GeoMex
JF-Expert Member
- Jan 10, 2014
- 5,431
- 19,913
Soma vizuri uelewe FIDIA na FAINIKati ya jela 5yrs na fidia billion 5 bora nini..??🤔
😂😂
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Soma vizuri uelewe FIDIA na FAINIKati ya jela 5yrs na fidia billion 5 bora nini..??🤔
😂😂
Duuh noma kweli rafiki angu!!! Wangemuacha tu huyu chalii maana hiyo m5 ni kama wemkomoa tu coz wanajua kabisa hana kibunda chote wamelamba dadekiSomeni muelewe vizuri ni kwamba ameshakubaliana na DPP. Kwa mfumo mpya wa Plea Bargain
Wameshaangalia kwenye akaunti ana 5.4billion wamekubaliana unakiri kosa tunazichukua hizi halafu tunapunguza mashtaka
So 5.4 ya FIDIA washachukua
Halaf wanakupa adhabu ndogo ya FAINI ya million 5 au Jela miaka mi5
So wameshampukutisha kila kitu dogo hadi hiyo mil5 kashindwa kulipa kaenda rumande
Fine ipo sawa na kiasi kilichopo kwenye accounts zake [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu imemhukumu mfanyabiashara, Tariq Machibya (29) maarufu Mr. Kuku kulipa fidia ya Sh5.4 bilioni baada ya kupatikana na hatia ya kushiriki biashara ya upatu na kukubali kupokea miamala ya fedha.
Pia, imemhukumu kulipa faini ya Sh5 milioni au kwenda jela miaka mitano sambamba na kuamuru Sh5.4 bilioni zilizopo kwenye akaunti ya mshtakiwa huyo kuhamishiwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwenye akaunti ya mkurugenzi wa mashtaka (DPP).
Hata hivyo, mshtakiwa ameshindwa kulipa faini na kurejeshwa rumande.
Mahakama imetoa hukumu hiyo baada ya kumtia hatiani katika mashtaka mawili ya kushiriki biashara ya upatu na kukubali kupokea miamala ya fedha baada ya kukiri mashtaka yake DPP.
Uuamuzi huo umetolewa leo Jumatano Desemba 16, 2020 na hakimu mkazi mfawidhi, Godfrey Isaya.
Awali, wakili wa Serikali mkuu, Paul Kadushi akisaidiana na wakili wa Serikali mwandamizi, Wankyo Simon amedai kuwa kesi hiyo imeitwa kwa ajili ya kusomewa mashtaka baada ya mshtakiwa huyo kukiri mashtaka yake kwa DPP baada ya kufanya majadiliano naye na kufikia makubaliano Desemba 7, 2020.
Amesema baada ya kufikia makubaliano na DPP amemfutia mashtaka manne kati ya saba yaliyokuwa yanamkabili.
Mashtaka aliyotiwa hatiani ni kusimamia biashara ya upatu na kupokea miamala ya fedha kutoka kwa umma bila kuwa na leseni.
Kati ya Januari 2018 na Mei 2020 katika maeneo mbalimbali ya jijini Dar es Salaam mshtakiwa anadaiwa kusimamia biashara ya upatu.
Machibya anadaiwa alijihusisha na biashara ya upatu kwa kukubali na kukusanya fedha kutoka kwa umma, akijifanya kwamba watafanya ujasiriamali wa ufugaji wa kuku na wangepata faida ya asilimia 70 ya mtaji wa awali waliowekeza kwa miezi minne na asilimia 90 ya mtaji wa awali waliowekeza kwa kipindi cha miezi sita, kiasi ambacho ni kikubwa katika biashara kuliko mtaji uliokusanywa.
Shtaka pili, siku na maeneo hayo mshtakiwa anadaiwa kuwa alikubali na kupokea miamala ya fedha za umma kiasi cha Sh17 bilioni bila kuwa na leseni.
Mwananchi
Pia soma
- Mr. Kuku Farm ni aina mpya ya DESI?
- Fahamu zaidi kuhusu Mr Kuku
- Wadau na wajasiriamali, naomba kujuzwa kuhusu Mr. Kuku Farms na uhalisia wa aina ile ya biashara
- Mtaalam wa kuwekeza kwenye kuku tayari ameshawaliza
- Mr. Kuku afikishwa Mahakamani akikabiliwa na mashtaka saba ikiwemo kufanya Biashara Haramu ya Upatu kwa kukusanya bilioni 17
- Wajasiriliamali wa Tanzania tuna lipi la kujifunza kutokana na makosa ya kiufundi / kitaalam ya Mr. Kuku
Fine na fidia iko pale pale.Hicho kiasi cha 5.4 bilioni kilichopo kwenye acc ya mshtakiwa ambacho kinahamishiwa kwenye akaunti ya DPP ndio faini yenyewe au ndio kutaifisha faini ipo palepale?
Mr kuku leo hii ameshindwa lipa faini ya 5million?
Hata kama wamepita na hizo za kwenye account,inamaana hakua na upande wa pili ...
Hapo sawa.. aende tu kutumikia hana namnaPesa yote ameshaporwa na DPP.
Hana kitu, account zilifungwa na pesa zinahamishiwa BoT.
Nyie ni wale watu ambao mpaka wakutane na madhara ndiyo waelewe somo.Hizi kesi sa kukubali mashitaka na kulipa fine ni mbinu za kuibia watu pesa.
Binafsi mpaka leo sijaelewa kosa la mr kuku. Maana kama mradi ulikuwa active na watu wanawekeza kwa free consent sasa kosa lipo wapi?
Hicho kiasi cha 5.4 bilioni kilichopo kwenye acc ya mshtakiwa ambacho kinahamishiwa kwenye akaunti ya DPP ndio faini yenyewe au ndio kutaifisha faini ipo palepale?
Najua hilo ndio maana nikaandikaSoma maelezo vizuri.
Watu wameshaamisha mzigo
Sawa tichaSoma vizuri uelewe FIDIA na FAINI
Hio ni FIDIA faini kashindwa kulipa ndomaana kaenda jela.
Mtu alikuwa na bil5.4 ila kashindwa kulipa mil5
Hahahaaa raha sana saivi yani wanakwangua kila kitu
Kwasasa ana miaka 29 akifungwa miaka 5 anatoka akiwa na 34.Hapo sawa.. aende tu kutumikia hana namna
Imekula kwakeKwasasa ana miaka 29 akifungwa miaka 5 anatoka akiwa na 34.
Kapoteza mwelekeo.
Ubaya ni kwamba alikua na makosa ya sh bil 17 so kwa muda wote huu wako wananegotiate ni pamoja na kuuza kila kitu alichonunua kwa hiyo hela. Ndio wamebahatika kupata hiyo bil 5.4Mr kuku leo hii ameshindwa lipa faini ya 5million?
Hata kama wamepita na hizo za kwenye account,inamaana hakua na upande wa pili ...
Pitia pitia komenti zingine nimeelezea hili swala vizur bossSaa kashindwa vipi wakati kwenye account take kulikuwa na bilioni 5?.
si wangezichukua alafu wamuachie
Asante kama umeelewa bossSawa ticha