Mo afafanua ununuzi wake kwa Simba

Mo afafanua ununuzi wake kwa Simba

anachonunua ni hisa na ndio maana tunasema kwa kuwahi huenda amerahisisha mahesabu ya hisa lakini pia ilitakia ifahamike thamani yote ya simba kwa uyakini ndio tujue thamani ya kila hisa kama ni 500 au pungufu au zaidi na ndio maana linaitwa SOKO LA HISA kwa watu kununua hisa kulingana na uwezo wao kwa uelewa wangu

Unachosema ni sawa, ila kwa case ya Simba ni ngumu sana kiutekelezaji!

Ngoja tusubiri tuone wataalamu watakachoshauri, ila mimi kwa mtazamo wangu namwona Mo anataka kujimilikisha timu kijanja, yaani atoe hela bil 20 kuinunua timu halafu aje aiendeleze kwa kutumia bili 20 hiyo hiyo! Logic zinagoma hapo.
 
Mimi tatizo langu ni kwenye kununua au kuwekeza, mfumo ninaouona hapa ni wa kuwekeza ila Mo anatumia lugha ya kununua.

Kwa sababu kununua ni vile unatoa hela watu wanachukua hela wanakukabidhi timu, sasa kwenye kuiendesha inabidi utafute hela nyingine siyo utegemee ile uliyotumia kununulia timu.

Chukulia mfano huu; mimi nina nyumba, nikuuzie upande wa nyumba halafu kwenye ukarabati wa nyumba yote tutumie ile hela uliyonunulia upande wa nyumba, sasa huo ni ununuaji au ni uwekezaji?
Hehe...ni kununua kwa aina yake, kumbuka lilikuwa jengo kubwa mnalala watu wachache, anatoa hiyo pesa mnaitumia kulikarabati jengo na kuwa safi, mnampatia vile vyumba vingi ambavyo havikuwa vikitumika avitumie na nyie mnabaki na sehemu ndogo inayowatosha lakini kuta zikiwa hazipitishi nyoka na wala mvua ikinyesha hamlowi..ni faida.
 
Mkuu hili kuyumba kwa uchumi wa vilabu ni wimbi la dunia nzima si Simba tu.

Yanga wanasahau mapema hata Manji alishawahi kudokeza hili la Yanga Kampuni na Katiba yao ilipitishwa kwa nusu saa tu pale Police Mess ambapo Maniji alitaka 75% na 25% awanunulie Yanga hizo hisa

Kama tunafuatilia kwa makini, hamasa ya soka imeshuka duniani kote kutokana na mdororo wa kiuchumi na pengine njia mbadala kwa vilabu vingi kwa sasa ni kutegemea zaidi wazalishaji wa bidhaa za ndani kuwadhamini.

Roy Miller kutoka kitengo cha biashara ya michezo katika chuo kikuu cha Liverpool anasema kuwa hali kama hiyo haijawahi kuonekana kwa muda mrefu na ni ishara ya kwamba uchumi uko katika hali mbaya.

Wachambuzi wanaamini hata hivyo kuwa vilabu vikubwa kama vile mabingwa wa Uingereza Manchester United, Real Madrid na kadhalika siku zote zitaendelea kuwavutia wafadhili na washabiki wengi, lakini kwa vilabu vidogo hali ni tofauti.

Ligi kuu ya Uingereza ndiyo ligi yenye kuingiza fedha nyingi kabisa ambapo mwaka jana mapato yake yalifikia kiasi cha paundi billioni 1.5.Lakini ni vilabu vinane tu kati ya 20 vya ligi hiyo vinavyojiendesha kwa faida.

Maswali yameibuka juu ya majaaliwa ya udhamini wa kampuni ya kimarekani ya AIG kwa timu ya Manchester United wa dhamani ya paundi millioni 56.5 ambayo ni rekodi nchini Uingereza.Kampuni hiyo ya kimarekani imelazimika kuokolewa na serikali iliyonunua hisa kubwa za asilimia 80 baada ya kuwa katika hali mbaya ya kuelekea kuwa mufilisi.

