DOKEZO Mpangaji wangu kageuza Nyumba yangu kuwa kiwanda bubu cha kutengeneza vinywaji vikali feki kama Konyagi, K Vant nk

DOKEZO Mpangaji wangu kageuza Nyumba yangu kuwa kiwanda bubu cha kutengeneza vinywaji vikali feki kama Konyagi, K Vant nk

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Shida hapo wewe upo position mbaya sana, akikamatwa lazima mwenye nyumba nawe ukamatwe, sasa usipokamatwa watajua wewe ndio umewachoma...Israel...
Mtafute Masauni uongee nae
 
Wapendwa habarini.Mimi ni Mtumishi wa Umma nipo Dodoma.Nina nyumba yangu nimeijenga Boko.Nilimaliza kuijenga Mei mwaka huu na Juni nikapata Mpangaji(Mme na Mkewe).Nilishukuru maana Mpangaji huyu alijitambulisha kwamba ni Mfanyabiashara anayefuata mizigo China hivyo yupo busy sana,alinilipa Kodi ya miaka miwili(nilifurahi sana).Mwanzoni mwa mwezi huu wa Septemba jirani yangu ambaye tumetengana ukuta(fensi)alinipigia na kuniuliza kama nimeigeuza nyumba yangu kuwa godown au kiwanda cha kutengeneza vinywaji maana alidai kunakuwa na kelele za chupa kugongana usiku,nilimjibu hapana lakini nitafanya uchunguzi.

Juzi Jumapili nilikuwa Dar, hivyo mchana nilienda hapo Boko nyumbani kwangu bila kuwapa taarifa. Cha kushangaza nikakuta kafunga CCTV Camera kwenye pembe zote za fensi pamoja na kuweka Mlinzi getini.Nilivyojitambulisha getini Mlinzi hakufungua geti alinizuia kuingia(imagine nyumba yangu lakini nazuiliwa kuingia).

Nikiwa pale getini nahojiana na Mlinzi ,ilikuja gari la Polisi ikasimama kwa mbali, kijana mmoja akatoka ndani ya nyumba yangu na kwenda kwenye ile gari na kuwapa naamini pesa na gari ya Polisi ikaondoka, kijana akarudi akaingia ndani,akafunga mlango, hapo mimi nimezuiwa getini. Kwa kifupi ni kwamba Mpangaji wangu huyu anazalisha bidhaa feki(vinywaji feki) na kuziingiza sokoni.

Msiri wangu ameniambia Konyagi, KVant, Gin na vinywaji vingine vikali vinazalishwa ndani ya nyumba yangu na kuingizaa sokoni. Naogopa asije akakamatwa mwisho wa siku Serikali ikatahifisha nyumba yangu maana nimeambiwa hilo ni Kosa la Uhujumu Uchumi.

Naomba msaada taarifa hii nikaitoe wapi maana msiri wangu kaniambia Polisi wanajua na huwa wanaenda kuchukua posho kama nilivyoshuhudia mimi mwenyewe hivyo hata nikiripoti kwao itakuwa ni kazi bure.

Naomba mwenye mawasiliano na Viwanda vinavyotengeneza Konyagi,K Vant na hizi Pombe Kali za chupa anisaidie tafadhali Ili niwajulishe tushauriane cha kufanya

Nitashukuru sana wapendwa,siku njema
Kwenye mkataba wa kupangisha nyumba nafikiri Kuna kipengere kinamukataza mpangaji kutofanya shughuli zozote tofauti na kukaa, na siyo godown au kiwanda. Chukua mtendaji, police na Mwanasheria wako. Fukuza huyo kwa kuvunja masharti ya mkataba. Huyo atakuwa mchaga wengi ndo zao kutengeneza pombe fake

View: https://youtu.be/yJmml9e7eFs?si=NQwXk--fLOB_J_gK

Angalia yanaweza kukuta kama huyu mzee kupangisha mtu bila kujua historia yake, kafanya mauwaji uko na wakati huo anakaa kwenye nyumba yako, unaunganishwa kwenye case ya kunyongwa.
 
Hii dunia haiko fair kabisa jamani eee watumishi tufanye biashara tuwe madon Sasa ona mwamba kajenga ila kajamaa kamemlipa hela ya miaka miwili kakenua meno yote kisa Kodi ya Miaka miwili .

Kimbembe mwamba ana kiwanda ndani ya nyumba na kaweka na ulinzi kwanini wewe mwenye nyumba usiwe mtumwa ? Hapo mwanangu wewe mfuate huyo mkemia mchane unahitaji nyumba yako maana unarejea dasalam ila mpe hela iliyobaki lakini akitoka tu ,fika ofisi ya mjumbe na balozi pamoja na mtendaji waeleze kilichokuwa kinaendelea na nini uliamua kufanya ili uwe salama .

Maana hata ukimuamisha sio kwamba tutaacha kuja kuchukua posho hapo ,ni lazima tutakuja tu kikubwa ni nyumba ile ile .
 
