Mr. Kuku ahukumiwa kulipa fidia TSh. Bilioni 5.4, faini Tsh. Milioni 5 au jela miaka 5

Mr. Kuku ahukumiwa kulipa fidia TSh. Bilioni 5.4, faini Tsh. Milioni 5 au jela miaka 5

Papaa Mobimba

JF-Expert Member
Joined
Jan 27, 2018
Posts
882
Reaction score
3,337
Mahakama ya Hakimu Mkazi, imemhukumu mfanyabiashara Tariq Machibya maarufu Mr Kuku, kulipa faini ya sh. milioni tano au kwenda jela miaka 5, baada ya kutiwa hatiani kwa makosa mawili ambayo ni kujihusisha na biashara ya upatu kwa kukusanya fedha kutoka kwa umma na kukubali kupokea miamala ya fedha bila ya leseni.

Katika hukumu hiyo, Mr. Kuku amehukumiwa kulipa faini ya Tsh. Milioni 2 au kifungo cha miaka 5 na katika kosa la pili ametakiwa kulipa faini ya Tsh. Milioni 3 au kifungo cha miaka 5. Ikiwa atashindwa kulipa faini, vifungo ni vyote kwa pamoja

Pia mahakama hiyo, imemuamuru fedha sh. bilioni 5.4 ambazo ziko benki ya CRDB kwenye akaunti ya mshtakiwa huyo kwenda kwenye akaunti ya Mkurugenzi ya Mashitaka nchini( DPP) iliyoko benki Kuu ya Tanzania( BoT).

Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi Godfrey Isaya, baada ya upande wa jamhuri kuingia makubaliano ya kulipa kiasi hicho.

Akisoma hukumu hiyo Hakimu Isaya, alisema mshtakiwa anamtia hatiani kama alivyoshitakiwa ambapo mshitakiwa ameshindwa kulipa fedha hizo na alipelekwa rumande.

Pia soma
 
Mimi hata ingekua nilipe 1b & 10 years, ningeenda 10 yrs.
Mimi hata ninayo sitoi,
5yrs vs 5bln, ni very simple Multiple choice.
Choice aliyopewa ni alipe faini ya 5 million au jela 5years

Hiyo 5 billion ya fidia kuilipa ni lazima; Bila kujali aende jela asiende ndio maana account zake wamezifreeze.
 
Hizi kesi sa kukubali mashitaka na kulipa fine ni mbinu za kuibia watu pesa.

Binafsi mpaka leo sijaelewa kosa la mr kuku. Maana kama mradi ulikuwa active na watu wanawekeza kwa free consent sasa kosa lipo wapi?
Kosa lake hakuwa na leseni ya kupokea fedha kutoka kwa umma, isingewekwa sheria ya namna hii tungelizwa sana wengi
 
Hicho kiasi cha 5.4 bilioni kilichopo kwenye acc ya mshtakiwa ambacho kinahamishiwa kwenye akaunti ya DPP ndio faini yenyewe au ndio kutaifisha faini ipo palepale?
 
Mimi hata ninayo sitoi,
5yrs vs 5bln, ni very simple Multiple choice.

Mimi hata ingekua nilipe 1b & 10 years, ningeenda 10 yrs.

Someni muelewe vizuri ni kwamba ameshakubaliana na DPP. Kwa mfumo mpya wa Plea Bargain

Wameshaangalia kwenye akaunti ana 5.4 bilioni wamekubaliana unakiri kosa tunazichukua hizi halafu tunapunguza mashtaka

So 5.4 ya FIDIA washachukua

Halafu wanakupa adhabu ndogo ya FAINI ya million 5 au Jela miaka mitano

So wameshampukutisha kila kitu dogo hadi hiyo mil 5 kashindwa kulipa kaenda rumande
 
Sasa si kwenye akaunti kuna iyo Billion 5.4 sasa iyo 5 itumike kama Fidia hafu iyo pont 4 (Mil 400) jamaa awape Mahakama Mil 5 yao hafu ibaki Mil 395.

Mil 100 hivi aende vacation viwanja vya mbele kama week 2 hivi hafu arudi kuanza upya.

Atawapata wajinga wengine tu.
 
Hicho kiasi cha 5.4 bilioni kilichopo kwenye acc ya mshtakiwa ambacho kinahamishiwa kwenye akaunti ya DPP ndio faini yenyewe au ndio kutaifisha faini ipo palepale?
Hio ni FIDIA faini kashindwa kulipa ndio maana kaenda jela.

Mtu alikuwa na bil5.4 ila kashindwa kulipa mil 5.

Hahahaaa raha sana sahivi yani wanakwangua kila kitu.
 
Back
Top Bottom