Timu nyingine ya ligi kuu ya Uingereza ya West Ham Unitd hivi sasa haina udhamini katika jezi zao baada ya kampuni iliyokuwa ikiidhamini ya XL Leasure Group kufilisika.Nayo West Bromwich Albion iliyopanda daraja imeshindwa kupata ufadhili kufuatia kujiondoa kwa aliyokuwa mfadhili wake kampuni ya simu ya Ujerumani ya T-Mobile.

Newcastle United nayo ilikaribia kuwa katika hali hiyo baada ya mfadhili wake benki ya Northen Rock kuokolewa na serikali ya Uingereza kufilisika ambapo huko Italia timu ya Lazio kwa sasa inacheza bila ya kuwa mfadhili .

Hata hivyo kwa mujibu wa wachambuzi na watalaam wa masuala ya ufadhili katika michezo, timu kama Manchester Uinted haitopata shida kupata ufadhili mwengine iwapo serikali ya Marekani itaamua kuondoa ufadhili wake baada ya kuwa imechukua hisa kubwa katika kampuni ya AIG. Pippa Collet ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni inayohusika na ufadhili kwenye sekta ya michezo anasema kuwa udhamini katika kandanda kwa muda mrefu umekuwa ukipewa thamani kubwa kuliko inavyostahili, na kwamba hivi sasa kunafanyika marekebisho katika soko la udhamini.

Tanzania haipo kwenye kisiwa, unaona hata mfadhili wa hivi karibuni wa simba kwa kiasi kikubwa HZP amenza kuchoka kutumia fedha zake kusajili, ilihali hata idadi ya watazamaji imepungua sana, na mzalishanji wa bidhaa anayejitutumua kwa sasa ni Azam pekee kupitia udhamini wa TV yake

hakuna namna

nitaurid nikupe udadavuzi wa HISA ZA MO
West Bromwich albion wamepanda daraja gani kutoka daraja gani!!!???.....
 
Hehe...ni kununua kwa aina yake, kumbuka lilikuwa jengo kubwa mnalala watu wachache, anatoa hiyo pesa mnaitumia kulikarabati jengo na kuwa safi, mnampatia vile vyumba vingi ambavyo havikuwa vikitumika avitumie na nyie mnabaki na sehemu ndogo inayowatosha lakini kuta zikiwa hazipitishi nyoka na wala mvua ikinyesha hamlowi..ni faida.

Mkuu hii falsafa yako nimeielewa sana. Nadhani ndicho kinachoenda kutokea, ila sasa bora tungekubaliana kumpangisha tu kuliko kusema tumemuuzia.

Isije yakawa yale ya kwenye story ya Abunuwas, nyumba ina gorofa, ground floor ikauzwa, siku ya siku mmiliki wa ground floor akamwambia yule wa gorofani kwamba yeye anataka kubomoa nyumba yake, hivyo mwenye gorofa inabidi alishikirie
 
Mo alisema hiyo 20bil ataikopeshea serikali baada ya miaka kadhaa watavuna return ya hela ambayo itakayo tumika kujenga timu ikiwa pamoja na kujenga kiwanja etc...

Hizo hisa 49% zilizo baki ni za mashabiki na wapenzi wa simba hata wew unaweza kwenda kununua hzo hisa kama una hela!!
Mo alisema na siyo 'Simba ilisema'.
 
Mimi nina maswali wadau mnisaidie:-

1. Simba ni ya nani? Nani anaiuza? Na atapata faida kiasi gani kwenye huo mchakato?

2. (Hili linaendana na nilo la 1), ikishatolewa hiyo 20bil, hela za kuiendesha timu zitatoka humo humo au hizo zinakuwa ni za manunuzi tu, hivyo mmiliki atakuja na hela nyingine ya kuendeshea timu?

