Mo Dewji amshauri Kocha Omog aachie ngazi, Simba yavunja naye Mkataba

Mo Dewji amshauri Kocha Omog aachie ngazi, Simba yavunja naye Mkataba

Haji Manara alicho post jana sicho kizuri kwa kocha na tazama na kwa hili la Mo sijui Omog yupo kwenye hali gani sasa
 
Wakati zimebaki siku chache tuumalize mwaka sinema mpya imeanza kule msimbazi.. Na hii ni kutokana na ukweli kwamba matokeoya aibu ya jana dhidi ya timu ya daraja la pili ya Grean warrios ambapo simba licha ya kuingiza wachezaji wao wakubwa waliambulia vilio.. Cha ajabu leo kumezuka mtifuano wa mawazo baina ya washabiki baada ya press ya manara ambae ni msemaji wa simba kutangaza wamevunja mkataba na kocha wao huyo omog.. Je ukiachana na suala la matokeo ya jana kuna lingine linalomuondoa omog simba ??
 
twitt ya mwenye simba... ilikuwa ina nguvu kuliko hisa za wanachama...! "sijakabiziwa simba ila kwa busara ni bora kocha aiache timu, mimi kama mwanachama...." hii twitt mzee ilikuwa ina kitu ndani yake... angekabidhiwa tungeona mambo ya wamiliki wa chelsea wanatumia pesa zao kufukuza na kununua...
 
  • Thanks
Reactions: Lee
c2895081d5df660e391e37410a250191.jpg

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI*
*_____________________________________*
Klabu ya Simba na kocha wake mkuu Joseph Omog, wameamua kwa pamoja kuvunja mkataba baina yao kwa makubaliano maalum yanayozingatia maslahi ya pande zote mbili.
Klabu inamshukuru kocha Omog na inamtakia kila la kheri kwenye maisha yake nje ya Simba.

Kwa wakati huu Timu yetu itakuwa chini ya kocha msaidizi Masoud Djuma na itaendelea na mazoezi kesho,na kupumzika siku ya Jumatatu kwa mapumziko ya sikukuu ya Christmas na itaingia kambini Jumanne kabla ya safari ya Mtwara,ambapo tutacheza na Timu ya Ndanda kwenye mchezo wa Ligi kuu wiki ijayo.

Pia kwa niaba ya uongozi, benchi la ufundi na wachezaji.tutumie nafasi hii kuwaomba radhi sana Wanachama na washabiki wetu kwa matokeo ya jana, sote tumeumia ila ndio mchezo wa mpira ulivyo, na tuwaombe muwe watulivu katika kipindi hiki ili tufikie malengo yetu. *Mwisho*
klabu inawatakia nyote Sikukuu njema ya Noeli na mapumziko mema ya wikiendi.
IMETOLEWA NA.... *Haji S MANARA*
Mkuu wa Habari Simba Sc

*SIMBA NGUVU MOJA*

Wamemuonea
 
Naona nyota njema ya mikia kuukosa ubingwa
 
Mo kama anataka mafanikio hapo Simba anapaswa afukuze pia viongozi wote akianza na Manara na Makofia! Atafute watu wengine watakaomsaidia kuendesha timu! Pole Omog
 
Omog sio kocha bora aende kwanzacwalichelewa kumtimua huyu mganga Wa kienyeji
 
Sio omog tu hadi viongozi wa mbwa koko Sc muwaondòe...hiýo timu kiđomo domo ndo kimewaponza na bado
 
Back
Top Bottom