Mradi wa Bwawa la Nyerere tulijilisha upepo au ndiyo mwendelezo wa siasa chafu za kibepari?

Mqkamba kawekwa hapo Kama mtego huonmradi ukifeli ndio utampoteza makmba kwemy siasa

Mam mjanja kamuweka ili amalize kisiasa huyu makamba
Nape na Ridhiwani nao wapo kwa mtego? Huoni kuna pattern hapo?
 
Ndugu yangu MALCOM LUMUMBA

....Long time no see!!

Kwa heshima ya ndugu Jinga la Zamani alienialika, wacha nami niseme machache.

Hapa wacha niende moja kwa moja kwenye JNHPP ili nisiifanye post yangu kuwa ndefu maradufu..

Kwa hapa tulipofikia, hatuwezi kuendelea na yale mambo ya ku-abandon miradi mikubwa wakati tayari imeshameza mabilion ya pesa! Kwa maana nyingine, JNHPP Must Continue kwa sababu tayari pesa nyingi imeshaingia!!

Hata hivyo, wakati mradi huu unaanza binafsi niliupinga! Sikuupinga kwa sababu za kimazingira wala kwamba ni unsustainable lakini mimi ni muumini mkubwa wa Economic Multiplier Effect na Optimal Resources Allocation.

Dhana hii ya Multplier Effect nishaieleza sana huko nyuma! Na kwavile I believe in Multiplier Effect, kama ningewekewa option ya either JNHPP or LNG Project (Gas Industry) kama source ya uzalishaji umeme, I'll ALWAYS be in favor of the Gas Industry kwa sababu huko kuna HIGHER multplier effect kulinganisha na umeme wa maji!!

There's no match between the two!

Bidhaa Kuu kutoka JNHPP ni UMEME PEKEE, and there's little (if any) to no by-products zinazoweza kuzalishwa kupitia JNHPP! Kinyume chake, Bidhaa Kuu ya LNG Project ni Gas na sio umeme lakini hapo hapo unaweza pia kupata UMEME + TAKATAKA ZINGINE!

Kumbe basi, 99% ya Multiplier Effect inayoweza kupatikana kupitia JNHPP pia inaweza kupatikana kutoka LNG Project. Kinyume chake, mengi unayoweza kupata kupitia LNG Project HUWEZI KUYAPATA kupitia JNHPP!

JNHPP itatupatia tu UMEME utakosaidia ku-boost sekta zingine za kiuchumi na labda kufanya Electricity Export but only regionally. Multiplier Effect tunayotarajia hapa inaweza kutokana na kuongezeka kwa uzalishaji kwa sababu tutakuwa na umeme wa uhakika.

Hata hivyo, YOTE hayo pia unaweza kuyapata kupitia LNG Project...

Wakati hali ni hiyo kwa KNHPP, LNG Project inaweza kukupatia AT LEAST yafuatayo:-

1. Umeme... Wakati Umeme sio Main Product from LNG Project, pale JNHPP umeme ndiyo MAIN PRODUCT itakayotokana na investment husika!

Kwa maana nyingine, faida yoyote ya kiuchumi INAYOWEZA kupatikana kwenye JNHPP Project ambayo umeme wake ndio Main Product, pia INAWEZA kupatikana, tena kwa ukubwa wa maradufu kutoka LNG Project kupitia umeme unaoweza kuzalishwa ingawaje sio Main Product!

Na kama tunasema LNG Project izalishe UMEME TU basi umeme huo unaweza kutumika kote Sub-Saharan Africa tena kwa miongo kadhaa wakati JNHPP Project haina uwezo hata ku-sustain hata uchumi kama wa South Africa!

In fact, hata Kenya ukiwaambia waachane na vyanzo VYOTE vya umeme walionao na watumie umeme kutoka JNHPP tena peke yao, bado umeme huo HUWEZI kuwatosha!!

