Movement: Tunataka Katiba Mpya Tanzania

Movement: Tunataka Katiba Mpya Tanzania

Hivi Nagu alisoma Sheria au ana experience ya Mambo ya Sheria hadi awe na akili timamu za kuongoza hiyo wizara?

Imenibidi niulize maana naona anaongea kama KADA wa CHAMA badala ya waziri wa sheria na katiba.
 
Angalau kakiri kwamba CCM kuwa madarakani ni ujanja ujanja tu maana katiba inawapa upendeleo na mabadiliko yanatakiwa . Hili ni muhimu sana na sasa litavaliwa njuga ili kuleta usawa na maendeleo kwa Tanzania na si CCM kwanza Tanzania nyuma no . JK umesikia waziri wako anasema Katiba ni mbovu lakini hamjaamua lini iwe imara ?
 
Angalau kakiri kwamba CCM kuwa madarakani ni ujanja ujanja tu maana katiba inawapa upendeleo na mabadiliko yanatakiwa . Hili ni muhimu sana na sasa litavaliwa njuga ili kuleta usawa na maendeleo kwa Tanzania na si CCM kwanza Tanzania nyuma no . JK umesikia waziri wako anasema Katiba ni mbovu lakini hamjaamua lini iwe imara ?

Lunyungu, Asante.

CCM ni waoga mno hawako tayari kuishi bila dola na katiba ya sasa.Mtu huru mara nyingi husema kuwa hawa jamaa bila dola na katiba mbovu ya sasa ni weupe sana!!!
 
Wanabodi,
Hivi waziri wa Katiba na Sheria huchaguliwa na nani? huyu ndiye mwajiri wake! na mwajiri wake anasema nini kuhusu Katiba!..

Safari ni ndefu sana ukitazama mgangilio wa serikali yetu toka chama kimoja!..maslahi ya wananchi ni ya mwisho ktk utaratibu wetu. Inabidi tukubali ukweli kwamba mabadiliko ya KATIBA yatashindwa Mahakamani na hata Bungeni...tunaweka matumaini ya bure hamala ambapo kesii hi ya Nyani na hakuna hakimu isipokuwa Ngedere!...
 
Nagu bure kabisa yule. Hivi kweli alifikaje kupata madaraka yale? Namjua kipindi fulani akiwa Meneja kwenye mojawapo ya viwanda vya Morogoro pale alikuwa mchangamkiaji sana wa vijana wa kiume. Sijui siku hizi labda amekuwa mtu mzima hivyo katulia mambo hayo lakini nadhani busara haijamjengeka bado.

Tunajua kuwa kuna tume kadhaa zilizokuwa zinaongozwa na majaji ziliweka bayana kuwa katiba hii ina mapungufu halafu dada huyu waziri wa sheria anasema hakuna haja ya kubadiri katiba? Yaani anawaona wale majaji waliopendekeza mabadiliko ya katiba ni viazi?
 
Another waste, hawara turned politician by Sumaye, hiyo peke yake tu speaks all!

But, ni changamoto nzito kwa wananchi na upinzani kuingia mtaaani ili kujenga hoja ya kuibadili katiba yetu, maana sio siri inahitaji viraka! Ni muhimu waziri wa sheria kawa mwanasheria!
 
hivi bado yuko serikalini huyu? maana nasikia liakuwa mgonjwa mgonjwa huyu
mambo ya utu uzima

uuuuuuu.JPG
 
hata wabunge hawana haki ya kuiona bali ni wanene wachache tu wenye haki hiyo!
~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~

Mikataba ya madini kutopelekwa bungeni
na Peter Nyanje na Rachel Chizoza, Dodoma

SERIKALI imesema haitakuwa tayari kupeleka bungeni mikataba mbalimbali inayohusu madini, kwani kufanya hivyo ni kukiuka kanuni na taratibu za miktaba husika, Bunge limeelezwa.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, alipojibu swali la Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed (CUF), aliyeuliza swali la nyongeza bungeni hapo kuwa, serikali inatumia kifungu gani kuwanyima wabunge nyaraka mbalimbali za kiserikali pamoja na mikataba.

