Kategele
JF-Expert Member
- Oct 7, 2017
- 1,055
- 2,466
Atakuwa kalishwa kichwa cha samaki Mgebuka huyu siyo bure😁😁
Katapishwe ulicholishwa
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Katapishwe ulicholishwa
Sifanye hivyo aisee hawa viumbe usile nao maagano. Andika jina lako tu kama ni mke wa ndoa hakuna wa kuwahangaisha. Wala usiandike jina la mtoto plz jitahdin kujifunza kutokana na historia.Mkuu, pole. Hope mtapata ufumbuzi mujarabu wa hiyo kadhia.
Mimi baada ya kuona jinsi wife anavyowapenda wanae (tuna watoto 2, mmoja miaka 5 mwingine miaka 2), nikaona sio kesi akiandika jina lake kwenye umiliki wa kiwanja. Mungu jaalia, tunaweza anza ujenzi mwakani, lakini hata nyumba nataka iwe Kwa majina yake. Sababu ni zipi?
1. Najua hawezi watelekeza watoto (labda apigwe ndumba), so pale patakuwa pa watoto. Hata likitokea la kutokea, siombei, watoto watakuwa na kwao.
2. Nimeshuhudia issues za mirathi, ndugu wamechukua mirathi ya watoto,(ilikuwa 19M). Yaani baba na mama wamekufa, mjomba akapewa zoezi la kusimamia mirathi ya marehemu dada yake, ndo mirathi ya wadogo wawili waliokuwa chini ya 18 ikapigwa. Nilijifunza kuwa mzazi, baba au mama atakuwa na uchungu zaidi na mali za watoto kuliko mtu wa nje.
Labda nakosea, labda sijui, kikubwa fuata moyo wako
hapana mimi namuona yuko sahihi, inaonesha mwanamke wake anataka kumpanda juu bila kumshirikisha yupo sahihi kabisa baba unatakiwa uwe na sauti yenye mamlaka wanawake tuna manyanyaso sana hapo akimpa hio ruhusa ya kujiandika jina la mwanamke bas wakigombana kidogo utasikia toka kwenye nyumba yangu yan hawa bila huyo mwanaume kua na sauti kama hivo atanyanyasikaNilivyosoma stori aisee,nimependa namna unavyoweka waz majibu ya mke...umepata mke mwenye hekima sana...ana majibu yenye busara na upole....nikirudi kwako....embu rahisisha tu mambo... Mwache aandike kwa jina lake maana hata kiwanja ni chake....yaan ukiona MTU anakwambia ngoja nikajifikirie ujue bado hajaafiki....watoto analea mama pale ,wewe unakuja Mara mojamoja,kwann usimwamini mkeo...mbona kama umekaa attention sana...hata mkiachana kwa ajili ya watoto bado itakubidi uwaachie Nyumba(kwa mwanaume Mwenye akili hawez taka watoto wataabike pa kuishi)....ulisema una kiwanja...kama ulivyosema wewe ni mwanaume ,kichwa cha familia...em pambana tena jenga kwenye kiwanja chako then waandike wanao...Usitumie ubabe,tafadhali...mwachie tu kama zawadi hiyo Nyumba.... Ni mkeo huyo analea na kuishi hapo na watoto wako.(usipojiangalia,ndoa yako ndo inaenda kufall apart Mkuu)
Barikiwa Dada,ni kwelihapana mimi namuona yuko sahihi, inaonesha mwanamke wake anataka kumpanda juu bila kumshirikisha yupo sahihi kabisa baba unatakiwa uwe na sauti yenye mamlaka wanawake tuna manyanyaso sana hapo akimpa hio ruhusa ya kujiandika jina la mwanamke bas wakigombana kidogo utasikia toka kwenye nyumba yangu yan hawa bila huyo mwanaume kua na sauti kama hivo atanyanyasika
unasema akajenge kwengine awaachie hii pia naipinga mwanamke ana kiwanja baba amejenga, baba ametaka anunue kiwanja ili amiliki vyote kihalali bila kunyanyaswa yupo sahihi tena akimpa hizo hela ampe kwa maandishi na mbele ya shahidi huyo mwanamke au wakiona wameshindwa kama inawezekana wawaandikishe watoti wao umiliki
Amina momMali na vyote vilivyo ndani ya Dunia ni batili, tuutafute ufalme wa Mungu
Mkeo mbinafsi. Inaonekana anapata ushauri toka nje yenu. Inaweza ikawa ndugu au rafiki ambaye kwake amefanikiwa kufanya atakavyo.. Nakushauri yafuatayo;Sasa nimeongea na mke wangu kuhusu nyumba ambayo nimejenga kwenye kiwanja chake kuhusu umiliki kwasababu yeye alitaka kuandika jina lake tena kwa Siri.