Hapa ili nieleweke labda niseme hivi: Kwa sasa Umeme wa Gas uliopo kwenye Gridi ya Taifa ni almost 57% ya umeme WOTE huku hydropower ikichangia roughly 37%! Hata hivyo, 57% hiyo inatokana na less than 7.5 Trillion Cubic Feet of Gas ambazo ndizo zimeanza kuchimbwa kutoka Songongo, Mkoani Lindi na Madimba, mkoani Mtwara! U

Ukitoa hizo 7.5 Trillion Cubic Feet of gas ambazo zimeanza kuchimbwa, kuna almost 50 Trillion Cubic Feet of gas ambazo HAZIJAGUSWA! And remember, hiyo 57% ya umeme unaozalishwa sio unatokana na full capacity ya hizo 7.5 Trillion Cubic Feet za gas... hell no!

NInachotaka kusema ni kwamba, at full capacity, hizo 7.5 Trillion Cubic Feet zinaweza kuzalisha maradufu ya umeme utakaozalishwa na JNHPP na hapo bado zile 50 Trillion Cubic Feet HUJAZIGUSA!

2. Gas.. Hii ndiyo MAIN PRODUCT from the LNG Project. Hapo juu tumeshaona Umeme unavyoweza kuwa another product from the LNG Project, BUT...

(a) Gas For Export: LNG ni biashara kubwa sana duniani, na kwahiyo ni EXPORTABLE Product world-wide na sio tu regionally kama tunavyoweza kusafirisha the ONLY JNHPP Product!

Watu wanaposikia Lindi inataka kujengwa LNG Plant, akili yao wanadhani ni substitutes ya JNHPP! Kwamba, lengo ni tufanye gas processing kisha gas itumike kuzalisha umeme!

Kutokana na imani hiyo ndo maana unakuta Wafuasi wengi wa JPM wanapinga sana ule mradi kwa kile wanachodhani una lengo la kufuta JPM Legacy kwenye Bwawa la Nyerere!!!

Hapa ieleweke tu kwamba HAKUNA MJINGA ANAYEWEZA KUWEKEZA USD 30 BILLION for kwa ajili ya kuzalisha umeme kwa nchi maskini kama Tanzania! Hizo almost TRILLIONS 70 zinarudi rudi vipi ikiwa main product ni umeme?!

Hiyo investment inafanyika kwa sababu almost 50 Trillion Cubic Feet of UNDEVELOPED GAS ni Huge Opportunity for Export na sio eti kuzalisha umeme ili hatimae kuua Legacy ya JPM kwenye Bwawa la Nyerere!

(b) Gas For Domestic and Industrial Use:- Asikuambie mtu... this's a huge business opportunity!

Tuchukue mfano mdogo tu wa hii tenda ambayo ilitangazwa na TPDC...



Kabla hata hatujaingia huko kwenye gesi yenyewe, hebu tutafakari hiyo project! Yaani tunahitaji kiwanda kitakachoweza kuzalisha vifaa vifuatavyo:- HDPE pipes, HDPE fittings, Domestic Gas Meters and associated fittings, Commercial Gas Meters and associated fittings, and PRMS.

Na kwavile hiyo inaangukia kwenye Local Content, hiyo kazi inatakiwa kufanywa na Watanzania as per Sheria ya Mafuta na Gesi ya 2015!

Now tujiulize!!

Kama tunaamua gas infrastructure zifike hadi wilayani, hapo atakayepata tenda atalazimika kuzalisha hivyo vifaa kwa wingi gani, na angetoa ajira za moja kwa moja ngapi, indirect employment ngapi, na Wauza Mama Lishe wangeuza sahani ngapi za ubwabwa, ugali, chapati and everything else?

That's what we call: ECONOMIC MULTPLIER EFFECT! Gesi ipo LIndi na Mtwara lakini effect yake inasababisha kujengwa kwa kiwanda cha kutengeneza vifaa vya kujengea miundo mbinu ya usambazaji gesi! Hapo zitazalishwa aina ya ajira kama nilivyotaja hapo juu!

LNG Project inayopelekea kujengwa kiwanda tajwa hapo juu, effect yake itamkuta hadi muuza Mama Lishe, Muuza Genge, Mangi na Mpemba na maharage unga na mchele wao dukani, mkulima aliyezalisha hizo bidhaa, n.k kwa sababu pesa itakayotokana na hizo shughuli itakuwa inaenda moja kwa moja kwa wananchi na pesa hizo kuambukiza sekta zingine za kiuchumi na kijamii!

