Mnaopekua simu za wapenzi/waume/wake zenu huwa mnataka nini kifuate?

Mnaopekua simu za wapenzi/waume/wake zenu huwa mnataka nini kifuate?

Ni matani tu ya kazini hayo,alichotakiwa kufanya ni kumwuliza tu kwanini huyo mtu anakuita hivyo, kwanini achati nae sasa,itamsaidiaje zaidi yakumfanya apaniki na kujipa misongo ya mawazo bila sababu.
Utani inabidi uzingatie wewe ni nani kwa wakati huo, yaani ni mke au mume wa mtu utani usivuke mipaka. Mimi naamini hata huyo mwanamke angekuta sms ya namna hiyo kwa jamaa ndani pangekuwa pa moto pia, hata wewe ungekuta sidhani kama usingefikiria mengine. Ni bora utani wa hivyo uishie kwenye kuongea tu, sio hadi kwenye kuchat huku unajua huo ni ushahidi endapo mume/mke ataona hamtaelewana na iko wazi kabisa hata kwa akili ya kawaida tu
 
Kuna binti kaja kwenye kikundi leo analia, jana mume karudi nyumbani amelewa binti kafungua simu amekuta meseji za kimapenzi za wanawake, picha za utupu kutoka kwa wanawake watatu na wawili kati yao ni wafanyakazi wenzake na mumewe. Asubuhi hii ameondoka nyumbani akaenda kanisani na hajaongea na mumewe bado.

Nina swali la msingi kwa wapekua simu: Hivi, mkiwa mnapekua hizo simu za wapenzi au wenza wenu, huwa mnafikiria na next step itakua nini? kama unahisi mume au mke anachepuka, je ukimkamata ni kweli anachepuka utafanyaje? au mnapekuaga tu ili umshike na kosa ila hujafikiria kitakachofuata.

Haya mshaurini huyu mwanamke mwezetu afanyaje maana haelewi cha kufanya. Ndoa ina miaka 8, wana watoto wawili, yeye ni mama wa nyumbani na kama familia wanajiweza kiasi kiuchumi.

Msisahau, kupekua simu ni kosa la jinai:
View attachment 3254745

View: https://youtu.be/y8jYZw60zPw?si=WOl6F_9z4FbSdgdN

Akina sisi simu ya mtu ikiita hata niulizwe nani huyo anapiga huwa namjibu njoo mwenywe na kama yupo bafuni eti niletee simu namwambia oga wewe mtatafutana ukitoka 😂😂😂

Niliwahi mfuma anafunua yangu eti ngoja niangalie kama kuna mtu atanipa presha ya kushuka 😂😂

Majina yangu mengi ni fundi spare temeke, fundi interior design, engineering 4D33, mchonga bush temeke, fundi rejeta mbagala, fundi tension spring leaf, "aliyepigwa chai Schiphol" 😂 😂😂😂
Mshangazi dot com
 
Utani inabidi uzingatie wewe ni nani kwa wakati huo, yaani ni mke au mume wa mtu utani usivuke mipaka. Mimi naamini hata huyo mwanamke angekuta sms ya namna hiyo kwa jamaa ndani pangekuwa pa moto pia, hata wewe ungekuta sidhani kama usingefikiria mengine. Ni bora utani wa hivyo uishie kwenye kuongea tu, sio hadi kwenye kuchat huku unajua huo ni ushahidi endapo mume/mke ataona hamtaelewana na iko wazi kabisa hata kwa akili ya kawaida tu
Ni sawa mkuu,nilichoandika hapo, tatizo liko kwa approach ya mwanaume,why aanze kuchati na dume jenzake,badala yakumuoji mkewe!??,.ni nini hii kama si wivu wa ovyo?
 
Nakubaliana na wewe partially.