Nimemuuliza kwanza kwamba tangu tuoane hatujawahi kuongelea kuhusu hicho kiwanja chake.
Akanikumbusha kwamba wakati tunaoana Mimi nilimshauri akiuze na ilituletea mtafaruku kweli. Na ni kweli nilisita sana kujenga kwenye kiwanja cha mke wangu kwasababu nilishaona ni mtu mpenda vyake na asiye na muda na vyangu ilihali tayari sisi ni mke na mme.
Na niwarudishe kidogo kilichonifanya nimuona wa tofauti kidogo baada ya kuhamia pale siku moja mwisho wa mwezi nilienda kuitembelea familia.
Asubuhi tukiwa Mimi na watoto akaleta mada kwamba Joyce (sio jina halisi) ambaye yeye ni shangazi kwa Joyce. Joyce ameniomba Jack (sio jina halisi) yaani mtoto wa Joyce aje aishi hapa na aende shule akikaa kwetu.
Sasa Joyce tuliwahi kukaa naye kama ndugu yake mke wangu akawa anatusaidia kazi lakini alikuja kuondoka kwa ugomvi na mke wangu.
Aliponipa hizo histori akili yangu iliyafanya mrejeo haraka sana nikakumbuka jinsi Joyce alivyoondoka kwa shangazi yake kwa maneno.
Nikamwambia wife hilo kwasasa haitawezekana na sababu niliyompa ni kwamba mtoto wetu kwasasa anasoma English medium halafu huyu Jack akija aende shule ya kawaida ( serikali) Mimi sitajisikia vizuri na haitakuwa sawa hata kwa tafsiri za watu wengi. Nikamshauri kwamba kama ni kwa ajili ya kwenda shule basi aende kwa Shemeji ( kaka yake wife) ambaye kimsingi yupo karibu na shule hiyo ya serikali na ni baba mdogo wake Joyce. Mke wangu alikuja juu sana na kuzua ugomvi kidogo nimpige. Lakini maneno yaliyonikera sana ni kwamba Mimi siwataki ndugu zake na huwa nakuja hapa kuleta vurugu na kwamba anajuta kuolewa na mimi na akakimbilia nje baadae nilimuita akaje tukaongea nikaamua kutulia ili nione maisha yanaendaje baada ya pale.
Na hapa wiki moja kabla alinijulisha swala la kuwekewa bcone kwenye like eneo kwamba inahitahijika 100,000 akanipa na time limit sikutaka maneno nikampa ile hela akalipa niliporudi akanionesha risiti nikamwambia wafuatilie waweke. Wiki inayofuata akanitaarifu kwamba wameshaweka bcone lakini wanahitaji passport 7 kwa maandalizi ya hati nikamwambia sawa.
Nilipoenda nikamwambia ebu nenda idara ya maji ukaulizie utaratibu wa kupata maji kwa bomba binafsi yaani kufungiwa mita ya maji kwenye hiyo nyumba.
