Mpango wowote wa TRA kukamata wasiodai risiti hautofanikiwa hadi pale Wamachinga watakapoondolewa

Mpango wowote wa TRA kukamata wasiodai risiti hautofanikiwa hadi pale Wamachinga watakapoondolewa

Watu wakipigwa faini wataacha kununua vitu barabarani na badala yake kuingia madukani na kununua humo. Huu msako ukifanywa kwa weledi utawaondoa Wamachinga wote wanauza vitu vya madukani barabarani na hivyo kuongeza pata la Taifa.
Ni sawa lakini pawepo na specific name ya nani ni machinga na nani ni mfanyabiashara.
Kwa kuwa naweza kuwa machinga lakini nina stoo kubwa ya kutunzia bidhaa.
Urashimishaji wa biashara zinazofanywa na machinga ni jambo muhimu ili kuweka usawa/mzani ya ulipaji kodi kwa ufasaha.
 

Ni vigumu sana kujua nani kanunua bidhaa zake wapi, hii ni kwa sababu Wamachinga wanauza kila kitu kinachouzwa madukani tena bila kikwazo chochote.

Wamachinga wanauza nguo, simu, vifaa vya simu, vifaa vya mahospitalini, vifaa vya shule, TV , vifaa vya majumbani na maofisini, ikiwa ni pamoja na dawa za binadamu, dawa za meno na dawa za magonjwa mengine zinapangwa barabarani kuanzia Kariakoo, Manzese hadi Mbagala huku zikipigwa jua kutwa nzima.

Wamachinga hawana machine za EFD na wala hawabughuziwi kwenye hilo huku wakifanya biashara kubwa kuliko wenye maduka na taarifa za sasa za Kariakoo zinaonyesha kwamba Wamachinga ni almost 70% ya wafanyabiashara wote, sasa kwa hali hii unawezaje kumuuliza mtu risiti ya alichonunua?

Labda TRA iseme kwamba imelenga kuwakomoa wauzaji wa jumla ambao ndio unaweza kuwatofautisha na wengine, Vinginevyo TRA yaweza kushitakiwa mahakamani kwa kumkamata aliyenunua kwa wamachinga ambao wanauza kila kitu kuliko hata maduka halali, maana hakuna duka lolote la halali linaloweza kuuza kandambili, chupi za watoto na humo humo likauza na dawa za binadamu pamoja na sumu za panya.

Watu wengi wataumia. Na biashara zitakufa.
Ikumbukwe pia kwamba Watanzania hawajui lolote kuhusu sheria za uuzaji wa baadhi ya bidhaa , wanachoangalia ni bei rahisi pekee , kwahiyo kumkamata huku akiwa kanunua kihalali kwa muuzaji aliyevaa kitambulisho halali cha Mmachinga utakuwa uonevu wa kutisha.
 
Ni sawa lakini pawepo na specific name ya nani ni machinga na nani ni mfanyabiashara.
Kwa kuwa naweza kuwa machinga lakini nina stoo kubwa ya kutunzia bidhaa.
Urashimishaji wa biashara zinazofanywa na machinga ni jambo muhimu ili kuweka usawa/mzani ya ulipaji kodi kwa ufasaha.
MATCHING GUY - mtu anayetembeza vitu mitaani na siyo anayepanga vitu barabarani
 
Kwasisi wakazi wa barabara zote wamejenga vibanda wamachinga mbele ya maduka na walikatazwa wasibuguziwe wapange bidhaa hata mlangoni kwa ofisi ya mkuu wa wilaya kisa wana kale kakaratasi ka 20,000 na watu wengi wananunua bidhaa kwao.. lakini hizi bidhaa zinatoka madukani wanapewa chinga anauza naye kwa bei itakayomlipa aliyoambiwabna tajiri anarejesha... walipotoa vitambulisho vya machinga hapo ndio biashara iliishia hapo
 
Ni mtego wa fursa, hawa watakamatwa kwa wingi na kukubaliana kulipa faini hivyo serikali itaingiza mabilioni kufidia tulizoziponda wakati wa uchaguzi.
Shida ya hizi sheria utumika Kama fursa za kujipatia kipato kwa baadhi ya walinda sheria.Imehisiwa pia kuna michezo ufanyika ya kuwakamua wafanyabiashara wanatumwa watu wakanunue vitu kisha ugoma kuchukua risiti then uenda uza cd kwa maafisa kwamba wameuziwa bila risiti then mfanyabiashara ukamatwa uyamaliza kwa nusu ya pesa ya faini.
 
