rodrick alexander
JF-Expert Member
- Feb 12, 2012
- 16,784
- 23,312
Utakuwa umeandikiwa mahali na mumeo, wewe ukaamua kunakili na kuhamishia humu. Una ushahidi wa mimi kuongea huo ushuzi ulioandika? Kwanza yeye Omog ni nani mpaka asitimuliwe? Wamefukuzwa makocha bora duniani, itakuwa yeye?! Kama aliyekuajiri hajaridhika na utendaji wako anakutimua muda wowote bila kujali kelele za yeypte yule. Alaf we unaleta habari za kununua mechi yanga, kuna mtu kaiongelea yanga hapa? Au ndio kujishtukia?Nyie ndio mliokuwa mnadai Yanga ananunua mechi,malinzi na mwesiga wanawahujumu!mikia kila kukicha mnakuja na sbb mpya
Asee, hao watu wameniudhi sana. Wafukuzwe au wapigwe adhabu kali ili wajue madhara ya ujinga waliofanya. Shabalala unaenda kupiga penati ya mwisho kisha unampa kipa anadaka kama mpira wa netball? Hovyo sana yule dogo.Wanamuonea angefukuzwa mkude na yule shabalala washenzi sana
Aende tu. Na Simba isiishie kwa kocha pekee. Uwekwe mfumo wa kutrack wachezaji na kuwapa "approval rate" kwa kuangalia namna alivyojituma uwanjani. Akipata rate ndogo au ikionekana amecheza chini ya matarajio akatwe sehemu ya mshahara wake. Hii ndio itaondoa ugoigoi wa wachezaji. Zama za kufungwa kijinga halafu kusema ndio mchezo utadhani mechi za chandimu ikome ndani ya Simba.Aende tu, kwanza watanzania hakuna tunachokijua wala hatukijui tunachokitaka kwenye michezo. Angebaki hadi mwisho wa msimu, halafu akatoka patupu. Yangekuja majitu hapa na "mathread" yao hapa "oooh tuliwaambia hapa Omog sio kocha!" Afadhali ametupisha, huyo mgeni hata akifeli atakuwa na kisingizio cha ugeni. Yaani watu tunashuhudia mechi kibao tu za ligi, timu inacheza ugoro tu, morali iko chini alafu mwalimu upo tu!! Na umeshindwa kurekebisha hadi mzunguko wa kwanza karibia unaisha upo tu! Baadae unakuja kufungwa na timu isioeleweka, uendeleee kuachwa tu?! Kunyangisi!! Haiwezekani... Ila asisahau tu kufikisha salamu kwa ndugu Jama Mba!!
Achana na mnyama. Kule Jangwani mnakoendeshwa kisanyansi kuna nini cha maana?Ila simba ni litimu linalo endeshwa kienyeji enyeji sana, ingawa mimi ni mshabiki wa yanga, nimesikitishwa sana na matusi ya hanzpopo aliyowatukana wachezaji, timu ya simba ilikuwa imeanza kuimarika vizuri ila matusi na comments za vile zina demoralize spirit ya wachezaji, kwa kufungwa mechi 1 tena kwa bahati viongozi wanapoteza imani kwa wachezaji? Hapana something iz wrong, na kwa stahili mpira wetu hauwezi kuendelea
Niyonzima,Boko,Mavugo...Sure mkuu. Pale Simba tuna ' mizigo ' tu.
Yani unapewa stahiki zako zote halafu ndo wanacheza utumbo vile?! Foolish.!
Heri wewe mnazi wa Jangwani umenena vizuri. Siyo wengine mapovu yanawatoka utafikiri Simba SC ndo timu ya kwanza kufukuza kochaMpeni chake asepe.
Umesahau cha FA!!!?Inatosha aisee! Hana mbinu mpya kwa wachezaji waliopo. Anapanga kwa kukariri. Zidane amebeba makombe matano lakini atatolewa mkuku. Omog hana hata kikombe cha kahawa alaf avumiliwe! Utakuwa uzwazwa huo.
kocha sio busara kymuobdoa kwa matokeo ya mechi mojaWakati zimebaki siku chache tuumalize mwaka sinema mpya imeanza kule msimbazi.. Na hii ni kutokana na ukweli kwamba matokeoya aibu ya jana dhidi ya timu ya daraja la pili ya Grean warrios ambapo simba licha ya kuingiza wachezaji wao wakubwa waliambulia vilio.. Cha ajabu leo kumezuka mtifuano wa mawazo baina ya washabiki baada ya press ya manara ambae ni msemaji wa simba kutangaza wamevunja mkataba na kocha wao huyo omog.. Je ukiachana na suala la matokeo ya jana kuna lingine linalomuondoa omog simba ??