Moja ya dalili ya kijana kukosa maadili ya wazazi ni kuwafanya Wasanii wa muziki, drama na Filamu kuwa Role Model

Moja ya dalili ya kijana kukosa maadili ya wazazi ni kuwafanya Wasanii wa muziki, drama na Filamu kuwa Role Model

For sure.
Yaani watoto wengi wamelelewa na movie pamoja na muziki huku wazazi wao wakiwa busy
 
Mimi Nakubali Hoja Zako Kwa Kujiangalia Mimi Mwenyewe Na Wale Wanaonizunguka.

Wakati Ninakua Nilikuwa Mpenzi Wa Music Sana Kitu Ambacho Kilinifanya Baadae Nipate Tabu Maishani Kwani Nilipoteza Wazazi Angali Mdogo Sana Na Kutokana Na Familia Nyingi Za Kiafrika Nililazimika Kuanza Kujitegemea
Hapa Ndo Changamoto Zilipoanza Na Nililelewa Kiuwana Muziki Huku Nikiamini Ipo Siku Mziki Utanitoa Kitu Ambacho Kilifanya Niwe Mvivu Na Kushindwa Kuwa Mchakalikaji Nilikuja Kubadilika Baadae Sana Baada Ya Kupigwa Sana Na Maisha.

Ni Stori Ndefu Ngoja Niishie Hapa .

Next Time .
 
Mpo salama Kabisa!

Ukiona watoto au kijana ambaye ni fuata mkumbo, fasheni, mfuasi na kawageuza Wasanii wa Muziki, Drama, na Filamu kuwa Role model ujue tayari mzazi au mlezi kuna mahali amefeli.

Na ili umfelishe mtu yeyote au Jamii yeyote itakupasa uwape nguvu Wasanii wa drama, Filamu na Muziki. Ndio Njia rahisi Kabisa ya kumfelisha Mtu hasa Akiwa mchanga Kabisa, kijana.

Jamii Makini na ambazo zinaweza WA kufanya mabadiliko makubwa kwa wakati hujao hudhibiti Sana Masuala ya Filamu, Muziki na drama. Huyapa kipombele kidogo na kuyadhibiti yasionekane kirahisi kwa Watoto na vijana wadogo.

Ni kupitia Muziki, drama na Filamu ndipo mtoto anaweza kuharibiwa vibaya future yake, mitazamo yake, uwezo wake wa kufikiri na mitindo yake ya Maisha.

Wazazi wenye mipango ya kutawala wengine, wazazi wenye kuandaa watoto kuwa success Planner, huwadhibiti watoto kuangalia mambo ya hovyo mtandaoni na kwenye Luninga.

Mtoto wa Miaka chini ya kumi na nane. Hatoweza Kupata faida yoyote Ile kwa kuangalia na kusikiliza Muziki wa kisasa, drama na Filamu za kisasa zilizojaa Maudhui yaliyokosa maadili.

Vijana wengi wa Miaka ya 80-90 walioharibika kwa kutumia madawa ya kulevya, kujiingiza kwenye ushoga na usagaji, kutembea uchi , kujichora Tattoo wengi wao ni matokeo ya kuwaiga Wasanii wa Muziki, drama na Filamu.

Mimi ni Mtunzi wa Simulizi pamoja na scene za drama na Filamu. Kama Mtunzi ambaye zipo baadhi ya scene nilizozitunga kwa baadhi ya Filamu na tamthilia. Ninafahamu Kile ninachokisema kutokana na Kazi za utunzi, uongozaji na utayarishaji wa Filamu.

Haiwi bahati mbaya Wasanii kukaa uchi. Haiwi bahati mbaya kwenye Filamu kuonyesha urahisi katika maisha, na wahusika kukaa uchi. Sio kwa bahati Mbaya..
Unafikiri haiwezekani Wasanii wa Muziki, drama au Filamu kuigiza Bila uchafu na mambo yasiyofaa. Inawezekana Kabisa.

Ni jukumu la mzazi kudhibiti mtoto wake mwenye umri chini ya miaka 18 anayemtegemea na ambaye yupo nyumbani kuangalia Muziki wa kisasa, drama na Filamu.