Hapo umeshazalisha tu vifaa tajwa... what next?

Hivyo vifaa vikishazalishwa ina maana itabidi iwepo kampuni nyingine/zingine za kutandaza hizo infrastructure Tanzania mzima! Kampuni hiyo nayo itatoa ajira za moja kwa moja, kwa vibarua na wauza Mama Lishe ambao pia wataambukiza sekta zingine kama nilivyotaja hapo juu!

Aidha, projects zote mbili... za kuzalisha vifaa na kusambaza miundombinu pia zitazalisha PAYE na Kodi zingine kwenda serikalini, na hatimae kuleta direct effect kwenye public services zitolewazo na serikali!

THAT'S WHAT WE CALL MULTIPLIER EFFECT in the national economy ambayo inapatikana hata kabla gesi yenyewe HUJAIGUSA!

Gesi imeshazalishwa, and ready for different uses! Je, miundo mbinu itaweza kufika kila mahali? HELL NO! This HELL NO is another business opportunity kwa sababu hatimae kutakuwa na new opportunity to Gas Vendors! Wenye uwezo watajenga Gas Fuelling Stations!

That's what we call Multiplier Effect!!

3. Gas By-Products:-

Nimeshajaza server tayari kwahiyo hapa niongee kidogo tu ingawaje kuna mengi zaidi ya kuongea!

Mali Ghafi zinazotokana na uchakataji wa gesi zinaweza kutumika kutengeneza bidhaa mbalimbali! Hapa tusiende mbali! Tayari kuna project ya USD 1.9 Billion kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanda cha Mbolea ambacho kinatarajia kutumia Gas By-Products!

Tanzania hii HAKUNA Kiwanda chenye thamani hata nusu ya hicho kiwanda!! Now tujuulize: Kiwanda kama hicho kinaweza kuzalisha direct and indirect employment to the company ngapi, Mama Lishe wangeuza kiasi gani kwa vibarua na wafanyakazi, PAYE and other taxes zingelipwa kiasi gani...

THAT'S WHAT WE CALL MULTIPLIER EFFECT!

Sio viwanda vya mbolea peke yake vinavyoweza kutumia Gas By-Products! Kuna at least 4 MORE products, including Plastic Products zinazoweza kuzalishwa kupitia Natural Gas By-Products!!!

FAIDA zote hizo nilizotaja hapo juu, HUWEZI KUZIPATA kupitia JNHPP!!

Sasa akina sisi tulikuwa tunapinga JNHPP kwa sababu tunaamini LNG Project inaweza ku-offer almost everything that can be offered by JNHPP but MANY MORE at much HIGHER VALUE than what JNHPP can offer!!!

Kwenye uchumi tunazungumzia dhana ya optimal allocation of resources!! Tunaambiwa resources, kwa muktadha huu pesa, ni SCARCE! Hivyo basi, kidogo utakachopata unatakiwa ku-allocate kule utakopata MAXIMUM RETURNS, and not just RETURNS!

LNG Project inaweza Kujenga JNHPP with our own money in less than 5 years lakini JNHPP KAMWE haiwezi kuwa na uwezo wa ku-fully finance LNG Project!! Kumbe basi, kama tunaamini Hydropower ni CHEAP source of electricity, bado tungeweza kujenga mradi huo kwa pesa zetu sisi wenyewe miaka michache tu baada ya kuanza kuzalisha gesi!

ALL IN ALL, should we expect CHEAP ELECTRICITY from JNHPP?!

Kwa maoni yangu, sioni hiyo cheap electricity inapatikana patikana vipi!!

Kwahiyo ndugu yangu Malcom, ule mpango wako wa kusambaza mashine za kusaga Tanzania mzima kwa sababu kuna umeme wa bei rahisi unakuja, man, ningekushauri pitia vizuri plans zako kwa sababu I strongly believe umeme wa bei rahisi HAUTAKUWEPO!!

WHY?

1. Mradi utatumia takribabi Sh 7 TRILLION. Hapo zijaweka riba za mabenki kwa sababu funding sources zingine zinatoka kwenye private banks!

Sasa kama tunadhani umeme utakuwa wa bei rahisi, who will pay hizo TZS 7 Trillions + Interests?! LAZIMA Watumiaji tulipe hizo gharama!!!

