Mrejesho: Faida nilizopata baada ya kuwatoa watoto wangu shule ya English Medium na kuwarejesha kayumba

Sawa mkuu, naamini uko sahihi kabisa, ila na wanaopeleka watoto wao shule wanazotaka pia wako sahihi kabisa.
 
Ukiona huwezi kusomesha mtoto English medium School basi wewe huna uwezo huo, full stop! Hizo sababu nyingine unazotoa si kweli, imagine umewatoa watoto kwenye shule nzuri unajisifu umenunua kiwanja cha laki 9 Mvuti! Hakuna kitu muhimu kama elimu ya msingi iliyo bora na inayokwenda na wakati.
Masikini wanapenda sana kujifariji na sababu za kipuuzi.
 
Ni kweli mkuu ila Nina watoto wanasoma shule moja jijini 2M per each, Kwa mwaka 4.M yaani mkuu inanisononeshansana kuona wanakaririshwa tu. Nimewaza sans baada ya kusoma Uzi huu.

Kibaya zaidi mkurugenz ameweka burser/mhasibu Hana huruma.

Naendelea kuwaza lkn elim ni Bora kuliko kiwanja. Lkn wapi Sasa tunakwenda.


Mimi n mtumish wa imma. Serikalini ndio kumejaa walimu very professional. Lkn serikali inawakosea san na wao hawafanyi vema. Ila wapo vzr wakiwezeshwa.

Kwa Sasa naona si English Media Wala feza school hakuna lolote.


Huyu accountant ameniingiza kwenye matatizo makubwa mno.
Nakumbuka ilikuwa Januari nikiwa nimeandaa ada kama kawaida kianzio. Si akaikataa bana! Watoto wawili Kila mmoja laki Nne jumla laki nane, alidai Kila mmoja lazima owe 600K. Niliingia mkopo ambao unaniandama hadi sasa....


Mmiliki wa shule nilimuamini nikadamp wanangu lkn alitubadilia, alikataa hata end of Januari nikamilishe aligoma. Iliniuma Sana. Kwa hiyo mleta Uzi huu hili suala ni seriasi sana.
 
Elimu ni nini?
 
Ni kweli mkuu ila Nina watoto wanasoma shule moja jijini 2M per each, Kwa mwaka 4.M yaani mkuu inanisononeshansana kuona wanakaririshwa tu. Nimewaza sans baada ya kusoma Uzi huu
Gutuka mkuu usiendelee kupigwa.
 
Tatizo la kusoma st kayumba unakuwa huna strong connections unless ziwe zile special schools. Yaani utajikuta unamaliza lakini marafiki zako wengi watakuwa katika positions ambazo hazimsaidii mtu kati yenu kuondoka katika poverty circle

Yaani circle nzima ya marafiki si ajabu ukakuta huna contact ya kukuambia kuna nchi flani ulata ina fursa flani
 
Nilisimamisha ujenzi kwa takribani miaka 6,tokea nimechukua maamuzi magumu ya kumpeleka mtoto wangu kayumba ujenzi unaenda kwa kasi ya ajabu,hili kwa wale wazee wa kukwapua nadhani hawatanielewa,ila kwa sisi tunaotegemea mshahara wa mwezi watajua naongea nini.Kizuri zaidi mwanangu ni kicwa na huku aliko bado anawapelekesha,kwa hiyo namshukuru Mungu kwa kunipa maamuzi sahihi...
 
Wow... very inspiring.

Niseme tu, primary nilisoma bweni, nikapangiwa shule ya serikali mbali. Nilipataga bendel memmorial na Mary Gorethy lkn sikwenda kwakua aunty yangu alisoma hiyo shule ya serikali miaka ya 90s. Ilikua bora sana kielimu miaka hiyo. Basi nikaenda. Sikua natumia sana nguvu kusoma. Wapo waliotoka shule za kayumba hata majina yao kuandika hawakua wakijua. Ilinishangaza sana. Lakini wapo wa kayumba waliokua wakikimbiza snaa. Wapo pia waliotoka shule za english mediums wengine moshi na arusha. Walifanya vizuri hawa wote. Mimi sikua natumia msuli wala
Kwa kweli nilikua natumia kingereza changi vizuri[emoji28][emoji23][emoji23]
Ila nilikua naumwa umwa maana sijazoea mazingira. Ila shule ni nzuri kwa kweli. Iko mazingira rafiki. Baada ya form 1 mzazi akataka nirudisha private. Kwakweli nilikataa. Niligoma. Unapata wapi maisha ya kisela kama haya[emoji23] yaan kusema kweli, kama hujasoma shule ya bweni ya serikali hujaenjoy. Kwanza nilikua kiongozi toka naanza mpaka namaliza form four. Na shule ina shamba kubwa tu. Sema sikuwahi lima. Kuna viwanja vya kufyekaaa. Yaan kila kazi inajitegemea. Kwakweli ulikua msingi mzuri sanaa. Na sijawahi jutia sema wengi niliosoma nao wa mikoa tofauti wana roho za uchoyo wala siyo bajeti mpaka ukubwani huku.
Nadhani ni nature ya mazingira yao. They dont wanna spend big to get bigger. Simaanishi starehe hapa hapana.

