Mwarabu mlokole
JF-Expert Member
- Jul 8, 2023
- 231
- 386
Imegeuka me versus you sasa?Wewe tajiri networth yako ni how much Million Dollars ? Tuanzie hapo mkuu
This is what I was talking aboutDaah... Haya mambo ya mtu kipato cha chini kujitutumua kusomesha watoto English medium yanachangamoto zake.
Jirani yangu hapa kafirisika kauza ardhi hadi mlangoni kisa watoto wasome private.
Matokeo wakwanza kamaliza form 4 yupo nyumbani wawili bado anapambana nao ila hali tete kwelikweli
Kuna shule mtu anamaliza wote wanakuwa bodabodaTatizo la kusoma st kayumba unakuwa huna strong connections unless ziwe zile special schools. Yaani utajikuta unamaliza lakini marafiki zako wengi watakuwa katika positions ambazo hazimsaidii mtu kati yenu kuondoka katika poverty circle
Yaani circle nzima ya marafiki si ajabu ukakuta huna contact ya kukuambia kuna nchi flani ulata ina fursa flani
Basi kumbe wewe ni mbumbumbu wa pesa. Huna elimu ya pesa. Huna mahusiano mazuri na hela...Imegeuka me versus you sasa?
Wewe watoto wako wapo Kayumba kwa kukimbia ada ya 4mil mimi watoto wangu wapo shule hizo ulizokimbia,na sio ya 4mil ni multiple ya hiyo 4mil,yaani mara kadhaa za kutosha
Kwahilo tu sina haja ya kutaja networth...na wanaume hua hatutaji networth,unaona tu action then wewe mwenye kuuliza maswali unapiga hesabu kwenye ubongo wako mwenyewe!
Sasa huoni we ni masikini?Nilisimamisha ujenzi kwa takribani miaka 6,tokea nimechukua maamuzi magumu ya kumpeleka mtoto wangu kayumba ujenzi unaenda kwa kasi ya ajabu,hili kwa wale wazee wa kukwapua nadhani hawatanielewa,ila kwa sisi tunaotegemea mshahara wa mwezi watajua naongea nini.Kizuri zaidi mwanangu ni kicwa na huku aliko bado anawapelekesha,kwa hiyo na mshukuru Mungu kwa kunipa maamuzi sahihi...
Kusomesha English Medium ni ushamba tu.Miezi michache iliyopita nilianzisha Uzi hapa jf wenye title" Tunaowatoa watoto wetu shule za English Medium na kuwarejesha kayumba njooni tufarijiane hapa"
Soma: Tunaowatoa watoto wetu shule za kiingereza njooni hapa tufarijiane
Lengo la Uzi lilikuwa kupata watu watakao nipa "faida" nitakazozipata kwa kuwarejesha watoto wangu Kayumba plus maneno ya kunifariji ambayo yatasaidia kujustify uamuzi wangu.
Sababu ya kuwarejesha kayumba wanangu ni kuyumba kiuchumi. Nilipata maoni mengi mazuri. Miongoni mwa maoni niliyopata hapa JF ni pamoja na:
1. Itanisaidia kuokoa pesa ambayo ninaweza ku invest katika maeneo mengine muhimu kama vile kuwanunulia viwanja na kuwajengea nyumba watoto wangu so that wanapofika level ya chuo at least kila mtu awe na nyumba yake moja.
2. Sitokuwa na stress za ada plus mbaya kuliko zote ile stress maalumu ambayo mzazi unaipata wakati mtoto wako amerudishwa nyumbani ada, wakati wenzake plus jirani zako wanaosoma kayumba wanaenda shule.
Nje ya JF nilipata ushauri kutoka kwa
1. Binti yangu; yeye yupo form three shule ya kayumba pia. Nilimsomesha English Medium kuanzia la kwanza. Anasema daddy kuna watoto wamesoma shule za kiswahili lakini wapo vizuri sana darasani kuliko waliosoma shule za kiingereza.
2. Brother wangu wa mtaani ambaye na yeye kawarudisha watoto wake kayumba. (huyu kasomesha hadi chuo but still bado ana watoto wa primary). Alikuwaga kichaa wa shule za English medium.
Anasema mdogo wangu mtoto wako umsomeshe kayumba au English Medium mwisho wa siku wote watakufa watazikwa…(anataja jina la makaburi ya mtaani kwetu)
Akaongeza: Tofauti ya kayumba na English Medium ni lugha tu lakini mwisho wa siku wote wanaandaliwa kuajiriwa..
Kingine siku hizi watoto wanaharibika sana so hakuna guarantee mtoto wako atakuja kuwa nani hapo baadae.
Akaongeza "shule nyingi za English Medium zinawafanya wanafunzi hasa watoto wa kiume kuwa watoto walaini laini (ana experience na watoto wake mwenyewe na rafiki zake). Halafu haziwafundishi watoto kuhusu uhalisia wa maisha zaidi ya kuwakaririsha masomo so bora umpeleke kayumba akapambane na kukomaa huko.
MIEZI MIWILI BAADA YA KUFANYA UAMUZI.
1. Nimenunua kiwanja nje ya mji ( ilala rural/ mvuti) kwa Tsh. laki tisa na mwezi ujao Insha'allah nitapiga msingi( fundi wangu yupo Kinondoni ambae alinijengea nyumba yangu ya kwanza utaratibu wake wa kazi huwaga ni wewe ukiwa na hela yoyote hata laki tano niite kwa lako tano hiyo hiyo nitafanya kitu. Next time ukipata laki tatu niite. Hadi nyumba yako itakamilika. Huyu ndo alinifanya nikajenga nyumba yangu ya kwanza. Tukiwa Kinondoni shamba au Hananasif tunaangalia ndondo anapokea simu za watu anaowajengea nyumba anasema “huyu anauza mchicha, huyu mama lishe etc”. Nikawa inspired.