3. Tumeambiwa 20bil ni kwa asilimia 51, je hiyo 49% inayobaki nani atamiliki? Atatoa hela equivalent au hizo share zitakazobaki zitakuwa na thamani tofauti?

4. (Hili linaendana na nilo la 3), ikitokea wanunuzi wakakosekana hisa zitakazobaki zitaenda wapi? Na mmiliki atabaki Mo peke yake?
Na MO akishachukua 51% yeye ndo mwenye maamuzi ya vikao.
49% haiwezi kuilazimisha jambo 51%.
Kwa hiyo swala la hata nani atapata share ya hizo 49% ataamua MO isipokuwa pale tu maamuzi yatafanyika kabla ya kumkabidhi MO na iwe sehemu ya mkataba wa makabidhiano
 
Unachosema ni sawa, ila kwa case ya Simba ni ngumu sana kiutekelezaji!

Ngoja tusubiri tuone wataalamu watakachoshauri, ila mimi kwa mtazamo wangu namwona Mo anataka kujimilikisha timu kijanja, yaani atoe hela bil 20 kuinunua timu halafu aje aiendeleze kwa kutumia bili 20 hiyo hiyo! Logic zinagoma hapo.

Precisely....kimsingi hiyo ndiyo position yangu...na hapo ndipo umakini wa wanasimba unatakiwa kuwepo

Hii timu ina historia yake ...kumpa tu mtu mmoja hivi bila utaratibu makini ni hatari

Hii kazi ingefanywa na professional firm ya sharia katika kushauri structure nzuri
 
Kuna hicho kipande nime-quote inanipa picha kwamba jamaa siyo kwamba anataka kuinunua Simba bali anataka kuwekeza na aweze ku-control matumizi ya hela anayoinvest!

Kwa sababu kama ni kununua ilitakiwa hiyo hela wapewe wauzaji, yeye akishakuja aje na hela yake ya kuendeshea timu ile aliyonunulia asiitegemee tena, inakuwa kama unanunua nyumba halafu hela hiyo hiyo ndo unaitumia kwenye ukarabati.
Unafahamu biashara za vilabu zilivyo?
 
Hapana mkuu, leta ufafanuzi ndugu.
Pitia kidogo tu katika vilabu vichache hapa duniani vilivyonunuliwa na mchakato wa ununuaji ulivyokuwa.

Tuna hofu tu ambayo kimsingi mwezi mmoja au hata chini ya hapo kila kitu kinashughulikiwa vizuri na club inaendeshwa kisasa.

Simba haiwezi kuja kukaa vizuri tena,wafadhili nao hali zao za kiuchumi zimeyumba.Inaendeshwa kwa hasara na bado fedha zinaliwa sana hapo Simba...

Watanzania sijui nani katuloga kila kitu ni mashaka mashaka tu....wakati unachotakiwa ni kutathmini mali zako,kuweka vigezo na masharti then mnasonga mbele.Kuna makampuni yanaweza kukufanyia yote hayo maana inaelekea hatuna wataalam au hatutaki kuwatumia.

Katika hili,vigezo vikitengenezwa vyema wala hakuna cha kuhofia.

Wewe unauliza fedha atapewa nani...pitia masuala kidogo ya mambo ya share na hisa.
 
Pitia kidogo tu katika vilabu vichache hapa duniani vilivyonunuliwa na mchakato wa ununuaji ulivyokuwa.

Tuna hofu tu ambayo kimsingi mwezi mmoja au hata chini ya hapo kila kitu kinashughulikiwa vizuri na club inaendeshwa kisasa.

Simba haiwezi kuja kukaa vizuri tena,wafadhili nao hali zao za kiuchumi zimeyumba.Inaendeshwa kwa hasara na bado fedha zinaliwa sana hapo Simba...