Alienda baadae akaniambia wanahitaji tujaze fomu na passport mbili na fomu hurusiwi kuchukua unajazia kule idara ya maji nikamwambia sawa. Jioni akaniambia kesho nataka nikapige zile picha ajaze hizo fomu na kupeleka zile picha 7 kwa ajili ya hati Mimi nikaitikia sawa. Asubuhi kulipokucha nikamwambia simamisha Hilo zoezi hadi nije. Lakini nilimpigia simu jamaa yangu ambaye naye amejaza hiyo fomu nikamuulizi hivi hizi fomu hurusiwi kutokana nazo ukajazie nyumbani? Jamaa akasema mbona Mimi nilijazie nyumbani nikarudisha!
Nikamwambia sawa. Mimi nilikuwa naendelea kukusanya data zangu. Jana nikafanya ziara ya kustukiza nikafika nyumba lakini nikiwa njiani niliandika sms kumjulia hali yeye na watoto nikamwambia nipo njiani nakuja huko. Basi nikafika yeye alikuwa ametoka na watoto nikafungua nikaingia nikampigia akasema anakuja na kweli wakawasili na watoto, watoto wangu wananipenda sana wakafurahi stori mbili tatu.
Mimi sitaka kikao kichukue muda nikaanza kikao na yeye nikamwambia Mimi nimekuja kwa mazungumzo na wewe akastuka sana. Nikamwambia mazungumzo ni ya kawaida ya kifamilia. Tukaongea nikamwambia hiki kiwanja si unajua ni chako akasema ndio. Nikamwambia lakini bahati nzuri tumejaliwa kujenga nyumba ya familia, akasema ndio. Nikamwambia kuna vitu tusipoyaweka sawa huko mbeleni vitatuletea shida akashangaa. Nikamwambia kwasasa tunaelekea kwenye swala la umiliki sasa tuamue Mimi na wewe mmliki wa nyumba ya familia yetu kwenye kiwanja chako kitakuwa na umiliki wa nani? Hana jibu! Nikamuuliza je maji na hilo suala la picha za hati miliki ungeandika? Akasema Mimi nilijua ni vitu vya kawaida Wala sikufikiria yote hayo! Nikamuuliza kwa mkuu wa familia ni nani akasema ni wewe ( Mimi). Nikamuuliza Sasa mbona siku ile ulifanya tu kunipa taarifa tu unataka kwenda kupiga picha bila kuuliza tuandike jina la nani? Akasema Mimi niliona hata nikiandika jina langu ni sawa tu na kwasababu nilikupa taarifa niliona hakuna shida.
Nikamwambia sasa Mimi natambua kwamba kiwanja ni chako lakini nimejenga nyumba ya familia yangu ambayo ni sisi sote. Nimekuja tupate mwafaka wa hicho kiwanja na Mimi nipo kwa ajili kuidhamini familia yangu na katika hii familia tunao jielewa kwasasa ni Mimi na wewe vijana wetu bado wadogo. Nikamwambia Mimi nina majibu yangu lakini nahitaji majibu yako juu ya kiwanja hiki. Nikamkumbusha; kwamba siku ile ulivyoongea maneno ya kwamba Mimi huwa nakuja kukuletea vurugu na kwamba unajuta kuolewa na mimi nilizingatia na hivyo sitakubaki kuiweka rehani familia kwa kuruhusu mambo yaende kiholela. Akahamaki na kudai kwanini namkumbusha mambo ya zamani nikamwambia haikuwa sehemu ya mada lakini nimeona nikukumbushe ili ujirekebishe kimawazo, kauli na kimtazamo na ufahamu mipaka yake kama mke. Akasema Yale alitamka kwa hasira kwasababu ulinikemea mbele ya watoto n.k nikamwambia Mimi uliniletea mada yako mbele ya watoto na nilipopinga wewe ndo ukaleta ugomvi. Akasema tuyamalize kwanza haya ndo tuje swala la umiliki wa nyumba. Ila nikamwambia Mimi siwezi tena kukuruhusu kumiliki hii nyumba kwasababu hutahili utashindwa kuzuia hisia zako na utaendelea kuropoka zaidi na huenda hata kuna siku utamleta mwanaume humu na sitaweza kuzuia. Naye akasema na wewe unaweza kumleta mwanamke halafu unitoe Mimi.
