ruaharuaha
JF-Expert Member
- Feb 14, 2018
- 3,586
- 3,857
Wafanyabiashara Waarabu hawakubagua sana. Hujui habari za watumwa Wazungu waliopelekwa Unguja pia? Soma habari za Salme, mtoto wa Sultani aliyemzaa na mama mtumwa kutoka Kaukazi? Zamani zaidi walinunua watumwa huko Urusi, sababu moja kwamba lugha za Ulaya Mashariki zinaitwa "slavonic" (=kitumwa) hadi leo.
Nayajua yote hayo. Wazungu waliwachukua wengi, kama Wareno walinunua wengi tu kutoka kwa Waarabu wengi walipelekwa Brazil, Carribean. Lakini ni wengi zaidi walipelekwa Uarabuni, upande wa pili wa jangwa la sahara.
Kwa zaidi ya miaka 600 Waarabu walikuwa wakiwauza Watanganyika na weusi wengine. Ukiangalia hata sasa unaona kuna mchanganyiko South America, North America, Ulaya kidogo weusi wanapewa nafasi japo kiduchu.
Umeshawahi kuona wapi kiongozi mweusi Uarabuni, japo mamilioni walitumika kule kwa zaidi ya miaka mia sita. Pembe za ndovu, rasilimali na bara hili.
Kiuhalisia hakuna watu wabaguzi kama Waarabu hasa kwa mtu mweusi.