Mongella, Mkuu wa Mkoa wa Arusha amesema wakazi wa Ngorongoro wanabomoa makazi yao kwa hiyari, Wakazi 296 wajiandikisha kuhamia Tanga

Mongella, Mkuu wa Mkoa wa Arusha amesema wakazi wa Ngorongoro wanabomoa makazi yao kwa hiyari, Wakazi 296 wajiandikisha kuhamia Tanga

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Baada ya Serikali kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kueleza kuwa imekamilisha maandalizi ya msingi katika makazi mapya yaliyopo Handeni Mkoani Tanga, ambapo yanatarajiwa kutumiwa na Wananchi watakaohamishiwa hapo hivi karibuni, Serikali imezungumzia jinsi Wakazi wa Ngorongoro wanavyoboa nyumba zao kwa hiyari ili Wahamie Tanga

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongella amesema zoezi la kuwahamisha wakazi hao kwa awamu ya kwanza litahusisha Kaya 23.

“Wananchi tumewaambia hatutagusa majengo yao, watabomoa wenyewe na tumetoa fursa, pamoja na fidia, mali wanazotaka kuzichukua wachukue, watapelekwa hadi Handeni bure.

Video zimeonesha wakazi wanaoishi ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa hiari yao wenyewe wakianza kufungasha mizigo yao na kuvunja makazi yao ya hifadhini hapo tayari kuelekea Kijiji cha Msomera Wilayani Handeni Mkoani Tanga.

1 (2).jpg

wahamiajipic.jpg
“Kule miundombinu inazidi kuimarishwa nyumba 103 ziko tayari, Juni 15, 2022 tunaanza awamu ya kwanza ya kupeleka mifugo, mali zao pamoja na wao wenyewe kwani tumeshajitayarisha,” amesema Mongella.

Wafugaji hao wamesema wameridhia kuondoka katika maeneo hayo kwani wanafidiwa kila kitu ikiwamo kujengewa nyumba na huduma mbalimbali. Wamemshukuru Rais Samia kwa kuwasikiliza na kuwaandalia makazi mapya yaliyo bora yenye Umeme, Maji, Huduma za afya na sehemu ya kufugia mifugo na kulima pia

Wameongeza kuwa fursa hiyo waliyopewa ni bahati na upendeleo kwa wana-Ngorongoro kwani licha ya kupewa nyumba, mashamba na huduma nyingine lakini wamewezeshwa ili kuweza kuendana na kasi ya maendeleo.

“Kuna shule, hospitali nzuri, miundombinu ya maji vikiwepo visima ambapo katika mzunguko wa nyumba kuna ekari 3 mbali na mashamba yenye ekari 5,” amesema Beatrice Soka.
 
Back
Top Bottom