Mrejesho: Faida nilizopata baada ya kuwatoa watoto wangu shule ya English Medium na kuwarejesha kayumba

Mrejesho: Faida nilizopata baada ya kuwatoa watoto wangu shule ya English Medium na kuwarejesha kayumba

Nilisoma shule ya kupitia kwenye umande halafu dawati mnakaa watoto wanne. Kabla ya kuingia darasani ilikuwa kila mtu afagie mraba wake ambao prefect atapita kukagua kuwa mraba umefagiliwa vizuri ndipo mtoto anaingia darsani. Zaidi ya nusu ya darasa walikuwa hawana viatu.
 
Algore shule za private walimu huwa wanapika matokeo ili kuwa brain wash wazazi.

pride darasa linapo kuwa na watoto wengi inasaidia pia kumchallenge mtoto kwa sababu huo ndio uhalisia katika maisha halisi. Darasa lenye watoto wachache mfano watoto 10 au 20 mtoto hapati changamoto kwa watoto wenzake.

Plus private school watoto wanakuwa spoon fed.

Kumbuka Lengo pekee la kumpeleka mtoto shule ya Msingi sio tu ili afaulu kwenda secondary lakini pia ajifunze kuhusu maisha.

Kumpeleka mtoto kwenye shule ambayo darasani wanakaa watoto watano tu kwanza atakuwa selfish, atakosa network ya watu ( kujuana na watu wengi: It is a proven fact that ur network is ur networth)..

Mtoto aliesoma kwenye shule yenye watoto wengi hawezi kutishwa na uwingi wa candidates lets say kwenye interview ambayo wamekuwa shortlisted watu elfu moja. Jambo hilo linaweza kumu intimidate mtoto alie soma kwenye shule ambayo darasa moja wanakaa watoto8


Kuhusu kujiamini kwenye maisha experience inaonyesha watoto walio soma kayumba hujiamini mara mia ya wale walio soma English Medium.

Wana uthubutu wa kufanya na kujaribu mambo mengi kwa sababu mazingira magumu " tough environment" ya st kayumba yamewashape,tofauti na wa English Medium ambao hawana uthubutu wa kujaribu kwa sababu walizoea kuwa spoon fed na kurahisishiwa mambo.


Mifano: Diamond, Shilole, Mobetto etc.

Mwisho: ni ujinga kumpeleka English Medium mtoto ako akafundishwe na mwalimu ambae amesoma kayumba.
Pole sana mkuu, fanya kile kiko ndani ya uwezo wako. Watoto wangu wanasoma private kwani nazijua changamoto lukuki za public school.
 
Watanzania mnapenda sana kupigwa aisee.

Yani nikatoe milioni 4 ili mtoto wangu afundishwe A for Apple? Mwisho wa siku Hesabu sifuri sayansi sifuri ila anajua tu KIINGEREZA cha kubabaisha.


Pesa haitumiki kizembe namna hiyo.. Muweke st kayumba weka usimamizi kama.msingi wa KIINGEREZA mtafutie walimu na programme nzuri za KIINGEREZA ili anapoingia form one masomo ya secondary yasimsumbue.


Acheni utoto nyie...


Kwanza hampo hata smart mngekuwa smart mngewauliza kwanza watoto wenu wanataka kuwa nani ndo muwapeleke kwenye shule inayo toa programme husika. Sio una hangaika kumkaririsha English Medium kumbe mwenzako anataka kuwa kama Konde Boy..

vinginevyo nyie na wanao somesha watoto wao st kayumba wote mpo sawa ila wenzenu wajanja nyie mnapigwa mamilioni wenzenu hawapigwi
Tatizo ni kutaka kuwapangia wengine cha kufanya, haiitaji kuwa milionea kumpeleka mtoto wako shule nzuri, ambazo nyingi ni around 3M kwa mwaka. Wengine tunaishi maisha tuliyonayo kwa sababu wazazi wetu walitusomesha. Watoto wangu wanasoma na watasoma shule zinazoeleweka. Wewe pambana na hali yako tu mkuu, huku mikoani matajiri wenye elimu ndogo ndio wanainvest sana kwenye elimu ya watoto wao.
 
Safi sana mkuu hizi English Medium ni ubabaishaji tu. . Wanao wapeleka watoto huko acha waendelee kupigwa
Mara nyingi makuzi ya mtu uamua maisha atakayoishi, ndio maana hekima ya kawaida kuna mambo huwezi pangia watu wayafanyeje. Huna haja ya kushupaza shingo kutetea hicho unachokiamini kwani maisha halisi hayatakuwa hivyo unavyofikiri kamwe. Heshimu wanaopeleka watoto wao shule wanazoona ni sahihi kwa future yao.
 
