Morogoro: Mpangaji afungiwa ndani Saa 27 na Mmiliki wa nyumba kwa madai ya kukiuka Notisi ya kuhama

Morogoro: Mpangaji afungiwa ndani Saa 27 na Mmiliki wa nyumba kwa madai ya kukiuka Notisi ya kuhama

Mkuu sheria ya upangaji haielekezi hatua za aina hiyo. Kasome ile sheria vizuri. Usiwapoteze wenye nyumba!!!
Sasa kama mimi nimekosea na kuwapoteza wenye nyumba basi ingekuwa busara wewe uwaeleze hiyo Sheria inasema nini?
Hamlipi kodi na nyumba za watu mnazichafua; mkipewa notisi ya kuhama mnaleta jeuri, ndio maana mnatupiwa vyombo nje!
 
Sasa kama mimi nimekosea na kuwapoteza wenye nyumba basi ingekuwa busara wewe yeleğe hiyo Sheria inasema nini?
Mkuu nimekushauri hivyo kwa nia nzuri. Mara nyingi sisi watanzania huwa tunashauriana mambo mengi kwa kudhania na kwa mazoea.

Ndugu yangu kila kazi, shughuli au biashara nchini inaongozwa na sheria yake. Ni muhimu kabla hujaanza shughuli au biashara yoyote ukaielewa sera na sheria yake.

Maana ikitokea changamoto utapimwa, kushtakiwa kwa kutumia hiyo sheria.

Kuhusu zinakopatikana, tembelea maduka ya serikali ya vitabu au ofisi mchapaji wa serikali.
 
Mkuu nimekushauri hivyo kwa nia nzuri. Mara nyingi sisi watanzania huwa tunashauriana mambo mengi kwa kudhania na kwa mazoea.

Ndugu yangu kila kazi, shughuli au biashara nchini inaongozwa na sheria yake. Ni muhimu kabla hujaanza shughuli au biashara yoyote ukaielewa sera na sheria yake.

Maana ikitokea changamoto utapimwa, kushtakiwa kwa kutumia hiyo sheria.

Kuhusu zinakopatikana, tembelea maduka ya serikali ya vitabu au ofisi mchapaji wa serikali.
Ungekuwa na busara kama ungeielezea Sheria hiyo badala ya kunishauri niende kununua kitabu cha sheria!
Mimi nadhani niko sahihi kuwa mpangaji akikiuka mkataba wake lazima afukuzwe kufuatana na masharti ya mkataba; kupewa notisi ya mwezi mmoja ni moja ya masharti hayo yanayompa nafasi mpangaji kutafuta makazi mapya!
Hebu elezea sheria inayosema tofauti na haya niliyoyaeleza!
 
Sisi tunaopangisha watu tunaelewa sana
Mkuu ni muhimu sana wenye nyumba wakaelewa kuwa sheria ya upangaji inamlinda mpangaji sana kama ilivyo kwa mwanamke na mtoto wanavyolindwa.

Mwenyewe nyumba akijiendea kihasara kwa mpangaji anayejielewa na anayeielewa sheria anamfilisi mazima.
 
Ungekuwa na busara kama ungeielezea Sheria hiyo badala ya kunishauri niende kununua kitabu cha sheria!
Mimi nadhani niko sahihi kuwa mpangaji akikiuka mkataba wake lazima afukuzwe kufuatana na masharti ya mkataba; kupewa notisi ya mwezi mmoja ni moja ya masharti hayo yanayompa nafasi mpangaji kutafuta makazi mapya!
Hebu elezea sheria inayosema tofauti na haya niliyoyaeleza!
✍️🙏
 
Aende kwenye Baraza la ardhi la kata au wilaya ndo watoe amri ya kuondolewa ,nashangaa huyo wakili aliye mshaur alisoma chuo Burundi au somalia?
Kwani wakati anampangisha walikwenda baraza la Aridhi la kata!? Sasa hivi kutoka kwenye nyumba ya watu ndiyo mnataka hadi baraza la ardhi la kataa ndiyo litowe amri!? Kwani hiyo nyumba ni ya baraza!? Mwenye mali anataka mali yake na apewe bila shida za mabaraza!!
 
Mkuu, madam makubaliano yakiwepo utaratibu ni kufuata sheria.
Hilo ndo la msingi (kufuata sheria)ila inawezekana pia mwenye nyumba naye kwa Hasira akaamua kuact kibabe kutokana na usumbufu anaoupata.
 
Wakuu, huu ni Uungwana kweli?

