"Mnatuchukuliaje? Watumwa wenu?" Waziri mkuu wa Pakistan awachana EU kwa kuishinikiza Pakistan kuilaani Russia

Bora khan kasema ukweli.
Haya Mambo ndo waliyafanya kwa mababu zetu kwenye Vita vikuu vya dunia.vita waanzishe wao wanataa na nyie mpigane. Mkijitenga unaonekana wabaya.
Sasa sisi tupigane tumechokozwa na Nani?
 
USA na wenzake watapoteza ushawishi sana baada ya mgogoro huu, kwan Waarabu ndo kabisa hawamuelwi toka zaman sema wanamtafutia mbadalaa wake ambaye atakuwa Russia

Uko sahihi mkuu, yaani hadi Saudia na Umoja wa Falme za kiarabu (UAE) wameamua kuwa nyutro ili kulinda mahusiano yao na Russia na pia maslahi yao na Russia

View attachment 2142568

Mabepari mnaambiwa mbalance shobo

Haya Kiko wapi na waziri wenu
 

Alidhani akisema hivyo hatanyofolewa kwenye uwaziri mkuu
 
Bunge limeshamuondoa madarakani avumilie labda russia itamrudisha tena madarakani maana ni supa pawa kwa sasa baada ya US kuangushwa na urusi!!
 
Wazungu hawaamini kuwa vita ipo barani kwao...washenzi sana
 
Hivi Pakistan ni nchi ya kutolea mfano, huyu wangemshauri apambane na makundi ya kigaidi huko nchini kwake wala siyo kumwambia mambo ya Urusi.
Huelewi! Ungeelewa, usingesema ulichosema! Sijui kwa nini watanzania tunakurupuka sana kutoa majibu!
 
Kumekucha huko 🇲🇷🇲🇷🇲🇷 kibaraka wa Putin wamemng'oa .
 
Lakini kasema ukweli.
Yaani mtu unagombana nae wewe ila na Mimi unataka nigombane nae
Mfano wewe na mimi ni majirani tumegombana , harafu anatokea mtu anakuja nyumbani kwangu anakamata kipaza sauti anasema "TUSICHAGULIANE MARAFIKI " hivi utamuelewa mtu huyo?.
 
Sio kazi rahisi ki hivyo!!Urusi au china sio leo wala kesho kuwa taifa lenye ushawishi duniani kama ilivyo USA, kutokana na kutokuwa na sifa hizi, nguvu ya kiuchumi, ki siasa na ki utamaduni.
Nguvu za kiuchumi za USA zimetengenezwa kupitia hela yao USD na SKU control siasa za Nchi za Ulaya& Arabs.Ushawishi katika siasa za Asia unapungua siku hadi siku,kwenye uchumi baada ya hii vita tayari kuna mtikisiko tena mkubwa.

Kinachoendelea kumbeba in ushawishi wake katika siasa za Ulaya mashariki-kwa kutumia mgogngo wa Urusi kuwalaghai EU.Katika hili baada ya hii vita taa nyekundu imisha waka katika Nchi hizo.
 
Mbona msimamo wake wa kishujaa.Kwanini sasa ametolewa madarakani.Au athari ya propaganda za magharibi kama yaliyompata Gadafi baada ya kutoa hotuba UNGA ya kuIponda UN na kuibeza US.
 
Hapo umenena
 
Sawa siwezi kumchukia.si kaamua kuchagua upande anaotaka.?
Kwanini nimlazimishe awe upande wangu.
Mimi kuna watu nimegombana nao lakini kuna marafiki zangu wanaongea nao na sioni tatizo Wala kuwapangia.yaani usiongee na fulani kisa nimegombana nae.
Sio Sawa
Mfano wewe na mimi ni majirani tumegombana , harafu anatokea mtu anakuja nyumbani kwangu anakamata kipaza sauti anasema "TUSICHAGULIANE MARAFIKI " hivi utamuelewa mtu huyo?.
 
Kumekucha huko 🇲🇷🇲🇷🇲🇷 kibaraka wa Putin wamemng'oa .
Ni ujinga tu wa siasa za Pakistan ndio umekufanya kuelewa hivyo na kuona ajabu...

Pakistan sio Tanzania, Pakistani imekuwa na mawaziri wakuu 29 toka mwaka 1947, na kati ya hao wote hakuna hata mmoja aliyemaliza kipindi kamili cha uongozi wake (miaka 5)

Kuondoka kwa Imran Khan ofisini hakuifanyi Pakistan kuwa kibaraka wa Marekani...

Endelea kuwa mtumwa wa Marekani, we si waona heshima utumwa?!

 
Bunge limeshamuondoa madarakani avumilie labda russia itamrudisha tena madarakani maana ni supa pawa kwa sasa baada ya US kuangushwa na urusi!!
Ni ujinga tu wa siasa za Pakistan ndio umekufanya kuelewa hivyo na kuona ajabu...

Pakistan sio Tanzania, Pakistani imekuwa na mawaziri wakuu 29 toka mwaka 1947, na kati ya hao wote hakuna hata mmoja aliyemaliza kipindi kamili cha uongozi wake (miaka 5)

Kuondoka kwa Imran Khan ofisini hakuifanyi Pakistan kuwa mtumwa/kibaraka wa Marekani...

Endelea kufurahia utumwa (wa Marekani), sio ajabu kwa mtu mweusi kupenda utumwa...Imran Khan na wapakistani wote kwa ujumla hawana asili ya kupenda Utumwa
 
sorry mkuu unaweza kunipitisha kidogo historia ya taifa hili ? Maana nimeshangaa prime ministers 29 duu.
Tatizo nini hawa siasa zao .?
 
Hii nchi nguumu saana......na hawa jamaa ishu yao ilianza kabla hata ya mrusi kuvamia huko ukraine ila wengi wanafikiri ametolewa sababu ya kutounga mkono mambo ya mabepari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…