Miezi michache iliyopita nilianzisha Uzi hapa jf wenye title" Tunaowatoa watoto wetu shule za English Medium na kuwarejesha kayumba njooni tufarijiane hapa"

Soma: Tunaowatoa watoto wetu shule za kiingereza njooni hapa tufarijiane

Lengo la Uzi lilikuwa kupata watu watakao nipa "faida" nitakazozipata kwa kuwarejesha watoto wangu Kayumba plus maneno ya kunifariji ambayo yatasaidia kujustify uamuzi wangu.

Sababu ya kuwarejesha kayumba wanangu ni kuyumba kiuchumi. Nilipata maoni mengi mazuri. Miongoni mwa maoni niliyopata hapa JF ni pamoja na:

1. Itanisaidia kuokoa pesa ambayo ninaweza ku invest katika maeneo mengine muhimu kama vile kuwanunulia viwanja na kuwajengea nyumba watoto wangu so that wanapofika level ya chuo at least kila mtu awe na nyumba yake moja.

2. Sitokuwa na stress za ada plus mbaya kuliko zote ile stress maalumu ambayo mzazi unaipata wakati mtoto wako amerudishwa nyumbani ada, wakati wenzake plus jirani zako wanaosoma kayumba wanaenda shule.

Nje ya JF nilipata ushauri kutoka kwa

1. Binti yangu; yeye yupo form three shule ya kayumba pia. Nilimsomesha English Medium kuanzia la kwanza. Anasema daddy kuna watoto wamesoma shule za kiswahili lakini wapo vizuri sana darasani kuliko waliosoma shule za kiingereza.

2. Brother wangu wa mtaani ambaye na yeye kawarudisha watoto wake kayumba. (huyu kasomesha hadi chuo but still bado ana watoto wa primary). Alikuwaga kichaa wa shule za English medium.

Anasema mdogo wangu mtoto wako umsomeshe kayumba au English Medium mwisho wa siku wote watakufa watazikwa…(anataja jina la makaburi ya mtaani kwetu)

Akaongeza: Tofauti ya kayumba na English Medium ni lugha tu lakini mwisho wa siku wote wanaandaliwa kuajiriwa..

Kingine siku hizi watoto wanaharibika sana so hakuna guarantee mtoto wako atakuja kuwa nani hapo baadae.

Akaongeza "shule nyingi za English Medium zinawafanya wanafunzi hasa watoto wa kiume kuwa watoto walaini laini (ana experience na watoto wake mwenyewe na rafiki zake). Halafu haziwafundishi watoto kuhusu uhalisia wa maisha zaidi ya kuwakaririsha masomo so bora umpeleke kayumba akapambane na kukomaa huko.


MIEZI MIWILI BAADA YA KUFANYA UAMUZI.

1. Nimenunua kiwanja nje ya mji ( ilala rural/ mvuti) kwa Tsh. laki tisa na mwezi ujao Insha'allah nitapiga msingi( fundi wangu yupo Kinondoni ambae alinijengea nyumba yangu ya kwanza utaratibu wake wa kazi huwaga ni wewe ukiwa na hela yoyote hata laki tano niite kwa lako tano hiyo hiyo nitafanya kitu. Next time ukipata laki tatu niite. Hadi nyumba yako itakamilika. Huyu ndo alinifanya nikajenga nyumba yangu ya kwanza. Tukiwa Kinondoni shamba au Hananasif tunaangalia ndondo anapokea simu za watu anaowajengea nyumba anasema “huyu anauza mchicha, huyu mama lishe etc”. Nikawa inspired.

2. Kuhusu somo la kiingereza nimenunua vitabu na CDs ambayo madogo watakuwa wanajifunza wakiwa home plus tuition ya nguvu ya kiingereza.

Mungu akinipa uhai nitafanya vitu vikubwa sana kwenye familia yangu.

Kama uwezo wako mdogo, unaishi nyumba ya kupanga uswahilini, uchumi wako umeyumba, sikushauri uhangaike na English medium.

Mpeleke mwanao kayumba wewe upambane
Huku ni kuyumba kiuchumi tu hakuna kingine.
Ndomaana akasema tuje tufarijiane. Mara zote mtu mwenye matatizo au majanga anapewa faraja.
 