Binafsi, naamini kukagua simu ya mtu ni kukosa trust. Mtu unakua na mashaka yanayokufanya usimuamini mwenzako. Binafsi sijawahi kujisikia kushika simu ya mwenza wangu kwa sababu namuamini. Yeye pia hajawah,i ila inaweza kutokea nahitaji kufanya kitu na simu yangu iko mbali basi naomba kutumia yake na hajawahi kusita kunipatia.

Nafikiri kuaminiana ni nguzo muhimu ya mahusiano, kwenye kujenga uaminifu hapo ndiyo kipengele.
Kinachosababisha simu inakaguliwa ni muhusika kuonyesha simu yake ni special. Unafikili wanaokagua wanaanza tu!?Huwa Kuna viashilia vya kimsukumo, ndoa inayovunjika Huwa Ina dalili(keys), anachofanya muhusika ni kutembea na hizo keys,.


Niliwahi kuwa na uhusiano wa namna hiyo, siku niliyoongozwa kukagua simu, ndio siku nilikuwa nimejiandaa kuachana, and I was comfortable for that,


Angalizo tu,kama una amani usikague,ila ukiwa na hisia mbaya ,just kagua, ukikaa kimya utakuja kulishwa ARV bila sababu ya msingi


Bora uteseke miezi kadhaa, kuliko kuumia maisha,
 
Muda mwinginee unaweza ukawa huna idea ya kupekua lakini ukaazima simu yake ufanye mawasiliano labda, mara paaap text inaingia kwa juu pale "mpenzii nimemiss Ile ya Jana" na Wala hujatuma wewe hiyo text lazima utataka kujua zaidi ni nani anayetuma mesejii za hivoooo ndo kukutana na maajabu🥶🥶🥶
 
Ni sawa mkuu,nilichoandika hapo, tatizo liko kwa approach ya mwanaume,why aanze kuchati na dume jenzake,badala yakumuoji mkewe!??,.ni nini hii kama si wivu wa ovyo?
Yeah hapo ilibidi amalizane na mke wake, Nakumbuka kuna staff mwenzetu kipindi ndo kaoa tu ndoa bado changa ilikuwa mke wake akitongozwa tu,jamaa anamfata mwanaume aliyemtongozea mke wake na kuanzisha magomvi.


Jamaa aligombana karibu na kila mwanaume pale mtaani kumbe mke wake ni kicheche balaa anamchora tu. Alipokuja kugundua mke wake ndo chanzo na anagongwa mbaya saizi kapoa hamfatilii tena na kulichopo wanashindana tu mwanaume kaamua nae kuwa kiwembe
 
Hiyo tabia anayo mke wangu. Yani dakika moja ya kupoteza, simu imepekuliwa kila engo. Why kuyatafuta mambo yatakayokuumiza? umekuta mawasilano tata, vipi utavunja ndoa?
wazee wetu hawakutaka shida kabisa, wakiwa wanatoka safari walitanguliza koti au mzigo nyumbani wao wakibaki vijiweni kwa muda. Hii ni kumfanya mke ajiandae, kama alikuwa na makandokando yake ayaondoe ili maisha yaendelee
 
Hiyo tabia anayo mke wangu. Yani dakika moja ya kupoteza, simu imepekuliwa kila engo. Why kuyatafuta mambo yatakayokuumiza? umekuta mawasilano tata, vipi utavunja ndoa?
wazee wetu hawakutaka shida kabisa, wakiwa wanatoka safari walitanguliza koti au mzigo nyumbani wao wakibaki vijiweni kwa muda. Hii ni kumfanya mke ajiandae, kama alikuwa na makandokando yake ayaondoe ili maisha yaendelee
Kwa baadhi ya wasomaji watakua wanajisikia kuvurugigwa ubongo,wakisikia kuwa kuna wazee walikuwa hivyo,wanaona kama walikuwa hamnazo kichwani au limbwata liliwatawala,,kumbe wangejua ilikuwa ni hekima ya hali ya juu na walidumu kwa mda mrefu kwenye ndoa zao.
 
Back
Top Bottom