2. Kuhusu somo la kiingereza nimenunua vitabu na CDs ambayo madogo watakuwa wanajifunza wakiwa home plus tuition ya nguvu ya kiingereza.
Mungu akinipa uhai nitafanya vitu vikubwa sana kwenye familia yangu.
Kama uwezo wako mdogo, unaishi nyumba ya kupanga uswahilini, uchumi wako umeyumba, sikushauri uhangaike na English medium.
Mpeleke mwanao kayumba wewe upambane kutafuta hela.
Haya ndo maisha watu wanafurahia[emoji16]
Medium nyingi ada haivuki 3mil kwa mwaka, ambazo ni sawa na 300,000 kila mwezihata English Medium hakuna connection. Connection unazo zizungumzia wewe zipo international kama IST. Hata hivyo kiuhalisia hazipo kwa sababu wanao soma huko wengi wametoka familia zinazo ishi kizungu ( kibepari) na ubinafsi.
St. Kayumba utapata network kubwa kwa sababu mnasoma watu wengi. Unlike English Medium darasa moja watu wanane hakuna connection yoyote ya maana.
Usisahau mkuu asilimia kubwa ya wazazi wanao somesha watoto wao hizo English Medium ni mahohehahe tu wenye hela za mawazo ambao hufuata mkumbo na kujionyesha kwamba na wao wanaweza kusomesha watoto English Medium lakini kiuhakika hawana lolote la maana kwenye maisha yao..
Wanaosomesha watoto English Medium ni masikini tu ambao wameamua kujipa matumizi ya sio ya lazima sawa na mfanyakazi mwenye mshahara wa laki nne ambae amenunua iPhone ya milioni mbili baada ya kujibana kwa miezi mitano.
English Medium ni Kayumba ambazo zinafundisha kwa KIINGEREZA.
Kuna watu wanadhani kuteseka ndo kumfundisha mtuFaida ya mtoto kusoma shule bora ni kumjengea kujiamini
Unachukualia sampo space ya watu 3 kwenye kundi la wanafunzi zaidi ya milioni 14 walio mashuleni mwaka huuBut the evidence says no. Uhalisia unaonyesha watoto walio soma kayumba ndio wanajiamini zaidi kwenye maisha kuliko hao wa st. English Medium.
Akina Diamond, Konde Boy, Shilole wote wamesoma kayumba ila wana confidence kuliko.
Halafu hivi sio nyie mnaosemaga watu ambao hawajasoma kabisa ndio wana uthubutu kuliko wasomi?
Kusomesha English Medium ni ushamba tu.
Tambua kwamba mwalimu wa kwanza na mwalimu mkuu wa mwanao ni wewe mzazi.
Kama mzazi umesoma na ulikuwa unayamudu masomo hakikisha unakuwa mwalimu kwa mwanao.
Akiwa shule ya msingi ndo msingi wa yote.
Elimu ya Tanzania imesimama katika nguzo kuu mbili. Nguzo hizo ni Hisabati na Kiingereza.
Mwanao akiwa shule ya msingi hakikisha unakagua madaftari yake ya Hisabati na Kiingereza. Hakikisha unampa mazoezi (homework) za hisabati na kiingereza na kwamba hakikisha muda wote yuko sura za mbele kwenye mtaala wa hisabati na kiingereza ili akienda darasani iwe ni marudio.
Akihitimu darasa la saba na alama A ya hisabati na A ya kiingereza hapo kazi umeshamaliza katika suala zima la masomo. Ataelewa masomo mpaka chuo kikuu. Hapo sasa utabaki na shughuli ya kukabiliana na changamoto za balehe.
kwani kasema yeye tajiri?Sasa huoni we ni masikini?
Unafanyaje ujenzi kwa miaka yote hiyo?
Jifunze watawala wanavyotutesa, imetokana na makuzi mabovu, wana roho ngumu na mbaya.Kuna watu wanadhani kuteseka ndo kumfundisha mtu
Ndo maana hakuna mtawala ambaye anasomesha mtoto wake hizi shule za hovyo, ukienda Feza wamejaa watoto wao wanasoma mtaala wa NECTA wengine CambridgeJifunze watawala wanavyotutesa, imetokana na makuzi mabovu, wana roho ngumu na mbaya.
Makuzi huchangia 80% kumtengeneza au kumharibu mtu.
Waache watu wajifariji humuNdo maana hakuna mtawala ambaye anasomesha mtoto wake hizi shule za hovyo, ukienda Feza wamejaa watoto wao wanasoma mtaala wa NECTA wengine Cambridge
Tanzania ni masikini sababu watu wanafurahia umasikiniWaache watu wajifariji humu
Kibaya zaidi tunakiana tuwe maskini woteTanzania ni masikini sababu watu wanafurahia umasikini
Mi mtoto wangu atasoma shule bora zisizo karirisha kufaulu.Kibaya zaidi tunakiana tuwe maskini wote
Yaani brother.. Inatia huruma sana, kuna shule mtu akisoma anakutana na exposure na connections za kutosha.Kuna shule mtu anamaliza wote wanakuwa bodaboda