha Ufundishaji na Ufunzaji katika Elimu ya Msingi.

Watanzania kwa umoja wetu tuendelee kumuombea Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kazi anayofanya usiku na mchana kuhakikisha gurudumu hili linasonga ni kubwa saana, toka amechukua kijiti hakuna mradi uliosimama, hakuna mkandarasii anayelalamika kutolipwa. Miradi yote ya barabara , maji vituo vya Afya, Umeme sasa karibia vitongoji vyote 64,384 vimeunganisha na umeme.

Mabilionsi ya fedha yanapelekwa kwenye Elimu, Afya, SGR,Bwawa la Mwalimu Nyerere, Ruzuku kwenye mbolea, mafuta Elimumsingi bure etc.

Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu, Serikali ya Awamu ya sita chini ya Samia Suluhu Hassan imeweka mkazo sana katika utoaji wa mikopo isiyo na riba kwa Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu ( Mikopo ya asilimia 10). Kwa mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetoa zaidi ya bilion 59.2 kutoka Halmashauri 184.

Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu badala ya kuendelea kutumika kwenye makongamano na kutukana kwenye mitandao, tujiunge kwenye vikundi tuazishe makapuni tukachukue mikopo isiyo na riba kutoka katika Halashauri zetu, Serikali kwa mwaka huu wa fedha imetenga zaidi ya bilioni 75.98 kwa ajili ya mikopo isiyo na riba ya Vijana, Wanawake na Watu wenye ulemavu. Uamuzi ni wetu Vijana.

Hongera sana ndugu Innocent Bashungwa (MB) , Waziri Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,. Hongera sana Dr. Festo Dugange (MB) na David Silinde (MB) Naibu Waziri Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Timu yenu OR - TAMISEMI kwa usimamizi wa utekelezaji wa Miradi inayotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita, hakika mmekuwa wasimamizi wa nguvu kubwa anayopeleka Mh Samia Suluhu Hassan katika kuwaletea Watanzania maendeleo, licha ya changamoto zilizopo lakini Watanzania tunaona kazi mnazofanya. Watanzania wataendelea kuwaombea ili malengo, matamanio na matarajio ya Mh Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania yafikiwe.

Watanzania kwa Umoja wetu tuendelee kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mungu ampe Afya njema kwa kazi anayofanya usiku na Mchana.

TUJIANDAE KUHESABIWA KWA MAENDELEO YA TANZANIA, UJANJA NI KUSENSABIKA.
MUNGU IBARIKI TANZANIA
MUNGU MBARIKI RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, SAMIA SULUHU HASSAN
Yaani wewe unaonekana kutumwa na ushapokea ujira tayari. Ni sawa hatukatai ila unaposema nchi mzima ni uongo. Mimi kule village kwangu barabara mvua ikinyesha hata bodaboda haziendi. Shule niliyosoma kwenye hizi pesa ya COVID hakuna Darasa hata tundu ya choo iliyojengwa Kwa kupata fungu Hilo.

Dar ninakoishi barabara ni mbovu haisemekani na Kuna Mbunge (Kawe) wakipewa mil. 500 hatuoni hata moramu yenyewe!
Sasa unapoleta hadithi za nchi mzima ni shida.
 
Unajua nyie chawa ni watu wasahaulifu sana. Baada ya JPM (rip) kufariki na watu kuanza kuelezea mafanikio yake, mliwaambia legasy haitetewi, bali hujitetea yenyewe! Well, sasa mko bize na uchawa wenu kutetea mafanikio ya awamu ya 6 (btw, sina tatizo na rais Samia), kwa nini msiyaache hayo mafanikio yakajionyesha yenyewe huko huko watu waliko? Kwa nini mnatumia nguvu nyingi hivyo kutaka kuwaaminisha watu?
Mwacheni Rais afanyekazi, uwezo na mafanikio yake vitaonekana kwa watu.
 
