Dogo alitoroka Shule akaenda anakokujua mwenyewe. Aliporudi aliruka ukuta ili aende bwenini kulala, Mazingira yalikuwa ya giza lakini pia sheria ni kuwa lazima uwe na uniform ya shule muda wote uwapo nje ya shule- Mwizi ana alama! Askari alikuwa anajiami kwani alikuwa anamshambulia mtu asiyejulikana alieruka ukuta wa shule usiku na kwenye giza nene.Marehemu alitakiwa ajitambulishe na pengine ata kumwita mlinzi kwa jina lake ingesaidia kutoshambuliwa zaidi mpaka ikapeleka kifo chake. (HAYA NI MAWAZO YANGU SIO UKWELI WOWOTE NISINUKULIWE VIBAYA)Duhh
Dogo alitakiwa ajitambulishe na ata kumwita jina Kamanda! Uenda angepigwa ubapa mmoja tu na angeishia suspension na angerudi shule.Nadhani mwanafunzi alikuwa anaenda disco ( adolescence / Nyege). Mlinzi hakuwa na nia ya kuua bali alitaka kukamata aliyemdhani ni jambazi au mbakaji labda, ndio maana hakutumia bunduki (kama alikuwa nayo).
Yeah, ila adhabu ya miaka minne kwa manslaughter ni ndogo, walau mitanoDogo alitakiwa ajitambulishe na ata kumwita jina Kamanda! Uenda angepigwa ubapa mmoja tu na angeishia suspension na angerudi shule.
Wapo tele bado🤣🤣🤣msipeleke watoto wenu scolastica
Watauawa halafu kunakuwa hamna kesi
Msijesema hatujawaambia🤣🤣
Haya👌👌🤔
Mtu kukufia ghafla sio rahisi jamani,we unavyosikia mtu mpaka anamchoma kwa gunia mbili za mkaa mchezo,mara mwingine anabomoa sakafu anazika ndani na mwingine anaenda kutupa huko mtoni,kifo cha ghafla acha kabisa.Watakuwa waliogopa shule kupata jina baya na kupoteza biashara, maana mlinzi kuua mwanafunzi (hata kama alidhani ni jambazi) ni kitu kinachotisha sana wazazi, kwahiyo mwenye shule ili kulinda biashara yake nadhani waliamua kuficha ushahidi wa mauaji mtoni
Oya kwa yoyote humu aliyekuria / kuishi mazingira Yale ya Himo na anaepaelewa kule mto Ghona hadi kule nyuki hd kipande cha mieresini tujuane, binafc kitambo sana pande zile [emoji3] karibu na Shule ya scolastica kuna hospitali ya Dokta wangu pendwa Dkt. Lazaro I wish km mpk Leo Bado yupo site ile aiseeMahakama imemuachia huru aliyekuwa mlinzi wa Shule ya Sekondari Scolastica, iliyopo mji mdogo wa Himo wilayani Moshi, Hamis Chacha (34) aliyehukumiwa kifo kwa kosa la kumuua kwa makusudi mwanafunzi wa shule hiyo, Humphrey Makundi.
Chacha ameachiwa huru baada ya jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani Tanzania kusikiliza rufaa, kushusha shitaka lake kutoka mauaji ya kukusudia na kuwa ya bila kukusudia, baada ya kubaini hakuwa na nia ovu ya kuua.
Maelezo ya kosa hilo yanaeleza kuwa Septemba 6, 2017 saa 2 usiku, katika mji wa Himo, mlinzi huyo alimuua mwanafunzi Humphrey aliyekuwa kidato cha pili kwa kumpiga na ubapa wa panga.
Baada ya kesi kusikilizwa, Juni 3, 2019 Jaji Firmin Matogolo alimtia hatiani.
Kwa mujibu wa maelezo hayo, siku hiyo (Septemba 6, 2017) mlinzi akiwa doria nje ya uzio wa shule, alisikia kishindo cha mtu kuruka ukuta kutoka ndani ya shule.
