Moshi: Mlinzi aliyehukumiwa kifo kwa Mauaji ya Mwanafunzi wa Sekondari ya Scolastica aachiwa huru

Moshi: Mlinzi aliyehukumiwa kifo kwa Mauaji ya Mwanafunzi wa Sekondari ya Scolastica aachiwa huru

Dogo alitoroka Shule akaenda anakokujua mwenyewe. Aliporudi aliruka ukuta ili aende bwenini kulala, Mazingira yalikuwa ya giza lakini pia sheria ni kuwa lazima uwe na uniform ya shule muda wote uwapo nje ya shule- Mwizi ana alama! Askari alikuwa anajiami kwani alikuwa anamshambulia mtu asiyejulikana alieruka ukuta wa shule usiku na kwenye giza nene.Marehemu alitakiwa ajitambulishe na pengine ata kumwita mlinzi kwa jina lake ingesaidia kutoshambuliwa zaidi mpaka ikapeleka kifo chake. (HAYA NI MAWAZO YANGU SIO UKWELI WOWOTE NISINUKULIWE VIBAYA)
 
Nadhani mwanafunzi alikuwa anaenda disco ( adolescence / Nyege). Mlinzi hakuwa na nia ya kuua bali alitaka kukamata aliyemdhani ni jambazi au mbakaji labda, ndio maana hakutumia bunduki (kama alikuwa nayo).
Dogo alitakiwa ajitambulishe na ata kumwita jina Kamanda! Uenda angepigwa ubapa mmoja tu na angeishia suspension na angerudi shule.
 
Dogo alitakiwa ajitambulishe na ata kumwita jina Kamanda! Uenda angepigwa ubapa mmoja tu na angeishia suspension na angerudi shule.
Yeah, ila adhabu ya miaka minne kwa manslaughter ni ndogo, walau mitano
 
Watakuwa waliogopa shule kupata jina baya na kupoteza biashara, maana mlinzi kuua mwanafunzi (hata kama alidhani ni jambazi) ni kitu kinachotisha sana wazazi, kwahiyo mwenye shule ili kulinda biashara yake nadhani waliamua kuficha ushahidi wa mauaji mtoni
Mtu kukufia ghafla sio rahisi jamani,we unavyosikia mtu mpaka anamchoma kwa gunia mbili za mkaa mchezo,mara mwingine anabomoa sakafu anazika ndani na mwingine anaenda kutupa huko mtoni,kifo cha ghafla acha kabisa.
Mungu amrehemu aendelee kuwafariji wazazi wake na waloua bila kukusudia awasamehe kwakweli
 
Title ya uzi na uzi husika ni vitu viwili tofauti.

Sio kwamba imemuachia huru, hapana ni kuwa rufaa yake imekubaliwa nusu ila wakamrudisha kwenye kosa la kuua bila kukusudia, kisha kwenye adhabu wazee wakajikuta imeshakamilika.

Sasa swali la msingi ni je, Mahakama ya rufaa inaweza kuwa mahakama ya kusikiliza kesi mpya? trial court jibu la awali kabisa ni hapana, sasa swali ni je, kilichofanyika ni marejeo, mapitio au kusikilizwa kesi trial?

Huu mjadala niishie hapa, ntaend kusoma zaidi na zaidi
 
Mahakama imemuachia huru aliyekuwa mlinzi wa Shule ya Sekondari Scolastica, iliyopo mji mdogo wa Himo wilayani Moshi, Hamis Chacha (34) aliyehukumiwa kifo kwa kosa la kumuua kwa makusudi mwanafunzi wa shule hiyo, Humphrey Makundi.

Chacha ameachiwa huru baada ya jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani Tanzania kusikiliza rufaa, kushusha shitaka lake kutoka mauaji ya kukusudia na kuwa ya bila kukusudia, baada ya kubaini hakuwa na nia ovu ya kuua.