M

Mfumuko wa Bei haujaletwa na mh Rais Bali umetokana na Vita vya huko ukrein, Na katika kulikabili Hilo ili kuleta unafuu katika maisha ya mtanzania mh Rais anatoa Ruzuku katika secta muhimu ambazo zinagusa maisha ya watanzania wengi na Ni injini ya uchumi wetu, Kama alivyofanya kwenye mafuta na mbolea.
Watu wajinga kama wewe mpo wengi sn, Zanzibar wao wanaishi sayari gani au wao vita ya Ukraine haiwahusu?
 
Mpuuzi mkubwa, hata wakoloni walileta reli, shule, makanisa na barabara, mfumuko wa bei sisi ndiyo tatizo letu
Tofautisha mfumuko wa bei (inflation) na kupanda bei bidhaa (price hike). Baada ya hapo ndipo uje uandike humu siyo kutapika pumba kama Bata anakunya
 
Unajua nyie chawa ni watu wasahaulifu sana. Baada ya JPM (rip) kufariki na watu kuanza kuelezea mafanikio yake, mliwaambia legasy haitetewi, bali hujitetea yenyewe! Well, sasa mko bize na uchawa wenu kutetea mafanikio ya awamu ya 6 (btw, sina tatizo na rais Samia), kwa nini msiyaache hayo mafanikio yakajionyesha yenyewe huko huko watu waliko? Kwa nini mnatumia nguvu nyingi hivyo kutaka kuwaaminisha watu?
Mwacheni Rais afanyekazi, uwezo na mafanikio yake vitaonekana kwa watu.
Acha utoto UmkhontoweSizwe, Kama kuna mazuri waacheni watu waongee, mbona nyie mkikosoa watu hawalalamiki.
 
Mafanikio ya wananchi ni kuwa huru ktk Nchi Yao.

Wananchi wawe huru kuchagua viongozi wawatakao, Sanduku la kura lililoibwa 2020 ndo lilimweka alipo sasa, Je amefanikiwa kuondoa wizi huo?

Maendeleo ni Uwezo wa wananchi kuwawajibishwa Viongozi wabovu wawatakao, Leo wanatutukana hadharani wakisema tuhamie Burundi na hatuna la kuwafanya.

KATIBA mpya ndo italeta maendeleo ya Kweli.

Ameeeen
Watanzania wako huru, ndio maana hata wewe uko huru kutoa maoni yako bila shida
 
Yaani wewe unaonekana kutumwa na ushapokea ujira tayari. Ni sawa hatukatai ila unaposema nchi mzima ni uongo. Mimi kule village kwangu barabara mvua ikinyesha hata bodaboda haziendi. Shule niliyosoma kwenye hizi pesa ya COVID hakuna Darasa hata tundu ya choo iliyojengwa Kwa kupata fungu Hilo.

Dar ninakoishi barabara ni mbovu haisemekani na Kuna Mbunge (Kawe) wakipewa mil. 500 hatuoni hata moramu yenyewe!
Sasa unapoleta hadithi za nchi mzima ni shida.
Mkuu Vyura99tu data haziongopi, wapi nimesema uongo hapo? Hakuna mtoto wa Kitanzania anayesomea chini ya mti kwa sasa, yawezekana Shule unayosema ni kweli haijapokea( Japo sina uhakika kuwa ikose fedha IMF, EP4R, Umaliziaji wa maboma, etc ) lakini pia Shule zinapewa kutokana na mahitaji, kuna shule zina excess ya madarasa na miundo mbinu ya vyoo..
 
Mkuu Vyura99tu data haziongopi, wapi nimesema uongo hapo? Hakuna mtoto wa Kitanzania anayesomea chini ya mti kwa sasa, yawezekana Shule unayosema ni kweli haijapokea( Japo sina uhakika kuwa ikose fedha IMF, EP4R, Umaliziaji wa maboma, etc ) lakini pia Shule zinapewa kutokana na mahitaji, kuna shule zina excess ya madarasa na miundo mbinu ya vyoo..
Rais Samia ni mtu wa vitendo sana kuliko sifa, ni mpenda haki na siyo mtu wa DHULUMA. Kikubwa anafanya kazi zake vizuri kwa ajili ya wananchi wa Tanzania. Wala hafanyi kwa ajili ya kutaka abakie madarakani mwaka 2025.