Mwisho akasema nimpe muda atafakari swala la umiliki wa hii nyumba halafu atanipa jibu kwamba hawezi kupata jibu la haraka. Lakini nimemwambia Mimi ndiye nina wajibu na jukumu la kulinda, kuhifadhi na kutunza mali za familia hivyo yeye ni mtu wa pili kutoka kwangu na akaona ugumu nipo tayari kumpa pesa yenye thamani ya kiwanja chake yeye atajua atazifanyaje hizo hela lakini kiwanja kiwe chini ya familia na chini yangu kama mwenyewe dhamana ya familia namba moja.
Kwa hiyo namsubiri aamue then nami nitaweka msimamo wa kiti. Japo sasa amenuna lakini mgonjwa haulizwi dawa. Mimi kiukweli sina plan B ya hilo nahitaji heshima iwepo kwangu kama mwenye nyumba na siwezi kuwa mtalii kwenye familia yangu. Lazima kiti kiheshimiwe bila hivyo panya watatawala.
Naomba kuwasilisha kwa ajili yenu kujifunza na kutoa ushauri.
Asanteni
Pia soma: Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga
Utalia muda si mrefuAkasema Mimi niliona hata nikiandika jina langu ni sawa tu na kwasababu nilikupa taarifa niliona hakuna shida.
Haya uliyoyasema ni ya zamani..!! Siku hizi tathmini inafanywa ya eneo pekee na kilichomo juu ya eneo peke yake..!! Halafu hata mkiachana, zile mambo za kusema nyumba inabaki kwa wtoto yameshabadilika..!! Mnaambiwa hata kama msingekuwa na nyumba au mali au eneo, watoto mngewalea tu..!! Hivi vinathaminishwa na kupigwa bei halafu mnagawana kilichopatikana.Hiyo nyumba ni ya mwanamke jipe muda tuu. Samahani sijaongea ulichotaka kusikia.
Na mwanamke unakubalije kufidiwa pesa na mumeo huku mko ndani ya ndoa?Mkuu una ka element ka kitapeli. Andikeni majina yenu yote kwenye hati na sio eti kutaka kuwa kichwa cha nyumba kwa kupachika jina lako pekee. Kiwanja ni chake. Pesa unayotaka kumfidia kajenge kwenye kiwanja chako. Unachowaza leo hujui kitawasumbua vipi wanao miaka ijayo
Shukrani kwa ushauri mkuu. Ingawa kuandika majina hakumaanishi kumiliki. Hata nikiandika Kwa majina yangu haitimaanisha nina umiliki wa 100%, kwenye kutengana kuna kugawana 50/50.Duu u
Sifanye hivyo aisee hawa viumbe usile nao maagano. Andika jina lako tu kama ni mke wa ndoa hakuna wa kuwahangaisha. Wala usiandike jina la mtoto plz jitahdin kujifunza kutokana na historia. Ukitaka kuwajua hawa viumbe kosa kaz mwaka ushindwe kuhudumia nyumba Ndio utajua hujui.
Mbona mnawekana kwenye mkao wa kuachana? Mwenye kiwanja ndiye mwenye nyumba. Sasa ataandikaje jina lako wakati 'hati' inasoma jina lake?Wanaume tunapitia magumu sana, mm sikupi pole ila nakushauri uendelee kuwa na msimamo wa unachokitaka.
Ukijilegeza tu UMEKWISHA.
Kazia hapo hapo mkuu. Nakuunga mkono asilimia 100Sasa nimeongea na mke wangu kuhusu nyumba ambayo nimejenga kwenye kiwanja chake kuhusu umiliki kwasababu yeye alitaka kuandika jina lake tena kwa Siri.