2. Watanzania tunadhani umeme utakaozalishwa pale ni MWINGI kweli kweli!!

Guys, kinachozalishwa pale sio kwamba Umeme Mwingi bali Umeme unazalishwa kwa ajili ya jamiii yenye Umaskini Mwingi!!

Kama nilivyosema hapo awali, Kenya ni nchi maskini tu! Lakini leo tuseme Kenya iachane na vyanzo vyote vya umeme inavyotumia hivi sasa na badala yake waanze kutumia umeme MWINGI utakazozalishwa pale JNHPP, katu Umeme huo HAUTAWATOSHA!!

Hata Tanzania kwenyewe, na umaskini wetu huu halafu tuseme tufunge vyanzo vyote vya umeme tulionao na tuanze kutumia tu Umeme MWINGI kutoka JNHPP... it'll take us less than 5 years kabla hatujaanza kuwa na uhaba wa kutisha wa umeme kwa sababu pale hakuna umeme mwingi bali tuna umaskini mwingi unaofanya less than 3000MW zionekane ni umeme mwingi!

Ninachojaribu kusema ni nini: Endapo uchumi wetu unaongeza kwa angalau 10% TU, umeme kutoka JNHPP + Available Sources HAUTAWEZA kuhimili uchumi huo ambao kimsingi na wenyewe utakuwa ni uchumi wa kimaskini tu!!!

Kwa maana nyingine, hata kabla hatujamaliza deni la TZS 7 Trillion za JNHPP basi kuna uwezekano mkubwa sana demand ya umeme nchini inaweza kuongezeka hapo mbeleni na kumeza umeme wote tulionao hivi sasa + Umeme wa JNHPP!

Demand ikiwa kubwa, watakachofanya TANESCO ni ku-DISCOURAGE Matumizi Makubwa ya Umeme! Una-discourage Matumizi Makubwa ya Umeme sio kwa kutoa elimu bubu watoazo kwenye ma-tv bali watafanya hivyo kwa kupandisha bei ya umeme ili hatimae muache matumizi holela ya umeme, kama mlivyoacha kutumia majiko ya umeme bila hata kutandikwa bakora!!

Na hapa tukumbushane kwamba, kama kweli tunaamini bei itakuwa ndogo basi ni hiyo bei ndogo ndiyo itakuwa chanzo cha kukaribisha bei kubwa! Umeme ukiwa nafuu, matumizi ya umeme yataongezeka! Watu watatupa majiko yao na pasi zao za mkaa kwa sababu umeme ni cheap!

Wafanyabiashara wataachana na mashine za kusaga zinazotumia mafuta na kuhamia mashine zinazotumia umeme kwa sababu umeme ni cheap!

Matumizi ya vifaa vya umeme yataongezeka kwa sababu umeme ni cheap!!! Huku Uswahilini ule ugomvi wa wapangaji kwamba tuwe tunazima mafriji na mafriza yetu, ugomvi huo utapungua kama sio kwisha kabisa kwa sababu umeme ni cheap, na watu watakuwa wanajiachia!!

OUTCOME?

Increased power consumption!! Njia ya kupambana na hilo? Nishasema hapo juu: discourage power consumption by increasing the price!!

IT'S SIMLE ECONOMY!

Is JNHPP White Elephant Project?

Yakitokea niliyosema hapo juu, HAIWEZI KUWA White Elephant Project lakini yasipotokea inaweza isiwe White Elephant Project lakini inaweza kuwa a STRUGGLING PROJECT!!

Tunahitaji uchumi mkubwa zaidi ili tuweze ku-consume hizo additional MW zitakazozalishwa! But don't forget, huo uchumi ukitokea itamaanisha NO MORE CHEAP ELECTRICITY kwa sababu power consumption itakuwa kubwa!!

Na isipotokea, ina maana Project Haitaweza kuzalisha pesa ya kutosha kulioa madeni yake, and hence becoming a STRUGGLING PROJECT!!

Yaani ndo ile inaitwa Ukichimama Nchale, Ukikimbia Nchale!! Sasa chagua mwenyee udungwe nchale wakati umesima au wakati unakimbia... MAUMIVU YAPO PALE PALE!!

