Mrejesho: Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga

Mrejesho: Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga

Nilivyosoma stori aisee,nimependa namna unavyoweka waz majibu ya mke...umepata mke mwenye hekima sana...ana majibu yenye busara na upole....nikirudi kwako....embu rahisisha tu mambo... Mwache aandike kwa jina lake maana hata
Wanawake nawapenda sana! Nyumba hii aiandike jina la mke; apambane ajenge na kiwanja chake ndicho aandike majina ya Watoto.
 
Usingemuambia kuhusu kumlipa hela, ungemueleza tu kuwa hiyo nyumba ya hapo ni mnaandika majina yenu. Kisha pesa ya kumlipa ukawekeza sehemu bila kumwambia, hiyo nyumba hata akiruhusu uandike jina lako kwa tamaa zake atakusumbua.

Sitisha maendelezo fanya yako ki jay mo.
 
Nilivyosoma stori aisee,nimependa namna unavyoweka waz majibu ya mke...umepata mke mwenye hekima sana...ana majibu yenye busara na upole....nikirudi kwako....embu rahisisha tu mambo... Mwache aandike kwa jina lake maana hata kiwanja ni chake....yaan ukiona MTU anakwambia ngoja nikajifikirie ujue bado hajaafiki....watoto analea mama pale ,wewe unakuja Mara mojamoja,kwann usimwamini mkeo...mbona kama umekaa attention sana...hata mkiachana kwa ajili ya watoto bado itakubidi uwaachie Nyumba(kwa mwanaume Mwenye akili hawez taka watoto wataabike pa kuishi)....ulisema una kiwanja...kama ulivyosema wewe ni mwanaume ,kichwa cha familia...em pambana tena jenga kwenye kiwanja chako then waandike wanao...Usitumie ubabe,tafadhali...mwachie tu kama zawadi hiyo Nyumba.... Ni mkeo huyo analea na kuishi hapo na watoto wako.(usipojiangalia,ndoa yako ndo inaenda kufall apart Mkuu)
Moja ya ushauri mbovu kabisa ni kuwaandika watoto kwenye nyumba au mali unazotafuta baba/mama...

Mali zote zinapaswa kuandikwa majina ya baba/mama, watoto wana nafasi yao lakini kamwe,kamwe kamweeee, usifanye makosa ya kuandika resources zako kwa majina yao, they are growing and they have their own roles to play kutengeneza maisha yao, wajibu wa wazazi ni kuwatengenezea watoto mazingira wezeshi kujiandalia kesho yao!

Mali zote ni za mke na mume, mpaka watakapofariki wote, then watoto warithi mali za wazazi wao, muhimu ni kuandika wosia tu na kuuhifadhi mahali salama bila watoto kujua wosia wako mpaka utakapojiridhisha kwamba wamejitengenezea maisha yao!

Narudia usithibutu kuwapenda watoto wako kwa kiwango cha kuwaandika kwenye kila resource yako, utawaharibu na watakuua kwa pressure...!
 
Sasa nimeongea na mke wangu kuhusu nyumba ambayo nimejenga kwenye kiwanja chake kuhusu umiliki kwasababu yeye alitaka kuandika jina lake tena kwa Siri.

Nimemuuliza kwanza kwamba tangu tuoane hatujawahi kuongelea kuhusu hicho kiwanja chake.

Akanikumbusha kwamba wakati tunaoana Mimi nilimshauri akiuze na ilituletea mtafaruku kweli. Na ni kweli nilisita sana kujenga kwenye kiwanja cha mke wangu kwasababu nilishaona ni mtu mpenda vyake na asiye na muda na vyangu ilihali tayari sisi ni mke na mme.

Na niwarudishe kidogo kilichonifanya nimuona wa tofauti kidogo baada ya kuhamia pale siku moja mwisho wa mwezi nilienda kuitembelea familia.

Asubuhi tukiwa Mimi na watoto akaleta mada kwamba Joyce (sio jina halisi) ambaye yeye ni shangazi kwa Joyce. Joyce ameniomba Jack (sio jina halisi) yaani mtoto wa Joyce aje aishi hapa na aende shule akikaa kwetu.