Alipofuatilia aliona mtu akikimbia, alimkimbiza na alipomkaribia alimpiga kwa ubapa wa panga lakini hakusimama.
Mlinzi aliendelea kumkimbiza, umbali mfupi baadaye, mtu huyo alianguka. Alimsogelea na kumpiga tena kwa ubapa wa panga, mtu huyo ambaye wakati huo hakuwa amemtambua hakuamka tena.
Mlinzi huyo alimpigia simu mmiliki wa shule, Edward Shayo na mwalimu wa nidhamu, Laban Nabiswa; walibaini mtu yule ni mwanafunzi Humphrey Makundi (16) na alikuwa amekufa, ndipo walijadiliana na kuamua kuutupa mwili katika Mto Ghona ulio jirani na shule. Mwili uligundulika Septemba 12, 2017 katika mto huo ukiwa umeanza kuharibika na ilibainika ni wa mwanafunzi huyo.
Shayo, Nabiswa na Chacha walikamatwa na kuhusishwa na mauaji ya kukusudia ya mwanafunzi huyo.
Baada ya Mahakama kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili, iliwaondoa Shayo na Nabiswa katika kosa la mauaji ya kukusudia na kuwatia hatiani kwa kosa dogo la kuficha taarifa za tukio hilo na kuwahukumu kifungo cha miaka minne jela.
Wawili hao walishamaliza kutumikia vifungo vyao gerezani na kurejea uraiani; mlinzi huyo akimtumia Wakili David Shillatu alikata rufaa kupinga kutiwa hatiani na adhabu ya kifo aliyopewa akiegemea katika sababu kuu mbili za rufaa.
Moja walipinga uchukuaji wa maelezo ya ungamo kwa mlinzi wa amani kuwa hayakufuata mwongozo wa Jaji Mkuu na hayakuungwa mkono na ushahidi mwingine, hapakuwa na nia ovu; na pili shitaka halikuthibitishwa bila kuacha shaka.
Chanzo: Mwananchi
Bwana Shayo pesa anazo bhn[emoji1787][emoji1787][emoji1787]msipeleke watoto wenu scolastica
Watauawa halafu kunakuwa hamna kesi
Msijesema hatujawaambia[emoji1787][emoji1787]
Haya[emoji108][emoji108][emoji848]
Kule kumtupa ndiko kulikowafunga wenzake adhabu ndogo.Kwanini wamtupe? Maamuzi mengine ya kijinga sana.
AmenMarehemu aendelee kupumzika kwa amani mahali pema, wazazi poleni sana.
Nadhani mantiki (logic) imefanya kazi yake. Maana kesi mpya ya ‘kuua bila kukusudia’ ikisikilizwa, there can be only one outcome, regardless ya hukumu, ni kwamba the guy walks free. Akishindwa kesi na kuhukumiwa adhabu stahiki (miaka 4) basi atakuwa amashamaliza adhanu yake (time served), hivyo he walks. Akishinda kesi, he walks.Title ya uzi na uzi husika ni vitu viwili tofauti.
Sio kwamba imemuachia huru, hapana ni kuwa rufaa yake imekubaliwa nusu ila wakamrudisha kwenye kosa la kuua bila kukusudia, kisha kwenye adhabu wazee wakajikuta imeshakamilika.
Sasa swali la msingi ni je, Mahakama ya rufaa inaweza kuwa mahakama ya kusikiliza kesi mpya? trial court jibu la awali kabisa ni hapana, sasa swali ni je, kilichofanyika ni marejeo, mapitio au kusikilizwa kesi trial?
Huu mjadala niishie hapa, ntaend kusoma zaidi na zaidi
Na huyu OCS Juma alibaki salama kwenye utumishi wa umma??
