Mpina kuwapeleka Mahakamani Waziri Bashe na Bodi ya Sukari kwa kutoa idhini ya vibali vya kuagiza sukari kinyume cha Sheria

Mpina kuwapeleka Mahakamani Waziri Bashe na Bodi ya Sukari kwa kutoa idhini ya vibali vya kuagiza sukari kinyume cha Sheria

Mkuu naona CCM inakulipa vizuri sana kutwa kuipigia debe japo haiuziki😂😂😂😂
mimi sihitaji malipo wala faida yoyote,

Neema na Baraka za Mungu zanitosha,
kua na nguvu, maarifa, ufahamu, uelewa na uwezo wa kutosha sana kukabiliana na uongo hasira na ghadhabu za wenye mihemko isiyobadili chochote kwa mpotoshaji na muongo huyo :pedroP:
 
Kwa mahakama zetu ambazo zinasubiri maelekezo toka juu asitarajie kama zitasikiliza kesi yake au kutoa maamuzi yenye haki.
Lakini angalau atakuwa ameonyesha uzalendo!
Siyo lazima sana kushinda bali serikali jinsi itakavyodeal na hilo jambo ujumbe utafika kwamba tuna serikali ya aina gani
 
Luhuga Mpina ameyasema hayo katika Mkutano wake na Waandishi wa Habari uliofanyika jana tar 29 kuelekea 30, ikiwa ni mara ya kwanza kuzungumza baada ya kupewa adhabu ya kutohudhuria vikao 15 vya bunge.

Kusoma taarifa hiyo zaidi ingia kwenye link hii: Bunge lajadili juu ya adhabu ya Mbunge Luhaga Mpina. Laamua kumfungia vikao 15

Akihitimisha taarifa yake Mpina alieza maadhimio yake kama ifuatavyo;

- Kupeleka malalamiko yake ya kuondolewa bungeni kwa uonevu na kutokutendewa haki na Spika wa Bunge Tulia Ackson kwenye vyombo vya sheria ili vikapime na kutoa haki kwa mujibu wa katiba ya Tanzania na sheria za nchi.

- Kumpeleka Mahakamani Waziri wa Kilimo Ndg. Hussein Bashe na Bodi ya Sukari chini ya ibara ya 26 na 27 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kitendo cha kutoa idhini ya vibali vya kuagiza sukari kinyume cha sheria na kulisababishia taifa hili hasara kubwa.

- Kuyafikisha Mahakamani makampuni yote yaliyojihusisha na ungizaji wa sukari nchini kinyume cha sheria.


===

Pia soma:

"The strongest man in the world is the one who stands alone" unknown author. Go mpina go. Taratibu wajinga watakuelewa na werevu tutakuunga mkono katika mioyo yetu
 
Hii clip ingewekwa yote kuanzia mwanzo, Kuna maelezo mengi yanakosekana.

Tukirudi kwenye mada, Mpina ajue tu hizo mahakama zitapokea maagizo kutoka juu na baadae hao majaji au mahakimu watazawadia vyeo vya juu zaidi kama asante.

Hii ndio Tanzania yetu chini ya Ma-CCM.
 
Kwa mahakama zetu ambazo zinasubiri maelekezo toka juu asitarajie kama zitasikiliza kesi yake au kutoa maamuzi yenye haki.
Lakini angalau atakuwa ameonyesha uzalendo!
Yaah! Mahakama zetu zitasema kesi hii inakiuka inaingilia kanuni na madaraka ya bunge.

Si inafahamika kwamba mbunge hawezi kushitakiwa kwa jambo aliliolisema bungeni? Pascal Mayalla tunaomba msaada wako please!
 
K
Luhuga Mpina ameyasema hayo katika Mkutano wake na Waandishi wa Habari uliofanyika jana tar 29 kuelekea 30, ikiwa ni mara ya kwanza kuzungumza baada ya kupewa adhabu ya kutohudhuria vikao 15 vya bunge.

Kusoma taarifa hiyo zaidi ingia kwenye link hii: Bunge lajadili juu ya adhabu ya Mbunge Luhaga Mpina. Laamua kumfungia vikao 15

Akihitimisha taarifa yake Mpina alieza maadhimio yake kama ifuatavyo;

- Kupeleka malalamiko yake ya kuondolewa bungeni kwa uonevu na kutokutendewa haki na Spika wa Bunge Tulia Ackson kwenye vyombo vya sheria ili vikapime na kutoa haki kwa mujibu wa katiba ya Tanzania na sheria za nchi.

- Kumpeleka Mahakamani Waziri wa Kilimo Ndg. Hussein Bashe na Bodi ya Sukari chini ya ibara ya 26 na 27 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kitendo cha kutoa idhini ya vibali vya kuagiza sukari kinyume cha sheria na kulisababishia taifa hili hasara kubwa.

- Kuyafikisha Mahakamani makampuni yote yaliyojihusisha na ungizaji wa sukari nchini kinyume cha sheria.


===

Pia soma:

Kwa hio yy anacholalamika ni sukari kuagizwa nyingi au kampuni hazina uwezo kama alivosema.
 
Nipo na wewe Mpina
 
Kwani una undugu na Bashe wewe ndo Bashe?
hakuna haja ya undugu kwenye mambo haya ya kizalendo lwa maslahi ya taifa,

bali kusema ukweli na kujitenga na uongo, upotoshaji, kiburi na jeuri na halafu eti ukajipiga kifua kwenda na uongo wako mahakamani, na mahakama yenye weledi kama ya Tanzania ikabariki uzushi wako, thubutu :pulpTRAVOLTA:

lazma mahakama ikushikishe adabu:pedroP:
 
Mbona hiyo kesi inaishia kwa Registrar tu? Haikidhi viwango vya kufungua kesi. Asitapetape aende tu kwa Superdoll wakayamalize
Hata waliovunja hiyo Sheria walijua mahakama haina meno. Lakini mwacheni atumie Hali yake.
Muhimu zaidi ni kujifunza namna kuwa katiba mpya pekee ndo suluhisho la haya makandokando
 
Back
Top Bottom