Sasa Joyce tuliwahi kukaa naye kama ndugu yake mke wangu akawa anatusaidia kazi lakini alikuja kuondoka kwa ugomvi na mke wangu.

Aliponipa hizo histori akili yangu iliyafanya mrejeo haraka sana nikakumbuka jinsi Joyce alivyoondoka kwa shangazi yake kwa maneno.

Nikamwambia wife hilo kwasasa haitawezekana na sababu niliyompa ni kwamba mtoto wetu kwasasa anasoma English medium halafu huyu Jack akija aende shule ya kawaida ( serikali) Mimi sitajisikia vizuri na haitakuwa sawa hata kwa tafsiri za watu wengi. Nikamshauri kwamba kama ni kwa ajili ya kwenda shule basi aende kwa Shemeji ( kaka yake wife) ambaye kimsingi yupo karibu na shule hiyo ya serikali na ni baba mdogo wake Joyce. Mke wangu alikuja juu sana na kuzua ugomvi kidogo nimpige. Lakini maneno yaliyonikera sana ni kwamba Mimi siwataki ndugu zake na huwa nakuja hapa kuleta vurugu na kwamba anajuta kuolewa na mimi na akakimbilia nje baadae nilimuita akaje tukaongea nikaamua kutulia ili nione maisha yanaendaje baada ya pale.

Na hapa wiki moja kabla alinijulisha swala la kuwekewa bcone kwenye like eneo kwamba inahitahijika 100,000 akanipa na time limit sikutaka maneno nikampa ile hela akalipa niliporudi akanionesha risiti nikamwambia wafuatilie waweke. Wiki inayofuata akanitaarifu kwamba wameshaweka bcone lakini wanahitaji passport 7 kwa maandalizi ya hati nikamwambia sawa.
Nilipoenda nikamwambia ebu nenda idara ya maji ukaulizie utaratibu wa kupata maji kwa bomba binafsi yaani kufungiwa mita ya maji kwenye hiyo nyumba.

Alienda baadae akaniambia wanahitaji tujaze fomu na passport mbili na fomu hurusiwi kuchukua unajazia kule idara ya maji nikamwambia sawa. Jioni akaniambia kesho nataka nikapige zile picha ajaze hizo fomu na kupeleka zile picha 7 kwa ajili ya hati Mimi nikaitikia sawa. Asubuhi kulipokucha nikamwambia simamisha Hilo zoezi hadi nije. Lakini nilimpigia simu jamaa yangu ambaye naye amejaza hiyo fomu nikamuulizi hivi hizi fomu hurusiwi kutokana nazo ukajazie nyumbani? Jamaa akasema mbona Mimi nilijazie nyumbani nikarudisha!

Nikamwambia sawa. Mimi nilikuwa naendelea kukusanya data zangu. Jana nikafanya ziara ya kustukiza nikafika nyumba lakini nikiwa njiani niliandika sms kumjulia hali yeye na watoto nikamwambia nipo njiani nakuja huko. Basi nikafika yeye alikuwa ametoka na watoto nikafungua nikaingia nikampigia akasema anakuja na kweli wakawasili na watoto, watoto wangu wananipenda sana wakafurahi stori mbili tatu.
Mimi sitaka kikao kichukue muda nikaanza kikao na yeye nikamwambia Mimi nimekuja kwa mazungumzo na wewe akastuka sana. Nikamwambia mazungumzo ni ya kawaida ya kifamilia. Tukaongea nikamwambia hiki kiwanja si unajua ni chako akasema ndio. Nikamwambia lakini bahati nzuri tumejaliwa kujenga nyumba ya familia, akasema ndio. Nikamwambia kuna vitu tusipoyaweka sawa huko mbeleni vitatuletea shida akashangaa. Nikamwambia kwasasa tunaelekea kwenye swala la umiliki sasa tuamue Mimi na wewe mmliki wa nyumba ya familia yetu kwenye kiwanja chako kitakuwa na umiliki wa nani? Hana jibu! Nikamuuliza je maji na hilo suala la picha za hati miliki ungeandika? Akasema Mimi nilijua ni vitu vya kawaida Wala sikufikiria yote hayo! Nikamuuliza kwa mkuu wa familia ni nani akasema ni wewe ( Mimi). Nikamuuliza Sasa mbona siku ile ulifanya tu kunipa taarifa tu unataka kwenda kupiga picha bila kuuliza tuandike jina la nani? Akasema Mimi niliona hata nikiandika jina langu ni sawa tu na kwasababu nilikupa taarifa niliona hakuna shida.

