Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
Mkuu
Wananchi ndo wakulaumiwa, wananchi wakiipa kura upinzani 90% na ccm 10% nafikiri wataiba wee mpaka watashindwa kuiba kura na hatimaye upinzani kushika hatamu. Sijasoma katiba hasa kwenye hiyo kipengele sijui inasema je?
Unajua kaka, katiba yetu inahitaji kuchambuliwa kwa kina kwa sababu ina mapungufu mengi sana. Nadhani kijamvi hiki kinaweza kusaidia kuibua mawazo mazuri ya kuiboresha katiba yetu. Sasa nilipokuwa najiandaa kuanzisha thread ya namna hiyo nikagundua kuwa tukichambua ile version ya kiswahili inawezekana tukawa tunakosea kwa sababu inaweza ikawa ina tofauti na version ya kiingereza.Mkuu kama tusipoweza jivunia lugha yetu bungeni basi ndio tumedoda Utumwani..
Katiba yenyewe ipo katika lugha gani ?
Kuna nakala iliyoandikwa kiswahili, na vile vile ipo nakala iliyoandikwa kwa kiingereza!!!
nimefurahi kuona kiswahili kimepewa kipaumbele kwenye poll hapo juu. Watanzania wengi hawana kiingereza cha kutosha kuweza kuifahamu katiba pia si muhimu kwa vile tuna lugha yetu..hata hivyo makala nyingi ninazosoma kwenye thread tofauti humu hushindwa hata kuelewa kiswahili kinachozungumzwa na inasikitisha kuona kuwa tunakubali standard ya lugha yetu kuporomoka, au pengine ni mimi tu nnahisi hivyo
KISWAHILI
-------------------------------------------------------------------------------------------------- KIINGEREZA[/SIZE][/U]
Tunaanza na DIBAJI - Preamble
Maoni Yangu
- Ni lazima Katiba hii ibadidlishwe kuondoa neno ujamaa katika dibaji hiyo na sehemu nyingineyo yoyote ya katiba; nitakuwa nalionyesha kwa rangi nyekundu kila tutakapolifikia. Siyo kweli kuwa Tanzania ni nchi ya kijamaa kwa vile imeshamiri ubepari. Tunaikosesha heshima katiba yetu kwa kuweka vifungu vya uongo, yaani ambavyo siyo vya kweli.
- Dibaji ya kiingereza inasema kuwa Tanzania ni "secular state" yaani haufungamani na dini yoyote, lakini tafsiri ya kiswahili haikonyesha hivyo. Sijui wenzangu mnaonaje hilo, je lilifanyika makusudi.
- Dibaji ya katiba hii inaonyesha kuwa Tanzania tunafuata utawala wa kidemokrasia uliojengwa kwa mihimili mitatu isiyoingiliana: Serikali, Bunge, na Mahakama. Halafu bunge linawakilisha wananchi likiwa na wajumbe waliochaguliwa na wananchi hao:
Je ni Kweli kuwa
- Bunge letu linawakilisha wananchi kama katiba inavyotaka iwapo kuna wajumbe ambao hawakuchaguliwa na wananchi? Kwa sasa bunge la Tanzania lenye wajumbe 325, waliochaguliwa na wananchi ni 231 tu, sawa na asilimia 71. Je bunge hilo kweli linafanaya kazi kwa niaba ya wananchi?
- Serikali haiingiliani na bunge huku ikiteua wabunge kuwa mawaziri, na veile vile rais kuteua wabunge wengine?
- Je ni kweli kuwa serikali inawajibika kwa bunge huku waziri mkuu akiwa na sauti ya mwisho bungeni na wakti mweingine hata kukemea wabunge?
Mkuu neno hili (Ujamaa) linakudhuru kitu gani wewe? Unataka tuweke neno la (Ubepari)? ndilo unalotaka? mimi sioni umuhimu wowote wa kulibadilisha hilo neno la (Ujamaa) kwani Siasa ya nchi yetu ni ya Kijamaa na kujitegemea sio Siasa ya Kibeparai mkuu upo na mimi?
Siyo kwamba nachukia ujamaa, lengo langu wakati naannzisha tthread hii ni kuangalia upungufu wa katiba yetu ili tupate mawazo ya kuinyoosha. Kuweka ndani ya Katiba kuwa tunajenga taifa la kijamaa ilhali tunajua kuwa hatufanyi hivyo, ni ama tudharau na kukiuka katiba yetu makusudi, au katiba hiyo siyo ni kitu serious.Mkuu neno hili (Ujamaa) linakudhuru kitu gani wewe? Unataka tuweke neno la (Ubepari)? ndilo unalotaka? mimi sioni umuhimu wowote wa kulibadilisha hilo neno la (Ujamaa) kwani Siasa ya nchi yetu ni ya Kijamaa na kujitegemea sio Siasa ya Kibeparai mkuu upo na mimi?
Ninataka kuanzisha thread ya kujadili Katiba ya Tanzania. Nina kopi mbili za katiba hiyo, moja ni ya kiswahili, na moja ni ya kiingereza. Kwa bahati mbaya, kama tulivyoona kwenye hotuba ya bajeti, katiba hizo mbili zinatoa tafsiri zinazotofautiana katika baadhi ya vifungu vyake. Je ni lugha ipi itumike katika kujadili katiba hiyo kwa ufanisi?
Mahakama iliwahi kusema katika kesi ya Director of Public Prosecutions v. Daudi Pete [1993] TLR 22 (CA) katika ukurasa wa 23 kama ifuatavyo: "As the Constitution of the United Republic of Tanzania is established in the Kiswahili language, the controlling version in interpreting the Constitution is the Kiswahili and not the English version."
Kwa hiyo kama mnatafsiri Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, msitumie version ya Kiingereza, tumieni ya Kiswahili!
Mahakama iliwahi kusema katika kesi ya Director of Public Prosecutions v. Daudi Pete [1993] TLR 22 (CA) katika ukurasa wa 23 kama ifuatavyo: "As the Constitution of the United Republic of Tanzania is established in the Kiswahili language, the controlling version in interpreting the Constitution is the Kiswahili and not the English version."
Kwa hiyo kama mnatafsiri Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, msitumie version ya Kiingereza, tumieni ya Kiswahili!