๐— ๐—ฝ๐—ฎ๐—ธ๐—ฎ ๐——๐—ฃW ๐˜„๐—ฎ๐—ป๐—ฎ๐—ฐ๐—ต๐˜‚๐—ธ๐˜‚๐—ฎ ๐˜‚๐—ฑ๐—ต๐—ถ๐—ฏ๐—ถ๐˜๐—ถ ๐˜„๐—ฎ ๐—ฏ๐—ฎ๐—ป๐—ฑ๐—ฎ๐—ฟ๐—ถ ๐˜‡๐—ฒ๐˜๐˜‚ ๐—บ๐—ฎ๐—ฝ๐—ฎ๐˜๐—ผ ๐—ป๐—ถ ๐˜€๐—ถ๐—ฟ๐—ถ ๐—ธ๐—ฎ๐˜๐—ถ ๐˜†๐—ฎ ๐—ฆ๐—ฎ๐—บ๐—ถ๐—ฎ ๐—ป๐—ฎ wao

๐— ๐—ฝ๐—ฎ๐—ธ๐—ฎ ๐——๐—ฃW ๐˜„๐—ฎ๐—ป๐—ฎ๐—ฐ๐—ต๐˜‚๐—ธ๐˜‚๐—ฎ ๐˜‚๐—ฑ๐—ต๐—ถ๐—ฏ๐—ถ๐˜๐—ถ ๐˜„๐—ฎ ๐—ฏ๐—ฎ๐—ป๐—ฑ๐—ฎ๐—ฟ๐—ถ ๐˜‡๐—ฒ๐˜๐˜‚ ๐—บ๐—ฎ๐—ฝ๐—ฎ๐˜๐—ผ ๐—ป๐—ถ ๐˜€๐—ถ๐—ฟ๐—ถ ๐—ธ๐—ฎ๐˜๐—ถ ๐˜†๐—ฎ ๐—ฆ๐—ฎ๐—บ๐—ถ๐—ฎ ๐—ป๐—ฎ wao

Bro utaonekana msaliti lakini jina lako litakumbukwa siku ambayo wanyonywaji wataishiwa damu na kuanza kutapatapa kama wafa maji.

Hii nchi imejaa upuuzi wa hali ya juu. Wachache wanaoifaidi hawajali as long as wanapokea mikwanja ya kushanta kwenye offshore accounts na familia zao ziko well off

Kwa kweli uharamia aliotufanyia Rais Samia na genge lake kupitia ile IGA ya kishenzi, inatosha kufuta zuri lolote alilolifanya kwa Tanganyika. Lakini ipo pia ile mikataba ile 30 ya hovyo ya kuwagawia waarabu misitu na mbuga zetu za wanyama. Kwa uharamia ule, hawa watu kuna siku wataulipa. Katika uharamia huo wote, hakuna rasilimali hata moja ya Zanzibar, zote ni za Tanganyika.
 
iwe kweli au isiwe kweli, historia inatufundisha kwamba, hakuna mkataba hata mmoja ulio wacost watanzania ambao haukupigiwa kelele kabla ya kusainiwa. watanzania huwa wanapinga kwa kelele nyingi, viongozi wanalazimisha kwa maslahi yao na familia zao, na mwisho wao wenyewe wanakuja kukiri kwamba walikosea, hawafanywi chochote kwa kukosea huko, wanaendelea kumiliki utajiri mkubwa wao na familia zao, wanaandika vitabu, wanakufa, tunawapa heshima. imeisha hiyo. hakuna jipya duniani, kila kitu ni ubatili tu.
Kwa kweli huyu mzanzibari, kwa suala la kupora rasilimali za Tanganyika na kisha kuziuza kwa Waarabu, amewachafua wengi.
 
Siku Ile ya kusaini HJA pale Dodoma, ukiiangalia video Ile,

Yule mzungu alivyokuwa na wasiwasi, lazima tu ustuke, pale yalikuwa ni maigizo na utapeli.
Samia, Mbarawa, Rostam, Abdul na hawa wengine waliohongwa pesa ndogo ndogo, hawastahili kusamehewa milele. Uharamia wao utabakia katika historia kizazi hadi kizazi.
 
Bandari tulikua tunaendesha wenyewe tukakosa uaminifu wizi , rushwa na ukwepaji kodi ulikua mkubwa sana.hivi sasa mambo hayo hakuna .bandari ilikua ni kichaka cha wapigaji. Mama samia kafanya vizuri sana kuibinafsisha.
Ule siyo ubinafsishaji bali ni uporaji wa rasilimali. Soma IGA ndiyo utajua kuwa ule ni ushenzi wa hali ya juu.
 
