Mpinga Hayati Magufuli aangua kilio ndani ya treni ya SGR

Mpinga Hayati Magufuli aangua kilio ndani ya treni ya SGR

Ulifuatilia hoja zilizotolewa na wapinzani kuhusu mushkeli mkubwa uliomo kwenye uamuzi wa kununua ndege kwa cash bila business plan wala kuzingatia taratibu za manunuzi?

Huo mzaha wa mitaani kuhusu “mapanga boi” sio hoja ya kujadiliwa kwenye mada hii.

It was a bad decision; it still is. ATCL haitafufuka na italiletea taifa hasara ya mabilioni tukiendelea na ujinga wa kununua ndege “gizani” na kuzitumia bila mpangilio makini wa kibiashara.

Kuhusu watu kuzipanda, watazipanda tu zikiwepo kwa malipo kama wanavyopanda zingine zilizopo kwenye soko. Tanzania hatujawahi kuwa na shida ya usafiri wa ndege.

Hata SGR serikali ikipaparika kuendekeza hizo Safari fupi za abiria kufurahisha mashabiki kabla mradi haujakamilika na kuanza kusafirisha mizigo mikubwa itaishia kwenye mawe. TAZARA na TRC pamoja na ukongwe zinaponea ruzuku hadi leo.

Haya sio masuala ya propaganda nyepesi nyepesi.
Kwa sababu watu wengi wa Nchi hii na Africa yote wanaupenda sana ufisadi ndio maana kitu chochote cha maana kikianzishwa na wakakabidhiwa kukiendesha kitu cha kwanza watakachokifanya ni kutengeneza mipango na mbinu zao za kupiga pesa kupitia hicho walichokabidhiwa !

Au nasema Uongo ndugu zanguni ????! 😳🙄
 
Aliomba msamaha baada ya kugundua kuwa aliyetaka kumuua yupo ndani ya chadema na siyo Magufuli
Yeye alijua hana kosa, sasa anaombaje msamaha?

Ukiomba msamaha ina maana ushafanya kosa
 
Hata Kenya walikuwa wanashangilia hivyo hivyo baada ya kupata Barabara ya Thika super highway njia 8,Sgr nk wakati wa Kibaki na Uhuru.

Saizi mda wa kulipa madeni umefika wanachinjana,na Tzn shangilieni sana ila mda utakapofika wa kupandishiwa Kodi mlipe Madeni msije kutukana watakaokuwepo Madarakani kipindi hicho.

Mbaya zaidi mwakani wakati CAG analeta taarifa ya hasara msije kutoa povu,hayo mamiradi ya kupigia picha hayajawahi na hayatakuja kuondoa umaskini wa mtu yeyote.Utakamuliwa Kodi Ili kufidia kuyaendesha.

Kenueni sana ,Kuna Kilio pia kinakuja.

Inakuuma sana watanzania masikini kusafiri dar - Dom kwa masaa 3 tu
 
Nashangaa mwanaCCM kindakindaki kama Etwege litokee tukio kama hili halafu asirekodi ka clip kwa ajili ya ushahidi?

Hii story ni ya kutunga kwasababu hakuna ushahidi wa kusindikiza hadithi yake.

Wewe mwenyewe unaangua kilio kimyakimya ndani ya moyo wako
 
Pamoja na juhudi zote hizo Treni zinaitwa "Samia Express" 🙌
 
Inakuuma sana watanzania masikini kusafiri dar - Dom kwa masaa 3 tu
Mkuu Dar to Dom masaa matatu hata basi lolote linaenda sema kwakuwa nchi masikini bado zina limit speed 80 kwa saa ndiyo unaona zinatumia zaidi ya masaa hayo.

Sasa gari ina speed 180 hadi 240 ukisema itembee speed 180 tu kwa saa basi Dar to Dom ni masaa matatu.
 
Hii treni lazima ibinafsishwe, hatuwezi kuendesha treni ya umeme sisi, la zivyo tutaanza kuambiwa porojo za hasara kila mwaka. Kama ndege tu.
 
Tarehe 4, july, 2024 nikiwa kwenye treni ya umeme (SGR)ya Dar - Morogoro ambapo abiria wanatumia saa moja na dakika 49 tu kufika, hivyo kuokoa muda mwingi wa uzalishaji uliokuwa unapotea barabarani kwenye foleni, kwenye siti pembeni yangu alikaa kijana ambaye kwa muonekano yupo umri wa above 25 ambaye muda wote alionekana mwenye huzuni sana na majuto mengi.

Baada ya kufika kituo cha Soga mkoani Pwani nikamuona kijana ameanza kuangua kilio na ndipo ilibidi nimuhoji na abiria wenzangu wakataka kujua ni nini kinamsibu kijana huyu, kijana alieleza kuwa nafsi inamsuta kupanda hii SGR kwani alipinga ujenzi wake akiongozwa na Tundu Lisu na Chadema kwa ujumla alishiriki kumtukana hayati Rais Magufuli na kumkejeli pale alipoanzisha ujenzi wa reli ya umeme wakati huo ikiwa awamu ya tano!

Kijana anasema sasa analia na kusaga meno kwani Magufuli hayupo tena duniani na hajui atamuombea wapi msamaha ili nafsi yake iwe huru kwani mradi wa sgr Dar - Moro umekamilika na kuwa wenye manufaa makubwa kwa watanzania masikini na matajiri bila kujali vipato vyao.