Watanzania sijui nani katuloga kila kitu ni mashaka mashaka tu....wakati unachotakiwa ni kutathmini mali zako,kuweka vigezo na masharti then mnasonga mbele.Kuna makampuni yanaweza kukufanyia yote hayo maana inaelekea hatuna wataalam au hatutaki kuwatumia.

Katika hili,vigezo vikitengenezwa vyema wala hakuna cha kuhofia.

Wewe unauliza fedha atapewa nani...pitia masuala kidogo ya mambo ya share na hisa.
Ungempa huo mfano kungekuwa na tatizo!!!???
 
Kwa mifumo iliyopo ya hizi timu za Simba na Yanga, Mo anakuwa anakosea kuweka hizo fedha katika timu ya Simba.

Hizi timu nina matatizo ya muundo na mfumo.

Yanga ilijaribu wakati wa katibu mkuu wake marehemu George Mpondela alipopendekeza suala la kuigeuza Yanga kuwa kampuni na akashindwa.

Hizi timu ni kubwa na zina rasilimali na watu wa kutosha kuzifanya ziwe timu imara na zinazojendesha kibiashara kwa ufanisi unaotakiwa.

Wazo la Mo Dewji ni zuri lakini ni vema akaanzia chini asuke timu yake kama walivyoanza Bakhresa kwa Azam au awekeze kwenye timu ingine ndogo kama Kariakoo ya Lindi au aazishe na kuwekeza katika timu mpya kabisa "Brand new" tena ilaleta ahueni kimaisha na kimaendeleo akifanya hivyo huko kwao Singida.
 
Pitia kidogo tu katika vilabu vichache hapa duniani vilivyonunuliwa na mchakato wa ununuaji ulivyokuwa.

Tuna hofu tu ambayo kimsingi mwezi mmoja au hata chini ya hapo kila kitu kinashughulikiwa vizuri na club inaendeshwa kisasa.

Simba haiwezi kuja kukaa vizuri tena,wafadhili nao hali zao za kiuchumi zimeyumba.Inaendeshwa kwa hasara na bado fedha zinaliwa sana hapo Simba...

Watanzania sijui nani katuloga kila kitu ni mashaka mashaka tu....wakati unachotakiwa ni kutathmini mali zako,kuweka vigezo na masharti then mnasonga mbele.Kuna makampuni yanaweza kukufanyia yote hayo maana inaelekea hatuna wataalam au hatutaki kuwatumia.

Katika hili,vigezo vikitengenezwa vyema wala hakuna cha kuhofia.

Wewe unauliza fedha atapewa nani...pitia masuala kidogo ya mambo ya share na hisa.

Mkuu umeniacha ulivyonikuta!

Yaani maana yake ni kwamba sijaelewa kama nimejibiwa au labda nimejibiwa sijaelewa.
 
Mkuu hii falsafa yako nimeielewa sana. Nadhani ndicho kinachoenda kutokea, ila sasa bora tungekubaliana kumpangisha tu kuliko kusema tumemuuzia.

Isije yakawa yale ya kwenye story ya Abunuwas, nyumba ina gorofa, ground floor ikauzwa, siku ya siku mmiliki wa ground floor akamwambia yule wa gorofani kwamba yeye anataka kubomoa nyumba yake, hivyo mwenye gorofa inabidi alishikirie
Hahahahaa...nimecheka kwa sauti mpaka watu wamenishangaa.
 
Cha msingi Mo apewe tu timu, tumeshachoka kufungwa sisi nawashangaa sana mashabiki wanaopiga domo jamaa asipewe timu, mtakua wanasimba uchwara nyie
 
Mimi nina maswali wadau mnisaidie:-

1. Simba ni ya nani? Nani anaiuza? Na atapata faida kiasi gani kwenye huo mchakato?

2. (Hili linaendana na nilo la 1), ikishatolewa hiyo 20bil, hela za kuiendesha timu zitatoka humo humo au hizo zinakuwa ni za manunuzi tu, hivyo mmiliki atakuja na hela nyingine ya kuendeshea timu?

