Mohamed Dewji (MO) aliyepotea, apatikana. Amerudi nyumbani akiwa salama

Nanukuu ''Gari lile lile lilomteka ndo limemrudisha Mo''
Kwahiyo gari la surf bado linatamba hapa mjini.??

Na je limeludi toka nchi jirani liliko enda bila kujulikana ? maana yake mipaka ya nchi iko wazi tuuu.
 
Hilo ni wazo lako. Lakini mimi bado nasubiri MO atulize akili na atoe kilichomsibu. Nitasikiliza kutoka kwake kwani tukio kama hili akidanganya atakuwa anajidanganya mwenyewe. Ila nachojua kwa sasa yeye ameishukuru serikali mnayoituhumu ninyi.

Bila shaka pale Gymkhana unapajua, pia Colosseum hotel unapajua. Unataka kuniambia hao watekaji wananguvu ya kuteka mtu Oysterbay au Masaki na kumrudisha mtu mpaka pale Gymkhana bila hofu kabisa tena polisi na vyombo vya usalama viko kwenye tension ya kuwatafuta watekaji. Hii kidogo inaumiza kichwa na ile kauli ya Waziri na IGP kwamba nchi iko salama waifute mara moja maana haiwezekani tukawa salama huku kuna watu wanateka mtu maarufu sehemu sensitive na kumrudisha sehemu sensitive pia kiulinzi.
 
....ana biashara nyingi hapa mjini mtawala aliepo anapenda kuabudiwa kwa kila jambo hata kama lakijinga so kumtaja haimaanishi kuna msaada wowote aliopata maana tangu atekwe hata kukemea kashindwa unamshukuru kwa lipi MO amefanya namna hiyo kwaajili ya biashara zake
Kauli ya kumshukuru tu mheshimiwa rais mm ndo inanipa shida sana aisee,

Kwann amshukuru rais? Wakati watekaji walimchukua na wamemwachia bila nguvu yeyote kutumika

Shukrani kwa raisi ni za nn hasa?
 
Kwa hali ya kawaida Mo angeshikiliwa na Polisi ili kusaidia Polisi kukamilisha uchunguzi wao na sio anajitokeza nyumbani halafu watu tunakubali hali hiyo kirahisirahisi. Kumbuka Mondo yeye alipelekwa Polisi, alishikiliwa mpaka akakoma, na alifunguliwa mashitaka na kusimamishwa masomo. Sasa Polisi mbona hachukui hatua za kujiridhusha kama Mo alijiteka ama hapana? Si wamshikilie, wasimamishe biashara zake na wampeleke mahakani kama walivyofanya kwa Nondo?
 
Wenda wanadhani hata siye wa Kolomje wataweza kutudanganya Kuwa Kariakoo ipo pembezon mwa Mbuga ya Mikumi

Na tutakubali bila kutafiti hatat kidogo.


Nilikuwa sijawahi kulisikia na sikujua hilo eneo(Gymkhana) lilipo.

Baada ya kupata taarifa hizi nikaingia gopgle map kuona lililopo, nikabakia mdomo wazi....
 
Unaweza ukaipenda timu fulani lakini kila siku inakuangusha kwa kufungwa na kutumia formation mbovu. Kuna watu wanashindwa kucheza karata zao vizuri.
 
Chadema wamechukizwa mno na kupatikana kwa Mo maana kiki yao imebuna.

Shida na Matatizo yanayoipata Tanzania ndiyo ufahari wa Chadema!
huna akili wewe unaiunganishaje chadema na mambo ya kipuuzi kama haya! kwamba katekwa na chadema? mbona huhoji kwann mambo saba anamshukuru raisi kwani raisi ni polisi? japo uliiba mitihani yako lakini kuwa na akili japo za kizaliwa mkuu! ipo siku utatoka na mavi chooni ukiulizwa utasema chama ni chadema
 
Kiukweli mkuu bado tumelala, siku tukiamka dunia itakuwa imeisha

Nawakumbusha tena Mungu hana urafiki na wanafiki.
 
Hivi kulikua na haja gani ya kumshukuru Raisi wakati hajafanya kitu chochote kile wala hata kuonesha kukerwa hata kuifairji familia yake yani hata jeshi la polisi ila ukiangalia video jamaa anaonekana hakua comfortable kabisa
Hata mm nimejiuliza hivyo
 
Familia ya Mo Dewji na Mo mwenyewe wanarudiarudia sana "kumshukuru" Magufuli kwa kupatikana kwa Mo...hivi kwa kumbukumbu tu, Magufuli amefanya kitu gani hasa kusaidia kupatikana kwa Mo? Au ndo namna yao ya kutueleza kuwa hatma ya uhai wa Mo ilitegemea hasa HISANI ya Rais?
 
Sisi wote ni sisiemu. Tunajuana. Shupaza shingo ukweli ni huo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…