Waziri Karamagi alisema serikali haijakataa kumpa mbunge nyaraka mbalimbali zinazohusu serikali, lakini kuhusu mikataba, serikali haitakuwa tayari kuleta mikataba hiyo na kujadiliwa bungeni kwani mikataba hiyo huwa ni siri, hivyo kufanya hivyo itakuwa ni kuanika hadharani mikataba hiyo kitendo ambacho alisema hakiruhusiwi kisheria.

Naye Mbunge wa Viti Maalum, Halima Mdee (CHADEMA) katika swali lake la nyongeza, alisema serikali inaingia mkataba kwa niaba ya wananchi kwa maovu ambayo wanataka, hivyo kwa nini serikali haioni haja ya kuwapa wabunge mikataba hiyo nao waione, na badala yake mikataba hiyo imekuwa siri kubwa serikalini.

Akijibu swali hilo, waziri huyo alisema suala la mkataba wa biashara ni tofauti na suala la maovu, hivyo mbunge anaruhusiwa kupewa kipengele ambacho anaona ana shaka nacho, lakini si mkataba mzima.

Kwa kweli serikali haiwezi kuleta mkataba mzima bungeni, ili kila mbunge aweze kuuona, kwani mkataba ni suala la kiushindani, hivyo ukileta bungeni na kuanza kujadili huyu kafanya hivi kapata hivi, utakuwa unatangaza hadharani mkataba huo ambao ni siri na hauruhusiwi kufanyiwa hivyo, alisema.

Katika swali la msingi, mbunge, Hamad Rashidi Mohamed, aliitaka serikali kulieleza Bunge kuwa ilipanga kupitia mikataba mingapi na ni ipi kwa majina.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, alisema serikali ilipanga kupitia mikataba yote mitano ambayo iliingia na kampuni kubwa za uchimbaji wa dhahabu.

Mikataba hiyo ni kati ya serikali na Kampuni ya Bulyanhulu Gold Mine Limited inayomiliki mgodi wa Bulyanhulu ulioko katika Wilaya ya Kahama, Pangea Minerals Limited inayomiliki mgodi wa Tulawaka ulioko wilayani Biharamulo, North Mara Mine, wilayani Tarime, Geita Gold Mine Limited na Resolute Tanzania Limited inayomiliki mgodi wa Golden Pride, wilayani Nzega.

Hata hivyo, alisema kazi ya kupitia mikataba yote ilikamilika Julai 2006 na majadiliano kati ya serikali na kampuni moja moja yanaendelea, ili kuhakikisha taifa linanufaika ipasavyo na maliasili yake, lakini marekebisho ya mfumo wa kodi yanakusudiwa kufanywa katika sekta ya madini.
 
kuna dubious deals ndio maana hawawezi kupeleka bungeni, may be katika part of the contract kuna kuupeana hisa etc
 
Mikataba inayosainiwa kwa niaba ya wananchi iweje siri mbele ya wananchi wenyewe? Wawakilishi wa wananchi ni Wabunge, sio serikali. Serikali inatumia watendaji kama Kamishina wa Madini kufanya mazungumzo. Hawa si wawakilishi wa wananchi. Wasiingie mikataba inayowafunga wananchi kisheria kabla ya wananchi, kwa kupitia wawakilishi wao, kuiona na kuikubali.

Ushindani gani anaozungumzia Waziri? Kuna kuogopa kwamba wawekezaji wengine watatoa tamko kwamba walitoa mpango mzuri zaidi na ukakataliwa?