Nimemuuliza kwanza kwamba tangu tuoane hatujawahi kuongelea kuhusu hicho kiwanja chake.
Akanikumbusha kwamba wakati tunaoana Mimi nilimshauri akiuze na ilituletea mtafaruku kweli. Na ni kweli nilisita sana kujenga kwenye kiwanja cha mke wangu kwasababu nilishaona ni mtu mpenda vyake na asiye na muda na vyangu ilihali tayari sisi ni mke na mme.
Na niwarudishe kidogo kilichonifanya nimuona wa tofauti kidogo baada ya kuhamia pale siku moja mwisho wa mwezi nilienda kuitembelea familia.
Asubuhi tukiwa Mimi na watoto akaleta mada kwamba Joyce (sio jina halisi) ambaye yeye ni shangazi kwa Joyce. Joyce ameniomba Jack (sio jina halisi) yaani mtoto wa Joyce aje aishi hapa na aende shule akikaa kwetu.
Sasa Joyce tuliwahi kukaa naye kama ndugu yake mke wangu akawa anatusaidia kazi lakini alikuja kuondoka kwa ugomvi na mke wangu.
Aliponipa hizo histori akili yangu iliyafanya mrejeo haraka sana nikakumbuka jinsi Joyce alivyoondoka kwa shangazi yake kwa maneno.
Nikamwambia wife hilo kwasasa haitawezekana na sababu niliyompa ni kwamba mtoto wetu kwasasa anasoma English medium halafu huyu Jack akija aende shule ya kawaida ( serikali) Mimi sitajisikia vizuri na haitakuwa sawa hata kwa tafsiri za watu wengi. Nikamshauri kwamba kama ni kwa ajili ya kwenda shule basi aende kwa Shemeji ( kaka yake wife) ambaye kimsingi yupo karibu na shule hiyo ya serikali na ni baba mdogo wake Joyce. Mke wangu alikuja juu sana na kuzua ugomvi kidogo nimpige. Lakini maneno yaliyonikera sana ni kwamba Mimi siwataki ndugu zake na huwa nakuja hapa kuleta vurugu na kwamba anajuta kuolewa na mimi na akakimbilia nje baadae nilimuita akaje tukaongea nikaamua kutulia ili nione maisha yanaendaje baada ya pale.
Na hapa wiki moja kabla alinijulisha swala la kuwekewa bcone kwenye like eneo kwamba inahitahijika 100,000 akanipa na time limit sikutaka maneno nikampa ile hela akalipa niliporudi akanionesha risiti nikamwambia wafuatilie waweke. Wiki inayofuata akanitaarifu kwamba wameshaweka bcone lakini wanahitaji passport 7 kwa maandalizi ya hati nikamwambia sawa.
Nilipoenda nikamwambia ebu nenda idara ya maji ukaulizie utaratibu wa kupata maji kwa bomba binafsi yaani kufungiwa mita ya maji kwenye hiyo nyumba.
Alienda baadae akaniambia wanahitaji tujaze fomu na passport mbili na fomu hurusiwi kuchukua unajazia kule idara ya maji nikamwambia sawa. Jioni akaniambia kesho nataka nikapige zile picha ajaze hizo fomu na kupeleka zile picha 7 kwa ajili ya hati Mimi nikaitikia sawa. Asubuhi kulipokucha nikamwambia simamisha Hilo zoezi hadi nije. Lakini nilimpigia simu jamaa yangu ambaye naye amejaza hiyo fomu nikamuulizi hivi hizi fomu hurusiwi kutokana nazo ukajazie nyumbani? Jamaa akasema mbona Mimi nilijazie nyumbani nikarudisha!
