Mpango wowote wa TRA kukamata wasiodai risiti hautofanikiwa hadi pale Wamachinga watakapoondolewa

hahahaha watu wengi wanaokwepa ussue za kodi wanawatumua machinga....mtu anaduka lake ila bidhaa asilimia 40 zinatembezwa nje na machinga......

mkuu ila hiyo sukari nitaifuata nione kama inaquality nzuri. ...vipi upande wa Flat screen Tunduma bei ni nzuri au sawa na mbeya mjini?
 
Naunga mkono hoja yako ni kweli kabisa kuwa ni vigumu kuwa kamata watu ambao watakutwa na bidhaa zisizo na lisiti kwani wafanya biashara wanawatumia wamachinga kukwepa kodi huo ndio ukweli
 
Naunga mkono hoja yako ni kweli kabisa kuwa ni vigumu kuwa kamata watu ambao watakutwa na bidhaa zisizo na lisiti kwani wafanya biashara wanawatumia wamachinga kukwepa kodi huo ndio ukweli
Usinilishe maneno , kwani wamachinga mnaowapa vitambulisho hawana biashara zao wenyewe , na je mliwapa mashine za EFD ?
 
TRA wangekuwa wanaweza kuelewa uhalisia Basi ningewashauri waachane na hivyo vimashine. Toka vianzishwe zimepelekea kwa asilimia nyingi kuyumbisha biashara. Muuzaji akisema kiukweli kabisa kabisa akitumie Kama TRA walivyomeza Basi hiyo Kodi yake hawezi kuilipa na akiilipa Basi ujue amechota hadi kwenye mtaji, kwahiyo badala ya biashara kukua inaendelea kudhoofika.

Biashara hasa ya duka badala ya kukua believe me litaendelea kupwaya na hatimae kufa, ambalo kimsingi halipaswi kuwa lengo.
TRA wanavyomkomalia mtu mwenye kaduka at the same time wanatakiwa kutambua kodi zote anazolipa huyo mwenye kaduka zinazotoka humo humo ambapo na yeye anategemea kakue aendeshe pia maisha mengine
Mfano

TRA
Lesen
Service Levy
Ulinzi
Usafi
Fire
Afya
Frem

Hawa wote wanafika mlangoni kudai pesa. Haya mazingira kiuhalisia yana dhoofisha msingi na hatimae biashara kufa.

TRA ningewashauri waachane na mfumo wa kusema wanakadiria Kodi kutokana na Mauzo. Huo mfumo si sahihi na hauna uhalisia wa faida anayopata mwenye kaduka.

Biashara ya duka iwe jumla au rejareja ni biashara ambayo faida huwekwa ndogo Sana
Mfano hai let say mie nauza maji kwa jumla
Katoni moja naiuza 2500 hapo faida ni 100.

Kwa siku ikitokea nipo sehem ninayoweza uza katoni 100 kwa siku ina maana faida yangu kwa siku Ni elf10 tu. Na hapo TRA yeye kunikadiria kodi atauliza mauzo /day which means kwa mauzo ya katoni 100 niliyopata elf10 tu Kama faida yeye atapigia kwa 250000

250000x28x12 =84M then atakokotoa Kodi toka hapo wakati kiuhalisia wewe mtaji wako ni laki 2 na elf40 na ulikuwa unapata faida elf 10 Kila ambapo kwa mwezi Ni laki3 kwa mwaka Ni 3.6M
Sasa cheki hiyo difference wewe.

Sasa fahsm kwa kaduka kavinywa ambako unaweza uza katoni 100 /day ujue upo center mno na Kodi ya frem lazima iwe laki2 and above kwa mwezi ikiwa laki2 tu tayari frem unalipia 2.4 M
Sasa endelea kutoa hayo malipo unayotakiwa kulipia then ona Kama hiyo biashara Kama inaweza kuwa.
 
Hiv TRA uwa wanajaribu kuwahusisha wafanya biashara wanapotaka kufanya maamuzi yao kwel? Ama ndio ile sisi ni wasomi tunauwezo wa kufanya maamuzi na mamlaka tunayo.
 
Hiv TRA uwa wanajaribu kuwahusisha wafanya biashara wanapotaka kufanya maamuzi yao kwel? Ama ndio ile sisi ni wasomi tunauwezo wa kufanya maamuzi na mamlaka tunayo.
Hao ni wasomi waliotukuka , wanawezaje kuwasikiliza wengine ?
 
Nafikiri watakachofanya ni kukaa karibu na maduka au wauzaji wa bidhaa (say petrol station), kwa hivyo anayekukamata anakuwa na uhakika kabisa sehemu uliponunua bidhaa...
Tutaanza kuwa tunapiga simu tuletewe bidhaa majumbani
 
Katika jambo la hovyo serikali imejipiga ngwala ni kuruhusu machinga kila sehemu ...


Watu wanafunga maduka yao anatafuta vijana anawapa mizigo wanakuwa machinga na hawalipi Kodi ...


Serikali nawaomba acheni kuingiza siasa kwenye kila kitu, hapo TRA Wu weenda shule acheni watumie elimu zao kukusanya kodi. Mambo mengi hapo TRA yanafanywa na wanasiasa.
 
Watu wakipigwa faini wataacha kununua vitu barabarani na badala yake kuingia madukani na kununua humo. Huu msako ukifanywa kwa weledi utawaondoa Wamachinga wote wanauza vitu vya madukani barabarani na hivyo kuongeza pata la Taifa.
Yaani ninunue kitu kwa machinga we ti ara ei uje unipige faini? Haki yamungu nakufa na wewe, Hilo timbwili lake, mpaka jamii itashangaa,wawape basi risiti chinga.vinginevyo hao ti ara ei wakajifunze upya
 
Hili jambo hata mimi nilijiuliza sana kwani ni kweli wamachinga wanauza bila kuwa na hizo mashine za EFD.
 
Umeandika kitu cha kweli kabisa.nimeenda pale karume ,nikakuta mabegi yametundikwa,nikapiga haraka haraka hesabu ,nikagundua yule jamaa mtaji wake ni zaidi ya chinga wa kawaida ,nikajichekea mwenyewe kwamba muuzaji anatumia kitambulisho cha mmachinga
 
Kwamba wamachinga wako exempt kutoa risiti za mauzo? kama mdau hapo juu alivyosema ,wangewatafutia tuu kidigital flan hivi simple,pos machine kama zile wanazolipia parking za magari.ili watoe reciept.

serikali iingie gharama ya kuwakopesha
 

I agree with you 100%.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…