Hata kama kungekuwa na haja ya siri, basi Kamati husika za Bunge zinaruhusiwa kujadili hata siri za serikali. Mbona Kamati ya Ulinzi na Usalama inajadil siri nyingi tu? Kamati ya Uchumi na Maendeleo haiwezi kunyimwa kujadili mikataba kwa kisingizio kwamba ni ya siri.

CCM watawadanganya hata wabunge wao mpaka lini?

Augustine Moshi
 
Serikali yakataa mjadala wa Katiba

Na John Daniel, Dodoma

SERIKALI imesema haina mpango wa kuanzisha mjadala wa kitaifa kuhusu mabadiliko ya Katiba ya Nchi na kwamba hivi sasa inaendelea na utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa na wananchi kupitia Waraka Namba Moja wa Serikali mwaka 1998.

Pia imesisitiza kuwa haikuridhika na uamuzi uliotolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania katika kesi namba 10/2005 kuhusu kuwepo kwa mgombea binafsi katika uchaguzi mbalimbali hivyo imekata rufaa juu ya suala hilo katika Mahakama ya Rufaa ya
Tanzania.

Hayo yalisemwa bungeni jana na Naibu Waziri wa Sheria na Katiba, Bw. Mathias Chikawe, wakati akijibu swali la Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Bw. Zitto Kabwe (CHADEMA).

Katika swali lake, Bw. Kabwe aliitaka Serikali kutoa ufafanuzi kuhusu utekelezaji wa hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania, kuhusu mgombea binafsi na kuanzisha mjadala wa kitaifa ili kuifanyia marekebisho Katiba ambayo inatakiwa kutamka kuwapo kwa nafasi hiyo katika uchaguzi mbalimbali.

"Ni kweli Mahakama Kuu ya Tanzania imetoa hukumu ambayo inaitaka Serikali kuwasilisha bungeni Muswada wa Sheria ya kufanya mabadiliko katika Katiba ya Nchi ili kuruhusu
dhana ya ugombea binafsi katika uchaguzi, Serikali haikuridhika na uamuzi huo na hivyo imetaka rufaa katika Mahakama ya Rufani ya Tanzania. Kwa sasa Serikali haiwezi kujadili suala hilo kwa kuwa bado liko mahakamani.

"Kuhusu suala la kuanzisha mjadala wa mabadiliko ya Katiba ya nchi, napenda kueleza kwamba kwa sasa Serikali haina mpango huo, mambo mengi yalipendekezwa kupitia Waraka wa Serikali Namba Moja 1998, Serikali imekuwa ikirekebisha Katiba kwa kuzingatia mapendekezo hayo kwa awamu," alisema Bw. Chikawe.

Alisema Serikali iliutumia waraka huo kukusanya maoni ya wananchi kuhusu mabadiliko ya Katiba na kwamba kwa kuzingatia mapendekezo hayo, suala la uwakilishi mizania kuboresha mfumo wa uchaguzi ni miongoni ma masuala ambayo Serikali inayatekeleza na kwamba wabunge wa viti maalumu wanaingia bungeni kwa sheria hiyo.

"Hata hivyo napenda kumweleza Mbunge kwamba yeye akiwa raia wa nchi hii, ana haki ya kufikisha maoni au mapendekezo yake kwenye vyombo vinavyohusika, ikiwamo Wizara ya Katiba na Sheria ili yaweze kufanyiwa kazi wakati muafaka utakapowadia," alisema Bw. Chikawe.
 
