Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Ndugu zangu Watanzania,
Katiba siyo msaafu wala siyo Biblia. Katiba yetu ilitungwa na wanadamu ambao ni watanzania kwa lengo la kuwa kama muongozo wa masuala mbalimbali ya kuongoza Nchi yetu. Katiba Ni karatasi tu zilizojaa maneno ya namna gani ya jambo fulani lifanyike na hatua zipi zifanyike na kufuatwa katika kufikia hitimisho la jambo fulani.
Katiba yetu ipo kwa ajili yetu watanzania na ni kwa ajili ya ustawi wetu pamoja na Taifa letu kwa ujumla wake. Ni muongozo wa mambo yetu wenyewe.
Nilikuwa napenda kuwaambieni watanzania Wenzangu ya kuwa tufike wakati tutambue ya kuwa viongozi aina ya Rais Samia hawazaliwi kila siku na wala hawapatikani kila Nchi na wala siyo Rahisi kuwatengeneza .
Huyu Rais ni Mchapa kazi kwelikweli,ni mzalendo aliyetukuka na ambaye huwezi kumtilia shaka juu ya uzalendo wake,ni kiongozi mwenye maono,akili kubwa,upeo mkubwa na Karama ya uongozi. Ni kiongozi ambaye amejitoa na kujitolea Maisha yake Kama Sadaka kuwatumikia watanzania.
Ameyatoa Maisha yake kama Zawadi kwa Watanzania. Sasa kwanini tusithamini na kutambua Moyo huo wa upendo wa kipekee wa Rais wetu? Kwanini tusibadilishe katiba yetu ili Mama aendelee kuongoza Taifa letu.
Uzuri wa Mama yetu ni kuwa bado yupo imara kimwili na kiakili. Akili yake inachemka Muda wote na hapa unaweza kuona kupitia mipango yake na mambo makubwa aliyoyafanya na anayoendelea kuyafanya hapa Nchini.
Jiulizeni Angela Merkel aliiongoza Ujerumani kwa miaka mingapi.Kumbukeni ya kuwa Ujerumani ndio Taifa lenye uchumi mkubwa sana barani Ulaya. Na ni yeye aliyefanya kazi kubwa ya kuhakikisha kuwa Ujerumani inaendelea kuwa imara kiuchumi.
Sasa kwanini tusimpatie Mama yetu Muda zaidi wa kuongoza Taifa letu ili tufaidi vyema kazi ya mikono yake ? Mnafikiri ni Nchi gani hapa Afrika mashariki na ukanda huu wa kusini Mwa jangwa la Sahara itakayotufikia kiuchumi?
Huyu Hapa Mama wa Shoka Jasiri Muongoza Njia👎
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Katiba siyo msaafu wala siyo Biblia. Katiba yetu ilitungwa na wanadamu ambao ni watanzania kwa lengo la kuwa kama muongozo wa masuala mbalimbali ya kuongoza Nchi yetu. Katiba Ni karatasi tu zilizojaa maneno ya namna gani ya jambo fulani lifanyike na hatua zipi zifanyike na kufuatwa katika kufikia hitimisho la jambo fulani.
Katiba yetu ipo kwa ajili yetu watanzania na ni kwa ajili ya ustawi wetu pamoja na Taifa letu kwa ujumla wake. Ni muongozo wa mambo yetu wenyewe.
Nilikuwa napenda kuwaambieni watanzania Wenzangu ya kuwa tufike wakati tutambue ya kuwa viongozi aina ya Rais Samia hawazaliwi kila siku na wala hawapatikani kila Nchi na wala siyo Rahisi kuwatengeneza .
Huyu Rais ni Mchapa kazi kwelikweli,ni mzalendo aliyetukuka na ambaye huwezi kumtilia shaka juu ya uzalendo wake,ni kiongozi mwenye maono,akili kubwa,upeo mkubwa na Karama ya uongozi. Ni kiongozi ambaye amejitoa na kujitolea Maisha yake Kama Sadaka kuwatumikia watanzania.
Ameyatoa Maisha yake kama Zawadi kwa Watanzania. Sasa kwanini tusithamini na kutambua Moyo huo wa upendo wa kipekee wa Rais wetu? Kwanini tusibadilishe katiba yetu ili Mama aendelee kuongoza Taifa letu.
Uzuri wa Mama yetu ni kuwa bado yupo imara kimwili na kiakili. Akili yake inachemka Muda wote na hapa unaweza kuona kupitia mipango yake na mambo makubwa aliyoyafanya na anayoendelea kuyafanya hapa Nchini.
Jiulizeni Angela Merkel aliiongoza Ujerumani kwa miaka mingapi.Kumbukeni ya kuwa Ujerumani ndio Taifa lenye uchumi mkubwa sana barani Ulaya. Na ni yeye aliyefanya kazi kubwa ya kuhakikisha kuwa Ujerumani inaendelea kuwa imara kiuchumi.
Sasa kwanini tusimpatie Mama yetu Muda zaidi wa kuongoza Taifa letu ili tufaidi vyema kazi ya mikono yake ? Mnafikiri ni Nchi gani hapa Afrika mashariki na ukanda huu wa kusini Mwa jangwa la Sahara itakayotufikia kiuchumi?
Huyu Hapa Mama wa Shoka Jasiri Muongoza Njia👎
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.