Mfanyabiashara Mohammed Dewji 'MO' amesema ataifanya Simba kuwa klabu kubwa barani Afrika kwakua na viwanja viwili vya kisasa kimoja nyasi halisi na kingine za bandia kufuatia kushinda zabuni na kuwekeza hisa za zenye thamani ya sh billioni 20.
Mo amesema baada ya kufanikiwa kushinda zabuni hiyo anaenda kufanya mabadiliko makubwa na kuifanya timu hiyo kuwa ya kimataifa kwa kuijengea hostel za kisasa zenye vyumba 35, Mgahawa mkubwa wa kisasa, Gym yenye vifaa maalum vya wachezaji pamoja na Swimming Pool.
Mbali na hivyo Mo amesema pia wataanzisha kituo kikubwa cha kukuzia vipaji barani Afrika ili kusaidia kupatikana kwa wachezaji bora ambao watakuwa msaada kwa timu na taifa kwa ujumla.
Mo amesema kwa sasa Simba itakuwa haishindani na timu za nyumbani pekee bali na miamba ya Afrika kama TP Mazembe, Zamalek, Esparance kuwania mataji makubwa.
"Simba inaenda kuwa timu ya kisasa tutasajiri wachezaji bora wenye uwezo mkubwa, tutaboresha benchi la ufundi na miundombinu mizuri kama viwanja, hostel na mishahara mizuri kwa wachezaji wetu," alisema Mo.
Kwa sasa klabu ya Simba itakuwa katika kipindi cha mpito kabla ya mfumo huo kukamilika ambao unaweza kuchukua hadi miezi sita.
Source: SDF SPORTS