Moses Lijenje aliyetajwa kutupwa na Polisi kesi ya ugaidi ya Mbowe na wenzake ni nani?

Moses Lijenje aliyetajwa kutupwa na Polisi kesi ya ugaidi ya Mbowe na wenzake ni nani?

Sio Dereva ni Ghost katika hii kesi ila amehusika sana. Yuko kituo cha polisi Usa River ni mkuu wa upelelezi wilaya

Dereva bado hatujasikia vimeo vyake zaidi ya kumpiga ngumi Adamoo
Nasikia huyu jumanne ndiyo ilikuwa atoe ushahidi ile ijumaa lkn ndiyo wakamkimbiza nduki nduki.

Ilijulikana sababu ni nini ya kumuondosha jumanne asitoe ushahidi?
 
Ukifuatilia toka mwanzo Adamo alisema wanapobadilishwa vituo hulazimishwa na kupewa majina tofauti na majina yao halisi so unaweza kukuta huyo Moses lijenje ni katika mlolongo huo
Pia ukifatilia vizuri zaidi utagundua kwenye maelezo ya Kingai kuwa walizunguka moshi na boma kwa siku 2 kumsuka huyo Mosses Lijenje,

nadhani soon mwisho wa huyo Moses lijenje utawekwa bayana kwa kuunganisha dots kupitia maelezo ya mashahidi wanavyozidi kutoa maelezo.
 
Nasikia huyu jumanne ndiyo ilikuwa atoe ushahidi ile ijumaa lkn ndiyo wakamkimbiza nduki nduki.

Ilijulikana sababu ni nini ya kumuondosha jumanne asitoe ushahidi?
Inaonekana vitendo vyingi vya mateso vilifanywa na huyu j4 dhidi ya watuhumiwa,
labda kina kingai wameona cross examination ya j4 zitaibua mengine yasiyofaa kujulikana.
 
Ndio maana wanapigana kuendelea kuwa na madaraka...

Tuwakumbushe tu, haya mambo huwa hayana mwisho.

Kuna watu walishiriki uhalifu wakati wa vita ya pili ya dunia 1945 huko, mpaka leo wanapelekwa mahakamani kujibu.

1632774446781.png


Hawa washenzi wakiwa hai hata mwaka 2100 huko, vitukuu vyetu tunaomba mje kuwashughulikia kikamilifu.

1632774341346.png
 
Yapo mengi.

Kumbuka pia tuliambiwa muuza mechi alikuwa ni poti - Luteni Urio.

Kumbe Luteni Urio alikuwa ni mmoja wa waliokuwa wakiteswa Tazara na mahabusu pendwa Tazara na pia kule Mbweni.

Kumbe basi hadithi za Kingai kuitwa kwa DCI kuwa Urio alikuwa na taarifa za magaidi zinaweza kuwa ni hadithi zingine kama za sungura na fisi.
Hili ndilo limenishangaza,inakuwaje source ya tukio la maandalizi ya Ugaidi nae akamatwe ateswe halafu cha kushangaza kwenye kutuhumiwa kesi yeye hayupo lakini kwenye mateso alikuwepo.
 
Huyu komandoo wa pili anaonekana anayajua mengi hivyo tutajua mengi in advance kupitia kwake. Naona kaibua na linguine la shahidi wa jamhuri luteni mwenzao kuteswa kwanza kids kuibuka akiwa shahidi upande wa jamhuri. Mazingaombwe ya polisi yanaendelea kubainishwa.
 
Wakati shahidi namba mbili na mshitakiwa namba tatu Mohammed Abdilah Ling'wenya wa kesi ndogo katika kesi ya Ugaidi inayowakabili kina Mbowe alimtaja Mosses Lijenje kudaiwa kutupwa na polisi wakati akifanyiwa vitisho.

Mallya: Kitu gani Kiliendelea..?

Shahidi: Maaskari wakasema Mwenzenu Moses Lijenje tumeshamtupa, Ameshatangulia huku wakinigusa Kichwani na Kitu nilichokuwa nahisi kuwa ni Bastola, Ukileta Ujanja Ujanja na wewe tunakutupa

Mallya: Maneno haya ulikuwa unaambiwa wakati gani wakati wa Safari au baada ya Kufika


Huyu Moses Lijenje ni nani?

Je yupo wapi?

Je yupo hai?

Je anahusika vipi na hawa makomando?

Je anahusika vipi na hii kesi ya Mbowe?

Shahidi anaposema polisi kudai wameshamtupa wanamaanisha nini?

Hili limeniacha na maswali mengi sana ya kutafakari.
Aliyekuwa nahojiwa leo ambaye ni komando pia huyu hapa aliyepiga saluti

Kwa_ujibu_wa_watu_mbambali_huyu_jamaa_aliyepiga_salute_ndio_Mohamed_Ling'wenya_ambaye_leo_ndo_...jpg
 
Sio Dereva ni Ghost katika hii kesi ila amehusika sana. Yuko kituo cha polisi Usa River ni mkuu wa upelelezi wilaya

Dereva bado hatujasikia vimeo vyake zaidi ya kumpiga ngumi Adamoo
 
Hii kesi badala ya kuleta amani uraiani kwa kuwafungia gaidi mbowe na wenzake inakoelekea italeta machafuko nchini, kwa sababu hii kesi inaeleweka ni ya kisiasa, sasa haya mambo ya jeshi la polisi kuanza kuonekana linaua watu litawaletea shida hawa askari huku vituoni kwao mitaani.

huyu mama wa kizanzibar nimeishasema afute hii kesi, haya mambo ya askari kuua watu yalikuwa awamu ya tano huko, sasa hawa kina kingai wanataka kuanza kuyaambatanisha na awamu ya sita.
Kwanza, unamuomba rais kuingilia mahakama. Kama Mbowe na wenzake hawana hatia, ni kazi ya mahakamas kuamuwa kuwa hawana hatia. Je, kumshauri raisi aingilkie huo ni utawala bora. Kwani wewe una wasiwasi gani? Kama Mbowe hakutenda kosa la ugaidi, ataachiwa.
 
Halafu mnakwapua mpaka laki mbili na sitini za mtuhumiwa. Nilijua mna kiu ya damu tu ,kumbe mpaka MNA njaa kali mno.

Yaani RCO na jopo lake wanakwapua laki mbili na sitini?
Tangia walikuja kwangu kukagua sjui vinini saabu ya mume wangu wakaiba kasimu ka torch na viatu vya Mr hata sinaga imani na hao watu sjui nawaonaje! ( sio hao kwenye kesi ila ni polisi wenzao dah nlichoka)
 
Back
Top Bottom