Tatizo ni kutaka kuwapangia wengine cha kufanya, haiitaji kuwa milionea kumpeleka mtoto wako shule nzuri, ambazo nyingi ni around 3M kwa mwaka. Wengine tunaishi maisha tuliyonayo kwa sababu wazazi wetu walitusomesha. Watoto wangu wanasoma na watasoma shule zinazoeleweka. Wewe pambana na hali yako tu mkuu, huku mikoani matajiri wenye elimu ndogo ndio wanainvest sana kwenye elimu ya watoto wao.
Umasikini ni tatizo na Watanzania wanafurahi kuwa masikini na wanautukuza
 
Nilisoma shule ya kupitia kwenye umande halafu dawati mnakaa watoto wanne. Kabla ya kuingia darasani ilikuwa kila mtu afagie mraba wake ambao prefect atapita kukagua kuwa mraba umefagiliwa vizuri ndipo mtoto anaingia darsani. Zaidi ya nusu ya darasa walikuwa hawana viatu.
safi sana mkuu coz ulijifunza changamoto za maisha at that tender age
 
Kiwanja Mvuti???😁 Tatizo Pesa na wengi kama huyu mtoa Mada anajalibu kujustfy Umasikini wake kuwa alichofanya ni sawa.
Zipo faida za mtoto kusoma shule Za Private, Mtoto alieasoma Makurumla Secondary School uwezi mfananisha na yule aliesoma St. Joseph au Feza...Ikumbukwe hawa wote wanasoma syllabus moja na wanafanya mtihani wa Darasa la saba huo huo.
Isitoshe Mtoto anaesoma Feza , Watoto wenzanke anaosoma nao wanakuwa toka familia za watu wenye pesa, vyeo n.k anakuwa na Future Connection za huakika.Uwezi ukawa unasomesha mtoto wako kwa Mtogole Secondary School Yenye uhaba wa Walimu, Ukosefu wa Vifaa vya mahabara na Vitabu ukatagemea huyo mtoto akafaulu vizuri.Tafuta Hela acha fikira za Umasikini.Usintanie wewe
Diamond alisoma Feza?.. Konde Boy?. Connection ni akili na ujanja wa mtu mwenyewe binafsi wala haina uhusiano wowote na lugha aliyo tumia kusoma shule.


Wema alisoma Academy ila company yake ni kina Aunty Ezekiel na Gigy Money walioishia form two Kayumba.


Hamisa Mobetto kasoma st.kayumba tena form four leaver lakini ana connection na viongozi wakubwa nchini plus Artists wakubwa duniani akina Rick Ross etc.

Mange Kimambi kasoma Arusha school plus international schools ila kazi yake ni umbea ambao ulitakiwq kufanywa na akina Mwajuma wa Tandale pale.

Usiishi kwa kukariri mkuu.

Ishi kulingana na uhalisia wa nyakati zilizopo
 
Miezi michache iliyopita nilianzisha Uzi hapa jf wenye title" Tunaowatoa watoto wetu shule za English Medium na kuwarejesha kayumba njooni tufarijiane hapa"

Soma: Tunaowatoa watoto wetu shule za kiingereza njooni hapa tufarijiane

Lengo la Uzi lilikuwa kupata watu watakao nipa "faida" nitakazozipata kwa kuwarejesha watoto wangu Kayumba plus maneno ya kunifariji ambayo yatasaidia kujustify uamuzi wangu.

Sababu ya kuwarejesha kayumba wanangu ni kuyumba kiuchumi. Nilipata maoni mengi mazuri. Miongoni mwa maoni niliyopata hapa JF ni pamoja na:

1. Itanisaidia kuokoa pesa ambayo ninaweza ku invest katika maeneo mengine muhimu kama vile kuwanunulia viwanja na kuwajengea nyumba watoto wangu so that wanapofika level ya chuo at least kila mtu awe na nyumba yake moja.

2. Sitokuwa na stress za ada plus mbaya kuliko zote ile stress maalumu ambayo mzazi unaipata wakati mtoto wako amerudishwa nyumbani ada, wakati wenzake plus jirani zako wanaosoma kayumba wanaenda shule.

Nje ya JF nilipata ushauri kutoka kwa

1. Binti yangu; yeye yupo form three shule ya kayumba pia. Nilimsomesha English Medium kuanzia la kwanza. Anasema daddy kuna watoto wamesoma shule za kiswahili lakini wapo vizuri sana darasani kuliko waliosoma shule za kiingereza.