Sasa hapa ndipo ninaanza kuhisi harufu ya damu.
  1. Utendaji mbovu wa serikali unasababishwa na mapungufu ya katiba; serikali inaogopa katiba mpya kwa vile itawafanya wawe accountable kwa wananchi. Kama hawataki kuwa accoutnable kwa wananchi je, wako accountable kwa nani?
  2. Katiba hii iliandikwa zamani na inawezekana kabisa kuwa ilitosheleza katika mazingira ya wakati ule ambapo usiri ulikuwa ni wa muhimu kwa usalama wa taifa. Leo hii katika dunia ya utandawazi mambo yamebadilika sana kiasi kuwa katiba ile haitoshelezi tena.
  3. Kama serikali hawana cha kuhofia, kwa nini wasiruhusu taifa zima lishiriki katika kuandika katiba mpya? Kwani katiba ipo pale kwa ajili ya nani? taifa au serikali?
  4. Mzee Mwinyi aliruhusu mjadala wa vyama vingi, na ingawa asilimia kubwa ilikataa vyama vingi bado mzee yule aliona mbali akatoa RUKSA kwa vyama vingi. Je mnataka tumwite mzee Mwinyi tena arudi madarakani ili aturekebishia katiba pia?
 
Inasikitisha sana. Katiba yetu ina mapungufu mengi sana lakini wanayafumbia macho kama hawayaoni. Wanachagua yale wanayoyataka wao ambayo hayatawapunguzia madaraka yao pamoja na ulaji ili waweke viraka kwenye katiba. Kama hili la dual citizenship wanataka kuliruhusu lakini kuna wengine hawajui waanzie wapi.

Sasa kwa nini tusiichambue katiba yote ili kuja na katiba ambayo itaondoa mapungufu yote yaliyokuwemo kwenye katiba ya mwaka 47!?

Kama kuna mtu anaweza akaiweka katiba yetu hapa JF ili tuanze kuichambua kama Watanzania (siyo kama wana CCM, CHADEMA n.k.)
 
Nchi nyingi hata majirani wana mchakato wa kuangalia katiba zao- juzi tu Zambia wameanza mchakato, Kenya naamini itaangaliwa tena baada ya uchaguzi- CCM wanaogopa nini? Why are they so conservative kubadilika?

Kwa hiyo hadi CCM iondolewe madarakani ndo tuwe na katiba mpya? Sielewi huu woga unatokana na nini? Changes are for good of Tz, kuna watu kwani wanaitakia Tz mabadiliko mabaya?

Basi Mwalimu alivyofariki- hakuna wa kuuliza kitu CCM- hadi wajiskie wenyewe kwenye roho zao? Iko siku- Moi alidhani KANU siku zote NI Kenya- hata hapa Tz iko siku pia CCM watalazimishwa na nguvu za wananchi kuwa Tz sii ya CCM ni ya Wtz wote- kuna watu wengi sii wanachama wa vyama vya siasa! If is a matter of time!
 
Hawa jamaa hawawezi kuibadilisha hii katika kwa sababu ina maslahi na wao. kweli raisi anaweza kukubali kubadilishwa katiba wakati inampa ulaji?
 
Ninashauri kuwa tumwombe mzee wetu Rais Ali Hassan Mwinyi atungoze katika kuendesha mjadala wa kuboresha katiba yetu. Alitungoza kwenye mabadiliko makubwa ya kutoka kwenye uchumi wa kijamaa na kutuingiza kwenye uchumi wa soko huria, halafu akatungoza kutoka mfumo wa chama kimoja kutuweka kwenye mfumo wa vyama vingi, mnaonaje akitusaidia hili dogo la kutuongoza kufanya mjadala wa kuboresha katiba yetu hasa kwa vile viongozi waliopo sasa hawataki kusikia neno katiba?
 
Wazo zuri sana. Hivi katika petition Tanzania, kuna idadi maalum ya watu inayotakiwa au wanahitajika washiriki wengi iwezekanavyo?
 
Hili la mjadala wa Katiba halitatokea kama CCM hawataki period. What CCM wants CCM gets, it doesn't want this so we won't get it. Ndio maana mimi naona kujaribu kubadilisha Katiba wakati hauna nguvu ya kufanya hivyo ni kutwanga maji kinuni. Hadi pale wapinzani wananguvu ya kulazimisha siyo kuomba kama wanavyofanya sasa.
 
Back
Top Bottom