Maelezo ya kosa hilo yanaeleza kuwa Septemba 6, 2017 saa 2 usiku, katika mji wa Himo, mlinzi huyo alimuua mwanafunzi Humphrey aliyekuwa kidato cha pili kwa kumpiga na ubapa wa panga.

Baada ya kesi kusikilizwa, Juni 3, 2019 Jaji Firmin Matogolo alimtia hatiani.

Kwa mujibu wa maelezo hayo, siku hiyo (Septemba 6, 2017) mlinzi akiwa doria nje ya uzio wa shule, alisikia kishindo cha mtu kuruka ukuta kutoka ndani ya shule.

Alipofuatilia aliona mtu akikimbia, alimkimbiza na alipomkaribia alimpiga kwa ubapa wa panga lakini hakusimama.

Mlinzi aliendelea kumkimbiza, umbali mfupi baadaye, mtu huyo alianguka. Alimsogelea na kumpiga tena kwa ubapa wa panga, mtu huyo ambaye wakati huo hakuwa amemtambua hakuamka tena.

Mlinzi huyo alimpigia simu mmiliki wa shule, Edward Shayo na mwalimu wa nidhamu, Laban Nabiswa; walibaini mtu yule ni mwanafunzi Humphrey Makundi (16) na alikuwa amekufa, ndipo walijadiliana na kuamua kuutupa mwili katika Mto Ghona ulio jirani na shule. Mwili uligundulika Septemba 12, 2017 katika mto huo ukiwa umeanza kuharibika na ilibainika ni wa mwanafunzi huyo.

Shayo, Nabiswa na Chacha walikamatwa na kuhusishwa na mauaji ya kukusudia ya mwanafunzi huyo.

Baada ya Mahakama kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili, iliwaondoa Shayo na Nabiswa katika kosa la mauaji ya kukusudia na kuwatia hatiani kwa kosa dogo la kuficha taarifa za tukio hilo na kuwahukumu kifungo cha miaka minne jela.

Wawili hao walishamaliza kutumikia vifungo vyao gerezani na kurejea uraiani; mlinzi huyo akimtumia Wakili David Shillatu alikata rufaa kupinga kutiwa hatiani na adhabu ya kifo aliyopewa akiegemea katika sababu kuu mbili za rufaa.

Moja walipinga uchukuaji wa maelezo ya ungamo kwa mlinzi wa amani kuwa hayakufuata mwongozo wa Jaji Mkuu na hayakuungwa mkono na ushahidi mwingine, hapakuwa na nia ovu; na pili shitaka halikuthibitishwa bila kuacha shaka.

Chanzo: Mwananchi
Oya kwa yoyote humu aliyekuria / kuishi mazingira Yale ya Himo na anaepaelewa kule mto Ghona hadi kule nyuki hd kipande cha mieresini tujuane, binafc kitambo sana pande zile [emoji3] karibu na Shule ya scolastica kuna hospitali ya Dokta wangu pendwa Dkt. Lazaro I wish km mpk Leo Bado yupo site ile aisee

Naona Himo panaitwa mji siku hz haha,
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]msipeleke watoto wenu scolastica
Watauawa halafu kunakuwa hamna kesi
Msijesema hatujawaambia[emoji1787][emoji1787]
Haya[emoji108][emoji108][emoji848]
Bwana Shayo pesa anazo bhn
 
Kwanini wamtupe? Maamuzi mengine ya kijinga sana.
Kule kumtupa ndiko kulikowafunga wenzake adhabu ndogo.

Pia katika hukumu huangaliwa zaidi kiini cha kosa na kuthibitisha bila shaka utendwaji wake.

Kukimbia, kuficha ushahidi huwa haviangaliwi sana kwa sababu kutapatapa kukwepa mikono ya sheria ni jambo linalofahamika na linaloweza kufanywa na mtu yeyote.
 
Title ya uzi na uzi husika ni vitu viwili tofauti.

