nenda tbsWapendwa habarini.Mimi ni Mtumishi wa Umma nipo Dodoma.Nina nyumba yangu nimeijenga Boko. Nilimaliza kuijenga Mei mwaka huu na Juni nikapata Mpangaji(Mme na Mkewe).
Nilishukuru maana Mpangaji huyu alijitambulisha kwamba ni Mfanyabiashara anayefuata mizigo China hivyo yupo busy sana, alinilipa Kodi ya miaka miwili(nilifurahi sana). Mwanzoni mwa mwezi huu wa Septemba jirani yangu ambaye tumetengana ukuta(fensi) alinipigia na kuniuliza kama nimeigeuza nyumba yangu kuwa godown au kiwanda cha kutengeneza vinywaji maana alidai kunakuwa na kelele za chupa kugongana usiku, nilimjibu hapana lakini nitafanya uchunguzi.
Juzi Jumapili nilikuwa Dar, hivyo mchana nilienda hapo Boko nyumbani kwangu bila kuwapa taarifa. Cha kushangaza nikakuta kafunga CCTV Camera kwenye pembe zote za fensi pamoja na kuweka Mlinzi getini. Nilivyojitambulisha getini Mlinzi hakufungua geti alinizuia kuingia(imagine nyumba yangu lakini nazuiliwa kuingia).
Nikiwa pale getini nahojiana na Mlinzi, ilikuja gari la Polisi ikasimama kwa mbali, kijana mmoja akatoka ndani ya nyumba yangu na kwenda kwenye ile gari na kuwapa naamini pesa na gari ya Polisi ikaondoka, kijana akarudi akaingia ndani, akafunga mlango, hapo mimi nimezuiwa getini. Kwa kifupi ni kwamba Mpangaji wangu huyu anazalisha bidhaa feki(vinywaji feki) na kuziingiza sokoni.
Msiri wangu ameniambia Konyagi, K-Vant, Gin na vinywaji vingine vikali vinazalishwa ndani ya nyumba yangu na kuingizaa sokoni. Naogopa asije akakamatwa mwisho wa siku Serikali ikataifisha nyumba yangu maana nimeambiwa hilo ni Kosa la Uhujumu Uchumi.
Naomba msaada taarifa hii nikaitoe wapi maana msiri wangu kaniambia Polisi wanajua na huwa wanaenda kuchukua posho kama nilivyoshuhudia mimi mwenyewe hivyo hata nikiripoti kwao itakuwa ni kazi bure.
Naomba mwenye mawasiliano na Viwanda vinavyotengeneza Konyagi, K Vant na hizi Pombe Kali za chupa anisaidie tafadhali Ili niwajulishe tushauriane cha kufanya
Nitashukuru sana wapendwa, siku njema
WaTanzania ni watu wa kurukia mambo mtu ameona kwenye thread ameandika kila halafu anauliza swali tena.Kwamba hujasoma chochote alichoandika ukaamua ku comment tu?
Swali gani hili wakati mwenziyo kaeleza kila kitu vizuri kabisa?Vipi Kodi yako Hasumbui Kulipa.? na je unakaa nae nyumba moja au kiwanja kimoja?
Umejuaje..?
tatizo mkuu hatakiwi kukurupuka sijui kuripot kwa mjumbe au serikali ya mtaa au polisi tatizo watengeneza vitu feki washafika kote huko kuna watu wapo kwenye malipo yao hao wanakuwa ma infoma wao huko kwenye mamlaka sio ww ujipeleke kichwa kichwa eti naripot wanakuchora tu hivo vinywaji vina mpaka stika original ya TRA unafikiri wanazipata wapi..Atakimbiliaje polisi bila kuanza kureport kwa mjumbe na ofisi ya serikali yake kwanza kutoa taarifa
Hao watu wa mtaa ndiyo wanajukumu la kumuita/kuwaita wote wawili na kuwasikiliza
Polisi hiyo kwenda ni hatua nyingine kama wakishindwanda
We mleta uzi mtumishi wa umma gani hata procedure huzijui
Ova
Kwani wanavyotaifisha gari iliyokutwa imebeba magendo au madawa ya kulevya hua inakuaje mkuu?Watataifisha nyumba kwani iko chini ya Jina lao? Wewe umepangisha, yanayoendelea hapo huna udhibiti nayo, tena akijua umemshtaki unaweza shitakiwa kwa kusababisha au kuvunja mkataba kabla ya muda mliokubaliana.