2. Brother wangu wa mtaani ambaye na yeye kawarudisha watoto wake kayumba. (huyu kasomesha hadi chuo but still bado ana watoto wa primary). Alikuwaga kichaa wa shule za English medium.

Anasema mdogo wangu mtoto wako umsomeshe kayumba au English Medium mwisho wa siku wote watakufa watazikwa…(anataja jina la makaburi ya mtaani kwetu)

Akaongeza: Tofauti ya kayumba na English Medium ni lugha tu lakini mwisho wa siku wote wanaandaliwa kuajiriwa..

Kingine siku hizi watoto wanaharibika sana so hakuna guarantee mtoto wako atakuja kuwa nani hapo baadae.

Akaongeza "shule nyingi za English Medium zinawafanya wanafunzi hasa watoto wa kiume kuwa watoto walaini laini (ana experience na watoto wake mwenyewe na rafiki zake). Halafu haziwafundishi watoto kuhusu uhalisia wa maisha zaidi ya kuwakaririsha masomo so bora umpeleke kayumba akapambane na kukomaa huko.


MIEZI MIWILI BAADA YA KUFANYA UAMUZI.

1. Nimenunua kiwanja nje ya mji ( ilala rural/ mvuti) kwa Tsh. laki tisa na mwezi ujao Insha'allah nitapiga msingi( fundi wangu yupo Kinondoni ambae alinijengea nyumba yangu ya kwanza utaratibu wake wa kazi huwaga ni wewe ukiwa na hela yoyote hata laki tano niite kwa lako tano hiyo hiyo nitafanya kitu. Next time ukipata laki tatu niite. Hadi nyumba yako itakamilika. Huyu ndo alinifanya nikajenga nyumba yangu ya kwanza. Tukiwa Kinondoni shamba au Hananasif tunaangalia ndondo anapokea simu za watu anaowajengea nyumba anasema “huyu anauza mchicha, huyu mama lishe etc”. Nikawa inspired.

2. Kuhusu somo la kiingereza nimenunua vitabu na CDs ambayo madogo watakuwa wanajifunza wakiwa home plus tuition ya nguvu ya kiingereza.

Mungu akinipa uhai nitafanya vitu vikubwa sana kwenye familia yangu.

Kama uwezo wako mdogo, unaishi nyumba ya kupanga uswahilini, uchumi wako umeyumba, sikushauri uhangaike na English medium.

Mpeleke mwanao kayumba wewe upambane kutafuta hela.
Wacha tujifariji tu.

Hela ya ada ya mtoto wangu
Zamani nilikuwa napiga mahesabu nikipata kiasi kadhaa tu nafanya biashara.

Eti sasa hivi ndio pesa ya ada ya mtoto...Kum*nyok ELIMU.✍🏻
 
Primary sio eneo la kucheza nalo uko sahihi
Ndio.maana inaitwa elimu ya msingi

Msingi ukiwa mbovu huko mbele kilio
Kweli kabisa Mkuu mimi mwenyewe shahidi , ninao uwezo Mkubwa sana kwa hilo Sina shaka ila elimu ya msingi nilipiga kayumba na niseme ukweli lugha ilikuwa kikwazo kikubwa sana ata baada ya kumaliza chuo kikuuu na kuajiliwa , unakuta kwa uwezo ulionao unaaminiwa na kupewa majukumu makubwa Kuna wakati unapangiwa vikao na board of directors wengine wazungu unapima maji unaona kabisa hapa - hiki ni kina kirefu , ilinisumbua sana ikabidi niende British school pale mwenge kujipiga msasa , si haba kwa sasa Niko vzr naweza nikapiga umbea kwa ung'eng'e , kwahiyo guys msipuuzie msingi ni kitu cha kuzingatia sana kwa mtoto.
 
Kama uwezo wa kipato ni mzuri, private school ni mahali sahihi kupeleka mtoto, shule za uma haswa kwa primary na olevel changamoto ni nyingi sana sana

Hizo unazo ziita changamoto ndio zinazo wafanya wazazi wengine wawapeleke watoto wao kwenye shule hizo ili waanze kujifunza kuhusu changamoto za maisha tangu wakiwa wadogo.

Hizo changamoto ni sehemu ya makuzi kwa mtoto pia.


Binafsi siwezi mpeleka mtoto wangu sehemu ambayo haina changamoto
 
Back
Top Bottom