Nasemaje,

Ubatili huu utakomeshwa tu,

Na HAKIKA tutawafukuza hao maharamia.

Kesi Iko mahakamani na mahakamani ilikiri IGA ni BATILI.

Hatimaye tutashinda.
Ni kweli. Mahakama ilisema wazi kuwa mkataba ni batili kwa kuwa unapingana na sheria za nchi, lakini kwa vile bunge limeridhia, hawana uwezo wa kuingilia maamuzi ya mhimili mwingine!!
 
Tayari DP World wameshachukua udhibiti wa bandari ambayo ni urithi wetu kutoka kwa Mungu.

1. Mpaka sasa Rais hajaweka wazi Tanzania itapata Tsh. ngapi kwa mwezi kupitia mapato ya bandari ambayo kuanzia sasa yatakusanywa na DP World kama taarifa ya TPA niliyoambatanisha hapa inavyoeleza.

2. Kwamba hapo awali mapato yetu pale bandarini yalikuwa wazi ila kwa sasa yatakuwa siri kati ya DP World na Samia.

3. Pamoja na uboreshaji wa bandari hizo kupitia pesa zetu na mkopo kutoka WB bado Samia na serikali yake hawajaweka wazi kwamba hao DP World wamewekeza kiasi gani zaidi ya kuja kuvuna shamba ambalo tumelilima kwa jasho na damu kwa ajili ya watoto wa Tanganyika na Tanzania.

4. Mpaka sasa Samia na serikali yake wamekataa kuweka wazi mikataba ya kukabidhi bandari hizo kwa waarabu wa DP World. Tunaambiwa ni uwekezaji lakini hatuoneshwi mikataba hiyo ili tuipitie tuone kama uwekezaji huo una faida au hasara.

Samia anapaswa kupingwa na kila mtu mwenye akili timamu na mzalendo wa taifa hili. Sisi hatuna nchi nyingine isipokuwa hii Tanganyika aliyotupa Mungu. Sasa kama Samia atakuwa anaendelea kuingia mikataba ya siri na mibovu ya kuuza rasilimali nitakuwa tayari kwa lolote kulinda rasilimali na ardhi ya nchi yetu.

Mungu bariki Tanganyika.

Mungu bariki Zanzibar.

Mungu bariki Tanzania.

Mdude Mpaluka Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.View attachment 2959439
apo kwenye Mungu ibariki zanzibar umekosea
 
Somo kwa โ€˜bi-tozoโ€™ na maraisi watakao mfuatia hawa ndio watanzania.

Poyoyo mmoja anaweza andika ujinga kutoka kichwani kwake kuhusu income ya shirika ni mijitu ikadhani ana hoja.

Hata hiyo accounting software aiwezi kukupa daily update ya makusanyo iwapo kodi za serikali zinakuwa verified na system nyingine.

Worst alichoweka mleta mada kama sehemu ya ushahidi wake wa records za makusanyo (on bookkeeping entries) ni image ambayo yenye maelezo mengine kabisa na accounting records.

Mtu kajiwekea tu image na kuandika ujinga kama evidence.

Sasa kuna watu wamempa likes kwa huo upuuzi aliondika mleta and gullible enough to support that nonsense.

Ndio โ€˜bi-tozoโ€™ aelewe kuwaletea maendeleo watanzania ni kazi ya kujitolea unaweza tukanwa kwa habari zisizo na kichwa wala miguu.

Na punguani kama ninyi ndio mtamwangamiza bi Tozo.

Ile IGA ni ya kishenzi kabisa kwa sababu inapora sovereignity ya nchi, na pia inakiuka sheria za nchi.

Kikubwa ambacho nampongeza mleta mada, ni kuwakumbusha Watanzania kuwa bandari yetu imeporwa na hawa maharamia kwa kushirikiana na wasaliti wa nchi kupitia IGA ya kishenzi.
 
Tayari DP World wameshachukua udhibiti wa bandari ambayo ni urithi wetu kutoka kwa Mungu.

1. Mpaka sasa Rais hajaweka wazi Tanzania itapata Tsh. ngapi kwa mwezi kupitia mapato ya bandari ambayo kuanzia sasa yatakusanywa na DP World kama taarifa ya TPA niliyoambatanisha hapa inavyoeleza.