Watu wakipigwa faini wataacha kununua vitu barabarani na badala yake kuingia madukani na kununua humo. Huu msako ukifanywa kwa weledi utawaondoa Wamachinga wote wanauza vitu vya madukani barabarani na hivyo kuongeza pata la Taifa.

Madhara ya huu ushauri wako unayajua? Jiandae kupigwa ngeta kwa vijana kukosa kipato.
 
Nafikiri watakachofanya ni kukaa karibu na maduka au wauzaji wa bidhaa (say petrol station), kwa hivyo anayekukamata anakuwa na uhakika kabisa sehemu uliponunua bidhaa...
 

Ni vigumu sana kujua nani kanunua bidhaa zake wapi, hii ni kwa sababu Wamachinga wanauza kila kitu kinachouzwa madukani tena bila kikwazo chochote.

Wamachinga wanauza nguo, simu, vifaa vya simu, vifaa vya mahospitalini, vifaa vya shule, TV , vifaa vya majumbani na maofisini, ikiwa ni pamoja na dawa za binadamu, dawa za meno na dawa za magonjwa mengine zinapangwa barabarani kuanzia Kariakoo, Manzese hadi Mbagala huku zikipigwa jua kutwa nzima.

Wamachinga hawana machine za EFD na wala hawabughuziwi kwenye hilo huku wakifanya biashara kubwa kuliko wenye maduka na taarifa za sasa za Kariakoo zinaonyesha kwamba Wamachinga ni almost 70% ya wafanyabiashara wote, sasa kwa hali hii unawezaje kumuuliza mtu risiti ya alichonunua?

Labda TRA iseme kwamba imelenga kuwakomoa wauzaji wa jumla ambao ndio unaweza kuwatofautisha na wengine, Vinginevyo TRA yaweza kushitakiwa mahakamani kwa kumkamata aliyenunua kwa wamachinga ambao wanauza kila kitu kuliko hata maduka halali, maana hakuna duka lolote la halali linaloweza kuuza kandambili, chupi za watoto na humo humo likauza na dawa za binadamu pamoja na sumu za panya.

Ikumbukwe pia kwamba Watanzania hawajui lolote kuhusu sheria za uuzaji wa baadhi ya bidhaa , wanachoangalia ni bei rahisi pekee , kwahiyo kumkamata huku akiwa kanunua kihalali kwa muuzaji aliyevaa kitambulisho halali cha Mmachinga utakuwa uonevu wa kutisha.
Wewe una akili kama mimi.
Excellent marverlous.
 
Watu wakipigwa faini wataacha kununua vitu barabarani na badala yake kuingia madukani na kununua humo. Huu msako ukifanywa kwa weledi utawaondoa Wamachinga wote wanauza vitu vya madukani barabarani na hivyo kuongeza pata la Taifa.
Wakishaondolewa barabarani unadhani nini kitatokea kama si uhalifu na ujambazi
 
Tunakoenda tutakuwa tunaagiza bidhaa zinatukuta majumbani!
Na biashara hii ndiyo inayokuja juu kwa sasa agiza tunakuletea mpaka mlangoni japo hapa tunawashtua wakuda huenda wakuda nao wakaanza kuagiza bidhaa ili ukimfikishia tu akudai risiti au umwonyeshe godown lipo wapi
 
Ni Kweli ulichosema,watakamata wanaotoka Petrol station na sehemu tunaponunua vitu ambapo hakuna bidhaa zilizobebwa na wamachinga.Kuna siku nimenunua kitu dukani kariakoo nikasahau kuchukua receipt nikiwa njiani nikampigia mwenye duka nikamwambia anitumie receipt yangu nimesahau wasije wakanikamata akanijibu waambie umenunua kwa wamachinga nilicheka sana (kama mazuri) kwani tunaikosesha nchi kodi ujue
Nimewaza sana hilo la kutoka Petrol Station. Ndipo watakapopigia sana.
 