Nikamwambia sawa. Mimi nilikuwa naendelea kukusanya data zangu. Jana nikafanya ziara ya kustukiza nikafika nyumba lakini nikiwa njiani niliandika sms kumjulia hali yeye na watoto nikamwambia nipo njiani nakuja huko. Basi nikafika yeye alikuwa ametoka na watoto nikafungua nikaingia nikampigia akasema anakuja na kweli wakawasili na watoto, watoto wangu wananipenda sana wakafurahi stori mbili tatu.
Mimi sitaka kikao kichukue muda nikaanza kikao na yeye nikamwambia Mimi nimekuja kwa mazungumzo na wewe akastuka sana. Nikamwambia mazungumzo ni ya kawaida ya kifamilia. Tukaongea nikamwambia hiki kiwanja si unajua ni chako akasema ndio. Nikamwambia lakini bahati nzuri tumejaliwa kujenga nyumba ya familia, akasema ndio. Nikamwambia kuna vitu tusipoyaweka sawa huko mbeleni vitatuletea shida akashangaa. Nikamwambia kwasasa tunaelekea kwenye swala la umiliki sasa tuamue Mimi na wewe mmliki wa nyumba ya familia yetu kwenye kiwanja chako kitakuwa na umiliki wa nani? Hana jibu! Nikamuuliza je maji na hilo suala la picha za hati miliki ungeandika? Akasema Mimi nilijua ni vitu vya kawaida Wala sikufikiria yote hayo! Nikamuuliza kwa mkuu wa familia ni nani akasema ni wewe ( Mimi). Nikamuuliza Sasa mbona siku ile ulifanya tu kunipa taarifa tu unataka kwenda kupiga picha bila kuuliza tuandike jina la nani? Akasema Mimi niliona hata nikiandika jina langu ni sawa tu na kwasababu nilikupa taarifa niliona hakuna shida.
Nikamwambia sasa Mimi natambua kwamba kiwanja ni chako lakini nimejenga nyumba ya familia yangu ambayo ni sisi sote. Nimekuja tupate mwafaka wa hicho kiwanja na Mimi nipo kwa ajili kuidhamini familia yangu na katika hii familia tunao jielewa kwasasa ni Mimi na wewe vijana wetu bado wadogo. Nikamwambia Mimi nina majibu yangu lakini nahitaji majibu yako juu ya kiwanja hiki. Nikamkumbusha; kwamba siku ile ulivyoongea maneno ya kwamba Mimi huwa nakuja kukuletea vurugu na kwamba unajuta kuolewa na mimi nilizingatia na hivyo sitakubaki kuiweka rehani familia kwa kuruhusu mambo yaende kiholela. Akahamaki na kudai kwanini namkumbusha mambo ya zamani nikamwambia haikuwa sehemu ya mada lakini nimeona nikukumbushe ili ujirekebishe kimawazo, kauli na kimtazamo na ufahamu mipaka yake kama mke. Akasema Yale alitamka kwa hasira kwasababu ulinikemea mbele ya watoto n.k nikamwambia Mimi uliniletea mada yako mbele ya watoto na nilipopinga wewe ndo ukaleta ugomvi. Akasema tuyamalize kwanza haya ndo tuje swala la umiliki wa nyumba. Ila nikamwambia Mimi siwezi tena kukuruhusu kumiliki hii nyumba kwasababu hutahili utashindwa kuzuia hisia zako na utaendelea kuropoka zaidi na huenda hata kuna siku utamleta mwanaume humu na sitaweza kuzuia. Naye akasema na wewe unaweza kumleta mwanamke halafu unitoe Mimi.
Mwisho akasema nimpe muda atafakari swala la umiliki wa hii nyumba halafu atanipa jibu kwamba hawezi kupata jibu la haraka. Lakini nimemwambia Mimi ndiye nina wajibu na jukumu la kulinda, kuhifadhi na kutunza mali za familia hivyo yeye ni mtu wa pili kutoka kwangu na akaona ugumu nipo tayari kumpa pesa yenye thamani ya kiwanja chake yeye atajua atazifanyaje hizo hela lakini kiwanja kiwe chini ya familia na chini yangu kama mwenyewe dhamana ya familia namba moja.
