KENZY
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 32,529
- 76,691
Alinifumania lile fumanizi ambalo halina kupinga! Yaani, fumanizi la 100 percentage...
Zikapita siku mbili hanitafuti, nami nikawa kimya na mawazo sijui naanzia wapi kujitetea. Nikaona isiwe tabu, nikaenda kulanduka na Serengeti lager kama 5 hivi, kisha nikampigia simu!
Nikajua hata atakuja juu, lakini mtoto wa watu ndo kwanza akawa mpole kama maji ya kwenye mtungi! Baada ya salamu, nikamuuliza, 'Umenisamehe?' Akacheka kidogo halafu akakaa kimya.
Nikamuuliza tena, 'Au ndo umeniacha tayari?'
Akavuta pumzi akajibu, 'Nimekuacha na sijakuacha pia!' Hapo hapo akakata simu!
Nikapiga tena, akaniuliza, 'Nini?' Nikamwambia, 'Nakupenda.'
Akajibu, 'Nakupenda na sikupendi pia.'
Nipo matatani, ananichanganya sana, sielewi hapa majibu yake mawili mawili yananitia sonona na mtanziko wa mawazo! Kwa ambaye amekutana na swahibu kama hili ulifanyaje kuyaweka mambo sawa? Kijana wenu penzi bado nalitaka maana mtoto miuno kama feni bovu!
Zikapita siku mbili hanitafuti, nami nikawa kimya na mawazo sijui naanzia wapi kujitetea. Nikaona isiwe tabu, nikaenda kulanduka na Serengeti lager kama 5 hivi, kisha nikampigia simu!
Nikajua hata atakuja juu, lakini mtoto wa watu ndo kwanza akawa mpole kama maji ya kwenye mtungi! Baada ya salamu, nikamuuliza, 'Umenisamehe?' Akacheka kidogo halafu akakaa kimya.
Nikamuuliza tena, 'Au ndo umeniacha tayari?'
Akavuta pumzi akajibu, 'Nimekuacha na sijakuacha pia!' Hapo hapo akakata simu!
Nikapiga tena, akaniuliza, 'Nini?' Nikamwambia, 'Nakupenda.'
Akajibu, 'Nakupenda na sikupendi pia.'
Nipo matatani, ananichanganya sana, sielewi hapa majibu yake mawili mawili yananitia sonona na mtanziko wa mawazo! Kwa ambaye amekutana na swahibu kama hili ulifanyaje kuyaweka mambo sawa? Kijana wenu penzi bado nalitaka maana mtoto miuno kama feni bovu!