Ila this kayumba had the best experience.
Primary shule ya masista walikua wanatubebesha mawe mtoni na kulima juu. Sema ni kupanda karanga[emoji23] kufua pia tulikua tunawafulia hadi wadogo wa madarasa. Still was a good experience too. Imenifaa kimaisha kwakweli japo wazazi walipojua masista wanatupa hizo kazi ilikua hekaheka kubwa sana. Wazazi wetu wa dar kasoro wazazi wangu tuu nahisi walitaka watoa watoto wao kwa hasira ile shule kwa aina ya kazi tuluzopewa[emoji23]
Wazazi wangu hawana malezi ya kudekadeka. Na usiombe uwe na kesi.
Nimekuja enda baobab advance ni upumbavu tu. Huko ni daddy na mammy. Adhabu unapewa mopper na squeezer usukume maji kwenye verandah mtu analia mpk kamasi anataka mzazi amuhamishe shule anateseka. Mtu anakuja na pafyumu 5 tofauti za bei tofauti tena za bei ya ndege. Kwakweli mimi nilishindwa kama ilivyo ada kwa wagumu wenzangu. Watu mnakula soseji, makuku, samaki etc mchuzi mtaam kbs wanalalamikia principal wazazi wao wanalipa ada kubwa sana wanataka fanya mgomo wakati o level yangu huo ni msosi wa 5 star hotel[emoji23][emoji23][emoji23] aaah ujinga kbs.

Nakubaliana na ambao wanasema kama uwezo upo peleka mtoto English Medium hizi za kawaida ili mtoto awe na base ya Lugha vizuri halafu baada ya hapo tupa kayumba tu kwa kweli. Ila kayumba yenyewe inategemea pia. Kuna kayumba ni kilio. Hazifai. Ila niliona serikali ilifanya ukarabati baadhi ya shule za serikali zile kubwa. Hata yangu imependeza kweli. Rai yangu wakarabati zote aisee. Ni shule nzuri mno. Zaidi wajitahidi kwa waalimu waliopo katika hizi shule kubwa walau wawe degree holders.

Mimi nadhani Elimu bora iwe kwa vitendo zaidi. Na kama mzazi una biashara zako basi wanao wawe wanafika pia na wanapractice hasa wakati wa likizo. Haya mashule ya gharama yapogi tu. Ila kayumba experience was the best for me kwa kweli.
 
Yaaan nisikudanganye. Mimi somo la hesabu nilikua mbovu kweli. Yaani mbovu. Nadhani pia ni kufata mkumbo wa watu ooh mathematics blah blah. Nilikua nachapwa na mwalimu wake. Ilibidi siku moja nimfate ofisini tu nimwambie mwalimu utanipiga uniue. Kati ya kondoo wako 234 naomba unitoe hapo mimi kondoo mmoja tuu maana tunakielekea utaniua. Kuna madam wa kiswahili akasikia akaniuliza kwani mock ulipata ngapi.? Nikameonyesha paper langu. Aliangua kicheko staff nzima na walimu wengine walipoona. Badi mwalim wa hesabu akaja class qkatangaza kuanzia siku hiyo ni maamuzi ya mtu aingie kipindi cha maths ama lah. Na kweli nina F. inaniumaje.
 
Chamsingu waende shule tu mkuu, usiwaze sana

Mimi nimesoma hizo English medium za mamilioni na kweli faida yake nimeona ni kingereza tu hamna kingine[emoji28]

Elimu ya chuo au veta ndo ina umuhimu mkubwa
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] kabisaaaa. Hapo tu ndo tuliwabondea kayumba. Ila kayumba wana akili balaa. Basi tu yaani
 
Pole sana mkuu, fanya kile kiko ndani ya uwezo wako. Watoto wangu wanasoma private kwani nazijua changamoto lukuki za public school.
😁
 

Attachments

  • CF7C4099-37B1-4352-BD12-A889DB0DEDC1.jpeg
    9.1 KB · Views: 2
  • 4268C8B0-5AD6-408F-A201-D264760FF446.jpeg
    8.4 KB · Views: 2
  • F6E394E3-D4A9-44A3-A6E1-FCF7EE899E60.jpeg
    7.9 KB · Views: 2
  • 8AD4C34D-70D3-4B8E-B387-19EA1070E57F.png
    23.9 KB · Views: 2
😁😁
 
Wewe kama wewe lazima upate Faida Kwa sababu umepunguza matumizi

Ila Kwa watoto wako ni maumivu na hayo maumivu watakutanayo pale watakapoingia katika soko la ajira na kuitwa katika interview tena kama sector binafsi ndio kabisa lazima wawapishe walioyosoma private school

Mimi nimesoma kayumba kuanzia primary Hadi form six nilipoingia chuo ndio nikaanza kuona tofauti kati ya tuliyotoka kayumba na wale private school

Pia nilipoingia katika ajira sector binafsi ndio kabisa Kuna tofauti kubwa sana

Broo believe me usiwaone hao akina Joket au akina Babra ukazania walifika walipofika Kwa bahati mbaya sio kweli ila ukweli ni kwamba wazazi wao wali invest

Mimi binafsi nimeapa watoto wangu hawatasoma kayumba labda niwe Sina pesa
 
Hakika maisha yana grade..ndio mana kuna maduka posta...kuna maduka kariakoo..kuna kununua nyanya gengeni kuna kununja supermarket...kuna kwenda kununua nguo sagula sagula ilala, karume ila pia kuna kuingia boutique nk.nk....all in all tje function of Income...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…