Mnataka kumbebesha Hayati Magufuli madhambi yenu?

Summarize uandishi wako,Unaandika maneno mengi mno hueleweki lengo lako?

Jaribu kupangilia lengo kuu mwanzo mwa uzi wako

Mara unaitwa Sukuma Gang
Mara 2010 damu zilimwagika sana
Mara JPM 2015 kwani aliharibu uchaguzi
Mara Makamba Je ataachia jimbo la bumbuli

Ulimwengu wa sasa unahitaji maandishi mafupi sana ,
 
Wakubali tu. Ni mazuzu.

Hawa wanaodai hayati Rais J.P Magufuli ndie alipiga 'goli la mkono' au hawa wanaodai 2020 waliibiwa kura.

Mazuzuzeni yenu.
Yaani umaamini kabisa mwaka 2020 kulikuwa na UCHAGUZI Tanzania? Watu walikwenda vituoni kuweka alama ya wino kwenye vidole.

Mwaka 2020 aliamua kuziiba kura zote mwenyewe Magufuli kwa kutiki makaratasi kutokea Jamana Printers na Kambi ya Mbweni Kisha ma DSO na DED wakagawiwa makatasi yaliyopigwa. Zile kura tulizopiga wananchi hazikuhesabiwa kabisa.

Dhana ya kwamba Magufuli alikuwa anapendwa ni UWONGO, kadanganye wanao au wajinga wenzi
 
Mwaka 2020 hakukuwa na uchaguzi bali kulikuwa na uchafuzi. Ni aibu kwa level yako kama mwana JF mkongwe kuvaa miwani ya mbao kwenye huo uwendawazimu wa 2020
Sitetei kama kipofu...tuwe wa kweli. Unapolinganisha kitu unalinganisha na kingine. Ukisema "mtaa ule una nyumba moja mbaya sana, haina mabati mazuri wala milango imara".

tunaenda mtaani na kuangalia na kukuta kuna nyumba moja tu. Sasa unawezaje kulinganisha.

Uchaguzi au uchafuzi wa 2020 unaweza kulinganishwa na uchaguzi au uchafuzi wa 2010 na 2015 na chaguzi zilizotangulia. Au wewe unalinganisha na uchaguzi wa 2025 ambao utakuwa salama, wa haki na huru kwa sababu JPM mchafuzi mkuu keshakufa?
 
Na afe tena mara ya pili huko aliko. Tanzania pamekuwa mahali salama pa kuishi bila huyo shetani wa Chato
 
Ndugu!

Team mama wamekosa sera za maaana!!

Hapa nilipo umeme wamekata,sukari bei juu watasema nini!!?sisi wanaccm wenye akili.timamu tuwaelewe!!?

Mama kashindwa kutatua changamoto amebaki na proapaganda za chawa ambazo hazina mantiki!!

Mi nasubiri 2025 kama jamuhuri na Baraza la usalama wa taifa litampitisha huyu mama kugombea urais!!!nitafunga maombi ya siku tatu nikimuombea ashindwe kufanya kampeni Hadi turudi chimwaga Kwa mara nyingine!!!

Hatuna ajenda yeyote zaidi ya kuhubiri jinsia na uchawa!!!!!

THE STATE MSITUKOSEE WANACHAMA WA CHAMA CHA MAPINDUZI!HII MINNE INATOSHA KABISA ARUDI AKACHEZE NA WAJUKUU!!

RIP THADEY OLE MUSHI!!
 
2020 ule haukuwa wizi, ulikuwa ujambazi. Ubaya matendo mabaya huwa yanakuwa na athari hata kwa walioyafanya. Wanaoumia na wizi au ujambazi wote uliofanyika siku za nyuma ni wahusika wa wizi au ujambazi wenyewe. Sidhani kama kuna aliyefaidika toka kipindi hicho
 
Ahaaa!! January Makamba, mpuuzi mmoja, ambae hata mitihani ya O level ilimshinda, akaiba, akapewa uongoz wa, wizara mbalimbali na akashindwa na anaendelea kushindwa. Eti nae anatuambia, upumbavu na ujinga wake . Huyu Makamba junior hana akili ni mpumbavu na mjinga tu. Kama, mtu kama huyu anaweza kuongea ujinga na upumbavu kama huo. Huko wizara ni anaongozaje. Na kama, anaongea ukweli basi ajiuzuru mara, moja ubunge na uwaziri.Kwa kuwa ametamka kuwa aliingia kwa wizi wa uchaguzi.Aliyeleta utengano wa taifa ni mzee wake, mwenye akili mbovu kama yake. Wazuri hawafi.
 
Magufuli amesababisha hayo matatizo akitokea kusimamia Malaika ahera madukani...
 
Hakuna mwema hapa!

Hakuna was afadhali iwe kikwete,mama Wala jpm wote wanafanana tofayti ni style!!

Jpm hakuwa mnafiki.wa.kuzunguuka sana !alitumia Dola kubaki madarakani kama wenzake bila soni!!!

Hakutaka kujifanya eti anajali demokrasia alionyesha uhalisia was ccm was kuiba uchaguzi bila aibu ,sio kama kina jk na samiah wanafiki wanaita maridhiano halafu wanaudikteta chini chini!!