Ndo vile tu umeme utaingizwa Grid ya Taifa lakini kama ingekuwa unakuwa distributed kipeke yake peke yake, watu wangeukimbia huo kama wanavyolikimbia Daraja la Kigamboni!!!
 
Nimefurahi kukuona hapa kaka mkubwa, nikimalizana na pirika ntatulia nisome vizuri. Thank you for your time, I believe there's a lot to learn from your post.
 
Mkulu, Nina hamu sana kujua madhara ya miradi ya HEP kwa mazingira.

Lingine ni kuwa, kama kule jangwani Misri wanatumia Aswan dam with very little effect of evaporation. What about the place where there is a double maxima rainfall!!?
Wewe hujui km miti zaidi ya milioni moja kwa eneo la ukubwa wa mkoa wote wa Dar imekatwa kupisha ujenzi!!?

Unajua athari za kutokuwepo vegetation cover na uhusiano wake na climate hasa rainfall formation? Go back to school usinichoshe.
 
Wewe hujui km miti zaidi ya milioni moja kwa eneo la ukubwa wa mkoa wote wa Dar imekatwa kupisha ujenzi!!?

Unajua athari za kutokuwepo vegetation cover na uhusiano wake na climate hasa rainfall formation? Go back to school usinichoshe.

Zingine ni story tu mkuu wangu.

Here are the facts and figures:
Project Catchment Area: 1,590sqkM
Length of the dam: approx. 100km
Width of the dam: approx. 700m
Area of the dam: approx. 70kM
Height of the dam: approx. 130m

NB: The area of Dar region is 1,200sqkM.

Say again the size of land of which deforestation took place!!!?
Also understand the meaning of "catchment area".

Also you can walk through the below site for more insight.
 
Mkuu

Huu mradi unapigwa sana vita na lile genge na sasa hivi ni kama umepotezewa hivi. Wako busy kumtafutia Mchechu position.

Utaendelea lakini utafanyiwa sana figisu same to SGR unavyopigwa pancha.

Kama Taifa 10% zinaturudisha sana nyuma, zinakwamisha maendeleo ya nchi zote mbili. Tanzania Bara na Tanzania Visiwani.

Kwenye gas wajanja washaweka % zao kwenye kila mauzo yanayofanyika kutoka kwa supplier wa gas kwenda kwa Tanesco.

Gas iko Tanzania lakini hatuimiliki, inamilikiwa na kampuni fulani ya kibepari, Kampuni husika inafanya kuiuzia hiyo gas Tanesco.

Hayati Magufuli aliachana na umeme wa gas akaegemea upande wa maji zaidi sababu maji hatuuziwi kama ilivyo kwenye gas.

Ndiyo maana unaona sasa wanahamisha magori kwa gia ya kusafisha vinu vya gas (Tanesco) na kutuwekea mgao wa umeme kutuaminisha kwamba gas ni muhimu kuliko maji.


Kwa yaliyotokea kwenye mkataba wa Beker Botts yamechagiza kupunguza makali ya drama hiyo.

Bepari anaamini Africa ni bara la giza (Dark Continent) pamoja na kujitutumua kwetu katika utafutaji wa vyanzo vya uhakika vya nishati tajwa, bado tuko giza.

Bepari kwa kushirikiana watu wachache tuliowaamini kama viongozi anahakikisha tutaendelea kubaki na giza letu kwa vizazi na vizazi.

Naamini ili Nchi yeyote iwe na maendeleo hasa kwenye nyanja ya viwanda na teknolojia ni lazima kuwepo na nishati ya umeme wa uhakika , JNHPP ni nishati ya uhakika.

Tanzania ina geographical Location nzuri ambayo inaiwezesha nchi yetu kupata mvua za kutosha kabisa kwa mwaka.

Hivyo tukiacha siasa za matumbo na kutumika naamini umeme wa maji ni mwarobani thabiti wa kutatua changamoto zetu za kiuchumi na za kijamii.

Shukrani!
 
Now, this is how you dispel a lackadaisical propaganda: Numbers do not lie.
 
