Uchaguzi 2020 Morogoro: Mgombea ubunge wa CHADEMA Bi Devotha Minja awatoroka Polisi waliotaka kumkamata, gari lake lakamatwa

Uchaguzi 2020 Morogoro: Mgombea ubunge wa CHADEMA Bi Devotha Minja awatoroka Polisi waliotaka kumkamata, gari lake lakamatwa

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
11,795
Reaction score
36,704
Heche.JPG

Mwenyekiti wa timu ya kampeni ya Mgombea ubunge wa Morogoro mjini kwa tiketi ya CHADEMA na dereva wa mgombea Ubunge wa Morogoro mjini Bi Devotha Minja wamekamatwa na Polisi muda huu huku mgombea huyo akisakwa baada ya kuwatoroka polisi.

Inadaiwa gari yake pia imekamatwa na ilikuwa ni katika harakati za kumteka ili asirejeshe fomu ya ugombea leo.

Aidha sababu za waliokamatwa bado hazijawekwa wazi.

Maelezo haya ni kwa mujibu wa yeye Devotha Minja ambaye yupo mafichoni.

-----
Jeshi la Morogoro mjini, wamezingira ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Morogoro mjini, lengo likiwa nikumsubiri Devotha Minja wamkamate kabla ya kurudisha fomu, baada ya kupigwa simu na OCD akimtaka aripoti kituoni asubuhi hii.

Minja.JPG
 
Maelezo ya kimbeya hayajitoshelezi wamekamatwa kwa sababu gani? Chadema mna uandishi Fulani hivi wa kipungufu akili mkiripoti kitu kiasi kuwa hata mjinga akisoma anaona wazi kuwa mleta mada kichwani Hana kitu.

Andika vizuri sababu za kukamatwa na polisi ni nini
 
Lazima tuwe na muafaka wa Kitaifa kwamba tunataka nini kama Watanzania.

Majadiliano ya pamoja yatatuweka huru iwapo yatakuwa na nia thabiti na ya kizalendo.

Kuna shida katika Taifa letu. Kama Watanzania, tuna kila sababu ya kujadiliana kwa pamoja kwa ajili ya Taifa na amani yetu na umoja na mshikamano.
 
Kutokana na wimbi la wagombea wa upinzani kuwindwa na shetani kama swala ili watekwe au wauliwe huku viongozi wa dini na tume wakikaa kimya sababu wagombea wa CCM hawatekwi ni jukumu lao sasa wagombea wa upinzani kujihami binafsi na kurekodi matukio yote live watumie kofia,miwani, earphone, nguo zenye camera 360 degree warekodi kila kitu huku wakitembea na watu waliofully armed ili kujilinda endapo watafamiwa waweze kutoa fundisho ili wakamsimulie shetani aliyewatuma na sio kulalamika mnatekwa tekwa hovyo hovyo kirahisi tu kumbukeni mpo mawindoni sababu wanajua awatoboi kwenye sanduku.

Toeni funzo kama wananchi wa Ukara tembeeni hata na asidi atakaekugusa tu anayo ndo njia pekee ya kujihami,hatutaki watu wa kulialia safari hii.Rekodini matukio yote mrudishapo formu kama ushahidi na kuyarusha live watz wayaone.
 
Mwenyekiti wa CHADEMA Morogoro, dereva wa mgombea Ubunge wa Morogoro mjini Bi Devotha Minja wamekamatwa na Polisi muda huu huku mgombea huyo akisakwa.

Inadaiwa gari yake pia imekamatwa na ilikuwa ni katika harakati za kumteka ili asirejeshe fomu ya ugombea leo.

Maelezo haya ni kwa mujibu wa yeye Devotha Minja ambaye yupo mafichoni.
Kigogo alisema mapema hii kitu
 
Devota Minja mjanja Fulani Kuna tetesi alienda kutaka kuuza hiyo fomu alipwe akabidhi kwa mnunuzi Kisha asingizie kaporwa alipoona Takukuru wanafuatilia akaingia mitini
 
Maelezo ya kimbeya hayajitoshelezi wamekamatwa kwa sababu gani? Chadema mna uandishi Fulani hivi wa kipungufu akili mkiripoti kitu kiasi kuwa hata mjinga akisoma anaona wazi kuwa mleta mada kichwani Hana kitu

Andika vizuri sababu za kukamatwa na polisi ni nini
Sababu inajulikana ili wasirudishe fomu za uteuzi
 
kutokana na wimbi la wagombea wa upinzani kuwindwa na shetani kama swala ili watekwe au wauliwe huku viongozi wa dini na tume wakikaa kimya sababu wagombea wa ccm hawatekwi ni jukumu lao sasa wagombea wa upinzani kujihami binafsi na kurekodi matukio yote live watumie kofia...
Viongozi wa dini ni wanafiki wa kutupwa.
 
Devota Minja mjanja Fulani Kuna tetesi alienda kutaka kuuza hiyo fomu alipwe akabidhi kwa mnunuzi Kisha asingizie kaporwa alipoona Takukuru wanafuatilia akaingia mitini
Wewe jamaa huwa nimjinga sana, hivi unajisikia ufahari gani raia wenzako wanapopokonywa haki zao kisa vyama? Hivi na nafsi yako inafarajika kabisa kusikia wenzako wanakamatwa ili wasirudishe form? Kiukweli huwa najiuliza Wana CCM niraia wanchi gani, inawezekana sio Tz yetu iliyojaa upendo wanaoishi hawa viumbe.
 
Back
Top Bottom