Wapendwa habarini.Mimi ni Mtumishi wa Umma nipo Dodoma.Nina nyumba yangu nimeijenga Boko.Nilimaliza kuijenga Mei mwaka huu na Juni nikapata Mpangaji(Mme na Mkewe).Nilishukuru maana Mpangaji huyu alijitambulisha kwamba ni Mfanyabiashara anayefuata mizigo China hivyo yupo busy sana,alinilipa Kodi ya miaka miwili(nilifurahi sana).Mwanzoni mwa mwezi huu wa Septemba jirani yangu ambaye tumetengana ukuta(fensi)alinipigia na kuniuliza kama nimeigeuza nyumba yangu kuwa godown au kiwanda cha kutengeneza vinywaji maana alidai kunakuwa na kelele za chupa kugongana usiku,nilimjibu hapana lakini nitafanya uchunguzi.

Juzi Jumapili nilikuwa Dar, hivyo mchana nilienda hapo Boko nyumbani kwangu bila kuwapa taarifa. Cha kushangaza nikakuta kafunga CCTV Camera kwenye pembe zote za fensi pamoja na kuweka Mlinzi getini.Nilivyojitambulisha getini Mlinzi hakufungua geti alinizuia kuingia(imagine nyumba yangu lakini nazuiliwa kuingia).

Nikiwa pale getini nahojiana na Mlinzi ,ilikuja gari la Polisi ikasimama kwa mbali, kijana mmoja akatoka ndani ya nyumba yangu na kwenda kwenye ile gari na kuwapa naamini pesa na gari ya Polisi ikaondoka, kijana akarudi akaingia ndani,akafunga mlango, hapo mimi nimezuiwa getini. Kwa kifupi ni kwamba Mpangaji wangu huyu anazalisha bidhaa feki(vinywaji feki) na kuziingiza sokoni.

Msiri wangu ameniambia Konyagi, KVant, Gin na vinywaji vingine vikali vinazalishwa ndani ya nyumba yangu na kuingizaa sokoni. Naogopa asije akakamatwa mwisho wa siku Serikali ikatahifisha nyumba yangu maana nimeambiwa hilo ni Kosa la Uhujumu Uchumi.

Naomba msaada taarifa hii nikaitoe wapi maana msiri wangu kaniambia Polisi wanajua na huwa wanaenda kuchukua posho kama nilivyoshuhudia mimi mwenyewe hivyo hata nikiripoti kwao itakuwa ni kazi bure.

Naomba mwenye mawasiliano na Viwanda vinavyotengeneza Konyagi,K Vant na hizi Pombe Kali za chupa anisaidie tafadhali Ili niwajulishe tushauriane cha kufanya

Nitashukuru sana wapendwa,siku njema
mjinga wewe, sasa unaleta huku ni polisi au mjumbe?
 
Nenda ukaripoti Polisi hilo jambo

Ukizembea Siku Moja Zitakuja Mamlaka husika za Serikali kama vile TBS/TMDA n.k ambapo Kwa Sheria iliyopo,

Wanaweza kutaifisha mitambo pamoja na Mali zote ikiwemo hiyo nyumba yako wakiamini ni sehemu ya Mali za hao waharifu kumbe hao jamaa hiyo nyumba wamepanga kwako tu
 
Chagua la kufanya:-
  • Muuzie hiyo nyumba
  • Muite mzungumze kama mwanzoni alivyokufuata na mkaingia mkataba (hakikisha hapa usiwe peke yako), na umpatie utaratibu wa kuhama kama ataendelea kuzalisha vinywaji.
  • Tafuta mwanasheria akushauri kwenye hili jambo
 
Wapendwa habarini.Mimi ni Mtumishi wa Umma nipo Dodoma.Nina nyumba yangu nimeijenga Boko.Nilimaliza kuijenga Mei mwaka huu na Juni nikapata Mpangaji(Mme na Mkewe).Nilishukuru maana Mpangaji huyu alijitambulisha kwamba ni Mfanyabiashara anayefuata mizigo China hivyo yupo busy sana,alinilipa Kodi ya miaka miwili(nilifurahi sana).Mwanzoni mwa mwezi huu wa Septemba jirani yangu ambaye tumetengana ukuta(fensi)alinipigia na kuniuliza kama nimeigeuza nyumba yangu kuwa godown au kiwanda cha kutengeneza vinywaji maana alidai kunakuwa na kelele za chupa kugongana usiku,nilimjibu hapana lakini nitafanya uchunguzi.

Juzi Jumapili nilikuwa Dar, hivyo mchana nilienda hapo Boko nyumbani kwangu bila kuwapa taarifa. Cha kushangaza nikakuta kafunga CCTV Camera kwenye pembe zote za fensi pamoja na kuweka Mlinzi getini.Nilivyojitambulisha getini Mlinzi hakufungua geti alinizuia kuingia(imagine nyumba yangu lakini nazuiliwa kuingia).