Sio kwamba imemuachia huru, hapana ni kuwa rufaa yake imekubaliwa nusu ila wakamrudisha kwenye kosa la kuua bila kukusudia, kisha kwenye adhabu wazee wakajikuta imeshakamilika.

Sasa swali la msingi ni je, Mahakama ya rufaa inaweza kuwa mahakama ya kusikiliza kesi mpya? trial court jibu la awali kabisa ni hapana, sasa swali ni je, kilichofanyika ni marejeo, mapitio au kusikilizwa kesi trial?

Huu mjadala niishie hapa, ntaend kusoma zaidi na zaidi
Nadhani mantiki (logic) imefanya kazi yake. Maana kesi mpya ya ‘kuua bila kukusudia’ ikisikilizwa, there can be only one outcome, regardless ya hukumu, ni kwamba the guy walks free. Akishindwa kesi na kuhukumiwa adhabu stahiki (miaka 4) basi atakuwa amashamaliza adhanu yake (time served), hivyo he walks. Akishinda kesi, he walks.

Ila hapa kuna swali la kujiuliza, miaka mi4 ni adhabu tosha kwa kosa kubwa kama hilo? Hivi si ilibidi apigwe miaka kama 20 hivi au? Sheria inasemaje?
 
Na huyu OCS Juma alibaki salama kwenye utumishi wa umma??

"Mlinzi alishauri mtu yule asiyefahamika awahishwe hospitali kwani anaweza akawa bado yuko hai lakini Mkuu wa Shule, kwa kuhofia usumbufu ambao ungejitokeza, akashauri mtu yule atupwe kwenye Mto Ghona ulio umbali wa mita zaidi ya 300 kutoka ilipo shule ya Scolastica. Mwalimu Labani, akishirikiana na mlinzi, wakatekeleza ushauri ule huku mwenye shule akiwaambia mambo mengine yote wamwachie yeye."

"Mwenye shule akawasiliana na Inspekta Idd Juma ambaye alikuwa ni Mkuu wa Kituo cha Polisi Himo. Haikujulikana walichowasiliana lakini mnamo Novemba 10, 2017, polisi wa Himo, wakiwa na mkuu wao wa kituo, walienda mto Ghona na kuuopoa mwili ule na kuupeleka Hospitali ya Mawenzi. Kwenye miamala ilionekana Mzee Shayo alimtumia kiasi cha Sh500,000 Mkuu wa Kituo cha Himo."

Fortunatus Buyobe, mwandishi wa habari za uchunguzi

Hio kesi rushwa imetumika sana.

Huyo Shayo sio mwenye shule.
shule bi ya huyo mama anaitwa Scolastica.

Scolastica ni mpango wa kando wa wa mzee shayo. Maana shayo ana mke kabisa wa ndoa.

Hiyo shule chini ya mwl mkuu Michael Chapombe (mkenya) na huyo mwal Laban (mkenya) nadhani ni mwl wa nidhamu, ina kesi lukuki kupiga na kuumiza wanafunzi kituo cha polisi cha himo. Kimsingi kupiga wanafunzi na kuumiza ni kawaida yao hado ilipotokea huyo mwanafunzi aliekufa. Thanks kwa mzazi wa mtoto (makundi) alikuwa na msuli, vinginevyo ilishakuwa imepangwa kuwa mtoto ametoroka shule na uongozi wa shule hawajui alipo.

Kimsingi alietakiwa kuwa ndani ni huyo mama sio shayo. Huyo mama anaishi hapo hapo shule na mwanae kiongozi wa shule. Anaishi mira chache karibu na geti, na shayo mara nyingi huishi kwny hotel zake. Na mama ndiyo final say, kwahiyo kama kuna maamuzi ya kuufukia mwili, basi yalitoka kwa mama sio shayo. Nadhani pesa aliyotumia mama kuzima hiyo kesi na kupindisha, ndiyo ilifanya Shayo akalale ndani badala yake.
 