Nikamwambia sasa Mimi natambua kwamba kiwanja ni chako lakini nimejenga nyumba ya familia yangu ambayo ni sisi sote. Nimekuja tupate mwafaka wa hicho kiwanja na Mimi nipo kwa ajili kuidhamini familia yangu na katika hii familia tunao jielewa kwasasa ni Mimi na wewe vijana wetu bado wadogo. Nikamwambia Mimi nina majibu yangu lakini nahitaji majibu yako juu ya kiwanja hiki. Nikamkumbusha; kwamba siku ile ulivyoongea maneno ya kwamba Mimi huwa nakuja kukuletea vurugu na kwamba unajuta kuolewa na mimi nilizingatia na hivyo sitakubaki kuiweka rehani familia kwa kuruhusu mambo yaende kiholela. Akahamaki na kudai kwanini namkumbusha mambo ya zamani nikamwambia haikuwa sehemu ya mada lakini nimeona nikukumbushe ili ujirekebishe kimawazo, kauli na kimtazamo na ufahamu mipaka yake kama mke. Akasema Yale alitamka kwa hasira kwasababu ulinikemea mbele ya watoto n.k nikamwambia Mimi uliniletea mada yako mbele ya watoto na nilipopinga wewe ndo ukaleta ugomvi. Akasema tuyamalize kwanza haya ndo tuje swala la umiliki wa nyumba. Ila nikamwambia Mimi siwezi tena kukuruhusu kumiliki hii nyumba kwasababu hutahili utashindwa kuzuia hisia zako na utaendelea kuropoka zaidi na huenda hata kuna siku utamleta mwanaume humu na sitaweza kuzuia. Naye akasema na wewe unaweza kumleta mwanamke halafu unitoe Mimi.

Mwisho akasema nimpe muda atafakari swala la umiliki wa hii nyumba halafu atanipa jibu kwamba hawezi kupata jibu la haraka. Lakini nimemwambia Mimi ndiye nina wajibu na jukumu la kulinda, kuhifadhi na kutunza mali za familia hivyo yeye ni mtu wa pili kutoka kwangu na akaona ugumu nipo tayari kumpa pesa yenye thamani ya kiwanja chake yeye atajua atazifanyaje hizo hela lakini kiwanja kiwe chini ya familia na chini yangu kama mwenyewe dhamana ya familia namba moja.

Kwa hiyo namsubiri aamue then nami nitaweka msimamo wa kiti. Japo sasa amenuna lakini mgonjwa haulizwi dawa. Mimi kiukweli sina plan B ya hilo nahitaji heshima iwepo kwangu kama mwenye nyumba na siwezi kuwa mtalii kwenye familia yangu. Lazima kiti kiheshimiwe bila hivyo panya watatawala.

Naomba kuwasilisha kwa ajili yenu kujifunza na kutoa ushauri.

Asanteni

Ni ulimbukeni mwanaume kufikiri yeye ni kichwa na mmiliki, both you and your wife are selfish and uneducated..

Someni sheria. Hata ungeandika jina la nyau, Mali inayipatikana Mkiwa na Ndoa halali ni Mali yenu.

Kama mke wako alikuwa na kiwanja kabla ya ndoa, ujue anaweza kuwa na haki fulani kukizidi, umekosea kujenga.

Kama mwanaume na kichwa cha Familia. Achaneni na hizi harakati za kijinga ijengeni Familia.
 