Nikiwa pale getini nahojiana na Mlinzi ,ilikuja gari la Polisi ikasimama kwa mbali, kijana mmoja akatoka ndani ya nyumba yangu na kwenda kwenye ile gari na kuwapa naamini pesa na gari ya Polisi ikaondoka, kijana akarudi akaingia ndani,akafunga mlango, hapo mimi nimezuiwa getini. Kwa kifupi ni kwamba Mpangaji wangu huyu anazalisha bidhaa feki(vinywaji feki) na kuziingiza sokoni.

Msiri wangu ameniambia Konyagi, KVant, Gin na vinywaji vingine vikali vinazalishwa ndani ya nyumba yangu na kuingizaa sokoni. Naogopa asije akakamatwa mwisho wa siku Serikali ikatahifisha nyumba yangu maana nimeambiwa hilo ni Kosa la Uhujumu Uchumi.

Naomba msaada taarifa hii nikaitoe wapi maana msiri wangu kaniambia Polisi wanajua na huwa wanaenda kuchukua posho kama nilivyoshuhudia mimi mwenyewe hivyo hata nikiripoti kwao itakuwa ni kazi bure.

Naomba mwenye mawasiliano na Viwanda vinavyotengeneza Konyagi,K Vant na hizi Pombe Kali za chupa anisaidie tafadhali Ili niwajulishe tushauriane cha kufanya

Nitashukuru sana wapendwa,siku njema
...Nilivyojitambulisha getini Mlinzi hakufungua geti alinizuia kuingia(imagine nyumba yangu lakini nazuiliwa kuingia).... Nijuavyo mimi nyumba ukiikodisha/ ukimpangia mtu maana yake kwa kipindi cha huo mkataba nyumba inakuwa kwenye utawala wa mpangaji kwa maana ya masharti mbalimbali kuhusiana na hiyo nyumba. Otherwise kuna kitu nimejifunza kwenye hili...
 
Wapendwa habarini.Mimi ni Mtumishi wa Umma nipo Dodoma.Nina nyumba yangu nimeijenga Boko.Nilimaliza kuijenga Mei mwaka huu na Juni nikapata Mpangaji(Mme na Mkewe).Nilishukuru maana Mpangaji huyu alijitambulisha kwamba ni Mfanyabiashara anayefuata mizigo China hivyo yupo busy sana,alinilipa Kodi ya miaka miwili(nilifurahi sana).Mwanzoni mwa mwezi huu wa Septemba jirani yangu ambaye tumetengana ukuta(fensi)alinipigia na kuniuliza kama nimeigeuza nyumba yangu kuwa godown au kiwanda cha kutengeneza vinywaji maana alidai kunakuwa na kelele za chupa kugongana usiku,nilimjibu hapana lakini nitafanya uchunguzi.

Juzi Jumapili nilikuwa Dar, hivyo mchana nilienda hapo Boko nyumbani kwangu bila kuwapa taarifa. Cha kushangaza nikakuta kafunga CCTV Camera kwenye pembe zote za fensi pamoja na kuweka Mlinzi getini.Nilivyojitambulisha getini Mlinzi hakufungua geti alinizuia kuingia(imagine nyumba yangu lakini nazuiliwa kuingia).

Nikiwa pale getini nahojiana na Mlinzi ,ilikuja gari la Polisi ikasimama kwa mbali, kijana mmoja akatoka ndani ya nyumba yangu na kwenda kwenye ile gari na kuwapa naamini pesa na gari ya Polisi ikaondoka, kijana akarudi akaingia ndani,akafunga mlango, hapo mimi nimezuiwa getini. Kwa kifupi ni kwamba Mpangaji wangu huyu anazalisha bidhaa feki(vinywaji feki) na kuziingiza sokoni.

Msiri wangu ameniambia Konyagi, KVant, Gin na vinywaji vingine vikali vinazalishwa ndani ya nyumba yangu na kuingizaa sokoni. Naogopa asije akakamatwa mwisho wa siku Serikali ikatahifisha nyumba yangu maana nimeambiwa hilo ni Kosa la Uhujumu Uchumi.

Naomba msaada taarifa hii nikaitoe wapi maana msiri wangu kaniambia Polisi wanajua na huwa wanaenda kuchukua posho kama nilivyoshuhudia mimi mwenyewe hivyo hata nikiripoti kwao itakuwa ni kazi bure.

Naomba mwenye mawasiliano na Viwanda vinavyotengeneza Konyagi,K Vant na hizi Pombe Kali za chupa anisaidie tafadhali Ili niwajulishe tushauriane cha kufanya

Nitashukuru sana wapendwa,siku njema
Watataifisha nyumba kwani iko chini ya Jina lao? Wewe umepangisha, yanayoendelea hapo huna udhibiti nayo, tena akijua umemshtaki unaweza shitakiwa kwa kusababisha au kuvunja mkataba kabla ya muda mliokubaliana.
 
Mtafute yule mmiliki wa smart gin..ni bilionea yule ila anapatikana kirahisi sana.. mwambie kuna gin zinatengenezwa hapo kwa nyumba Yako na uyo mpangaji..I hope atakusaidia sana na unaweza pewa na nyumba nyingine bure sabb anawatafuta sana watu wanaoharibu biashara zake!!!
 
Back
Top Bottom