Naona na maji ya Kilimanjaro mkononi, hawa jamaa wa mkoa huu ni wabaguzi sana, huwezi kuta uhai maisha wala afya katika mkoa huu
 
Nadhani mantiki (logic) imefanya kazi yake. Maana kesi mpya ya ‘kuua bila kukusudia’ ikisikilizwa, there can be only one outcome, regardless ya hukumu, ni kwamba the guy walks free. Akishindwa kesi na kuhukumiwa adhabu stahiki (miaka 4) basi atakuwa amashamaliza adhanu yake (time served), hivyo he walks. Akishinda kesi, he walks.

Ila hapa kuna swali la kujiuliza, miaka mi4 ni adhabu tosha kwa kosa kubwa kama hilo? Hivi si ilibidi apigwe miaka kama 20 hivi au? Sheria inasemaje?
Kama tukitumia mantiki, Mahakama ya Rufaa haina mamlaka au uwezo wakusikiliza trial uwezo wake ni kisikiliza Rufaa, kufanya marejeo na mapitio pia.

Kama ni kesi kuanza kusikilizwa upya wanatoa amri ya kesi ikasikilizwe upya retrial hivyo ndivyo sheria inataka wafanye.

Hiyo ni sheria Mkuu, kama ni wakili utaelewa ninachojaribu kukiwaza ila kama si wakili, basi Mkuu sheria huwa inatasiriwa sio kuja na dhana iliyo nje ya hiyo sheria.
 
Wakati tunamuuliza kicheche kwanini aliua kuku bila hatia ........swali ni kwanini pia kuku Allenda kwenye mitaa ya kicheche bila sababu
 
Kama tukitumia mantiki, Mahakama ya Rufaa haina mamlaka au uwezo wakusikiliza trial uwezo wake ni kisikiliza Rufaa, kufanya marejeo na mapitio pia.

Kama ni kesi kuanza kusikilizwa upya wanatoa amri ya kesi ikasikilizwe upya retrial hivyo ndivyo sheria inataka wafanye.

Hiyo ni sheria Mkuu, kama ni wakili utaelewa ninachojaribu kukiwaza ila kama si wakili, basi Mkuu sheria huwa inatasiriwa sio kuja na dhana iliyo nje ya hiyo sheria.
Logic na common sense ya kufanya trial mpya huku outcome ikiwa ile ile (walks free) regardless ya verdict (guilty/ innocent) itakayotolewa ni ipi?

Hapo nimesema imetumika mantiki (logic).
 
Logic na common sense ya kufanya trial mpya huku outcome ikiwa ile ile (walks free) regardless ya verdict (guilty/ innocent) itakayotolewa ni ipi?

Hapo nimesema imetumika mantiki (logic).
Sheria haipo hivyo Mkuu, ukipata muda kaisome. Walitakiwa kuelekeza na kuishia hapo sio kuwa trial court hawana hayo mamlaka.

Kuendelea mbwle bila kuwa na mamlaka ni kutwngeneza sheria mbaya hasa kwa Mahakama ya juu.

Kama ni layman ni ngumu sana kuelewa hili ila ndio lilivyo. Logic hata kama ikiwa ina logic kiasi gani kama sio utaratibu ni ubatili tu.
 
Sheria haipo hivyo Mkuu, ukipata muda kaisome. Walitakiwa kuelekeza na kuishia hapo sio kuwa trial court hawana hayo mamlaka.

Kuendelea mbwle bila kuwa na mamlaka ni kutwngeneza sheria mbaya hasa kwa Mahakama ya juu.

Kama ni layman ni ngumu sana kuelewa hili ila ndio lilivyo. Logic hata kama ikiwa ina logic kiasi gani kama sio utaratibu ni ubatili tu.
Mahakama imetumia mantiki (Logic). Elewa basi, sheria huwa inatoa mwanya kwa Logic kutumika, na imetumika.

Assume hilo unalosema ni sheria linefanyika, ukiacha kupoteza muda na pesa, kuna utofauti gani na kama halikufanyika?
 
Back
Top Bottom