Mtoto aliyeanza kujitegemea, uliyemfunza akafunzika ndiye anaweza kuanza kuangalia hao wasanii kwani tayari ushamjenga na hawezi kuhadaika na Drama, ulaghai na propaganda mbaya zinazoendeshwa nao.

Watoto wadogo hawapaswi kuyachukulia maisha kama Entertainment na Sports. Kwani maisha sio burudani na michezo.
Maisha ni KAZI kwa asilimia tisini
Kisha burudani na Michezo ndio kwa asilimia 10.

Mtoto mdogo kuanza kuchukulia maisha ni burudani na Michezo ni kumfanya aendekeze Michezo na burudani kwa asilimia 90% na Kazi asilimia 10.

Ahsante Sana.

Mtibeli, Safarini
Huja yako ungeweka specifically kwa Tanzania
 
Ikiwa ni Tanzania pekee ,tatizo nini ushamba wa wazazi wapya na vizazi vyao?!!
Nchi nyingine za Afrika wamewezaje kuukwepa ushamba huo wa kimaisha?!!
Nimesema hivyo kwasababu binafsi nina experience mbovu na wasanii wa Tz..
Hivi mfano binti yangu nitajihisi furaha nikimuona ni role model wa msanii wa filamu?!
 
Nimesema hivyo kwasababu binafsi nina experience mbovu na wasanii wa Tz..
Hivi mfano binti yangu nitajihisi furaha nikimuona ni role model wa msanii wa filamu?!
Ni ngumu kujihisi furaha mkuu wangu......

Je tujenge "novelty centers" nyingi ambazo zitakuwa "programmed" kwa mitazamo yetu ya kukiokoa hiki kizazi cha "malimbukeni"?!!
 
Nililelewa katika nyumba ambayo mtoto chini ya miaka 18 hakuruhusiwa kuangalia televisheni zaidi ya vipindi vya watoto na taarifa ya habari tena wikiendi tu.....

Leo nikimzuia mwenzangu asivipe simu janja watoto naonekana "mkoloni" eti hizo simu wanawekewa "game za watoto" ilihali watoto wanaperuze hata wasipotakiwa "kwenda".....
 
Baelezee Batanzani

Huezi ukaepuka hali hio unaeza limit tu muda ya kuwaangalia, unawatafutia vitu ya kufanya. You have to be there for your kids bazee.

Kwa maendeleo ya Ulaya na Marekani, ya tech unakutana na katoto miaka 3 anayo simu janja, ana TicToC, Instar, netflix na apps nyingi tu zingine za mitandao ya jamii.

banakutana na basanii mastaa banaonekana kama wamefanikiwa sana mapedeshe, mundani batoto banaoneshwa maisha na mafanikio kuwafanya kuwa mifano ya kuiga.
Nyumba wanayoishi inafanana na banda la Kuku Kenya. Wanaita Trailer park cjiu nn Watoto hawana maadili, wazazi hawana maadili unamkuta mzazi amevaa singlendi cku nzima ti wanaita wife beater, unategemea watoto wawe na role model hapo? Bac wanaingia kwenye cmu janja kuangalia tictoc. kutafuta rolemodel wake iwe ni msanii, drama n.k apate kuescape na mateso ya kuangalia bazazi wanalewa cku nzima.

Kwa mutechnology ya leo, huezi ukaepuka

Nikupe mfano Juzi nilikuwa natizama fainali za NFL footbal, wakati kocha wa Eagles akihojiwa familia yake ikaja kumlaki na kumpongeza, kilichonishtua ni pale mwanae wa miaka ka 2 tatu hivi akabebwa na babake, mkononi kana simu ya iPhone. Unafikiri atakuwa anafanyia nn cmu hio?

Balinishangaza pia kuwaona batoto bya miaka 9,10,13,15 vinazimia ety kwasababu wamemuona Taylor Swift. Nilisikitika sana banajiita Swiftiz

tusiwache batoto bawe kwa mutelefonee cku nzima. Tunaeza epuka kuporomoka kwa maadili ya batoto yetu
 
Back
Top Bottom