Huko Marogoro mwenye nyumba kamfungia ndani saa 27 mpangaji kisa amekiuka notisi

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, mmiliki wa nyumba Plot namba 149 BLOCK ‘A’ Kihonda Kilimanjaro, Dk. Lusako Mwakiruma ilioyopo Mtaa wa Kilimanjaro Manispaa ya Morogoro, amemfungia ndani mpangaji wake kwa saa 27 kisha kumtolea vitu vyake nje, kwa madai kuwa mpangaji huyo, Paschal Paulo alishindwa kupokea notisi ya kumtaka ahame kwenye nyumba hiyo ndani ya mwezi mmoja.
Sheria ya Ardhi, [Sura ya 113, Toleo la Mwaka 2019] Kifungu cha 101 kinamruhusu mwenye nyumba kusitisha mkataba wa pango endapo mpangaji atashindwa kulipa kodi ya pango kwa siku 30. Hata hivyo, kabla ya kusitisha mkataba huo, mwenye nyumba anapaswa kumpa mpangaji notisi ya siku 30, akimtaka alipe kodi anayodaiwa, na endapo mpangaji atashindwa kufanya hivyo, mkataba huo utasitishwa. Notisi hiyo haipaswi kuwa chini ya siku 30, ila inaweza kuwa zaidi ya hapo. Endapo siku za Notisi zitaisha bila mpangaji kulipa deni lote, mwenye nyumba atasitisha mkataba na atakuwa na haki ya kumuondoa mpangaji katika nyumba yake.
Utaratibu wa kumuondoa ni kama ufuatavyo;
  1. Endapo mpangaji atakua tayari kuondoka mwenyewe kwa amani, mwenye nyumba atasitisha mkataba na kumuamuru mpangaji aondoke.
  2. Endapo mpangaji atagoma kutoka kwa amani, mwenye nyumba atatakiwa kufungua shauri Mahakamani kuomba amri ya mahakama/Baraza kumfukuza mpangaji katika nyumba ile, na atatumia dalali wa Mahakama au dalali wa Baraza la Ardhi na kumuondoa mpangaji katika eneo hilo.
Sheria haijaweka aina ya Notisi kwamba ni lazima iwe barua ya karatasi, barua pepe, tangazo, au ujumbe mfupi wa maneno (SMS). Hivyo mwenye nyumba ameachiwa uhuru wa kuchagua aina ya Notisi itakayotumika pia kwa kuzingatia urahisi wa mpangaji wake kuipata. Aidha, Sheria imeelekeza taarifa gani lazima ziwepo kwenye Notisi hiyo, ikiwa ni pamoja na;
  • Aina ya uvunjifu wa mkataba uliofanywa na mpangaji;
  • Kiasi kinachopaswa kulipwa kutokana na uvunjifu wa mkataba huo;
  • Kipindi, kisichopungua siku thelathini tangu tarehe ya kupokea notisi, ili kulipa kiasi hicho;
  • Na kwamba iwapo mpangaji huyo hatalipa kiasi hicho ndani ya siku 30 tangu kutolewa kwa Notisi, mkataba utavunjwa.
Sheria pia inaelekeza kwamba endapo mpangaji amekataa kupokea Notisi, au hapatikani kwa urahisi, Notisi hiyo inaweza kubandikwa sehemu yoyote iliyokaribu na eneo hilo ama kutangazwa kwenye gazeti kwa kuzingatia aina ya umiliki wa eneo hilo.

Kwa kuzingatia hii taarifa ya Morogoro, kuna mkanganyiko, kuhusu upokeaji wa Notisi, na kama tatizo ni ulipaji kodi, au ubadilishaji wa matumizi hata hivyo; kwa kuzingatia kwamba mpangaji alikataa kuondoka, mwenye nyumba alitakiwa kufungua shauri mahakamani ili aweze kurudishiwa eneo lake kutoka kwa mpangaji.
 

Attachments

  • Kifungu cha 101 - Sheria ya Ardhi [2019].png
    Kifungu cha 101 - Sheria ya Ardhi [2019].png
    128.8 KB · Views: 2
  • 1731399947241.png
    1731399947241.png
    128.8 KB · Views: 2
Mwanaume na mwanamke wakiamua kuwa pamoja, baada ya muda mmoja wapo akiamua kuondoka mwenza wake atamlazimisha kuendelea na mahusiano?
Busara inaelekeza uhusiano ukisha lazima kutengana na sio kulazimisha uhusiano!
 
Safi kabisa hata hivyo nimkumbushe tu kama hatohama siku mbili hizi afunge ampige kibiriti humohumo.
 
Aende kwenye Baraza la ardhi la kata au wilaya ndo watoe amri ya kuondolewa ,nashangaa huyo wakili aliye mshaur alisoma chuo Burundi au somalia?
Stupid; mbona dukani tunaendaga kununua vitu kwa cash? Mbona kwenye vyombo vya usafiri tunalipa? Nyumba ni biashara kama zilivyo biashara zingine, serikali iiondoe hi sheria ya kipuuzi; kama inawapenda raia wake then zijengwe nyumba nyingi halafu serikali iwapangishe watu huko
 
Back
Top Bottom