Modus operandi ya Rais Magufuli ni ya ajabu!

Modus operandi ya Rais Magufuli ni ya ajabu!

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Utendaji kazi wa Rais Magufuli ni wa ajabu kweli.

Au naweza kusema ni ambao haufuati desturi ama kawaida ya utendaji wa mambo. Ni unorthodox, kwa kimombo 😜.

Hivyo ndivyo ninavyoweza kuuelezea kwa kifupi.

Fuatana nami nikuelezee kwa nini nasema hivyo;

Nimeangalia video fupi ya hotuba aliyoitoa Dkt. Bashiru mara baada ya kuapishwa kwenye hiyo nafasi yake mpya hapo jana.

Katika hotuba yake hiyo ambayo aliitoa bila kusoma, Dkt. Bashiru alisema kuwa jioni ya siku ile aliyoteuliwa, alikuwa yupo sehemu [nahisi labda alikuwa nyumbani kwake] akisoma mafaili ya kazi zake za ukatibu mkuu wa CCM, ndo eti akapata taarifa kupitia kwenye mitandao [ya kijamii] kwamba kateuliwa kuwa katibu mkuu kiongozi.

Huyu hapa Dkt. Bashiru kwa maneno yake mwenyewe:
Kwa kuokoa muda, anzia dakika ya 2:30 hadi 2:50.



Maneno hayo ya Bashiru yaliuvuta uangalifu wangu na kunifanya niwaze kidogo maana kama kumbukumbu yangu ni nzuri, hii si mara ya kwanza kwa mtu aliyeteuliwa na Rais Magufuli, kuujua uteuzi wake huo kupitia mitandao ya kijamii.

Kwa akili zangu hizi za kidato cha 4, mimi huwa nadhani kuwa Rais kabla hajamteua mtu kushika wadhifa au nafasi flani, Rais huongea na huyo mtu kwanza ili kuona kama huyo mtu yuko tayari kuyabeba majukumu ya kazi atakayo kumpa, na kuhakikisha kwamba huyo mtu anaukubali uteuzi huo kabla ya umma kufahamishwa.

Sasa kama Dkt. Bashiru alizipata taarifa za uteuzi wake huo kupitia kwenye mitandao kama tulivyozipata sisi wengine, ina maana hakukuwepo na mawasiliano kati ya mamlaka ya uteuzi na mteuliwa.

Kama hivi ndivyo ilivyo kwa utendaji wa Rais Magufuli, basi daah, sijui nisemeje tu.

Utateuaje mtu, tena wa cheo kilicho nyeti, halafu mtu huyo aujulie uteuzi huo kupitia mtandaoni?

The guy is cocking a snook at just about everything....norms, traditions, common sense, comity, presidential comportment, you name it!

Man oh man.
 
Siyo lazima ukiteuliwa upewe taarifa. Hizo ni hisia zako. Narudia: siyo LAZIMA
Ni lazima. Narudia ni lazima. Na inawezekana alifahamu kuwa anaweza teuliwa ila huenda taarifa ilikuwa sio rasmi kutoka kwa wanausalama hivyo hakuwa na uhakika. Lazima ujiandae kuwa kuna mabadiliko yanakuja kwenye maisha yako na kazi zako.


SISI SIO NG'OMBE KUWA MCHUNGAJI AKIAMUA KUKUSWAGA POPOTE UNAENDA. TUNA RATIBA PERSONAL, MAJUKUMU YA KITAIFA NA MIPANGO YA KIFAMILIA. HUWEZI KUJA TU UKAAMBIWA SS KUANZIA KESHO WW NI MBUNGE ACHA SHUGHULI ZAKO NENDA BUNGENI.
 
Na anawafukuza hivyo hivyo..
Kuna thread niliandika hapa hadi jumapili au siku za sikukuu usiku wa manane..anafukuza na kuteua...

Watu wanakula sikukuu na familia zao wanashangaa habari ziko social media wameteuliwa au washafukuzwa
 
Tangu miaka hiyo, kila mmoja atakuambia "nilikuwa sifahamu. Nimesikia tu redioni kwamba nimeteuliwa". Kwahiyo hakuna jipya hapo!! Sina hakika kama huwa wanasema kweli lakini majority kauli zao huwa zinafanana kuhusu ikiwa walifahamu ama la. Utawasikia "habari za uteuzi wangu nilizisikia tu redion/kwenye tv, au mtu alinipigia simu kuniambia rais kaniteua"!
 
Tatizo hili limeongelewa sana .

Nadhani bado upo nyuma sana na maigizo ya nchi hii , mfano wa corona tu ni jibu tosha!! Hao wote wawili wameongea kabla ya yote ya mbele .
Anateuaga watu bila kuwataarifu?
 