"Mlinzi alishauri mtu yule asiyefahamika awahishwe hospitali kwani anaweza akawa bado yuko hai lakini Mkuu wa Shule, kwa kuhofia usumbufu ambao ungejitokeza, akashauri mtu yule atupwe kwenye Mto Ghona ulio umbali wa mita zaidi ya 300 kutoka ilipo shule ya Scolastica. Mwalimu Labani, akishirikiana na mlinzi, wakatekeleza ushauri ule huku mwenye shule akiwaambia mambo mengine yote wamwachie yeye."
"Mwenye shule akawasiliana na Inspekta Idd Juma ambaye alikuwa ni Mkuu wa Kituo cha Polisi Himo. Haikujulikana walichowasiliana lakini mnamo Novemba 10, 2017, polisi wa Himo, wakiwa na mkuu wao wa kituo, walienda mto Ghona na kuuopoa mwili ule na kuupeleka Hospitali ya Mawenzi. Kwenye miamala ilionekana Mzee Shayo alimtumia kiasi cha Sh500,000 Mkuu wa Kituo cha Himo."
Fortunatus Buyobe, mwandishi wa habari za uchunguzi
Kama tukitumia mantiki, Mahakama ya Rufaa haina mamlaka au uwezo wakusikiliza trial uwezo wake ni kisikiliza Rufaa, kufanya marejeo na mapitio pia.Nadhani mantiki (logic) imefanya kazi yake. Maana kesi mpya ya ‘kuua bila kukusudia’ ikisikilizwa, there can be only one outcome, regardless ya hukumu, ni kwamba the guy walks free. Akishindwa kesi na kuhukumiwa adhabu stahiki (miaka 4) basi atakuwa amashamaliza adhanu yake (time served), hivyo he walks. Akishinda kesi, he walks.
Ila hapa kuna swali la kujiuliza, miaka mi4 ni adhabu tosha kwa kosa kubwa kama hilo? Hivi si ilibidi apigwe miaka kama 20 hivi au? Sheria inasemaje?
Logic na common sense ya kufanya trial mpya huku outcome ikiwa ile ile (walks free) regardless ya verdict (guilty/ innocent) itakayotolewa ni ipi?Kama tukitumia mantiki, Mahakama ya Rufaa haina mamlaka au uwezo wakusikiliza trial uwezo wake ni kisikiliza Rufaa, kufanya marejeo na mapitio pia.
Kama ni kesi kuanza kusikilizwa upya wanatoa amri ya kesi ikasikilizwe upya retrial hivyo ndivyo sheria inataka wafanye.
Hiyo ni sheria Mkuu, kama ni wakili utaelewa ninachojaribu kukiwaza ila kama si wakili, basi Mkuu sheria huwa inatasiriwa sio kuja na dhana iliyo nje ya hiyo sheria.
Sheria haipo hivyo Mkuu, ukipata muda kaisome. Walitakiwa kuelekeza na kuishia hapo sio kuwa trial court hawana hayo mamlaka.Logic na common sense ya kufanya trial mpya huku outcome ikiwa ile ile (walks free) regardless ya verdict (guilty/ innocent) itakayotolewa ni ipi?
Hapo nimesema imetumika mantiki (logic).
Hivi bachelor akifiwa na mtoto hawezi kua na uchungu?Binafsi ningeenda tafuta uchawi mkali Sana[emoji15][emoji15]
NB; mtoto anauma sana, ma bachelor hamuwezielewa hata nikiwaelewesha
Mahakama imetumia mantiki (Logic). Elewa basi, sheria huwa inatoa mwanya kwa Logic kutumika, na imetumika.Sheria haipo hivyo Mkuu, ukipata muda kaisome. Walitakiwa kuelekeza na kuishia hapo sio kuwa trial court hawana hayo mamlaka.
Kuendelea mbwle bila kuwa na mamlaka ni kutwngeneza sheria mbaya hasa kwa Mahakama ya juu.
Kama ni layman ni ngumu sana kuelewa hili ila ndio lilivyo. Logic hata kama ikiwa ina logic kiasi gani kama sio utaratibu ni ubatili tu.