Mkuu MBUZI kinachoendelea kwenye familia yako na kwangu kuko hivyo hivyo hapa nakaa kwenye nyumba ambayo kiwanja mke alikopa hela akanunua then tukaanza ujenzi tukahamia ila sikai nae hapa anakuja mara moja moja likizo na watoto kuna kipindi kulitokea mgogoro kidogo akadai anatafuta watu apauze( hati ya manunuzi ya kiwanja anayo yeye tena aliichukua kwa kuiiba na kule kuna jina lake) na hadi leo sijui kaificha wapi.

Hapa nimekaa mguu nje mguu ndani na nimeacha rasmi kufanya maendeleo yoyote kwenye hii nyumba. Najichanga nitafute kiwanja changu kimya kimya nijenge kimya kimya. Hawa wenzetu wana ubinafsi sana na hawafai kumiliki mali maana wana madharau flani hivi.

Aking'ang'ania kutaka umiliki mwachie mali zinatafutwa hizi.
 
Hivi kwanini wanawake hua wanakimbilia kusema mali ni za watoto?, kwanini wasi wajengee watoto wao maarifa ya kupambana na kupata vyao?

Binafsi,watoto wangu hawagusi mali yangu zaidi ya kuwajengea maarifa na akili za kutafuta chao.pia kuhusu mwamnake kuandika jina katika mali zako unakua umejiroga na kujijengea kaburi mwenyewe.

Kuhusiana na hii story, mkuu wewe ni mwanaume na kama mwanaume lazima ukubali kupambana, acha kufanya mambo kua magumu, jipange anza ujenzi katika kiwanja chako na kila kitu kitakua chako mengine funika kombe maana ulishayakanyaga mwenyewe kwa kuamua kwa kutumia hisia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna Makosa yapo kwenye mazungumzo kulazisha jina la Kiwanja kuwa la Mwamme ni Dhambi na Dhuruma.

Ni bora jina la Kiwanja muamdika majina ya watoto wenu.

Huyo ni mwanamke mawazo yake tofauti ataanza kuuliza na kuomba ushauri kwa wengine, ushauri akipewa Mbaya ni tatizo
 
Hakuna haja ya kukimbizana na mke wako. Trust baina yenu is not there and it will not there. Primary concern should be the well being of your children and their. Embark on plan B. Anza kujenga upya maisha yako na watoto.

Don't expect that things will be the same again. Allow her to do whatever she thinks is OK. Fanya yako and you may or may not tell her.
 
Mkuu, pole. Hope mtapata ufumbuzi mujarabu wa hiyo kadhia.
Mimi baada ya kuona jinsi wife anavyowapenda wanae (tuna watoto 2, mmoja miaka 5 mwingine miaka 2), nikaona sio kesi akiandika jina lake kwenye umiliki wa kiwanja. Mungu jaalia, tunaweza anza ujenzi mwakani, lakini hata nyumba nataka iwe Kwa majina yake. Sababu ni zipi?
1. Najua hawezi watelekeza watoto (labda apigwe ndumba), so pale patakuwa pa watoto. Hata likitokea la kutokea, siombei, watoto watakuwa na kwao.
2. Nimeshuhudia issues za mirathi, ndugu wamechukua mirathi ya watoto,(ilikuwa 19M). Yaani baba na mama wamekufa, mjomba akapewa zoezi la kusimamia mirathi ya marehemu dada yake, ndo mirathi ya wadogo wawili waliokuwa chini ya 18 ikapigwa. Nilijifunza kuwa mzazi, baba au mama atakuwa na uchungu zaidi na mali za watoto kuliko mtu wa nje.
Labda nakosea, labda sijui, kikubwa fuata moyo wako
Maamuzi yako yapo sawa kama mkeo anatoka kwa bwana, ila issue ya wewe kutangulia mbele za haki sio kitu ikiwa kwa sasa unaweza kuandikisha mali zako kama mirathi kabla halijatokea la kutokea... hapo sasa ndo uandike nani atabaki kuwa mmiliki wa nini.

Huwezi kusema unaogopa kuandika mirathi mapema na unahisi kama kujiombea kifo ilihali una hofu ya familia yako kuja kudhulumiwa yakitokea ya kutokea...

Note: kama mkeo hajatoka kwa bwana ukiandikisha jina lake umeisha issue ipo utajuaje maana binadamu hubadilika.
 