Kaka CHIGE nimetulia na kusoma vizuri huu mchango wako na nikiri nimejiufunza mengi sana. From Economic Stand-Point, you have made Hell of an argument. Kweli nakumbuka mwaka 2018 uliwahi kulizungumzia sana hili kule INTERNATIONAL FORUM. Hivyo kutoka kwenye haya uliyoyasema, mimi naomba niulize tu suala lifuatalo:

Hata kama huu mradi wa JNHPP hauna manufaa makubwa kiuchumi (The Multiplier Economic Effect) kama ilivyo gesi, kuna haji gani yoyote ya kufanya hujuma ??? Nasema haya kwasababu kauli kutoka juu zimekuwa nyingi sana, zinazokinzana na kubadilika-badilika. Kama gesi nayo ni njia sahihi, kwanini basi tusifanye miradi yote kwa pamoja: Kwani hatuwezi kuwa na JNHPP na miradi ya umeme wa gesi pia ???

Ikumbukwe kama ulivyosema, The Multiplier Effect: Hayo mashirika ya gesi yanazo faida nyingi zaidi kibiashara kutoka kwenye gesi. Gesi ina matumizi mengi kwa dunia hii ya leo zaidi ya ufuaji umeme. Gesi pekee inasaidia katika utengenezaji wa Petro-Chemicals ambazo hutumika kutengeneza bidhaa muhimu kama plastiki, rangi, mbolea na madawa ya binadamu na mengineyo. Au ni lazima hayo mashirika yauze pia gesi kwa TANESCO ili tuweze kufua umeme ???

Lakini pia, binafsi naona hakuna shida yoyote ile Tanzania yetu inaweza kupata kwa kuwa na umeme wa maji, gesi, upepo au nyuklia. Tena hili litakuwa jambo jema kabisa. Kama nilivyosema hapo juu kuhusu Tennessee Valley Authority (TVA), wana vyanzo vingi vya nishati. Wana umeme wa maji, gesi, upepo na nyuklia na hawapati tatizo lolote: Kwanini kwetu huku tatizo ndiyo lionekane sana. Kwani ???
 
Mi nauliza tu, na nitakuwa nayliza kila siku asubuhi na jioni kwa kila uzi wa bwawa la Nyerere. Crane la tani 26 liko wapi?
 
Ndugu yangu MALCOM LUMUMBA,

Amini usiamini, suala la Hujuma dhidi ya JNHPP ni Propaganda tu. Hakuna hujuma yoyote!! Ni saa chache tu zilizopita nilikutana na post moja ikizungumzia hilo suala la hujuma, na mtoa hoja hiyo akadai, kama si hujuma dhidi ya JNHPP basi kwa sasa Bwawa lingekuwa tayari.

Hapo hapo nikagundua mtoa mada HAKUWA NA TAARIFA SAHIHI. Wakati mradi unaanza, ilitarajiwa mradi ungekamilika na kuwa operational by June 2022. Kwa maana nyingine, hata kabla ya hiyo June 2022 haijafika, mtoa mada anaamini kama isingekuwa hujuma, hivi sasa mradi ingekuwa umeshakamilika!

Wakati mwingine watu huwa wanachanganya madesa kutokana na taarifa kama hizi, especially wanapoishia kusoma heading:-


Hiyo habari ni ya November 2021. Sasa watu wakiona habari kama hiyo wanakimbilia kusema "Kuna hujuma"! Lakini kisome kipande hicho cha habari kisha linganisha na CAG REport ya 2019/2020

Kama si kuchelea kuifanya post kuwa ndefu basi ningeweka angalau SECTION mzima ya taarifa husika. Hata hivyo, unaweza kufanya your own assignemnt kuhusu: Annual General Report of the CAG For the Financial Year 2019/2020.

Chapter 6, Page 117 ya taarifa hiyo ya CAG inazungumzia JNHPP. Aidha, subsction "c" on Page 121 utakutana na haya maneno:-

Unaona hapo Ripoti ya CAG ya 2019/2020 ilizungumzia mradi ku-delay kwa miezi 5, na sababu ndo hizo hizo zilizotajwa kwenye habari ya Habari Leo ya Nov 2021.