Kuna siku nilikuwa naenda Sumbawanga from Mbeya. Sasa kufika Tunduma nikaona abiria wengi tuu wananunua sukari from Zambia ambazo wamachinga wanauza openly hapo Tunduma. Tulipofika huko mbele wakaingia TRA na kutaka eti kukamata abiria walionunua sukari, which was 2 to 3 kgs kwa walio wengi. Bwana wee watu wakachachamaa kwamba how come hawaendi kuwakamata wauzaji pale Tunduma? Wengine wakasema wamenunua Mbeya kwenye maduka, yaani ilikuwa balaa, mwishowe ilibidi waondoke tuu.
 
Inabidi tu ibuniwe mifumo ya kodi kulingana na mazingira yetu. Kuna shughuli nyingi sana zinazofanywa na watu hazilipiwi kodi kutokana na sheria zilizowekwa za usajiri wa shughuli hizo zinazosabababisha zisitambulike rasmi, kule kukosa urasmi ndiko kunakosababisha serikali ikose mapato.

USHAURI WANGU KWA WATUMUSHI SERIKALI
Ebu tuache ubabe kwa kuwafokea watu kwamba kwa nini wanaanzisha shughuli Fulani bila kufuata utaratibu na kufunga, ebu tuwasaidie watu namna ya kufuata au kukamilisha taratibu hizo ili wawe walipa kodi wazuri.
Watumishi wengi wa serikali wanapenda kuonyesha mamlaka waliyonayo badala ya kusaidie watu.
Hiyo kuwafokea na kuchimba biti wanawaiga mabosi wao mawaziri...
 

Ni vigumu sana kujua nani kanunua bidhaa zake wapi, hii ni kwa sababu Wamachinga wanauza kila kitu kinachouzwa madukani tena bila kikwazo chochote.

Wamachinga wanauza nguo, simu, vifaa vya simu, vifaa vya mahospitalini, vifaa vya shule, TV , vifaa vya majumbani na maofisini, ikiwa ni pamoja na dawa za binadamu, dawa za meno na dawa za magonjwa mengine zinapangwa barabarani kuanzia Kariakoo, Manzese hadi Mbagala huku zikipigwa jua kutwa nzima.

Wamachinga hawana machine za EFD na wala hawabughuziwi kwenye hilo huku wakifanya biashara kubwa kuliko wenye maduka na taarifa za sasa za Kariakoo zinaonyesha kwamba Wamachinga ni almost 70% ya wafanyabiashara wote, sasa kwa hali hii unawezaje kumuuliza mtu risiti ya alichonunua?

Labda TRA iseme kwamba imelenga kuwakomoa wauzaji wa jumla ambao ndio unaweza kuwatofautisha na wengine, Vinginevyo TRA yaweza kushitakiwa mahakamani kwa kumkamata aliyenunua kwa wamachinga ambao wanauza kila kitu kuliko hata maduka halali, maana hakuna duka lolote la halali linaloweza kuuza kandambili, chupi za watoto na humo humo likauza na dawa za binadamu pamoja na sumu za panya.

Ikumbukwe pia kwamba Watanzania hawajui lolote kuhusu sheria za uuzaji wa baadhi ya bidhaa , wanachoangalia ni bei rahisi pekee , kwahiyo kumkamata huku akiwa kanunua kihalali kwa muuzaji aliyevaa kitambulisho halali cha Mmachinga utakuwa uonevu wa kutisha.
Mwanzo 47
18]Na mwaka ule ulipokwisha wakamjia mwaka wa pili, wakamwambia, Hatumfichi bwana wetu ya kwamba fedha zetu zimekwisha, na makundi ya wanyama ni mali ya bwana wetu, hakikusalia kitu mbele ya bwana wetu, ila miili yetu na nchi zetu.
[19]Kwa nini tufe mbele ya macho yako, sisi na nchi yetu? Utununue sisi na nchi yetu kwa chakula, na sisi na nchi yetu tutakuwa watumwa wa Farao; kisha utupe mbegu, tuishi wala tusife, wala nchi yetu isipotee.
[20]Basi Yusufu akamnunulia Farao nchi yote ya Misri; maana Wamisri waliuza kila mtu shamba lake; kwa sababu njaa ilikuwa imewazidi sana, nchi ikawa mali yake Farao
 
Na biashara hii ndiyo inayokuja juu kwa sasa agiza tunakuletea mpaka mlangoni japo hapa tunawashtua wakuda huenda wakuda nao wakaanza kuagiza bidhaa ili ukimfikishia tu akudai risiti au umwonyeshe godown lipo wapi
Unaagiza kwa mtu mnayefahamiana!
 
Back
Top Bottom