Mkuu, pole. Hope mtapata ufumbuzi mujarabu wa hiyo kadhia.
Mimi baada ya kuona jinsi wife anavyowapenda wanae (tuna watoto 2, mmoja miaka 5 mwingine miaka 2), nikaona sio kesi akiandika jina lake kwenye umiliki wa kiwanja. Mungu jaalia, tunaweza anza ujenzi mwakani, lakini hata nyumba nataka iwe Kwa majina yake. Sababu ni zipi?
1. Najua hawezi watelekeza watoto (labda apigwe ndumba), so pale patakuwa pa watoto. Hata likitokea la kutokea, siombei, watoto watakuwa na kwao.
2. Nimeshuhudia issues za mirathi, ndugu wamechukua mirathi ya watoto,(ilikuwa 19M). Yaani baba na mama wamekufa, mjomba akapewa zoezi la kusimamia mirathi ya marehemu dada yake, ndo mirathi ya wadogo wawili waliokuwa chini ya 18 ikapigwa. Nilijifunza kuwa mzazi, baba au mama atakuwa na uchungu zaidi na mali za watoto kuliko mtu wa nje.
Labda nakosea, labda sijui, kikubwa fuata moyo wako
Limbwata tayari limeshafanya kazi😀
 
Sasa nimeongea na mke wangu kuhusu nyumba ambayo nimejenga kwenye kiwanja chake kuhusu umiliki kwasababu yeye alitaka kuandika jina lake tena kwa Siri.

Nimemuuliza kwanza kwamba tangu tuoane hatujawahi kuongelea kuhusu hicho kiwanja chake.

Akanikumbusha kwamba wakati tunaoana Mimi nilimshauri akiuze na ilituletea mtafaruku kweli. Na ni kweli nilisita sana kujenga kwenye kiwanja cha mke wangu kwasababu nilishaona ni mtu mpenda vyake na asiye na muda na vyangu ilihali tayari sisi ni mke na mme.

Na niwarudishe kidogo kilichonifanya nimuona wa tofauti kidogo baada ya kuhamia pale siku moja mwisho wa mwezi nilienda kuitembelea familia.

Asubuhi tukiwa Mimi na watoto akaleta mada kwamba Joyce (sio jina halisi) ambaye yeye ni shangazi kwa Joyce. Joyce ameniomba Jack (sio jina halisi) yaani mtoto wa Joyce aje aishi hapa na aende shule akikaa kwetu.

Sasa Joyce tuliwahi kukaa naye kama ndugu yake mke wangu akawa anatusaidia kazi lakini alikuja kuondoka kwa ugomvi na mke wangu.

Aliponipa hizo histori akili yangu iliyafanya mrejeo haraka sana nikakumbuka jinsi Joyce alivyoondoka kwa shangazi yake kwa maneno.

Nikamwambia wife hilo kwasasa haitawezekana na sababu niliyompa ni kwamba mtoto wetu kwasasa anasoma English medium halafu huyu Jack akija aende shule ya kawaida ( serikali) Mimi sitajisikia vizuri na haitakuwa sawa hata kwa tafsiri za watu wengi. Nikamshauri kwamba kama ni kwa ajili ya kwenda shule basi aende kwa Shemeji ( kaka yake wife) ambaye kimsingi yupo karibu na shule hiyo ya serikali na ni baba mdogo wake Joyce. Mke wangu alikuja juu sana na kuzua ugomvi kidogo nimpige. Lakini maneno yaliyonikera sana ni kwamba Mimi siwataki ndugu zake na huwa nakuja hapa kuleta vurugu na kwamba anajuta kuolewa na mimi na akakimbilia nje baadae nilimuita akaje tukaongea nikaamua kutulia ili nione maisha yanaendaje baada ya pale.

