Mzee wako alikuwa anajali sana siri zake za kibenki lakini akaenda kwa wakubwa serikalini kuwaaambia jamani nina mamilioni ya dola NMB nataka kuyatoa. Wakamuomba azibakize NMB. Sielewi Mzee wako alikuwa anajali zaidi siri zake au kutishia na kubembelezwa na wazee wa serikali badala ya kuzitoa kimya kimya.
Turudi kwenye mada. Kuhusu siri za wateja, hata Ulaya serikali inajua una kiasi gani benki. Nchi za Umoja wa Ulaya unatakiwa kuripoti miamala ya Euro 10,000 na zaidi kama vile depositing, kwa hiyo akaunti, salio, jina, umezipata pataje, una mpango gani nazo, vyote vitajulikana. Hakuna siri. Na wakitaka kuzikwapua watafanya mchakato wa seizure and forfeiture kama DPP, Jeshi la Polisi na Mahakama walivyofanya kwa Mr. Kuku.
Hela zilikuwa za mkondo wa taasisi ya kiserikali, aliingiliwa kisiasa.
Ama una miss point yangu, ama unajitia ujinga wa makusudi.
Huko nchi za Ulaya na Marekani, kote, serikali inaweza ku garnish hela, hilo si ninalojadili hapa.
Nimefanya kazi kwenye mifumo ya benki ya kimataifa miaka mingi sana naelewa hili.
Tatizo ni due process.
CEO mstaafu wa CRDB, Charles Kimei, aliwahi kusema kimsingi anamuogopa sana Magufuli, na yuko tayari kufanya lolote atakalosema Magufuli.
Hii kauli kwa CEO wa benki ni kauli ya hatari sana.
Maana yake Magufuli anaweza kumwambia waibe hela benki wazipeleke kwenye kampeni za urais, na yeye kwa sababu anamuogopa sana Magufuli akakubali tu. Tafsiri ni kwamba ukiweka hela zako CRDB ya Kimei, ulikuwa unaweka hela katika benki yenye CEO asiye na banking integrity, anaogopa wanasiasa.
Kauli kama hii ikitolewa na CEO wa benki ya Marekani hapo hapo anatolewa kazini.
Huko Bongo hakuna mifumo iliyokomaa ya kitaasisi, hakuna due diligence. Watu wanaweza kukuona una hela nyingi wakakuonea wivu tu wakakutungia kesi ya uhujumu uchumi wakufilisi.