3. Tumeambiwa 20bil ni kwa asilimia 51, je hiyo 49% inayobaki nani atamiliki? Atatoa hela equivalent au hizo share zitakazobaki zitakuwa na thamani tofauti?

4. (Hili linaendana na nilo la 3), ikitokea wanunuzi wakakosekana hisa zitakazobaki zitaenda wapi? Na mmiliki atabaki Mo peke yake?

Majibu

1. Simba ya wanachama wa Simba. Hii club inamilikiwa katika zama za Mwl wetu JK Nyerere japo tupo kwenye digial world. Anayeuza ni wanachama wa Simba ambao wao ndio wamiliki. Faida atakayopa itaonekana baada ya mahesabu ya mwaka kufanyika

2. Hio 20bln ni kununua maamuzi yaani kumiliki Simba kwa 51%. Kwa maneo mengine kuiendesha na kuisimamia Simba iwe kwa kutumia hizo 20bln pamoja na hela zingine na Assets zingine Simba walizonazo

3 & 4. 49% wanaendelea kumiliki wanachama wa Simba. Hizo hisa so far bado wanamiliki wanachama, lkn baadaye wakiamua kuuza watajua wenyewe huko. Ila kitakachobadilika kikubwa sana ni kuwa Mo ndio mwenye last say kama Ibra alivyo Chelsea. Akiamua kula sahani moja na Kocha anakula, na wanachama hawatakiwi kufungua mdomo.

Akiamua mchezaji fulani asisajiliwe ndo inakuwa hivyo na wanachama wanatakiwa ku shut up!
 
Kuna hicho kipande nime-quote inanipa picha kwamba jamaa siyo kwamba anataka kuinunua Simba bali anataka kuwekeza na aweze ku-control matumizi ya hela anayoinvest!

Kwa sababu kama ni kununua ilitakiwa hiyo hela wapewe wauzaji, yeye akishakuja aje na hela yake ya kuendeshea timu ile aliyonunulia asiitegemee tena, inakuwa kama unanunua nyumba halafu hela hiyo hiyo ndo unaitumia kwenye ukarabati.
Mkuu umeongea ukweli mtupu na jamaa anatumia matatizo ya simba kumilliki kiulaini kwasababu simba ina madeni,uongozi mbovu ambao ushachokwa na wanachama na wapenzi na kukosa ubingwa miaka minne mfululizo ndio maana mo anatumia iyo advantage
 
Kwa mifumo iliyopo ya hizi timu za Simba na Yanga, Mo anakuwa anakosea kuweka hizo fedha katika timu ya Simba.

Hizi timu nina matatizo ya muundo na mfumo.

Inaonekana huelewi hata unachokisema

Simba wameshaona hayo matatizo ya Muundo na Mfumo ndio maana wameamua kuubadilisha

Na mfumo waliochagua Simba ni sahihi sana kwenda kwa kipindi hiki na ni mfuo unatumika na klabu zote zilizofanikiwa duniani na Africa

Tunachosema sisi....Ni Transformation hii ifanyike ki utaalamu sana ....Na kwa umakini mkubwa

Ila ishu kama tubadili mfumo au la...simba tumeshaaamua kuubadili huo mfumo
 
Mkuu umeongea ukweli mtupu na jamaa anatumia matatizo ya simba kumilliki kiulaini kwasababu simba ina madeni,uongozi mbovu ambao ushachokwa na wanachama na wapenzi na kukosa ubingwa miaka minne mfululizo ndio maana mo anatumia iyo advantage

However,...hata kama akitumia hiyo advantage...its not a problem so far

Timu ibadilishe mfumo iwe kampuni.......

Katika hiyo miaka yote 80 Timu ilikuwa na hela? na ilifanya nini? Mpira wa sasa sio wa ujanja ujanja kama simba na yanga za miaka 80 iliyopita
 
Back
Top Bottom