2. Kwamba hapo awali mapato yetu pale bandarini yalikuwa wazi ila kwa sasa yatakuwa siri kati ya DP World na Samia.

3. Pamoja na uboreshaji wa bandari hizo kupitia pesa zetu na mkopo kutoka WB bado Samia na serikali yake hawajaweka wazi kwamba hao DP World wamewekeza kiasi gani zaidi ya kuja kuvuna shamba ambalo tumelilima kwa jasho na damu kwa ajili ya watoto wa Tanganyika na Tanzania.

4. Mpaka sasa Samia na serikali yake wamekataa kuweka wazi mikataba ya kukabidhi bandari hizo kwa waarabu wa DP World. Tunaambiwa ni uwekezaji lakini hatuoneshwi mikataba hiyo ili tuipitie tuone kama uwekezaji huo una faida au hasara.

Samia anapaswa kupingwa na kila mtu mwenye akili timamu na mzalendo wa taifa hili. Sisi hatuna nchi nyingine isipokuwa hii Tanganyika aliyotupa Mungu. Sasa kama Samia atakuwa anaendelea kuingia mikataba ya siri na mibovu ya kuuza rasilimali nitakuwa tayari kwa lolote kulinda rasilimali na ardhi ya nchi yetu.

Mungu bariki Tanganyika.

Mungu bariki Zanzibar.

Mungu bariki Tanzania.

Mdude Mpaluka Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.View attachment 2959439
Wewe ni nani hata uanikiwe mapato ya biashara za watu?

Ngoja ripoti za kila mwaka uende BRELA ukachukuwe data za kampuni uitakayo.

Mnajifanya mnajuwa kumbe hamna unachokijuwa.
 
Mdude unapotosha kwa makusudi
Rais ana nguvu gani? Kuna bunge la Tanzania limebariki. Kama unavyosema ndio hivyo Kuna haja gani bodi ya mkopo kusomesha vijana wa Tanzania bara? Maana bunge ndio chenye nguvu nchini
Hakuna kitu pale, ni kwamba walishakaa na kukubaliana kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake sasa ole wako umtaje mwenzio watakusuta mpaka basi, hivi miaka 10 hadi 20 eti hakuna waziri aliyepatikana kwa rushwa, Tz ni ulaya aisee.
 
Ni kweli. Mahakama ilisema wazi kuwa mkataba ni batili kwa kuwa unapingana na sheria za nchi, lakini kwa vile bunge limeridhia, hawana uwezo wa kuingilia maamuzi ya mhimili mwingine!!
Na Bado utabaki kuwa BATILI sababu

1.Hapakuwa na uchaguzi 2020.

2. Wananchi hatukuwatuma wabunge kuuza bandari.
 
Angalau tulijua kuwa tulikuwa tunaibiwa, kulikuwa na option moja mbele, kufanya juu chini kukomesha huo wizi na uzembe, niliuliza hivi, ukiwa baba wa familia, na miongoni mwa watoto wako wakawa wanakuibia hapo nyumbani au shambani utatafuta baba mwingine aje kuisimamia familia yako? Au utatumia nguvu zako za ubaba kuhakikisha kuwa wizi unakoma? Ukishindwa hapo ubaba wako utakuwa na mushkeri.
Nchi inaendeshwa na sheria na taratibu zilizopangwa kwa yeyote atakaekua Rais. Familia yako siku nyingine anaendesha mkeo siku nyingine watoto au mama mkwe.
 
Kutoka CCM? zaidi atairudisha kwenye mikono ya mafisadi wa CCM waitafune hiyo pesa. Mimi naunga mkono bandari kupewa mwekezaji kama mkataba ukiwa rafiki ila sio kuwaachia hao TPA ambao kwa mwaka wa 15 sasa kila ripoti ya CAG inaonyesha wizi wa kutisha. Private sector huwezi iba utafukuzwa tu au kuleta delays ili uhongwe utaondolewa maana ni business oriented.

Mjadala uwe mkataba rafiki sio kuirudisha TPA ni yaleyale tu
Tunaungaga hivi hivi hoja ambazo ni hasara kwetu na mwisho Serikali huja na kauli mbiu ya kuomba msamaha tena tunaongoza kwa kuunga mkono hoja hiyo na kuifanya Serikali ituone mazuzu kila siku.
 
Nyie wajinga na Mwabukusi wako msiturudishe nyuma. Haya mambo ya kisheria na kibiashara hqmuyajui kwa vile hata elimu yenu ni ndogo.

Nenda kafanye unachojuwa zaidi kikupatie fedha ila hili siyo eneo lako. Linahitaji watu wenye akili zao lakini siyo mtu wa calibre yako.
Umeelewa hoja yake lakini mkuu
Au ndo wa kujibu kabla kuelewa
Wazee wa nusu degree
 
Back
Top Bottom