Mohamed Said ''Mzungu wa Unga,'' 2007 Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere

Mohamed Said ''Mzungu wa Unga,'' 2007 Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere

Mabesela,
In Shaa Allah nitaweka kidogo kidogo...
Nilitegemea wataweka ahadi yao kuwa ikiwa hawatakuta madawa ya kulevya katika mizigo yangu watanirejeshea uhuru wangu wataniachia niende nyumbani. Haikuwa hivyo. Wakanirudisha ofisini kwao. Sasa wakaacha madawa ya kulevya wakahamia katika vitabu na “audio cassette” nilizokuwa nimepewa kama zawadi kule Tehran wakaniluliza kwa nini naingiza vitu vile khasa kanda za Khomeni na vitabu vyake nchini. Nikawauliza, “Kwani kanda na vitabu vya Khomeni haviruhusiwi kuingizwa Tanzania? Maana mimi hata nyumbani kwangu hii leo mkifika nina vitabu vya Khomeni na wanafalsafa wengine kama Karl Marx ambao nimesomeshwa pale Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam. Sasa hapo ikaja kejeli. “Ala wewe mtu wa Kariakoo lakini umefika hadi Chuo Kikuu!” Sikujibu kitu. Awali waliponitia mbaroni waliniuliza kwetu na nikawaeleza kuwa nimezaliwa Kariakoo.

Hawakunipa jibu kuhusu kuingiza vitabu na cassette za Khomeni. Ikawa sasa kama vile wameishiwa maswali. Nikaona kuwa sasa ni zamu yangu nami kuwapiga maswali. Yule aliekuwa akinihoji nikamwambia, “Mimi wewe nakufahamu vizuri sana...'' Nilihisi amepata mfadhaiko kidogo akanambia,“Unanifananisha...'' Alikuwa anasema uongo lakini mie nikamkubalia. Hapo nikajua kuwa nishampata sasa hana nguvu tena ya kuuliza maswali. Kusema uongo ni dalili ya kujihami. Nikamrushia kombora lingine, “Sasa tuhuma za madawa ya kulevya zimekwisha tuko katika kwa nini naingiza vitabu vya Khomeni nchini?” Akanijibu kinyonge, “Tumeridhika huna madawa.” Kufika hapa tukawa tumemaliza mahojiano.

Wakati huo sasa ni usiku wa manane na nishapeleka SMS kwa sahib yangu mmoja bingwa wa mambo ya mtandao wa kompyuta kumjulisha kuwa nimekamatwa uwanja wa ndege kwa tuhuma za uongo za kuvusha mihadarati na yeye ile kuipata tu ule ujumbe wangu akaifahamisha dunia kuwa nimekamatwa uwanja wa ndege nikitokea mkutanoni Iran na nimebambikiziwa tuhuma za kuingiza nchini mihadarati. Waliponitia mbaroni tu walinionya kuhusu kutumia simu yangu ya mkononi lakini bahati nzuri hawakuninya’ganya. Aliyenipa onyo hili alikuwa mkuu wa kituo cha polisi cha uwanja wa ndege. Huyu rafiki yangu akawa kanisaidia sana maana hadi kumekucha wapenzi wangu wote ndani na nje ya nchi pamoja na vyombo vya habari vinavyonifahamu walikuwa na taarifa za kukamatwa kwangu. (Kwa kipindi takriban miaka ishirini nyuma kwa nyakati fofauti nimekuwa nifanya mahojiano na radio zote muhimu kama, BBC, VOA, Sauti ya Ujerumani, Sauti ya Iran nk.).

Nikawaomba wale watu wa Usalama waniachie basi nende zangu kulala nyumbani nirudi hapo kesho asubuhi kwa kuwa sikuwa nimebeba madawa ya kulevya. Wakaniambia, “Itabidi tukulaze hapa hadi asubuhi wakubwa wetu watupe amri ya kukuachia. Maana amri ya kukukamata wewe imetoka juu.”

CIMG0086.JPG


Mwandishi Akiwa Katika Studio za Radio Iran Tehran
Idhaa ya Kiswahili
 
John,
Hapana mimi naeleza kama ninavyokua kutokana na uzoefu.

Naamini kabisa kuwa wasingeweza kumfanyia mtu aliyetokea
Vatican haya waliyonifanyia mie.

Juu ya haya sikukatizi kuwa na fikra tofauti.
Vita ya dhati kupambana na madawa haramu haiangalii umetoka vatikani ama dubai ama irani, umetumia fasihi simulizi kwa ustadi kuficha meseji yenye propaganda ya chuki ya kidini dhidi ya ukristu.
 
Mbona huwa mkiguswa kidogo mnakimbilia kinga ya dini hio ni inferiority complex kwani maovu wameandikiwa watu wa dini Fulani,kama upo sawa acha wafanye kazi yao km hawajakutendea haki zipo mamlaka husika za juu unaweza kwenda kutoa malalamiko yako pia mahakama zipo kukutetea pia. Me MTU akianza kuhususisha dini ktk mambo namuona ana shida kidogo. Wao ufanya kazi Kwa taarifa wape ushiriano na pia ni haki yako kuwa na shahidi kabla ya kupekuliwa.
 