Kama hatutamtaka mwaka 2025 naamini atakaa pembeni lakini hawezi kufanya ule UHAYAWANI wa Magufuli wa kuiba chaguzi za vitongoji za 2019 na uchaguzi Mkuu wa 2020. Tuko mikono salama na Rais SSH

Wakati ndiyo utasema tusubiri 2025
 
Unavyoweweseka kuikandia serikali ya Mama yetu SSH utadhani kama kweli ni mpinzani haswaa wa utawala huu kumbe ni kanyaboya lililo kwenye bahari kusubiri mpumbavu anasemo kisha kuzama naye majini [emoji16]
Hata wew ? Kumbe umekufa macho
 
Ukiitembelea Tanzania utashangaa nakubali. Na mshangao wenyewe ni wa ajabu kidogo...watu hawapewi kulingana na mahitaji yao bali kwa kujuana.
Vipo vituo vya afya vinazidi hospitali za wilaya nyingine. Zipo wilaya hazikugusa vituo vyake vya afya wala hospitali zake ila wamepewa mpyaaa..kubwaaaa.
Kuna sehemu hawana hospitali za wilaya ila wamelazimika kuomba kutumia hospitali za dini kuziba mapengo.
Mfano.
Mkoa wa kilimanjaro...
Rombo hospitali ya wilaya ni ya dini
Moshi vijijini...hawana...
Moshi mjini...hospitali ya wilaya ya dini
Siha?
Ukiona kinachoita kituo cha polisi cha wilaya...toka Rombo hadi siha utashangaa....
Na ni wila za muda mrefuuuu
Halmashauri hazi majengo yake nk

Kwa kifupi taasisi zote za serikali hazina majengo yanayofanana na wilaya nyingine...tena mpyaaa...

Sent from my SM-N986B using JamiiForums mobile app
 
Watanzania wako huru, ndio maana hata wewe uko huru kutoa maoni yako bila shida
Ni kweli wako huru ndio maana wanatumia ID feki ila walioshindwa kustahimili njaa kama wewe inabidi wajianike ile walau watupiwe hata ka-mfupa.
 
Kaka, tatizo sio kumbeza Rais, na hakuna anayekataa kuwa Rais hafanyi mazuri. Anafanya mazuri kama walivyo fanya wengine.

Shida ni watu wenye upeo bapa wanaotumia muda mwingi na majukwaa ya hadhara kusifu na kulazimisha shangilieni, hasa kwenye mikutano mbali mbali, kiasi cha kusahau kwamba shauku ya watu iko kwenye kutatua kero za kimaendeleo.

Wanaofanya Rais aonekane anabezwa ni hao ambao wakiwa mbele yake hawaezi sema sentensi moja bila kuchomekea ama "piga makofi kwa mama Samia, ama Makofi mengi sana kwa Mama Samia, ama nani kama Mama Samia heee, ....hadi mwisho wa hotuba zao!

Hadi kichefuchefu - wengine huko nje hawako hivyo
Hivi kumsifia kila Rais kila wakati, mara kwa mara haikuwepo wakati wa Nyerere, Mwinyi, Mkapa nafikiri hata Kikwete. Ilianza sana wakati wa Mgafufuli kwa sababu ya kuogopa kutunguliwa. Nafikiri walimsoma kwamba alipenda kusifiwa, hivyo ikawa kama gia ya kupata kibali kwake. Sasa hivi inasikitisha sana, kwamba kila jambo ni kumtaja Rais, yaani serikali anayoiongoza haina kazi. Tanzania uongozi ni kazi kweli kweli.
Tambua kongozi kwamba kibali chako si kutaja taja jina la Rais bali ni utendaji wako.
Rais usifunikwe na sifa zao, wengine wana unafiki ndani yao. Usilewe sifa za wapambe wako, wanajua wasipokusifia hawatabaki wanaogopa, mtu mwoga ni hatari sana, anaweza kufanya jambo lisliotarajiwa. Tambua kusifiwa sio kupendwa. Chunguza na watambue wenye moyo wa uzalendo hasa eneo la rushwa.
Kila mmoja anapenda kusifiwa lakini ikae kwa utaratibu na hekima.
 
Back
Top Bottom