Ukifika mahakamani huna nyumba kwa hio fanya km umeitoa Sadaka km unataka kuufuatilia kiundani huo msala au waachie Polisi wafanye kazi yao ya kukusanya Posho, usijifanye unajua zaidi kuwazidi wao halafu huyo msiri wako hakutakii mema kakuset hio nyumba ikipigwa mnada atainunua yeye ndio imekula kwakoNaomba msaada taarifa hii nikaitoe wapi maana msiri wangu kaniambia Polisi wanajua na huwa wanaenda kuchukua posho kama nilivyoshuhudia mimi mwenyewe hivyo hata nikiripoti kwao itakuwa ni kazi bure.
Naomba mwenye mawasiliano na Viwanda vinavyotengeneza Konyagi, K Vant na hizi Pombe Kali za chupa anisaidie tafadhali Ili niwajulishe tushauriane cha kufanya
wengi watakuja hapa na kukuuliza kama anakulipa kodi au hakulipi, na wewe unaathirika nini? kwa uzoefu, kitakachotokea, akama anachofanya ni kosa la jinai, atakamatwa, na mitambo yake itataifishwa, na nyumba yako itataifishwa, wewe utahangaika sana kwenda mahakamani au kwa DPP kujieleza kwamba wasitaifishe nyumba yako iliyokuwa inatumika kutengenezea vinywaji kimakosa, kwamba isiunganishwe kwenye vitendea kazi vya kutaifisha. utapata shida sana. ila itakusumbua kwasababu hoja itakuwa, ulikuwa unajua au ulikuwa hujui? kama ulikuwa unajua nyumba yako inatumika kufanyia uhalifu na ukaacha hivyohivyo bila kureport au kustopisha, itaonekana uliridhia, na icho kinaweza kuwa kielelezo cha kutaifishwa na DPP. dpp ataiomba mahakama itaifishe, na akitoa maelezo ya kueleweka wewe ukawa hauna, nyumba yako itataifishwa na itauzwa pesa itaenda serikalini. chukua hatua, utanishukuru, ama la labda kama anafanya kazi kihalali ana vibali kila kitu.Wapendwa habarini.Mimi ni Mtumishi wa Umma nipo Dodoma.Nina nyumba yangu nimeijenga Boko. Nilimaliza kuijenga Mei mwaka huu na Juni nikapata Mpangaji(Mme na Mkewe).
Nilishukuru maana Mpangaji huyu alijitambulisha kwamba ni Mfanyabiashara anayefuata mizigo China hivyo yupo busy sana, alinilipa Kodi ya miaka miwili(nilifurahi sana). Mwanzoni mwa mwezi huu wa Septemba jirani yangu ambaye tumetengana ukuta(fensi) alinipigia na kuniuliza kama nimeigeuza nyumba yangu kuwa godown au kiwanda cha kutengeneza vinywaji maana alidai kunakuwa na kelele za chupa kugongana usiku, nilimjibu hapana lakini nitafanya uchunguzi.
Juzi Jumapili nilikuwa Dar, hivyo mchana nilienda hapo Boko nyumbani kwangu bila kuwapa taarifa. Cha kushangaza nikakuta kafunga CCTV Camera kwenye pembe zote za fensi pamoja na kuweka Mlinzi getini. Nilivyojitambulisha getini Mlinzi hakufungua geti alinizuia kuingia(imagine nyumba yangu lakini nazuiliwa kuingia).
