Mnapopewa ofa muwe mnaanza kujitathimini

Mnapopewa ofa muwe mnaanza kujitathimini

Yani mtu umemtoa Lunch au Dinner muwe mnaangalia kwanza mwenyewe kaagiza nini.

Tena jinsia ya KE ndio kabisa huko siwezi kuwazungumiza tujumuishe wote.

Yani ni metoa jamaa tendwe tukapate supu anaona mimi naagiza makongoro ya ng'ombe yeye anaagiza mchemsho wa kuku tena kidali. Kwa nini usisubiri kusikia muhusika kwanza.

Kuna wengine umeagiza chakula cha kawaida yeye anaagiza kushinda wewe.

Tuheshimiane tutakwepana: Jana nampa mtu ofa chukua bia anaona nakunywa balimi yeye anataka windock tena anabugia kwa sifa.
Ndo mana hua sipendi vitu vya offer
 
Ndicho kinacho fanyika

Umefika mtu anamuita muhudumu msikilize uyo mtu anaona jau wew unasema kuwa huru agiza unachojisikia unaagiza tena unakasilika tukueleweje
Uangalie na hali yake...agiza ambacho jamaa akikukimbia ulipe usijekupewa adhabu ya kuosha vyombo🤣🤣🤣
 
Nikikuweka huru kwa kweli chukua

Mimi kama nimemuita mtu namwambia mapema ndugu hapa nimekuja sikiliza mziki agiza choda tu kama unataka kinywaji kingine toa pesa yako mfukoni ivyo tu [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ukitaka kutoa hayo malalamiko ukimpatia mtu ofa inabidi umwanbie gharama ambayo upo comfortable kuitumia. Kama mhusika atahitaji kinywaji/chakula cha bei ya juu ajue atatakiwa kulipia pesa iliyobakia au kuchukua kinywaji/chakula ambacho kitaendana na pesa ambayo utakuwa tayari kulipia.
Kama umempeleka mtu mahali (labda ni ofa umempatia) unamwambia agiza unachohitaji na bila kumwambia balance usilalamikie bei.
No offence intended
 
Ase tutazinguana
Huu uzi ni mzuri japo mleta uzi kaandika kisela sana.
Hapa tunajifunza ustaarabu na sio kujiachia kupitiliza.
Mimi ukiniita kama sina pesa ya kutosha nitakunyqa zangu maji wewe kula tu🤣🤣🤣🤣

Vinginevyo uliyeniita nami nitachangia bill.
Ikiwa ni mtu mzito ndio nitakuachia bill yote hii ni kanuni kqangu.
 
Huu uzi ni mzuri japo mleta uzi kaandika kisela sana.
Hapa tunajifunza ustaarabu na sio kujiachia kupitiliza.
Mimi ukiniita kama sina pesa ya kutosha nitakunyqa zangu maji wewe kula tu[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Vinginevyo uliyeniita nami nitachangia bill.
Ikiwa ni mtu mzito ndio nitakuachia bill yote hii ni kanuni kqangu.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] hakuna kitu kna icho lazima nikuchafue
 
Back
Top Bottom