Kwa hiyo namsubiri aamue then nami nitaweka msimamo wa kiti. Japo sasa amenuna lakini mgonjwa haulizwi dawa. Mimi kiukweli sina plan B ya hilo nahitaji heshima iwepo kwangu kama mwenye nyumba na siwezi kuwa mtalii kwenye familia yangu. Lazima kiti kiheshimiwe bila hivyo panya watatawala.
Naomba kuwasilisha kwa ajili yenu kujifunza na kutoa ushauri.
Asanteni
Pia soma: Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga
Na mwanamke unakubalije kufidiwa pesa na mumeo huku mko ndani ya ndoa?
Kuna siku utatimuliwa nyumbaniMkuu, pole. Hope mtapata ufumbuzi mujarabu wa hiyo kadhia.
Mimi baada ya kuona jinsi wife anavyowapenda wanae (tuna watoto 2, mmoja miaka 5 mwingine miaka 2), nikaona sio kesi akiandika jina lake kwenye umiliki wa kiwanja. Mungu jaalia, tunaweza anza ujenzi mwakani, lakini hata nyumba nataka iwe Kwa majina yake. Sababu ni zipi?
1. Najua hawezi watelekeza watoto (labda apigwe ndumba), so pale patakuwa pa watoto. Hata likitokea la kutokea, siombei, watoto watakuwa na kwao.
2. Nimeshuhudia issues za mirathi, ndugu wamechukua mirathi ya watoto,(ilikuwa 19M). Yaani baba na mama wamekufa, mjomba akapewa zoezi la kusimamia mirathi ya marehemu dada yake, ndo mirathi ya wadogo wawili waliokuwa chini ya 18 ikapigwa. Nilijifunza kuwa mzazi, baba au mama atakuwa na uchungu zaidi na mali za watoto kuliko mtu wa nje.
Labda nakosea, labda sijui, kikubwa fuata moyo wako
🤣🤣🤣. Nina ka-salary ka kunipush siku mbili tatu mkuu. Sintoshindwa kujipanga na kujenga hata ka-master na sebule vya kuzeekea. Ila nitakuwa nimewaacha watoto wakiwa na nyumba. Najua, hatawatelekezaKuna siku utatimuliwa nyumbani
Mkuu Mbona unaongea Kama mtoto mdogo, hivi wewe kweli una Hata chumba kimoja kweli, yaani unasema muachie aandike jina lake na yeye ajenge Nyumba nyingine, hivi ujenzi Ni wa siku moja au? Unajua kipato Cha mleta hoja? Je Kama kastaafu na Sasa ndo kajenga!!?Ukishaona mnagombea umiliki wa nyumba huku mmeoana ujue ndoa inaelekea pabaya, akikataa umiliki wa pamoja mwachie tuu, anza kujenga yako na weka clear ni yako 100% na unafanya hivyo kwa sababu ya alichofanya nyumba ya kwanza, hakikisha unajenga nzuri kuliko yake, sounds utoto lakini dawa ya moto ni moto na kisheria wote mtashindwa mtaishia kugawana nusu kwa nusu tuu
Kweli..aacha mawenge....Tena angeandika watoto kama vipi...Mimi sioni shida..hiyo nyumba kwa mazingira yalivyo..pia hata angeandika mke sawa tu..Mimi sioni shida..hata kama kesho aseme tuachane..binafsi Siwezi kwenda kugombea eti hiyo nyumba..big no.Mkuu una ka element ka kitapeli. Andikeni majina yenu yote kwenye hati na sio eti kutaka kuwa kichwa cha nyumba kwa kupachika jina lako pekee. Kiwanja ni chake. Pesa unayotaka kumfidia kajenge kwenye kiwanja chako. Unachowaza leo hujui kitawasumbua vipi wanao miaka ijayo