MWAROBAINI NI KATIBA MPYA TU BASI NA SIO HAYA MAIGIZO!!
 
Kwangu Mimi issue sio uchaguzi.

Kwangu mimi ni watu kuwa busy kupambana na Marehemu huku wameacha majukumu yao ya msingi ya ujenzi wa Taifa.

Marehemu alifanya yake, Mwenyezi Mungu kachukua kiumbe chake, tunachotaka kuona kwao ni suluhu ya matatizo lukuki yanayowakabili Watanzania na nchi Kwa ujumla.
 
Na ukakoma kwani Sasa hivi hakuna watu katili tena. Au anaendeleza ukatili akitokea ahera madukani.?

..Magufuli alikuwa na mahabusu wa kisiasa 400+.

..Je, sasa hivi kuna mahabusu wa kisiasa?

..katika utawala wa Magufuli hata wanasiasa wanawake walikuwa wakipokea vipigo, na kudhalilishwa. Rejea matukio la Halima Mdee, Bulaya, Matiko, Ruge, kujeruhiwa.

..Je, sasa hivi kuna mwanasiasa yeyote mwanamama aliyejeruhiwa na vyombo vya dola?

..Ukiacha kuwadhuru watu kimwili Magufuli ndiye mtawala aliyefungulia wanasiasa kesi za kihunihuni, na aliyeengua wagombea wengi, kuzidi watangulizi wake.
 
Yaani umaamini kabisa mwaka 2020 kulikuwa na UCHAGUZI Tanzania? Watu walikwenda vituoni kuweka alama ya wino kwenye vidole.

Wewe kweli ni zuzu. Wapi hapo niliposema au kushwawishi kwamba Uchaguzi wa 2020 haukuwa wa kweli. Huwa unajipendkeza hapa na Watu wa Ulaya na Marekani. Kuna ripoti hata moja kutoka kwai inasema ule haukuwa Uchaguzi? Kwa maneno mengine... Porojo zako hazifanyi ule kutokuwa Uchaguzi.
Mwaka 2020 aliamua kuziiba kura zote mwenyewe Magufuli

Kwa hiyo alichaguliwa Magufuli peke yake.? Yaani aibe kura zote ili iweje? Nyuma Lowassa hakupata Kura? Tundu Lissu hakupata kura? Sasa hiyo lugha yako kuwa aliiba kura zote umepata wapi kama sio kupotosha umma.? Wacha uzuzu.
kwa kutiki makaratasi kutokea Jamana Printers na Kambi ya Mbweni Kisha ma DSO na DED wakagawiwa makatasi yaliyopigwa. Zile kura tulizopiga wananchi hazikuhesabiwa kabisa.
Wacha uongo. Huyo Magufuli alikuwepo kila sehemu? Where is your Logic?
Dhana ya kwamba Magufuli alikuwa anapendwa ni UWONGO
Hayo ni maoni yako Una haki. Lakini hayabadilishi ukweli.
, kadanganye wanao au wajinga wenzi
Una makasiriko sana mpaka mapovu yanakutoka.

...mpaka sasa unatumia nguvu kuuubwa za nini? kudai kwamba hakupendwa?? au Ndio kusema na wewe ulikuwa zuzu sasa umeamka?

Nyie CHADEMA pia mmejaaa madhambi mengi tu, na mseme mlishindwa kwa mbinu. Mtulie tu na msubiri 2050!
 
Wazo fyatu haswaa
Hakuna uchaguzi ulikuwa huru na haki. Wa mwaka 1995 mnakumbuka kilichojiri bara na Zanzibar?
 
Zigo la democracy na uchaguzi wa hovyo litamwandama magufuli vizazi na vizazi.
Mnahangaika na Magufuri aliyelala kwa amani, ila wezi wauaji na waharibufu kwa nchi yetu wapo nasi na wanaendelea na mikakati yao.

Rais aliyepo madarakani angekuwa mwema kuliko JPM angevunja bunge mara tu baada ya mazishi ya JPM.

Na kwa kuwa hakuvunja bunge maana yake alivutiwa na uchaguzi huo wa 2020 na yeye alishirikiana na JPM, huyo mama yupo hai anakula mema ya nchi pamoja na marafiki na watu wa nyumbani kwake tu.

Huku sisi tunabetua midomo tu...... "JPM alivuruga uchaguzi wa 2020, watu walijaa hofu, biashara zilifungwa ..."
Kwa nini tunapambana na mfu? Je tunawaogopa walio hai? wanaiba na kuuza rasrimali zetu mchana kweupee na kutuacha na miundombinu isiyokubalika kimataifa....

Wabongo tumekazana na taarabu.... "JPM alikuwa dikiteta...."

Nahisi aliyeturoga wabongo hakufanya makosa, tumekuwa kituko tangu tupate uhuru hadi leo hatujawahi kuwa huru kabisa.

Magufuli wala hajibu chochote kuhusu hizo lawama na hatajibu milele na milele.

Sasa basi tutaendelea kuwa wajinga wa kumlaumu mfu ilhali walio hai tunawaita waheshimiwa japo ni kausha damu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…