My take
Kwa maoni yangu vijana wa namna hii wako wengi wanapanda ndege, treni, flyover na kuwasha umeme wa bwawa huku nafsi zao zinawasuta sana maana walidanganywa na wanasiasa matapeli wasio na maono wala uzalendo wowote kwa taifa la Tanzania wakaishia kumtukana hayati Magufuli kwamba ni mshamba badala ya kutumia nguvu zao kuungana na Magufuli kujenga nchi wao wakatumia nguvu zao kumtukana na sasa wanajuta.
Unapokoseaga na kuonekana una IQ ndogo ni kuwahusisha hao CDM na kila mada yako. Unaweza kuwa na hoja zenye mashiko lakini uraibu wako kwa CCM umekuondolea uwezo wako wa kujenga hoja. Kama hiyo ndiyo sababu ya huyo kijana kulia na wewe unamsapoti, basi wote ni wale wale.
 
..mimi nilimpinga Magufuli kununua midege.

..midege inatuletea hasara ambayo hatukupaswa kuibeba.

..pamoja na hayo nitapanda Atcl ilimradi inanifikisha ninapotaka kwenda.

..pia nilipinga ujenzi wa mji Mkuu Dodoma. Fedha na rasilimali zilizotumia Dodoma zingeweza kufanya mambo mengi yenye tija.

..mtizamo wangu haunizuii kutembelea Dodoma.
Kwa niaba ya CCM tusamehe mkuu!
Ndo maana baada ya lile jamaa kupoteza fedha kuhamia Dodoma sasa tunafanya mambo ya maana.
...tumeshasambaza pikipiki nchi nzima. na Baiskeli zinakuja
 
Tarehe 4, july, 2024 nikiwa kwenye treni ya umeme (SGR)ya Dar - Morogoro ambapo abiria wanatumia saa moja na dakika 49 tu kufika, hivyo kuokoa muda mwingi wa uzalishaji uliokuwa unapotea barabarani kwenye foleni, kwenye siti pembeni yangu alikaa kijana ambaye kwa muonekano yupo umri wa above 25 ambaye muda wote alionekana mwenye huzuni sana na majuto mengi.

Baada ya kufika kituo cha Soga mkoani Pwani nikamuona kijana ameanza kuangua kilio na ndipo ilibidi nimuhoji na abiria wenzangu wakataka kujua ni nini kinamsibu kijana huyu, kijana alieleza kuwa nafsi inamsuta kupanda hii SGR kwani alipinga ujenzi wake akiongozwa na Tundu Lisu na Chadema kwa ujumla alishiriki kumtukana hayati Rais Magufuli na kumkejeli pale alipoanzisha ujenzi wa reli ya umeme wakati huo ikiwa awamu ya tano!

Kijana anasema sasa analia na kusaga meno kwani Magufuli hayupo tena duniani na hajui atamuombea wapi msamaha ili nafsi yake iwe huru kwani mradi wa sgr Dar - Moro umekamilika na kuwa wenye manufaa makubwa kwa watanzania masikini na matajiri bila kujali vipato vyao.

My take
Kwa maoni yangu vijana wa namna hii wako wengi wanapanda ndege, treni, flyover na kuwasha umeme wa bwawa huku nafsi zao zinawasuta sana maana walidanganywa na wanasiasa matapeli wasio na maono wala uzalendo wowote kwa taifa la Tanzania wakaishia kumtukana hayati Magufuli kwamba ni mshamba badala ya kutumia nguvu zao kuungana na Magufuli kujenga nchi wao wakatumia nguvu zao kumtukana na sasa wanajuta.
Habari hii bila clip ya kuonesha jinsi akilia inakaa uzushi!
 
Mkuu Dar to Dom masaa matatu hata basi lolote linaenda sema kwakuwa nchi masikini bado zina limit speed 80 kwa saa ndiyo unaona zinatumia zaidi ya masaa hayo.

Sasa gari ina speed 180 hadi 240 ukisema itembee speed 180 tu kwa saa basi Dar to Dom ni masaa matatu.

Kumbe hata akili huna kabisa
 
Hii treni lazima ibinafsishwe, hatuwezi kuendesha treni ya umeme sisi, la zivyo tutaanza kuambiwa porojo za hasara kila mwaka. Kama ndege tu.

Hii ndiyo sababu ilikufanya upinge ujenzi wake?
 
Unapokoseaga na kuonekana una IQ ndogo ni kuwahusisha hao CDM na kila mada yako. Unaweza kuwa na hoja zenye mashiko lakini uraibu wako kwa CCM umekuondolea uwezo wako wa kujenga hoja. Kama hiyo ndiyo sababu ya huyo kijana kulia na wewe unamsapoti, basi wote ni wale wale.

Cdm ni wapumbavu na wameshiriki sana kupotosha watanzania
 
Kwa niaba ya CCM tusamehe mkuu!
Ndo maana baada ya lile jamaa kupoteza fedha kuhamia Dodoma sasa tunafanya mambo ya maana.
...tumeshasambaza pikipiki nchi nzima. na Baiskeli zinakuja

Haha nyumbu hawezi kukuelewa
 
Back
Top Bottom