Na hapa wiki moja kabla alinijulisha swala la kuwekewa bcone kwenye like eneo kwamba inahitahijika 100,000 akanipa na time limit sikutaka maneno nikampa ile hela akalipa niliporudi akanionesha risiti nikamwambia wafuatilie waweke. Wiki inayofuata akanitaarifu kwamba wameshaweka bcone lakini wanahitaji passport 7 kwa maandalizi ya hati nikamwambia sawa.
Nilipoenda nikamwambia ebu nenda idara ya maji ukaulizie utaratibu wa kupata maji kwa bomba binafsi yaani kufungiwa mita ya maji kwenye hiyo nyumba.

Alienda baadae akaniambia wanahitaji tujaze fomu na passport mbili na fomu hurusiwi kuchukua unajazia kule idara ya maji nikamwambia sawa. Jioni akaniambia kesho nataka nikapige zile picha ajaze hizo fomu na kupeleka zile picha 7 kwa ajili ya hati Mimi nikaitikia sawa. Asubuhi kulipokucha nikamwambia simamisha Hilo zoezi hadi nije. Lakini nilimpigia simu jamaa yangu ambaye naye amejaza hiyo fomu nikamuulizi hivi hizi fomu hurusiwi kutokana nazo ukajazie nyumbani? Jamaa akasema mbona Mimi nilijazie nyumbani nikarudisha!

Nikamwambia sawa. Mimi nilikuwa naendelea kukusanya data zangu. Jana nikafanya ziara ya kustukiza nikafika nyumba lakini nikiwa njiani niliandika sms kumjulia hali yeye na watoto nikamwambia nipo njiani nakuja huko. Basi nikafika yeye alikuwa ametoka na watoto nikafungua nikaingia nikampigia akasema anakuja na kweli wakawasili na watoto, watoto wangu wananipenda sana wakafurahi stori mbili tatu.
Mimi sitaka kikao kichukue muda nikaanza kikao na yeye nikamwambia Mimi nimekuja kwa mazungumzo na wewe akastuka sana. Nikamwambia mazungumzo ni ya kawaida ya kifamilia. Tukaongea nikamwambia hiki kiwanja si unajua ni chako akasema ndio. Nikamwambia lakini bahati nzuri tumejaliwa kujenga nyumba ya familia, akasema ndio. Nikamwambia kuna vitu tusipoyaweka sawa huko mbeleni vitatuletea shida akashangaa. Nikamwambia kwasasa tunaelekea kwenye swala la umiliki sasa tuamue Mimi na wewe mmliki wa nyumba ya familia yetu kwenye kiwanja chako kitakuwa na umiliki wa nani? Hana jibu! Nikamuuliza je maji na hilo suala la picha za hati miliki ungeandika? Akasema Mimi nilijua ni vitu vya kawaida Wala sikufikiria yote hayo! Nikamuuliza kwa mkuu wa familia ni nani akasema ni wewe ( Mimi). Nikamuuliza Sasa mbona siku ile ulifanya tu kunipa taarifa tu unataka kwenda kupiga picha bila kuuliza tuandike jina la nani? Akasema Mimi niliona hata nikiandika jina langu ni sawa tu na kwasababu nilikupa taarifa niliona hakuna shida.

Nikamwambia sasa Mimi natambua kwamba kiwanja ni chako lakini nimejenga nyumba ya familia yangu ambayo ni sisi sote. Nimekuja tupate mwafaka wa hicho kiwanja na Mimi nipo kwa ajili kuidhamini familia yangu na katika hii familia tunao jielewa kwasasa ni Mimi na wewe vijana wetu bado wadogo. Nikamwambia Mimi nina majibu yangu lakini nahitaji majibu yako juu ya kiwanja hiki. Nikamkumbusha; kwamba siku ile ulivyoongea maneno ya kwamba Mimi huwa nakuja kukuletea vurugu na kwamba unajuta kuolewa na mimi nilizingatia na hivyo sitakubaki kuiweka rehani familia kwa kuruhusu mambo yaende kiholela. Akahamaki na kudai kwanini namkumbusha mambo ya zamani nikamwambia haikuwa sehemu ya mada lakini nimeona nikukumbushe ili ujirekebishe kimawazo, kauli na kimtazamo na ufahamu mipaka yake kama mke. Akasema Yale alitamka kwa hasira kwasababu ulinikemea mbele ya watoto n.k nikamwambia Mimi uliniletea mada yako mbele ya watoto na nilipopinga wewe ndo ukaleta ugomvi. Akasema tuyamalize kwanza haya ndo tuje swala la umiliki wa nyumba. Ila nikamwambia Mimi siwezi tena kukuruhusu kumiliki hii nyumba kwasababu hutahili utashindwa kuzuia hisia zako na utaendelea kuropoka zaidi na huenda hata kuna siku utamleta mwanaume humu na sitaweza kuzuia. Naye akasema na wewe unaweza kumleta mwanamke halafu unitoe Mimi.