Kamba zake hamjazizoea tu? Season one aliahidi kutokukubali teuzi nyingine na safari hii anataka kutuaminisha kuwa wengi wetu hatujui taratibu za uteuzi wa watumishi serikalini
 
na kutenguliwa ndio hivyo hivyo bila taarifa, jamaa anafanya mambo kwa jinsi anavyojisikia, hafuati sheria
 
Kawaida ya "mitume"..... yule aliyekuwa na wanafunzi 12, si unakumbuka wengi alikuwa anawaambia tu "nifuate" na wanamfuata?

Hivi Kangi Lugola yupo wapi siku hizi?
 
Utendaji kazi wa Rais Magufuli ni wa ajabu kweli.

Au naweza kusema ni ambao haufuati desturi ama kawaida ya utendaji wa mambo. Ni unorthodox, kwa kimombo 😜.

Hivyo ndivyo ninavyoweza kuuelezea kwa kifupi.

Fuatana nami nikuelezee kwa nini nasema hivyo;

Nimeangalia video fupi ya hotuba aliyoitoa Dkt. Bashiru mara baada ya kuapishwa kwenye hiyo nafasi yake mpya hapo jana.

Katika hotuba yake hiyo ambayo aliitoa bila kusoma, Dkt. Bashiru alisema kuwa jioni ya siku ile aliyoteuliwa, alikuwa yupo sehemu [nahisi labda alikuwa nyumbani kwake] akisoma mafaili ya kazi zake za ukatibu mkuu wa CCM, ndo eti akapata taarifa kupitia kwenye mitandao [ya kijamii] kwamba kateuliwa kuwa katibu mkuu kiongozi.

Huyu hapa Dkt. Bashiru kwa maneno yake mwenyewe:
Kwa kuokoa muda, anzia dakika ya 2:30 hadi 2:50.


Maneno hayo ya Bashiru yaliuvuta uangalifu wangu na kunifanya niwaze kidogo maana kama kumbukumbu yangu ni nzuri, hii si mara ya kwanza kwa mtu aliyeteuliwa na Rais Magufuli, kuujua uteuzi wake huo kupitia mitandao ya kijamii.

Kwa akili zangu hizi za kidato cha 4, mimi huwa nadhani kuwa Rais kabla hajamteua mtu kushika wadhifa au nafasi flani, Rais huongea na huyo mtu kwanza ili kuona kama huyo mtu yuko tayari kuyabeba majukumu ya kazi atakayo kumpa, na kuhakikisha kwamba huyo mtu anaukubali uteuzi huo kabla ya umma kufahamishwa.

Sasa kama Dkt. Bashiru alizipata taarifa za uteuzi wake huo kupitia kwenye mitandao kama tulivyozipata sisi wengine, ina maana hakukuwepo na mawasiliano kati ya mamlaka ya uteuzi na mteuliwa.

Kama hivi ndivyo ilivyo kwa utendaji wa Rais Magufuli, basi daah...sijui nisemeje tu...

Utateuaje mtu, tena wa cheo kilicho nyeti, halafu mtu huyo aujulie uteuzi huo kupitia mtandaoni??

The guy is cocking a snook at just about everything...norms, traditions, common sense, comity, presidential comportment, you name it!

Man oh man...

Matatizo ya nchi yetu na nchi nyingi za kiafrika ni kuendelea kutenda kama colonisers wetu walivyo tuelekeza! Ambayo tunaiita awe na experience! Akitokea kiongozi anayetenda kwa kutumia njia zake za kufanikisha jambo kwa haraka - tunakuwa wa kwanza kumuona hafai - kwasababu experience yetu amei side step! Bashiru amekuwa akifanya kazi kwa karibu sana na Magufuli, hilo ni jawabu tosha na mengine ni mazungumzo baada ya habari (yale ya hakujulishwa)! Hata kama hakujulishwa, anajua!
Mfano mwingine wewe mleta mada, naukubali uandishi wako sana, unavyowasilisha arguments zako n.k. Kama nikiambiwa kuteua mtu wa kufanya uandishi kwenye maswala haya unayokuwa unachangia, nitakupendekeza! Ukikataa, hilo swala jingine. Ila mimi naona unafaa. Baada ya kusema hayo, vyeo hivi vinakuwa vetted for, siyo for any Masanja and Marwa!
 
Hii inatokana na desturi ya kumtetemekea sn rais kisha njaa. MTU mwenye mahela yake humkurupushi maana unajua anaweza kataa ukadhalilika.
Kimsingi huwa anafukuza na kuteua ghafla hataki taarifa zivuje kwamba flani anakuwa flani ameathitika na zama zamkwere siri za sirikali kuvuja mapema.
Yote sawa alimradi viongozi wananyenyekea
 
Back
Top Bottom