Bora trump awapige vita tu... mtu anajilipua ili aue watu ni mtu wa kukaa nae kweli?
Chaggaa,
Hao wenye kufanya hivyo wanakwenda kinyume na mafunzo ya Uislam.

Mathalan leo kanisa na ushoga kwani Bwana Yesu ndiyo mafunzo yake?
Muhimu ni sisi kukemea mambo haya yote ili tuiishi kwa amani.
 
Tuthibitishie kuwa waliokukamata ni wakristo,naona mmejengewa misingi ya chuki,na kulalamika ndo maana kila kitu mtakitazama kwenye misingi ya dini,Leo hii waislamu wanazikimbia nchi zao sababu ya chuki za kuuwana waislamu Kwa waislamu wanakimbilia kwenye nchi za makafiri wakaonyeshwe Upendo, kwann wasiende kwenye nchi za waislamu wenzao? Imetoka list ya Wauza unga majina mengi ni waislamu rejea gazetini mtasema sasa wanaondamwa ni waislamu? Hapana msisingizie dini panapo maovu kujifichia kupata popularity km alivofanya Osama na Makundi ya kigaidi. Me ni mkristo kabla sijasoma habari za uchunguxi niliamini ugaidi na uislamu ni kitu kimoja baada ya kuujua ukweli, kumbe uislamu hauna uusiano na ugaidi, dhana ya ugaidi imeingizwa na Freemasons ktk uislamu rejea history ya ugaidi ulianza lini, nani waanzilishi, na nn ajenda yake kuelekea new world order,soma history ya mapinduzi ya Irani,soma kuhusu vita vya msalaba nk.lengo la ugaidi kwanza ni kuusambaratisha uislamu, kupata mafuta Kwa mabadilishano ya silaha, kuifanya middle east isitulie Kwa usalama wa Israel,na kujipatia himaya ya kidunia Kwa kujifichia kwenye dini, na wenye kujua ajenda kuu ya ugaidi ni viongozi wakuu wa Makundi hayo na si wapiganaji wao hawaelewi chochote wameaminishwa wanapigania dini.Sababu ukitaka waislamu wachinjane waaminishe wanapigania dini,kumbe wapo kutimiza matakwa ya Freemasons toka magharibi. Shida kubwa ya waislamu wengi wameshajijengea dhana ya tunaonewa,tunadhulumiwa ukimgusa muislam hata Kwa mambo nje ya dini anakimbilia kwenye dini tunaonewa sababu tu waislamu. Ukiwaambia mnaonewa nn hawajui inakuwa sawa na wimbo wa taifa Kwa kila moja.Cha msingi ondoeni ile dhana tunaonewa,tunachukiwa nk sababu hakuna MTU ashawahi zuiwa fanya yake ya halali Kwa kufuata sheria sababu ya dini yake.
 
Mpaka hapo ulipoishia ni kuwa message yako inalenga kwenye udini..! acha udini mkuu na propaganda za chuki dhidi ya muislamu na mkristu.
REJEA.

Nakuapieni nyie msingethubutu kumkamata Mkristo anaetoka Vatican mkutanoni. Lakini kwa kuwa mie ni Muislam sina wa kunitetea. Nchi hii nani atakuuliza kwa kumnyanyasa Muislam?” Walishtuka na wakawa wanyonge sana wakasema si kweli kuwa naponzwa na dini yangu.
Tatizo lenu kubwa mtu akieleza ukweli wa mambo mnasema udini kwani si sio ndio ukweli huo unafikiri wanaweza kumkatamata mkatoliki akitoka Vatican akiwekani kitu hicho hata siku moja
 
Eti akitoka Vatican akamatwi jaribu uone msipende sana kujifichia kwenye dini ufanyapo makosa,sidhani wanausalama wote huwa ni wa dini Fulani,alichofanya Jamaa apate popularity sababu tayari mtazamo wake ni wa kidini kila kitu.
 
Eti akitoka Vatican akamatwi jaribu uone msipende sana kujifichia kwenye dini ufanyapo makosa,sidhani wanausalama wote huwa ni wa dini Fulani,alichofanya Jamaa apate popularity sababu tayari mtazamo wake ni wa kidini kila kitu.
Kenstar,
Nakuomba nijibu kwa ukweli.

Wawaweza wakakamatwa maaskofu wakawekwa rumande Segerea
kisha wakalawitiwa?

Mbunge akalileta suala hilo Bungeni na Waziri wa Mambo ya ndani
akajibu kuwa uchunguzi utafanyika ili kujua kuwa isiwe hao maaskofu
walikuwa wakifanya mambo haya kabla.

Hili linawezekana?
 
Back
Top Bottom