Mwisho akasema nimpe muda atafakari swala la umiliki wa hii nyumba halafu atanipa jibu kwamba hawezi kupata jibu la haraka. Lakini nimemwambia Mimi ndiye nina wajibu na jukumu la kulinda, kuhifadhi na kutunza mali za familia hivyo yeye ni mtu wa pili kutoka kwangu na akaona ugumu nipo tayari kumpa pesa yenye thamani ya kiwanja chake yeye atajua atazifanyaje hizo hela lakini kiwanja kiwe chini ya familia na chini yangu kama mwenyewe dhamana ya familia namba moja.

Kwa hiyo namsubiri aamue then nami nitaweka msimamo wa kiti. Japo sasa amenuna lakini mgonjwa haulizwi dawa. Mimi kiukweli sina plan B ya hilo nahitaji heshima iwepo kwangu kama mwenye nyumba na siwezi kuwa mtalii kwenye familia yangu. Lazima kiti kiheshimiwe bila hivyo panya watatawala.

Naomba kuwasilisha kwa ajili yenu kujifunza na kutoa ushauri.

Asanteni

Pia soma: Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga
Mkuu
Nimesoma habari hii ya mrejesho kwa kituo lakini nilipogundua unatuhusisha masuala ya ndani kabisa ya familia yako nje ya mada kuu nimegundua kuwa unapitia wakati mgumu sana kwenye hiyo familia ambayo mkeo ndiye kiongozi wa familia huku wewe ukiwa ni wa pili yake.

Pia nimegundua kuwa hauna mshauri mzuri kutoka kwenye familia uliyozaliwa yaani kimsingi ukoo wenu hakuna wa kukushauri kama wapo basi kuna jambo umefanya wamekutenga au kukususa

Jambo la tatu, kapime DNA ya mwanao kisha kaa kiume kuamua future ya familia iweje.

Mambo mengine yanahitaji umri na kifua. Sisi wengine tunapitia misukosuko ya kifamilia lakini hautuoni kuja kuwaanika wenza wetu humu kwa sababu ni kweli tunatofautiana namna ya kumudu msongo lakini tunalinda staha za wenza hata kama wana upumbavu andamizi kama GENTAMYCINE🤣

Nakushauri,
Achana na hiyo project maana huyo mkeo hana muda mrefu na wewe. AshaanA kukuonesha namna usivyokuwa ndani ya nafsi yake. Wewe ni mpitanjia na kila dalili umeiweka kwenye huu uzi.

Ishi kwa akili
 
Nakwambia kwa uzoefu kama unaamua mke wako kila.kitu uandike kwa jina lake umejiroga.bora ungeandika kwa majina ya watoto.

Kama una hela tafuta na mali zako za siri lakini usisahau ilitokea la kutokea mnagawana pasu.

Aisee ndoa ni majanga.
Mm nimemuachia kila kitu hadi nimeanza upya mambo ya kesi siwezi nimechukua begi niko shamba NAJUA WANAUME HAWANIELEWA MAISHA NI MAPFUPI SANA HAKUNA ANAYEJUA KESHO YAKE MNAGOMBANIA UMILIKI WA PROPERTIES MNAISHIA KUUANA Yanini mie
 
Labda nakosea, labda sijui, kikubwa fuata moyo wako
Hapana, hukosei, uko sahihi, wazazi katika mipango yetu tunapaswa kwanza kuweka maslahi mbele ya watoto, kwa kuzingatia kuna kesho huenda mzazi mmoja au wote wasiwepo duniani.
 
Back
Top Bottom