Nikiwa pale getini nahojiana na Mlinzi, ilikuja gari la Polisi ikasimama kwa mbali, kijana mmoja akatoka ndani ya nyumba yangu na kwenda kwenye ile gari na kuwapa naamini pesa na gari ya Polisi ikaondoka, kijana akarudi akaingia ndani, akafunga mlango, hapo mimi nimezuiwa getini. Kwa kifupi ni kwamba Mpangaji wangu huyu anazalisha bidhaa feki(vinywaji feki) na kuziingiza sokoni.
Msiri wangu ameniambia Konyagi, K-Vant, Gin na vinywaji vingine vikali vinazalishwa ndani ya nyumba yangu na kuingizaa sokoni. Naogopa asije akakamatwa mwisho wa siku Serikali ikataifisha nyumba yangu maana nimeambiwa hilo ni Kosa la Uhujumu Uchumi.
Naomba msaada taarifa hii nikaitoe wapi maana msiri wangu kaniambia Polisi wanajua na huwa wanaenda kuchukua posho kama nilivyoshuhudia mimi mwenyewe hivyo hata nikiripoti kwao itakuwa ni kazi bure.
Naomba mwenye mawasiliano na Viwanda vinavyotengeneza Konyagi, K Vant na hizi Pombe Kali za chupa anisaidie tafadhali Ili niwajulishe tushauriane cha kufanya
Nitashukuru sana wapendwa, siku njema
Hapa ndiyo atauponza kabisaKama polisi wanahusika nao wewe shida yako ipo wapi? Vunga wewe mtafute mpangaji mwambie ishu ushaijua ila mwambie awe makini dili lisije kuwa dirisha
Mzee mwenye nyumba wajibu wake ni kuripoti polisi kuwa nyumba yake ana wasiwasi inatumika kwa uhakifu na mpangaji wake. Achukue RB au maandishi yoyote kuthibitisha katoa taarifa. Hapo sasa aanze taratibu za kumuondoa huyo mpangaji kwa msaada wa mjumbe,seriakli za mtaa na polisi. Polisi wakiamua kumuachia mbele kwa mbele sio tatizo lake tena.Sawa,ila kwa maelezo yake polisi hao hao wanakujaga kudaka hapo 😄
Anyway kikubwa aripoti,hata kikinuka atajitetea mbona nlitoa taarifa
Ova
Kweli kabisaMzee mwenye nyumba wajibu wake ni kuripoti polisi kuwa nyumba yake ana wasiwasi inatumika kwa uhakifu na mpangaji wake. Achukue RB au maandishi yoyote kuthibitisha katoa taarifa. Hapo sasa aanze taratibu za kumuondoa huyo mpangaji kwa msaada wa mjumbe,seriakli za mtaa na polisi. Polisi wakiamua kumuachia mbele kwa mbele sio tatizo lake tena.
Umeelezea vizuri sana. Na wengi humu wanaongea kama ulivyosema,kirahisirahisi tu.wengi watakuja hapa na kukuuliza kama anakulipa kodi au hakulipi, na wewe unaathirika nini? kwa uzoefu, kitakachotokea, akama anachofanya ni kosa la jinai, atakamatwa, na mitambo yake itataifishwa, na nyumba yako itataifishwa, wewe utahangaika sana kwenda mahakamani au kwa DPP kujieleza kwamba wasitaifishe nyumba yako iliyokuwa inatumika kutengenezea vinywaji kimakosa, kwamba isiunganishwe kwenye vitendea kazi vya kutaifisha. utapata shida sana. ila itakusumbua kwasababu hoja itakuwa, ulikuwa unajua au ulikuwa hujui? kama ulikuwa unajua nyumba yako inatumika kufanyia uhalifu na ukaacha hivyohivyo bila kureport au kustopisha, itaonekana uliridhia, na icho kinaweza kuwa kielelezo cha kutaifishwa na DPP. dpp ataiomba mahakama itaifishe, na akitoa maelezo ya kueleweka wewe ukawa hauna, nyumba yako itataifishwa na itauzwa pesa itaenda serikalini. chukua hatua, utanishukuru, ama la labda kama anafanya kazi kihalali ana vibali kila kitu.