Mnaomshinikiza Rais Samia amuachie huru Sabaya acheni, Mwacheni Sabaya avune alichopanda!

Kwahiyo wewe unafaidika nini kuna malipo unapata kutokana na mateso ya Sabaya yaani masikini mmejaa roho za chuki ndio maana umasikini hauishi wazungu wanatuponda kwa mawazo ya watu kama nyie kwamba waafrika wanachukiana wao kwa wao pasipo sababu ya msingi yoyote.
 
Kwangu mimi hao wakina mama wangefanya yafuatayo hapa chini ndio ningeona vilio vyao ni vya maana:-

1. Wangewatafuta wale wote wanaolalamika kutendewa uovu/dhuluma na Sabaya kwa njia moja au nyingine.

2. Wale wenye madai ambayo yapo ndani ya uwezo wa hao wakina mama wawaomba msamaha na wawalipe mara moja.

3. Wale ambao hawana uwezo wa kuwalipa wawaombe msamaha tu kwa dhati ya mioyo yao kwa niaba ya Sabaya.

Naamini wengi watakaoombwa msamaha hawatakuwa na mioyo migumu watasamehe tu hasa ikizingatiwa
kuwa watakaokuwa wanaomuombea msamaha Sabaya ni wakinamama tena watu wazima.

4. Baada ya hilo zoezi waende mahabusu wamweleze Sabaya hatua walizochukua na wamtake Sabaya na yeye akiri yale yote aliyoyatenda hata kama ni maovu kiasi gani na aombe msamaha kwa wahanga wote aliowaumiza kwa njia moja au nyingine kupitia barua ya wazi kwenye vyombo vya habari.

5. Baada ya hatua zote hizo waiachie mahakama ifanye kazi yake bila shinikizo. Maana mahakama ikiruhusiwa
kufanya maamuzi kwa shinikizo basi kila familia yenye mtu wao anayeshatakiwa watataka waende na wao
kulia mahakamani ili ndugu yao aachiwe.

6. Pia waache kumuingiza kiongozi wa nchi kwenye mtego kwani suala kama hilo lilishaleta sintofahamu kubwa
nchini pale raisi wa awamu ya pili alipoamuchia mtuhumiwa kepteni Aziz (kama nimekosea jina wahenga
watanisaidia)

Mwisho hao wakinamama wanapaswa wajue kuwa watu wengi walipitia maumivu makubwa sana ya kiakili,
kimwili, kisaikolojia na kiroho yaliyosababishwa na huyo Sabaya. Kwa hiyo maumivu anayoyapata sasa hivi Sabaya hayafiki hata robo tu ya aliyowapitisha wenzake kwani yeye mateso makubwa ni kukosa tu uhuru na wala sio maumivu ya kimwili. Lakini muhimu na kubwa ni msamaha tu kutoka kwa wahanga na wala sio kuachiwa huru. Kwani hata akiachiwa leo bado hatakuwa huru ikiwa wahanga bado hawajamsamehe. Lakini kukiwa na msamaha hata siku akiachiwa huru na mahakama basi atakuwa huru kuendelea na maisha yake kama kawaida bila matatizo yoyote.

Na kubwa la kujifunza ndugu zangu pale tunapoona watoto wetu au hata ndugu zetu wanawafanyia dhuluma watu wengine tuwakemee kwa nguvu zote hata kama wao ndio wanatuaptia mkate wa kila siku. Tusisubiri wakaharibikiwa ndio tutoke hadharani tena bila hata aibu badala ya kuomba msamaha kwa matendo yao maovu tunaomba mamlaka au viongozi wakubwa waingilie kati ili wawe huru.

Ni mtizamo tu.
 
Mbona Mbowe kasamehewa na hajana aloyapanda?
 
Mashtaka anayoshtakiwa sasa hivi ndugu Sabaya yanamhusu mwenyewe. Magufuli hausiki hata kidogo. Wamwache mzee wa watu apumzike. Hata Sabaya mwenyewe sasa hivi asimsingizie Magufuli wala serikali ya Magufuli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…