Hapo unapata picha gani! Wakati mdau yule akiamini kwa sasa ulitakiwa uwe umekamilika, kumbe taarifa sahihi ilibidi uwe umekamilika by June 2022 lakini bado pia ikatokea tena delay ya 5 MONTHS!!

Kinachoendelea hivi sasa ni hofu isiyo na maana yoyote kwa sababu hata ukiwauliza walio field, wanakuambia ujenzi unaendelea! Na kama ambavyo nilisema hapo kabla Legacy Defenders wanachanganya sana madesa! Kwa akili yao wao wanadhani LNG Project ni Power Generation Project inayolenga kuua Legacy ya JPM kupitia JNHPP kumbe ni vitu viwili tofauti!
Nakubaliana na wewe kwa 100%! Dunia ya leo, popote utakapoenda duniani wanazungumzia suala la Energy Mix kwa sababu No One Source is Enough especially dunia ya leo inayokumbwa na mabadiliko ya hali ya nchi!

Wewe ulitolea mfano wa sustainability ya TVA, and YOU'RE RIGHT lakini tusisahau wenzetu wapo more discipline. Wale hawawezi kufanya shughuli za kibinadamu kiholela pembeni mwa TVA lakini sisi tunaweza sana!

Na kimsingi, mimi siipingi JNHPP as JNHPP bali napinga issue mzima ya nishati ilivyokuwa handled. Seems like JPM aliaminishwa kwamba JNHPP ndo Alpha and Omega!! Matokeo yake nini?!

Baada ya kuwa tumeshavuta gesi kutoka Mtwara to Kinyerezi, Serikali ya JK ilikusudia kujenga 4 Power Generations Plants pale Kinyerezi! Lakini kwavile muda wake ulishaisha, akajenga tu Kinyerezi I, akaacha Kinyerezi II ikiwa kwenye mchakato.

JPM ilibidi sasa amalizie Kinyerezi II, III, na IV ili ku-guarantee umeme wa kutosha at least in the next few years. Hata hivyo, serikali ikafanya tu ile KInyerezi II ambayo mchakato wake ulishaanza, na III & IV zikapigwa chini na kuhamia kwenye Bwawa la Nyerere! Na kuna kila dalili JPM alikuwa misled kwa kuambiwa "umeme tulio nao unatosha" ndo maana akaamua kuachana kabisa na Kinyerezi bila kujua kwamba "umeme unatosha under ideal conditions."

Kwahiyo YES, hata baada ya kuona umuhimu wa JNHPP bado hatukutakiwa kuachana na vyanzo vingine ambavyo leo ukivigusia tu, utaambiwa FISADI au Unatumwa na Mafisadi ili wauze gesi kwa sababu watu wanaamini JNHPP ndo Alpha & Omega!!
 
Kwa Tz tatizo ni kubwa zaidi kwani wanaopinga mradi ndio wamepewa wasimamie!!!
 
Ndugu msomi umesahau mradi mkubwa wa INGA 1&2 ya DRC ambayo ingeweza kutoa umeme kwa nusu yote ya Afrika lakini mabeberu wameuua kabisa huo mradi,,,,Ona leo mabeberu wanazungumzia Russia kuivamia Ukraine kwa swala au sababu moja tu kubwa ambayo ni bomba la gesi kutoka Urusi hadi Ujerumani kupitia Ukraine. Kwa ufupi mabeberu hawapendi wafrika muwe na enough and reliable energy especially electricity ili kuwachelewesha kimaendeleo na kibaya na kuwarahisishia mabeberu huwatumia wafrika wenyewe kwani mzungu haji moja kwa moja kutusimamisha,,,Kumbuka ati Nape alipinga mradi wa bwawa la Nyerere kwa kigezo cha kipuuzi cha uharibifu wa mazingira,,Magufuli aliwaona mabeb eru kwa jicho la ndani sana Mungu amuweke mahali pema pepona na tutamkumbuka sana
 
Jambo usilojua ni kuwa kama Magufuli angekuwepo leo hii... huo mradi kitambo sana ungekuwa umekamilika... so hao walioamua kuhujumu ndo uwaulize kwanini hawajaumaliza ili mradi uanze kulipa deni la mkopo waliokopa... simple logic... acheni uchawi... Magu was a National Hero.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…